Ukweli kwa miaka kumi hii ambayo nusu imeongozwa na Magufuli na Nusu imeongozwa na mama Samia.
CCM wamefanya mambo makubwa mengi sana yanayoonekana kwa macho, bila mizengwe yanawapa uwezo wa kupata ushindi hata wangekuwa wanagombea urais Kenya, Zambia, Msumbiji, Congo, Rwanda, Uganda etc.
hakuna chama chochote ama Rais yeyote wa nchi zinazotuzunguka aliyefanya maendeleo mengi kwa nchi yake kuwazidi CCM kwa waliyofanya kwa Tanzania ndani ya miaka 10 hii
imagine kwa miaka zaidi ya 50 wamepita marais tofauti kwa awamu 4, wote hao kwa pamoja from 1961 mpaka 2015 waliweza kuzalisha umeme Megawatts 1600 tu kwa nchi nzima ya TANZANIA, tena hapo tumejumlisha mpaka umeme wa kampuni za kitapeli kama Richmond, iptl, songas, dowans etc.
ila sasa CCM ya miaka 10 hii imewavuka wote na kufikisha MW 4000, wamewapita awamu zote 4 za nyuma
CCM ya miaka 10 hii imejenga hospitali nyingi mpya kuliko zile ambazo zimejengwa na awamu zote 4
CCM ya miaka 10 hii imejenga Flyover nyingi mpaka imetufanya wa Tanzania wasishangae na kuona Fly over ni kitu cha ajabu
CCM ya miaka 10 hii imeleta mpaka treni ya umeme ya kwanza africa mashariki,, nchi jirani zinawaona viongozi wao ni matapeli sababu ya maendeleo ya ccm
KENYA ametuongoza kwa uzalishaji umeme kuanzia tunapata uhuru mpaka miaka 50 mbele,, ila CCM ndani ya miaka 10 hii imeifanya Tanzania impite mpaka kenya kwa uzalishaji umeme na maendeleo mengine
UKWELI 2015 - 2025 NI GOLDEN AGE YA CCM
Ni era pekee ambayo CCM inapinga makampuni ya kifisadi kwa vitendo, ambavyo hata wananchi tunaona
View attachment 3227724