Miaka ya 90 pale uwanja wa ndege mzee Mwinyi aliwahi kunipa hela, fulana kwa mkono wake mwenyewe kisha akanambia maneno haya...

Miaka ya 90 pale uwanja wa ndege mzee Mwinyi aliwahi kunipa hela, fulana kwa mkono wake mwenyewe kisha akanambia maneno haya...

Habari zenu wanaJF wenzangu,

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Nikiwa na umri mdogo nilihudhuria pale katika uwanja wa ndege wa kimataifa jijini Dar es salaam, kumuaga mzee wetu mzee Ally Hassan Mwinyi ambae alikuwa anaondoka kuelekea Zanzibar, baada ya utawala wake wa miaka 10 kuisha kikatiba.

Bibi yangu ambae alikuwa na umri sawa na marehemu mzee Mwinyi ila bibi alimzidi Mwinyi miezi miwili, alikuwa ni kiongozi wa kikundi fulan cha ngoma za kitamaduni zilizokuwa zinachaguliwa mara kwa mara kwenda kutumbuiza sehemu mbali mbali alizofika raisi Mwinyi enzi za utawala wake. Bibi yangu alikuwa na tatizo la ulemavu wa macho, hivyo mzee Mwinyi alitokea kumzoea na kumfahamu bibi yangu haraka sana (nahisi ni kutokana na ulemavu wake na pia kujituma hata pale alipokuwa mlemavu) mpaka kufikia kipindi mzee Mwinyi akawa anamwita bibi yangu "bi siti Mwinyi" kwa jina la utani.

Siku hiyo ya kumuaga mzee Mwinyi bibi na kikundi chake cha utamaduni walialikwa, hivyo wakati wakifanya maandalizi ya kujiandaa kwenda uwanja wa ndege mimi nikawa nang'ang'ania ili niende nao uwanja wa ndege kwa sababu usafiri ulikuwa wa bure tena basi la jeshi. Wakati huo nilikuwa bado kijana mdogo alafu ni mjukuu wa mwenye kikundi, hivyo hakuna aliepinga mimi kwenda hadi uwanja wa ndege kumuaga mzee Mwinyi.

Tulivyofika pale tukakuta vikundi vingine mbali mbali vya ngoma za kiutamaduni kutoka katika makabila na jamii mbali mbali, basi na sisi tukajumuika nao kumsubiri mgeni husika afike ili tumuage. Masaa mawili baada ya sisi kufika mzee Mwinyi alifika akiwa na familia yake akawa anapita katika kikundi kimoja kimoja ili kusikiliza nyimbo zao za kumuaga.

Alipofika pale katika kikundi cha bibi yangu alimsalimia bibi na kikundi chake chote kwa mkono, kisha akanisogelea na kuniuliza "mjukuu wangu wewe unaitwa nani?" Nikamjibu "naitwa M....", akaendelea "unasoma darasa la ngapi", nikamjibu ..., akauliza "umekuja na nani?" Nikamjibu "nimekuja na bibi yangu", bibi akaingilia kati na kumwambia "huyo ni mjukuu wangu", mzee Mwinyi akatabasamu akaingiza mkono mfukoni na kutoa kibunda cha pesa akanikabidhi nikakitia mfukoni.

Kulikuwa na jamaa pembeni (nahisi ni mlinzi au mpambe wake) akamwambia ampe tshirt 1 nyeupe iliyokuwa na picha yake akanikabidhi kama zawadi, kisha akanambia ๐Ÿ‘‰ "Mjukuu wangu dunia ya leo ni elimu, hivyo pamoja na kupenda kuongozana na bibi yako katika mambo haya ya kitamaduni, lakini hakikisha elimu ndio kinakuwa kipaumbele chako cha kila siku katika maisha yako". Nikaitikia kwa kichwa huku nikitabasamu ๐Ÿ˜Š na yeye akatabasamu ๐Ÿ˜Š

Kisha walinzi wake wakamwambia mzee muda wa ndege kuondoka unakaribia, akaendelea kuwaaga watu wengine mbali mbali waliokuwa pale uwanja wa ndege kumuaga, kisha akaingia ndani ya ndege huku akitupungia mkono.

