Miaka ya 90 pale uwanja wa ndege mzee Mwinyi aliwahi kunipa hela, fulana kwa mkono wake mwenyewe kisha akanambia maneno haya...

Miaka ya 90 pale uwanja wa ndege mzee Mwinyi aliwahi kunipa hela, fulana kwa mkono wake mwenyewe kisha akanambia maneno haya...

Daah ker elimu muhimu
Wazazi wa mzee Mwinyi walilenga kumpeleka Zanzibar kujifunza elimu akhera, maana hapa kwao bara elimu hiyo ilikuwa haipewi kipaumbele na serikali ya kikoloni.

Mzee alipofika kule Zanzibar akajiongeza kwa kusoma na elimu dunia, ambayo baadae ilikuja kumletea matokeao makubwa katika maisha yake hadi kupeleka kuwa raisi wa nchi mbili. Huku kwao kwa asili alipozaliwa na kule alipohamia.

So mzee Mwinyi aliuona ubora wa elimu ndio maana alinisisitiza nisimame na elimu iwe jua iwe mvua.
 
Mkuu Mr Dudumizi, simulizi yako inaniliza. Hasa hapo alipoagwa na kuelekea Zanzibar. Na leo ataagwa tena na kuelekea Zanzibar tena. Ila leo ni tofauti na mwaka 1995. Mwaka 1995 aliondoka akiwa hai, leo atasafirishwa akiwa si hai. Ni maisha tu!

Mimi nami nilikutana na kupokea zawadi kutoka kwake mwaka 1992 alipotembelea Shule yetu ya Msingi akiwa Rais. Alianzia mahali alipokwenda kutatua mgogoro wa ardhi baina ya wananchi. Alinipa zawadi baada ya kufanya vyema kwenye kujieleza mbele yake.

Pumzika pema Mzee Mwinyi, Rais wetu wa awamu ya pili!
Hakika mzee Mwinyi atakumbukwa na wengi kwa sababu ya kuwafanyia watu mema mengi.

Alikuwa tayari kutukanwa, kusimangwa, kuzushiwa ili kuifungua nchi na kuhakikisha kila mtu anapata kile anachotakiwa kupata. Aliruhusu biashara huru, kila mtu alisogezewa huduma alizokosa karibu yake, shule, maduka, hospital, vyakula, barabara na vitu vingine vingi ambavyo havikuwa vinapatikana kirahisi kabla ya uongozi wake.
 
Hakuwa na makuu hata. Siku moja alifika kwenye shule moja akajaribishwa bites kwe darasa akapata, kisha akaenda kujisaidia katika choo cha mkuu wa shule akisindikizwa na askari, alitushika mkono kusalimia. Hakukuwa na mbwembwe hata...
Nakumbuka akiwa raisi, mvua iliwahi kunyesha kubwa ikasabaisha uharibifu mkubwa maeneo mengi ya Dar es salaam. Mzee Mwinyi akiwa raisi alitembelea maeneo hayo tena akiwa mstari wa mbele kuwasaidia watu kutoa takataka mbali mbali katika mitaro iliyoziba.

Mimi nilimuona pale Manzese sokoni akiwa na buti za mvua akiingia matopeni kuwasaidia wafanya biashara kutoka vitu vyao vilivyoharibiwa vibaya na mvua.
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Nikiwa na umri mdogo nilihudhuria pale katika uwanja wa ndege wa kimataifa jijini Dar es salaam, kumuaga mzee wetu mzee Ally Hassan Mwinyi ambae alikuwa anaondoka kuelekea Zanzibar, baada ya utawala wake wa miaka 10 kuisha kikatiba.

Bibi yangu ambae alikuwa na umri sawa na marehemu mzee Mwinyi ila bibi alimzidi Mwinyi miezi miwili, alikuwa ni kiongozi wa kikundi fulan cha ngoma za kitamaduni zilizokuwa zinachaguliwa mara kwa mara kwenda kutumbuiza sehemu mbali mbali alizofika raisi Mwinyi enzi za utawala wake. Bibi yangu alikuwa na tatizo la ulemavu wa macho, hivyo mzee Mwinyi alitokea kumzoea na kumfahamu bibi yangu haraka sana (nahisi ni kutokana na ulemavu wake na pia kujituma hata pale alipokuwa mlemavu) mpaka kufikia kipindi mzee Mwinyi akawa anamwita bibi yangu "bi siti Mwinyi" kwa jina la utani.

