DOKEZO Michango imekuwa mingi Shule ya Msingi Njelela iliyopo Ludewa - Njombe, Mzazi ambaye hatatoa anakamatwa

DOKEZO Michango imekuwa mingi Shule ya Msingi Njelela iliyopo Ludewa - Njombe, Mzazi ambaye hatatoa anakamatwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Mliogwa

Member
Joined
Jun 6, 2024
Posts
37
Reaction score
37
IMG-20241112-WA0016.jpg
Wazazi wa Wanafunzi wa Shule ya Msingi Njelela iliyopo Kata ya Mundindi, Wilaya ya Ludewa, Mkoa wa Njombe wamekuwa wakilalamikia michango inayochangishwa shuleni hapo kuwa imekuwa ni kero kutokana na uongozi wa shule kutoa maelekezo kila mara.

Mfano, Wanafunzi shuleni hapo wanatakiwa kulipa Tsh. 15,000/-, Debe mbili za mahindi na lita moja ya mafuta kwa kila Mwanafunzi mmoja.

IMG-20241112-WA0011.jpg

Shule hiyo ya Serikali yenye Wanafunzi 400 (darasa la kwanza hadi la sita) ina Walimu sita wa kuajiriwa na Walimu wa tatu wa kujitolea ambapo wazazi ndiyo wanawalipa posho wale wa kujitolea Tsh. 100,000- kwa mwezi.

Mchanganuo wa michango hiyo ipo kama ifuatavyo: -
a) 5,000/- ya kukobolea Mahindi
b) 10,000/- inatumika kwenye matumizi mengine ikiwemo kulipia Walimu hao wanaojitolea.

Ikitokea Mzazi au Mlezi hajatoa mchango anamakatwa na Mgambo na kutupeleka kwa Ofisi ya Mtendaji, tunajiuliza mbona wanatukamata bila hata kutupa barua ya wito.

IMG-20241112-WA0007.jpg

Suala la michango ni hiyari lakini imekuwa kama Sheria na kama ni kuisaidia Serikali tumeshaisaidia sana, nadhani umefika muda na sisi tusaidiwe.

Tunapokamatwa tunalazimika kwenda kukopa kwa riba kubw aili Watoto wetu waweze kusoma.

Wazazi wanahoji matumizi ya fedha hizo ambazo wanasema hawajawahi kusomewa matumizi yake.

IMG-20241112-WA0006.jpg

Michango hiyo huitishwa na Walimu wenyewe, tunachohoji ni kuwa kwa nini Maafisa Elimu au Mkurugenzi wasiende shuleni hapo na kutangaza rasmi kuhusu michango hiyo na uhaba wa Walimu na kwamba wazazi wabebe jukumu la kujitolea kwa kutoa michango hiyo.

Aidha, walilalamika kuwa nguvu hutumika kwa Wazazi wanaochelewa kulipa kwa kukamatwa na migambo ya kijiji na kupelekwa kwa Mtendaji kujibu mashtaka.

Vilevile Wazazi wa kila kitongoji wana zamu ya kwenda kuwapikia Watoto wao shuleni kwa kujitolea.

Ukiacha kuwa wanatakiwa kulipa hiyo michango bado wanatakiwa kwenda zamu ya kuwapikia watoto na pia Wanafunzi ndiyo wenye jukumu la kukata kuni za shughuli hiyo.
WhatsApp Image 2024-11-26 at 13.07.35_27c8f0ea.jpg
 

Attachments

  • IMG-20241112-WA0014.jpg
    IMG-20241112-WA0014.jpg
    182 KB · Views: 5
  • IMG-20241112-WA0004.jpg
    IMG-20241112-WA0004.jpg
    123.4 KB · Views: 7
  • IMG-20241112-WA0008.jpg
    IMG-20241112-WA0008.jpg
    88.4 KB · Views: 7
  • IMG-20241112-WA0003.jpg
    IMG-20241112-WA0003.jpg
    167.8 KB · Views: 6
Mzee kama unasomesha mtoto shule ya kata unalalamika michango... Hapo nyumban sidhan kama familia yako ina kula chakula na kushiba...😂 Mwanaume unalalamika michango ya jero au buku
 
Michango imekuwa mingi Shule ya Msingi Njelela iliyopo Ludewa - Njombe, Mzazi ambaye hatatoa anakamatwa

View attachment 3172453
Wazazi wa Wanafunzi wa Shule ya Msingi Njelela iliyopo Kata ya Mundindi, Wilaya ya Ludewa, Mkoa wa Njombe wamekuwa wakilalamikia michango inayochangishwa shuleni hapo kuwa imekuwa ni kero kutokana na uongozi wa shule kutoa maelekezo kila mara.

Mfano, kuwa Wanafunzi shuleni hapo wanatakiwa kulipa Tsh. 15,000/-, Debe mbili za mahindi na lita moja ya mafuta kwa kila Mwanafunzi mmoja.

View attachment 3172454

Shule hiyo ya Serikali yenye Wanafunzi 400 (darasa la kwanza hadi la sita) ina Walimu sita wa kuajiriwa na Walimu wa tatu wa kujitolea ambapo wazazi ndiyo wanawalipa posho wale wa kujitolea Tsh. 100,000- kwa mwezi.