Mzee Mwinyi alikuwa mtu mwenye moyo wa utu, wala hakuwahi kuwa na visasi na watu.
Aliwapenda watu na yeye alipendwa na watu. Taifa limepoteza mtu muhimu sana, ila ndo hivyo kazi ya Mungu haina makosa. Tulikuja kutoka udongoni, na tutarudia huko huko udongoni.


Bibi yangu yeye bado yupo hai ila ameshapoteza kumbukumbu, muda mwingine anamsahau mpaka mama yangu ambae ni mtoto wake mwenyewe wa kumzaa. Kidogo anamkumbuka mama yetu mdogo ambae ndio anaishi nae kwa sasa.

Pumzika kwa amani mzee Mwinyi, Mw/Mungu ailaze roho yako mahali pema peponi ameena.
Wazee wa kuunga story za marehemu huwa wengi misibani hasa msiba wa tajir wanajikutaga wanamjua marehemu ili yapige menyu ya kutosha

Naona mzee wa kuunga na msiba wa tajiri umejiunga sio ...
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Nikiwa na umri mdogo nilihudhuria pale katika uwanja wa ndege wa kimataifa jijini Dar es salaam, kumuaga mzee wetu mzee Ally Hassan Mwinyi ambae alikuwa anaondoka kuelekea Zanzibar, baada ya utawala wake wa miaka 10 kuisha kikatiba.

Bibi yangu ambae alikuwa na umri sawa na marehemu mzee Mwinyi ila bibi alimzidi Mwinyi miezi miwili, alikuwa ni kiongozi wa kikundi fulan cha ngoma za kitamaduni zilizokuwa zinachaguliwa mara kwa mara kwenda kutumbuiza sehemu mbali mbali alizofika raisi Mwinyi enzi za utawala wake. Bibi yangu alikuwa na tatizo la ulemavu wa macho, hivyo mzee Mwinyi alitokea kumzoea na kumfahamu bibi yangu haraka sana (nahisi ni kutokana na ulemavu wake na pia kujituma hata pale alipokuwa mlemavu) mpaka kufikia kipindi mzee Mwinyi akawa anamwita bibi yangu "bi siti Mwinyi" kwa jina la utani.

Siku hiyo ya kumuaga mzee Mwinyi bibi na kikundi chake cha utamaduni walialikwa, hivyo wakati wakifanya maandalizi ya kujiandaa kwenda uwanja wa ndege mimi nikawa nang'ang'ania ili niende nao uwanja wa ndege kwa sababu usafiri ulikuwa wa bure tena basi la jeshi. Wakati huo nilikuwa bado kijana mdogo alafu ni mjukuu wa mwenye kikundi, hivyo hakuna aliepinga mimi kwenda hadi uwanja wa ndege kumuaga mzee Mwinyi.

Tulivyofika pale tukakuta vikundi vingine mbali mbali vya ngoma za kiutamaduni kutoka katika makabila na jamii mbali mbali, basi na sisi tukajumuika nao kumsubiri mgeni husika afike ili tumuage. Masaa mawili baada ya sisi kufika mzee Mwinyi alifika akiwa na familia yake akawa anapita katika kikundi kimoja kimoja ili kusikiliza nyimbo zao za kumuaga.

Alipofika pale katika kikundi cha bibi yangu alimsalimia bibi na kikundi chake chote kwa mkono, kisha akanisogelea na kuniuliza "mjukuu wangu wewe unaitwa nani?" Nikamjibu "naitwa M....", akaendelea "unasoma darasa la ngapi", nikamjibu ..., akauliza "umekuja na nani?" Nikamjibu "nimekuja na bibi yangu", bibi akaingilia kati na kumwambia "huyo ni mjukuu wangu", mzee Mwinyi akatabasamu akaingiza mkono mfukoni na kutoa kibunda cha pesa akanikabidhi nikakitia mfukoni.