Siku hiyo ya kumuaga mzee Mwinyi bibi na kikundi chake cha utamaduni walialikwa, hivyo wakati wakifanya maandalizi ya kujiandaa kwenda uwanja wa ndege mimi nikawa nang'ang'ania ili niende nao uwanja wa ndege kwa sababu usafiri ulikuwa wa bure tena basi la jeshi. Wakati huo nilikuwa bado kijana mdogo alafu ni mjukuu wa mwenye kikundi, hivyo hakuna aliepinga mimi kwenda hadi uwanja wa ndege kumuaga mzee Mwinyi.

Tulivyofika pale tukakuta vikundi vingine mbali mbali vya ngoma za kiutamaduni kutoka katika makabila na jamii mbali mbali, basi na sisi tukajumuika nao kumsubiri mgeni husika afike ili tumuage. Masaa mawili baada ya sisi kufika mzee Mwinyi alifika akiwa na familia yake akawa anapita katika kikundi kimoja kimoja ili kusikiliza nyimbo zao za kumuaga.

Alipofika pale katika kikundi cha bibi yangu alimsalimia bibi na kikundi chake chote kwa mkono, kisha akanisogelea na kuniuliza "mjukuu wangu wewe unaitwa nani?" Nikamjibu "naitwa M....", akaendelea "unasoma darasa la ngapi", nikamjibu ..., akauliza "umekuja na nani?" Nikamjibu "nimekuja na bibi yangu", bibi akaingilia kati na kumwambia "huyo ni mjukuu wangu", mzee Mwinyi akatabasamu akaingiza mkono mfukoni na kutoa kibunda cha pesa akanikabidhi nikakitia mfukoni.

Kulikuwa na jamaa pembeni (nahisi ni mlinzi au mpambe wake) akamwambia ampe tshirt 1 nyeupe iliyokuwa na picha yake akanikabidhi kama zawadi, kisha akanambia 👉 "Mjukuu wangu dunia ya leo ni elimu, hivyo pamoja na kupenda kuongozana na bibi yako katika mambo haya ya kitamaduni, lakini hakikisha elimu ndio kinakuwa kipaumbele chako cha kila siku katika maisha yako". Nikaitikia kwa kichwa huku nikitabasamu 😊 na yeye akatabasamu 😊

Kisha walinzi wake wakamwambia mzee muda wa ndege kuondoka unakaribia, akaendelea kuwaaga watu wengine mbali mbali waliokuwa pale uwanja wa ndege kumuaga, kisha akaingia ndani ya ndege huku akitupungia mkono.

Mzee Mwinyi alikuwa mtu mwenye moyo wa utu, wala hakuwahi kuwa na visasi na watu.
Aliwapenda watu na yeye alipendwa na watu. Taifa limepoteza mtu muhimu sana, ila ndo hivyo kazi ya Mungu haina makosa. Tulikuja kutoka udongoni, na tutarudia huko huko udongoni.


Bibi yangu yeye bado yupo hai ila ameshapoteza kumbukumbu, muda mwingine anamsahau mpaka mama yangu ambae ni mtoto wake mwenyewe wa kumzaa. Kidogo anamkumbuka mama yetu mdogo ambae ndio anaishi nae kwa sasa.

Pumzika kwa amani mzee Mwinyi, Mw/Mungu ailaze roho yako mahali pema peponi ameena.
Leo ndo nimejua kwann wewe ni mtata, mgumu kuelewa kama mawe Yale ya mtoni.

Bibi Yako yaezakuwa amekukabidhi mikoba😀
 
Hakuwa na makuu hata. Siku moja alifika kwenye shule moja akajaribishwa bites kwe darasa akapata, kisha akaenda kujisaidia katika choo cha mkuu wa shule akisindikizwa na askari, alitushika mkono kusalimia. Hakukuwa na mbwembwe hata...
Enzi hizo hapakuwa na hizi Takataka zinazojiita Chawa.

