Michano/Hiphop/Freestyle

Jengo linang'aa kama theluji/

Humo ukikaa jina halichuji/

Hakuna dagaa wala kunywa uji/

Ni chapaa na wanasema hawafuji/

Sio haramu/ japo wengine huingia kwa damu/ fahamu/ ni zamu kwa zamu/

Kalamu/ ya mwenye awamu/ ndio huamua hatamu/ tulie au tutabasamu/

Africa nabaki/ japo ndio kunasifika kukosa haki/

Wengine Ikulu wakifika kutoka hawataki/

Mpaka watakapo aibika, maandamano kutamalaki/

Ama itokee vita, Jeshi waingilie kati/

Chanzo ni ikulu/ thamani zaidi ya lulu/

Vikosi unaviamuru, na bado hulipi ushuru/

Unapangia wengine, bila kujua hali zao/

Wafanye kazi kama mashine, uchukue kilicho chao/

Fungu wamimine, kujua matumizi si kazi yao/

Na wakileta mengine, ni wachochezi hao/

Ila wapo pia, viongozi bora kwenye duru/

Mungu azidi kuwajalia, na husda awanusuru/
 
Ngumu kumeza, kama chupa ya Gongo/

Madogo wanaitweza, kwao ni sifongo/

Ngoma wanazoweza, ni binua mugongo/

Kata kwenye meza, na umba wako wa udongo/

Hizi vipi watasogea, maana haziwapi mood/

Kama wamesutwa umbea, wanajificha tukizama hood/

Kwenye vina tunaogelea, vipaji na juhudi/

Hip Hop inaendelea, kama 2pac karudi/
 
Mambo bado nuksi, nani sauti apaze/

Angani Mrusi, na moto wa Kamikaze/

Ukraine anga jeusi, Air defence hata ajaze/

Nato huu muda Mahususi, vipi wajibanze/

Wapige za utosi, au wakae kuyamaliza/

Vita siyo msosi, ya nini kushinikiza/

Inaumiza maboss, na masikini inawamaliza/

Na Kamanda aliyepewa vikosi, anazidi kuangamiza/
 
Bongo michosho na uozo, sipapendi kabisa
Kuishi nikuw bongozozo, sio kabisa
Watoto wanawaza utelezi, kupelekeana moto
Kichwan bongo ni mapenzi, kupelekeana moto
Mara ipi sexual fantasy, mara tunda kimasihara
Jana tupean nafasi, wataweka kodi mpka za nyara zetuu.
 
Bongo zozo/ Nchi ya Tozo/ Wabunge wa Muongozo/ bora liende/

Ukisapoti uozo/ utapewa pozo/ utavuta gozo/ asali na tende/

Utakunywa dumu la maziwa, popote utapeta/

Ila wagumu tunakaziwa, kama tyre la Trecta/

Maisha kama upatu, mwalimu ni wakati/

Je? unachagua kuramba viatu, ili upande chati/

Kama Steve na Mwijaku, uitukane Kaki/

Au utembee nyatu nyatu, kwa ajili ya uanaharakati/

Uhuru wa kusadikika, watu hawana shauku/

Ukweli umeadimika, kama mkojo wa kuku/
 
Kichwani nina mistari mingi kama zebra/
na bado haijulikani ni vipi nimeibeba/
nikichana ni unyama utadhani leba/

maukali tulianza muda mrefu/
Tangu
Skul viatu hatvai, mwendo wa pek pek/
na watu hawashangai cause maisha yao sio yetu/
kipindi watoto hawakai bila muv ya yesu/
halaf mis tz, wema sepetu/
 
Nikidrop street, waiteni wanajeshi sio polisi../

Nikishika maik, ni unyama kama bucha imevamiwa na fisi../

Naishi peace mpaka na masnitch, sina mapenzi ya kiki kama wema na idriss../
 
Nikidrop street, waiteni wanajeshi sio polisi../

Nikishika maik, ni unyama kama bucha imevamiwa na fisi../

Naishi peace mpaka na masnitch, sina mapenzi ya kiki kama wema na idriss../
Kijana umeanza kukwiva.
 