Kulikuwa na jamaa pembeni (nahisi ni mlinzi au mpambe wake) akamwambia ampe tshirt 1 nyeupe iliyokuwa na picha yake akanikabidhi kama zawadi, kisha akanambia ๐Ÿ‘‰ "Mjukuu wangu dunia ya leo ni elimu, hivyo pamoja na kupenda kuongozana na bibi yako katika mambo haya ya kitamaduni, lakini hakikisha elimu ndio kinakuwa kipaumbele chako cha kila siku katika maisha yako". Nikaitikia kwa kichwa huku nikitabasamu ๐Ÿ˜Š na yeye akatabasamu ๐Ÿ˜Š

Kisha walinzi wake wakamwambia mzee muda wa ndege kuondoka unakaribia, akaendelea kuwaaga watu wengine mbali mbali waliokuwa pale uwanja wa ndege kumuaga, kisha akaingia ndani ya ndege huku akitupungia mkono.

Mzee Mwinyi alikuwa mtu mwenye moyo wa utu, wala hakuwahi kuwa na visasi na watu.
Aliwapenda watu na yeye alipendwa na watu. Taifa limepoteza mtu muhimu sana, ila ndo hivyo kazi ya Mungu haina makosa. Tulikuja kutoka udongoni, na tutarudia huko huko udongoni.


Bibi yangu yeye bado yupo hai ila ameshapoteza kumbukumbu, muda mwingine anamsahau mpaka mama yangu ambae ni mtoto wake mwenyewe wa kumzaa. Kidogo anamkumbuka mama yetu mdogo ambae ndio anaishi nae kwa sasa.

Pumzika kwa amani mzee Mwinyi, Mw/Mungu ailaze roho yako mahali pema peponi ameena.
celebrity worship syndrome
 
Basi fanya ukamzike Babu kipenzi cha watanzania.
Alikuachia ushauri wa kuisaka elimu kama dira yako. Je ulifanikiwa kufanyia kazi ushauri wa mzee?
Amekuachia alama kubwa.
Innalillahi waina ilaihi raajiun
 
Nimeskia kuna ile chama cha wafanyakazi walimkacha Mwinyi akiwa rais kwenye maadhimisho ya Mei Mosi wakamualika Nyerere ambae kwa wakati huo alikua mstaafu. Nyerere nae alipofika Mbeya akamkandia sana rais (Mwinyi) lakini mzee wa watu wala hakumind, hakua na kinyongo na mtu na maisha yakaendelea. Nikakumbuka hiki kitendo angefanyiwa JIWE[emoji26] hilo balaa sijui angeamulia nani. R.I.P Alhaj Mzee Mwinyi.
 
Wazee wa kuunga story za marehemu huwa wengi misibani hasa msiba wa tajir wanajikutaga wanamjua marehemu ili yapige menyu ya kutosha

Naona mzee wa kuunga na msiba wa tajiri umejiunga sio ...
Kwa vile comment yako haibadili ukweli wa kile nilichokiandika, basi acha nikupuuze kama ulivyopuuzwa na wengine.
 
Mikoba ya bibi!!

Ili uendeleze ngoma za asili ๐Ÿ˜€
Bibi aliacha na kuegemea zaidi kwenye maswala ya dini. Na huo ndio ukawa mwanzo wa kusambaratika kabisa kwa kundi hilo la ngoma zao za kitamaduni.

Ilikuwa wakienda kwenye show wanalipwa na bibi anamgawia kila mmoja sawa na mungine. Alivyojitoa hakupatikana mwenye uwezo wa kuongoza vizuri kama yeye. Wakawa wakienda kupiga sehem wakirudi wanadhulimiana. Hela za kutunzwa bibi alikuwa hata akitunzwa anawapa na wenzake, lkn hawa wengine mtu akitunza anaichimbia kwenye matiti na kuibana na sidiria.