Viongozi walikuwa Real, hawakuwa wakipewa sifa za Uungu na wala kujiona wao ni Wa Pekee kama ilivyo sasa.
 
SIsi ni wanafiki sana, mtu akifa tunamsifia weee.

Mwinyi huyu aliyesababisha watumishi wa serikali waache kazi na kuingia kwenye biashara?

Mfumuko wa bei ulikuwa juu?

Nyerere kumlaumu kuwa aligeuza Ikuly kuwa nyumba ya walanguzi?

Akaiuza Loliondo?

Udini ukashamiri?

Mpeni mtu haki yake akiwa hai na akiwa mfu
Sipendi kuzungumzia udini maana hata kipindi cha hayati Magufuli serikali yake ilikuwa na mawaziri watatu tu waislam, huku waliobakia zaidi ya ishirini wakiwa wakristo. Kwako wewe hilo haukuliona maana huenda lilinufaisha upande wako.

Kumbuka raisi Mwinyi ndio raisi wa kwanza kumleta papa John Paul nchini Tanzania. Sasa huo udini wako unaosema hapa sijui ni udini upi?

Ngoja nijikite kwenye point za nje ya udini wako. Unasema Mwinyi alisabisha watumishi waache kazi, huo ulikuwa ni utashi wao. Lakini kwa vile katika taifa huwa kuna watu wengi huwa hawana kazi, basi walioacha kazi nafasi zao zilichukuliwa na watu waliokuwa hawana kazi tatizo liko wapi? Lakini umesahau kuwa wakati Mwinyi anaingia madarakani aliikuta hazina ya taifa ikiwa tupu, haina hela. Serikali nzima ilikuwa imefilisika na watumishi wengi walikuwa wanafanya kazi kizalendo tu bila kupata mshahara wowote. Alipoingia Mwinyi akaifungua nchi, wafanyakazi wakaanza kupokea, na wengine kuamua kuacha kazi ili kutoa fursa kwa wengine alaf wao wakajikita kwenye biashara, sasa kati ya mtu kufanya biashara bila kulipwa na yule anaelipwa na kuamua kujiongeza kufanya biashara ili kukidhi mahitahi ya maisha yake nani aliekosea?

Nyerere kamlaumu Mwinyi kuhusu loliondo, lakini Nyerere huyu huyu wakati wa utawala wake alizuia vyombo vya habari visiandike kuhusu matatizo wanayopitia wananchi kama vile kukosa mahitaji ya msingi madukani, watu wazima kuvaa midabwada na suruali za viraka, kuvaa chachacha, watoto kwenda shule bila viatu, kusababisha watu wenye maono makubwa kama kina Kambona kukimbia nchi nk. Nchi ilikuwa katika hali mbaya hadi kupelekea kuponea kupinduliwa mara mbili na baadhi ya wanajeshi, ambao walichoka na uozo wa serikali yake na kuamua kusimama upande wa wananchi.

Na bado mpaka leo hayati Nyerere tunamsifu kwa mema tu, hatujawahi kumsema kwa baya, ila haujaja kupinga sifa hizo alizopewa baada ya kufa. Wewe ndo mnafiki.
 
Atangazwe mwenye kheri kwenye upande wa Dini/Imani yake Hayati Mzee Mwinyi,,,ana mema mengi mnoo na kwa wengi pia!!###AmpumzikePanapostahili###
Swadakta kabisa, japo sina uhakika kama katika dini yake hilo swala linaruhusiwa.
 
Kibunda kilikuwa cha Sh. Ngapi?

Mimi alinipa bendera ya Tanzania siku aliyokuja Papa John. Tulikuwa miongoni mwa wapokea wageni.

RIP Mzee Mwinyi.
Kilikuwa elf 25, japo mimi niliambulia elf 10 zingine ziliishia kwa wakubwa na wadogo zangu.
 
mwenye ile picha ya
Chai na kikombe kinatoa mvuke anireply😂
Ninayo nyingine ila ni ya nyani naomba niitume wakati wenzangu wakijiandaa kuituma uliyoiomba
20240124_142909.jpg
 
Back
Top Bottom