Nimejikuta tu nipo kwenye hii sayari, aliyenileta hakuwa na mpango wa kujua kama nipo tayari..../

Ila kanifunza mengi kanifunza kukwepa hatari, kanifunza jinsi maneno ya watu yanavyoeza kugeuka bikari.../

Now nimeijua dunia kwa namna tofauti, ukiwa fair chochote utachokitaka haikupi..../

Upo duniani kwa kusudi, so nenda sawa na muda maana ukikuacha haurudi.../
 
Mkwaju wa nani mzee
 
Champion Freestyle;

Oyaa mitaa nnayotoka, ukizipata ni Freemason/

Hadi madogo wanalikoka, kama tuko motoni/

Hatukushoboka, wake za watu kama hatuwaoni/

Maana kipa alitoka, kwa walioshikwa ugoni/

Nyumba msanii, nyumba mganga/

Na bado haisaidii, wachawi waliwanga/

Tumeyaishi matendo, ya umasikini wa kutupwa/

Tukatengwa na warembo, kama buti la kuchumpa/

Oyaa siku hizi tunachezea bupa/

Kama condom tunatumia na kutupa/
 
Siyo kwa ubaya Freestyle;

Wivu chuki na roho mbaya, huletwa na umasikini/

Zisake siyo kwa ubaya, ufukara siyo dini/

Kuliko kuonekana Yahaya, bora ukafie hata mgodini/

Maisha ndiyo haya haya, ni msemo wa watu wa chini/

Wakikupiga vita, iwe chachu ya kusaka chapaa/

Sio kwamba wanakuita, eti ukawaombe msamaha/

Sio muda wa kulalamika, pumbavu watakuongezea jeraha/

Usipojikaza kuwajibika, kesho watakudharau tena jamaa/

Maisha vitendo/ ufukara sio nembo/ ila usiige tembo/ kubeba magendo/

Na ukipata kitengo/ usisahau nyendo/ hawaishi warembo/ usinunue upendo/ ukasau malengo/

Kupanga ni kuchagua, hivyo sikulazimishi kama dalali/

Siku utakayojua umekuwa, ni utakapolalamika bei ya sukari/
 
Mwaka umeisha afu sina malengo, daily nipo town kutazama tu majengo.../

Wengine walitimkia south kupiga deal za magendo, zikarudi maiti zenye midomo iliyo jaa mapengo.../

Deal za town nyingi hazilipi, hata milo mitatu siku hizi hazikidhi.../

Michongo haijatulia na bado naiseti, 2023 nafikiria bora nianze tu kubeti.../

Kuna manzi namfukuzia humu nataka tudate, akiniletea vibomu vya hela bora tu ni masturbate.../
 
Habari zilizovuma leo jukwaani

Umepitwa na jukwaa la michezo, huko hakuna mapenzi na habari za chombezo..../

Si unajua soka letu tupo msimu wa usajili, tetesi kibao kila mmoja kawq mbashiri.../

Sasa acha nikupashe yale yaliyojiri, naanza na taarifa ya mapema iliyokuja alfajiri.../

Habari iliripotiwa na Shafii Dauda, niliipata wakati nikiwa vingunguti barakuda.../

Ikidai Azam na Feisal mambo yameenda guda, na sasa kuondoka Yanga rasmi ni swala tu la muda.../
 
Ndugu Mwandishi Unawadhimu, Bila Shaka Umetumwa/ Uyu mtoto wa Salumu, Kwenye 18 Ashafumwa/mill 3 tu Ataki Anywe Sumu/ Mbaka 24 Ndo Anatemwa/Eti Wanapanga Kutuhujumu, si Quba Ndo Tulisoma/ Zitabaki Kuwa fununu, Dg msamaha Ashatuomba/ Wanajangwani tukomae umumu, Na tripu ii πŸ† yote tunayakomba.πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Pita huku Freestyle;

Ulisema ambayo hayapo/

Ukagombanisha couple/

Mpaka kwenye Ibada napo/

Waumini wakapeana kichapo/

Mnafiki pita huku...

Ulinunua used ukasema ni new/

Kila mradi ulipiga cha juu/

Tukihoji unatututumia crew/

Unadanganya maisha ni nafuu/

Mwanasiasa pita huku...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…