Mwisho kikundi kikaanguka chali ๐Ÿ˜€๐Ÿ˜‚
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Nikiwa na umri mdogo nilihudhuria pale katika uwanja wa ndege wa kimataifa jijini Dar es salaam, kumuaga mzee wetu mzee Ally Hassan Mwinyi ambae alikuwa anaondoka kuelekea Zanzibar, baada ya utawala wake wa miaka 10 kuisha kikatiba.

Bibi yangu ambae alikuwa na umri sawa na marehemu mzee Mwinyi ila bibi alimzidi Mwinyi miezi miwili, alikuwa ni kiongozi wa kikundi fulan cha ngoma za kitamaduni zilizokuwa zinachaguliwa mara kwa mara kwenda kutumbuiza sehemu mbali mbali alizofika raisi Mwinyi enzi za utawala wake. Bibi yangu alikuwa na tatizo la ulemavu wa macho, hivyo mzee Mwinyi alitokea kumzoea na kumfahamu bibi yangu haraka sana (nahisi ni kutokana na ulemavu wake na pia kujituma hata pale alipokuwa mlemavu) mpaka kufikia kipindi mzee Mwinyi akawa anamwita bibi yangu "bi siti Mwinyi" kwa jina la utani.

Siku hiyo ya kumuaga mzee Mwinyi bibi na kikundi chake cha utamaduni walialikwa, hivyo wakati wakifanya maandalizi ya kujiandaa kwenda uwanja wa ndege mimi nikawa nang'ang'ania ili niende nao uwanja wa ndege kwa sababu usafiri ulikuwa wa bure tena basi la jeshi. Wakati huo nilikuwa bado kijana mdogo alafu ni mjukuu wa mwenye kikundi, hivyo hakuna aliepinga mimi kwenda hadi uwanja wa ndege kumuaga mzee Mwinyi.

Tulivyofika pale tukakuta vikundi vingine mbali mbali vya ngoma za kiutamaduni kutoka katika makabila na jamii mbali mbali, basi na sisi tukajumuika nao kumsubiri mgeni husika afike ili tumuage. Masaa mawili baada ya sisi kufika mzee Mwinyi alifika akiwa na familia yake akawa anapita katika kikundi kimoja kimoja ili kusikiliza nyimbo zao za kumuaga.

Alipofika pale katika kikundi cha bibi yangu alimsalimia bibi na kikundi chake chote kwa mkono, kisha akanisogelea na kuniuliza "mjukuu wangu wewe unaitwa nani?" Nikamjibu "naitwa M....", akaendelea "unasoma darasa la ngapi", nikamjibu ..., akauliza "umekuja na nani?" Nikamjibu "nimekuja na bibi yangu", bibi akaingilia kati na kumwambia "huyo ni mjukuu wangu", mzee Mwinyi akatabasamu akaingiza mkono mfukoni na kutoa kibunda cha pesa akanikabidhi nikakitia mfukoni.

Kulikuwa na jamaa pembeni (nahisi ni mlinzi au mpambe wake) akamwambia ampe tshirt 1 nyeupe iliyokuwa na picha yake akanikabidhi kama zawadi, kisha akanambia [emoji117] "Mjukuu wangu dunia ya leo ni elimu, hivyo pamoja na kupenda kuongozana na bibi yako katika mambo haya ya kitamaduni, lakini hakikisha elimu ndio kinakuwa kipaumbele chako cha kila siku katika maisha yako". Nikaitikia kwa kichwa huku nikitabasamu [emoji4] na yeye akatabasamu [emoji4]

Kisha walinzi wake wakamwambia mzee muda wa ndege kuondoka unakaribia, akaendelea kuwaaga watu wengine mbali mbali waliokuwa pale uwanja wa ndege kumuaga, kisha akaingia ndani ya ndege huku akitupungia mkono.

