adriz
JF-Expert Member
- Sep 2, 2017
- 12,207
- 26,521
Moja kwa Moja.
Mwaka 2015 mitaa Fulani Dar es Salaam muda huo nipo kidato Cha kwanza (Form One) nilikuwa na hamu sana ya kumililiki simu , basi nikatafuta kibubu nikawa naweka pesa za shule kama akiba na kupiga mishe ndogo ndogo kitaa ili kujazia kibubu baada ya miezi kadhaa nikavunja nikachukua kiasi kidogo nikanunua Kiswaswadu kwa mtu.
Japo kulikuwa Kiswaswadu lakini kulikuwa na uwezo na Kasi ya ajabu kwenye masuala ya kimtandao mpaka YouTube ilikuwa Ina support vizuri ,sasa siku moja nilisoma stori kwenye gazeti nikaipenda na nilivyoona itakuwa ngumu kupata gazeti kila siku ikabidi niingie gugo kuisearch ndipo nikaletwa Jf rasmi kwa mara ya kwanza n kuanza kuisoma stori kupitia Jf . Kilichonivutia zaidi upande wa comments watu walikuwa wacheshi sana na jokes za maana zilikuwepo.
Mwaka huo huo ikaja 'Freebasics' kuperuzi kurasa mbalimbali ikiwemo Jf ikawa bure hapo ndio rasmi nikawa nashinda rasmi JF kwa masaa mengi haswa jukwaa la photos, nikawa najaribu kujiunga kama member ikawa inakataa mpaka mwaka 2017 kipindi nipo Kidato Cha Tatu wakati huo nina simu kubwa tayari ndipo siku moja nikadowload app ya Jf kujaribu kujiunga tena ikakubali nikawa Mwanachama wa JF.
Faida
1. JF imenifanya niwe mpenzi sana wa kusoma vitabu ; japo tokea niko shule ya msingi nilikuwa msomaji mzuri wa vitabu na makala mbalimbali za kidini, historia na siasa nilivyojiunga JF nikajiona bado nipo mweupe inabidi niongeze maarifa zaidi ili niweze kujitetea na kuweza kufanya mijadala humu.
2. Imenifanya nijue vitu vingi vipya , kuongeza Maarifa na kupata Marafiki mbalimbali ambao tupo karibu hata nje ya JF.
3. Nk..
Changamoto
JF ilikuwa inakula muda wangu sana mpaka nikawa nahisi najinyima muda wa masomo, baadae nikawa natenga muda Maalumu tu wakuperuzi(Kila siku saa 12 jioni mpaka saa 2 usiku)
Kukutana na mijadala mizito iliyonizidi umri haswa kule Intelligence ambapo nilikuwa napenda sana kutembelea , Kadri nilivyojilazimisha kusoma nikawa naelewa vizuri na kuiona kawaida .
Kasumba ya watu kudharau watoto , kipindi Cha nyuma ilikuwepo sana ilikuwa mtu akiteleza kidogo utasikia "hapa sio fesibuku dogo" au "Kwani shule zimefunguliwa? Hapo nikawa Muoga sana kuchangia na kama nikichangia lazima nijiridhishe kwanza na ikabidi niwe kama mtu mzima mpaka ikafika stage watu wengine kunifuata PM niwashauri kwenye mambo makubwa ambayo hata sijafikia na sina uzoefu nayo.
Mengineyo.
Tokea nijinge sijawahi kupata ban Wala kumiliki ID nyingine zaidi ya hii.
Huwa sipendi watu wanijue kama nipo Jf hata nikiperuzi huwa nahakiikisha hakuna mtu karibu anayekula chabo na Kuna mahali niliwahi kufanya kazi mfanyakazi mwenzangu (JF member) nilikuwa napiga strori nae akawa anasifia JF jinsi ilivyomsaidia kupata baadhi ya Info Mimi nikajifanya siijui kabisa alishangaa sana mtu kama Mimi sipo JF Wala siijui.