Mchanganuo wa michango hiyo ipo kama ifuatavyo: -
a) 5,000/- ya kukobolea Mahindi
b) 10,000/- inatumika kwenye matumizi mengine ikiwemo kulipia Walimu hao wanaojitolea.

Ikitokea Mzazi au Mlezi hajatoa mchango anamakatwa na Mgambo na kutupeleka kwa Ofisi ya Mtendaji, tunajiuliza mbona wanatukamata bila hata kutupa barua ya wito.

View attachment 3172457

Suala la michango ni hiyari lakini imekuwa kama Sheria na kama ni kuisadia Serikali tumeshaisaidia sana, nadhani umefika muda na sisi tusaidiwe.

Tunapokamatwa tunalazimika kwenda kukopa kwa riba kubw aili Watoto wetu waweze kusoma.

Wazazi wanahoji matumizi ya fedha hizo ambazo wanasema hawajawahi kusomewa matumizi yake.

View attachment 3172456

Michango hiyo huitishwa na Walimu wenyewe, tunachohoji ni kuwa kwa nini Maafisa Elimu au Mkurugenzi wasiende shuleni hapo na kutangaza rasmi kuhusu michango hiyo na uhaba wa Walimu na kwamba wazazi wabebe jukumu la kujitolea kwa kutoa michango hiyo.

Aidha, walilalamika kuwa nguvu hutumika kwa Wazazi wanaochelewa kulipa kwa kukamatwa na migambo ya kijiji na kupelekwa kwa Mtendaji kujibu mashtaka.

Vilevile Wazazi wa kila kitongoji wana zamu ya kwenda kuwapikia Watoto wao shuleni kwa kujitolea.

Ukiacha kuwa wanatakiwa kulipa hiyo michango bado wanatakiwa kwenda zamu ya kuwapikia watoto na pia Wanafunzi ndiyo wenye jukumu la kukata kuni za shughuli hiyo.
AISEEE HII CCM NDO ADUI NO1 WA ELIMU YA NCHI HII YAANI MADARASA YAPO HIVI NA BILA AIBU WATAWAOMBA KURA?
 
SASA kuchangia chakula cha Kula mwanao shuleni ndo ulalamike dunia nzima?

Moderator wafute Uzi huu haraka Sana.
Shida Iko hapo kuwalipa hao walimu wanao jitolea hiyo pesa ni kubwa sana ukichuka idadi ya wanafunzi 400 × 100,000=40,000,000/= Kwa mwezi na walimu wenyewe wako 3 sio sawa kabisa
 
Elimu ni gharama, changia mwanao apate lishe akiwa shule. Njaa ni janga kwa mwanafunzi, kukaa darasani bila kupata chochote ni kudhoofisha na kumdumaza mwanao.
 
Shida Iko hapo kuwalipa hao walimu wanao jitolea hiyo pesa ni kubwa sana ukichuka idadi ya wanafunzi 400 × 100,000=40,000,000/= Kwa mwezi na walimu wenyewe wako 3 sio sawa kabisa
Wewe ni mjinga Sana.

Unacholalamika ni kipi ?

Yaani kutoa hiyo michango isiyofika hata elfu 50 Kwa mwaka unaona tabu?

Unaona walimu wanafaidi?

Toa toto lako shule lifundushie nyumbani.
 
Shida Iko hapo kuwalipa hao walimu wanao jitolea hiyo pesa ni kubwa sana ukichuka idadi ya wanafunzi 400 × 100,000=40,000,000/= Kwa mwezi na walimu wenyewe wako 3 sio sawa kabisa
Kila mbuzi anakula kwa urefu wa kamba yake, kama kweli unawaonea huruma wazazi watafutie mfadhili... vinginevyo wewe pia unafitinisha uongozi wa shule dhidi ya wazazi.
 
Shida Iko hapo kuwalipa hao walimu wanao jitolea hiyo pesa ni kubwa sana ukichuka idadi ya wanafunzi 400 × 100,000=40,000,000/= Kwa mwezi na walimu wenyewe wako 3 sio sawa kabisa
Mchango ni 15,000 mara wanafunzi 400 = 6,000,000

Ndani ya hiyo 6M ndio wanalipa hao walimu wa kujitolea, 100,000 kila mmoja kwa mwezi.

Hata hivyo inafaa ripoti ya matumizi isomewe kwa wazazi.
 
Wewe ni mjinga Sana.

Unacholalamika ni kipi ?

Yaani kutoa hiyo michango isiyofika hata elfu 50 Kwa mwaka unaona tabu?

Unaona walimu wanafaidi?

Toa toto lako shule lifundushie nyumbani.
Punguza jazba basi au ndo stress zimekuzidi au una njaa ndugu, pole kama wewe ni mwalimu
 
Mchango ni 15,000 mara wanafunzi 400 = 6,000,000

Ndani ya hiyo 6M ndio wanalipa hao walimu wa kujitolea, 100,000 kila mmoja kwa mwezi.

Hata hivyo inafaa ripoti ya matumizi isomewe kwa wazazi.
Anha kumbe nilikuwa sijaelewa vizuri Asante Kwa ufafanuzi
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Waha na wabena ni watoto wa baba mmoja.

Wabishi Sana

Wafupi sana
 
Back
Top Bottom