Mzee Mwinyi alikuwa mtu mwenye moyo wa utu, wala hakuwahi kuwa na visasi na watu.
Aliwapenda watu na yeye alipendwa na watu. Taifa limepoteza mtu muhimu sana, ila ndo hivyo kazi ya Mungu haina makosa. Tulikuja kutoka udongoni, na tutarudia huko huko udongoni.


Bibi yangu yeye bado yupo hai ila ameshapoteza kumbukumbu, muda mwingine anamsahau mpaka mama yangu ambae ni mtoto wake mwenyewe wa kumzaa. Kidogo anamkumbuka mama yetu mdogo ambae ndio anaishi nae kwa sasa.

Pumzika kwa amani mzee Mwinyi, Mw/Mungu ailaze roho yako mahali pema peponi ameena.
Hata mimi nina mambo mengi ambayo nimeshuhudia Mzee huyu akionesha utu na uungwana wake. Uliloandika latosha na nashukuru umefanya kwa niaba yetu sote. Mwenyezi Mungu Amrehemu Mzee Mwinyi! RIP Mzee Ruksa!
 
Hata mimi nina mambo mengi ambayo nimeshuhudia Mzee huyu akionesha utu na uungwana wake. Uliloandika latosha na nashukuru umefanya kwa niaba yetu sote. Mwenyezi Mungu Amrehemu Mzee Mwinyi! RIP Mzee Ruksa!
Nashukuru sana ndugu yangu ๐Ÿ™๐Ÿ™๐Ÿ™
Mwenyezi Mungu amuweke miongoni mwa waliokuwa wema na wachamungu hapa duniani.
 
Basi fanya ukamzike Babu kipenzi cha watanzania.
Alikuachia ushauri wa kuisaka elimu kama dira yako. Je ulifanikiwa kufanyia kazi ushauri wa mzee?
Amekuachia alama kubwa.
Innalillahi waina ilaihi raajiun
Bahati mbaya msiba imetokea nikiwa nje ya nchi, lkn nimeanza kumuomba tangu niliposikia taarifa za kuumwa kwake, nikaendelea kumuombea hata baada ya kusikia taarifa za kifo chake.

Ushauri wa elimu niliufanyia kazi, japo sikufika mbali kivile, but i tried to follow his legacy. RIP mzee wetu mwema na mchamungu Ally Hassan Mwinyi.
 
Nimeskia kuna ile chama cha wafanyakazi walimkacha Mwinyi akiwa rais kwenye maadhimisho ya Mei Mosi wakamualika Nyerere ambae kwa wakati huo alikua mstaafu. Nyerere nae alipofika Mbeya akamkandia sana rais (Mwinyi) lakini mzee wa watu wala hakumind, hakua na kinyongo na mtu na maisha yakaendelea. Nikakumbuka hiki kitendo angefanyiwa JIWE[emoji26] hilo balaa sijui angeamulia nani. R.I.P Alhaj Mzee Mwinyi.
Mwinyi alitengenezewa mazingira ya kuchukiwa, kudhihakiwa na kufedheheshwa na mzee "mchonga" ili kuyafuta mazuri yake yote aliyofanya kwa taifa hili, na kamwe isije kuonekana kuwa amefanya mambo makubwa kwa taifa.

Hao wafanyakazi walimwalika mzee Nyerere na kumkacha Mwinyi huku wakiwa wameshapokea mshahara, wameshiba na kuvaa vizuri. Walisahau kuwa kabla ya Mwinyi kuingia madarakani wengi wao walikuwa wanafanya kazi bila mshahara, wengine wanakwenda shuleni wakiwa wamevaa midabwada baada ya kukosa hela ya kununua nguo lkn pia hata hizo nguo zilikuwa hazipatikani sokoni, wengine walikuwa wanashindia mlo mmoja tena wa mihogo ya kuchemsha nk.

Sema ndo hivyo, wengi walitengenezewa yale mazingira na kujikuta wanasahau kule walipotokea na kukandia neema waliyoipata kwa sasa.
 
Back
Top Bottom