#UziUnaendelea
Mwaka 2015 mitaa Fulani Dar es Salaam muda huo nipo kidato Cha kwanza (Form One) nilikuwa na hamu sana ya kumililiki simu , basi nikatafuta kibubu nikawa naweka pesa za shule kama akiba na kupiga mishe ndogo ndogo kitaa ili kujazia kibubu baada ya miezi kadhaa nikavunja nikachukua kiasi kidogo nikanunua Kiswaswadu kwa mtu.
Japo kulikuwa Kiswaswadu lakini kulikuwa na uwezo na Kasi ya ajabu kwenye masuala ya kimtandao mpaka YouTube ilikuwa Ina support vizuri ,sasa siku moja nilisoma stori kwenye gazeti nikaipenda na nilivyoona itakuwa ngumu kupata gazeti kila siku ikabidi niingie gugo kuisearch ndipo nikaletwa Jf rasmi kwa mara ya kwanza n kuanza kuisoma stori kupitia Jf . Kilichonivutia zaidi upande wa comments watu walikuwa wacheshi sana na jokes za maana zilikuwepo.
Mwaka huo huo ikaja 'Freebasics' kuperuzi kurasa mbalimbali ikiwemo Jf ikawa bure hapo ndio rasmi nikawa nashinda rasmi JF kwa masaa mengi haswa jukwaa la photos, nikawa najaribu kujiunga kama member ikawa inakataa mpaka mwaka 2017 kipindi nipo Kidato Cha Tatu wakati huo nina simu kubwa tayari ndipo siku moja nikadowload app ya Jf kujaribu kujiunga tena ikakubali nikawa Mwanachama wa JF.
Faida
1. JF imenifanya niwe mpenzi sana wa kusoma vitabu ; japo tokea niko shule ya msingi nilikuwa msomaji mzuri wa vitabu na makala mbalimbali za kidini, historia na siasa nilivyojiunga JF nikajiona bado nipo mweupe inabidi niongeze maarifa zaidi ili niweze kujitetea na kuweza kufanya mijadala humu.
2. Imenifanya nijue vitu vingi vipya , kuongeza Maarifa na kupata Marafiki mbalimbali ambao tupo karibu hata nje ya JF.
3. Nk..
Changamoto
JF ilikuwa inakula muda wangu sana mpaka nikawa nahisi najinyima muda wa masomo, baadae nikawa natenga muda Maalumu tu wakuperuzi(Kila siku saa 12 jioni mpaka saa 2 usiku)
Kukutana na mijadala mizito iliyonizidi umri haswa kule Intelligence ambapo nilikuwa napenda sana kutembelea , Kadri nilivyojilazimisha kusoma nikawa naelewa vizuri na kuiona kawaida .
Kasumba ya watu kudharau watoto , kipindi Cha nyuma ilikuwepo sana ilikuwa mtu akiteleza kidogo utasikia "hapa sio fesibuku dogo" au "Kwani shule zimefunguliwa? Hapo nikawa Muoga sana kuchangia na kama nikichangia lazima nijiridhishe kwanza na ikabidi niwe kama mtu mzima mpaka ikafika stage watu wengine kunifuata PM niwashauri kwenye mambo makubwa ambayo hata sijafikia na sina uzoefu nayo.
Mengineyo.
Tokea nijinge sijawahi kupata ban Wala kumiliki ID nyingine zaidi ya hii.
Huwa sipendi watu wanijue kama nipo Jf hata nikiperuzi huwa nahakiikisha hakuna mtu karibu anayekula chabo na Kuna mahali niliwahi kufanya kazi mfanyakazi mwenzangu (JF member) nilikuwa napiga strori nae akawa anasifia JF jinsi ilivyomsaidia kupata baadhi ya Info Mimi nikajifanya siijui kabisa alishangaa sana mtu kama Mimi sipo JF Wala siijui.
#UziUnaendelea