Michango ya harusi imekua kero kwangu, mbona mimi sikuchangisha mtu ata senti moja

Michango ya harusi imekua kero kwangu, mbona mimi sikuchangisha mtu ata senti moja

Na siku hizi kuna wapuuzi wanaomba hadi michango ya graduation, vipaimara sijui na Birthday. Shenzi kabisa sijui sherehe zao huwa ni dharula au wanahisi ni kitu flani cha lazima mtu kutoa.

Mwingine hujawasiliana naye zaidi ya miaka 3 ukiona simu inaita unawaza hapa kama sio mchango sijuiunakuta kweli anaomba mchango anaoa. Wadau wanazingua sanaa.
 
Na siku hizi kuna wapuuzi wanaomba hadi michango ya graduation, vipaimara sijui na Birthday. Shenzi kabisa sijui sherehe zao huwa ni dharula au wanahisi ni kitu flani cha lazima mtu kutoa.

Mwingine hujawasiliana naye zaidi ya miaka 3 ukiona simu inaita unawaza hapa kama sio mchango sijuiunakuta kweli anaomba mchango anaoa. Wadau wanazingua sanaa.
Imagine mchango wa kipaimara, upuuzi tu bora tuonekane mabandidu
 
Juzi tu hapa kuna jirani kafanya shughuli ya kufungua saluni yake, kachangisha watu na walienda na wakamzawadia!

Siku hizi michango kama hii ni biashara tu. Kuna hadi vikundi vya kuchangishana na kupeana zawadi.

Tuigeni kwa wenzetu waliopiga hatua kimaendeleo. Ukiwa na shughuli yako alika watu kadhaa hakuna michango wala nini
 
Plan yangu ya kuoa nimepanga watakao hudhuria harusi yangu ni wazazi wangu na ndugu watatu, wazazi wa mwanamke na ndugu zake 10 hakuna kuomba michango, wala hakuna habari za mziki na kukodisha kumbi za sherehe ndoa inafungwa Asubuhi hadi saa 12 kila mtu anarudi kwake.
Ya kwangu nilifanya hivi mpaka leo amani ndugu wanabaki wakishangaa tu hawazubutu kunisumbua kuchanga
 
Wenzetu walishatoka huko ,nasi tutafika tu kwenye ndoa za mikataba na harusi pasipo michango.

Kiukweli kama unataka kuoa ni vyema wewe muoaji na muolewaji kujipanga ,unaandaa watu wa kuwaalika majirani,ndugu ,jamaa na marafiki tu ambao ukipiga list yote hawazidi hata 200.

Sasa bajeti ya kulisha watu 200 mpaka utembeze bakuli? Kujipanga kwa 6m mwaka mzima hutashindwa? Kama sherehe tu unachangisha watu vipi kurun familia ,ujenzi ,ada za watoto nazo utachangisha maana hizo ndiyo kubwa kuliko hata gharama za harusi.

Tuondoe mentality ya kwamba lazima harusi uchangiwe....Nakubaliana na Mwana FA alivyosema kwamba yeye achangii harusi ya mtu yeyote.
 
Habari za kuchakarika wakuu,

Aisee hapa navyoandika nimeungwa kwenye magroup matatu ya harusi zinazokuja mwisho wa mwaka huu, 1 ni binti ndugu wa ukoo sio immediate family link kwa mababu huko, mmoja ni jamaa nilitinga nae job kabla sijahamia nilipo, mwingine jamaa tumesoma wote high school.

Me nilioa harusi ya kiislam very simple hawakuzidi watu 200 hv vyakula ilikua chai ya maziwa, tende, sambusa, kabab, cookies, kuku za kukaanga na juice za azam embe vichupa vidogo na maji vichupa vidogo na watu wote walikula na kubeba , eneo nyumba ya ndugu yake wife (hatukutaka ukumbi), kwa kifupi nilitoa 2M tu kufanikisha shughuli + mapambo, usafiri.

Kusema ukweli ukiangalia vzuri sku hz watu wanatumia michango kutafuta mitaji or else mana haiwezekani eti unaweka kiwango cha chini labda 100,000/=

Unakuta mtu hamjaongea kitambo hakuna ukaribu unashangaa simu imeita unapewa taarifa! punde umeungwa kwenye group watu wametiririka ma plege.

Mwezi uliopita kuna jamaa mwngine aliniunga kwenye group pledge kiwango cha chini 200,000 nikamwambia me ntakusupport laki akasema poa ila nilibanwa nikatuma 50k nikamwambia ingne ntamalizia. Asee simu zkawa za usumbufu nikawa simpokelei hadi sku naona status kaoa nikampa hongera akanilia buyu blue tick tu. Nikaja kuonana nae town ananipa attitude nkasema safi ndo imeisha hiyo ila najuta ata kwann nlituma 50 yani unamaind kisa sina? Na muda huo najua kabisa washkaji wetu wengine kweny hiyo circle hawakutoa kabisa.

Wadau mnaonaje hv inakuaje u force michango hivyo kwa jambo linalokuhusu ww na huyo mwenzio kwann utuwajibishe watu kutoa ma ahadi ya kishingo upande imradi tu tusigombane wakati hali yenyewe mambo kizungumkuti songombingo mafrekeche ya kutosha.

Kama hujajipanga kuoa si kausha kwanza, watu tuna support ila imekua too much imekua ni shuruti sasa dah, usipotoa unaonekana mbinafsi na haufungamani na jamii.

Sijioni nikiendelea kua mtoa michango sijioni kabisa kwanza in real sense nakuchangia kwenda kukojozana kwenye hotel honeymoon uko... Shabaash,!!
Yote hii ni kutaka kuiga kunya kwa tembo kupasuka msamba.
Fanyeni mambo kwa uwezo wenu. Hata chupa ya soda tu kwa waalikwa wa karibu inatosha na utaanza maisha bila stress
 
Back
Top Bottom