Michano/Hiphop/Freestyle

Michano/Hiphop/Freestyle

yo yo yoh
yote nayopitia ni kwasababu sina noti
maadui wamekua wengi kuliko machizi boti

mi husubiri tajiri ale ndipo nikombe sahani
Fid alisema bila hela hupati rafiki maishani

na ghetto sina taa mwezi ndo hunipa nuru
najilinda nisilale njaa kwa uji wa sukari guru

wadeni wangu wameniziba mdomo ili nisiwadai
watesi wangu wameziba promo nionekane sifai
Ila haina noma! haina homa! sikia

nipeni nafasi niendelee kupaza kwenye microphone
mistari yangu ni ya kipekee Ka mtende jangwani
Hawataki u starehe, na usipate kushiba/

Kisa ni Wakipekee, kama samaki asie na mwiba/

Maisha yasikunyookee, kila pande wanaziba/

Ili wakae waongee, siku wakisikia umeiba/

Iwe cheko/ zisake hata wakuone mental/ usishike beto/ kabebe hata pareto/ heshima ni kesho/ na wewe ni special/

Zisake kama una marejesho/ ipo siku itakuwa mpeto/ watashikwa na mchecheto/ wakikuona kina Mobetto/ na kukusaka mpaka geto/

Acha leo Wakipekee, waonyeshe kukuchukia/

Ila wajue paka mzee, hawezi kupotea njia/
 
Hawataki u starehe, na usipate kushiba/

Kisa ni Wakipekee, kama samaki asie na mwiba/

Maisha yasikunyookee, kila pande wanaziba/

Ili wakae waongee, siku wakisikia umeiba/

Iwe cheko/ zisake hata wakuone mental/ usishike beto/ kabebe hata pareto/ heshima ni kesho/ na wewe ni special/

Zisake kama una marejesho/ ipo siku itakuwa mpeto/ watashikwa na mchecheto/ wakikuona kina Mobetto/ na kukusaka mpaka geto/

Acha leo Wakipekee, waonyeshe kukuchukia/

Ila wajue paka mzee, hawezi kupotea njia/
Hahaa nakubali hujawahi kosea kuchora mistari mkuu.
 
Leteni michano vijana, naokoteza mistari yenu na kwenda studio sasa albam haijatimia na humu hamuendelei tena
 
Yesu ni bebe alisema rose muhando, uchumi umebana siwezi mudu hela ya bando..../

Mwigulu ajiuzulu maana hana mipango, tumechoshwa na tozo zilizokuwa kama michango..../

Alisema wahitimu wa vyuo fanyeni mjiajili, ila pesa ya mtaji hatuwapi hivyo tumieni akili.../

Kama ni hivyo basi tufanye dili, sisi tukupe umachinga we utupe uwaziri.../

Sijui ni akili yake au ndo stimu za wida, yani tozo zetu zinaishia ku-fund timu ya singida.../

Nchi imeingia kwenye mikopo isio na tija, hii dhambi haisameheki hata mfanye sala ya hija.../
 
Vyanzo vyako vya Story ni zipi?

*************************************

Story za mastaa unazipatia wapi, au club ukiwa umekamatia bapa la nyagi?

Au insta kwa mange kimambi, aliyefichua upigaji wa hela za vishkwambi.../

Mi story nazipatia jeiefu, kuna nyingi za uongo kugundua inahitaji uzoefu.../

Ili story yako isomwe na wengi hakikisha haiwi ndefu, punguza uzungu mwingi huku kingereza wengi tulipata efu/

Utaboa raia kiasi cha kutisha, kama utaweka story ya demu mkali bila picha.../

Mpenda totozi jukwaa la MMU haliwezi kukuboa, story za machangu huku ndio zinapofanya poa.../

Warembo wakali wapo, kama unataka oa.../
Story za dronedrake zipo, mwanaume kataa ndoa.../
 
Mdomo kataa ukimya,serikali njaa kali kunena
Kando mwa bara zima,vita ya uchumi inaua sana
Poteza Amani ya moyo,jenga watu kwa fikra pana
Kataza tamaa mbaya,piga kazi konde waachine wana.
Naandika!!
 
Mabaya na mazuri, ndiyo sifa ya ubinadamu/

Na kuzama kwenye kaburi, ndio mwisho wa hatamu/

Alikuwa mashuhuri, na hata umtukane anatabasamu/

Ila ukimletea sana jeuri, fact utazikuta Instagram/

The Kokobanga, visu juu ya gadem visu/

Dah! Mungu amepanga, machozi kwenye tishu/

Ulituhusia tupige kazi, 5 star hayo mambo ni gharama/

Ukatupa hasira za wazi, ili tukazane kupambana/

Hukupenda uduanzi, anaekosea ulimchana/

Hata aogopewe na shazi, hukuhofia mlivaana/

Pumzika Gademitti, Mungu akupokee vyedi/

Waliokuandama na mtiti, ulishawaambia case closed/
 
Nishachoka kushindana na haya maisha,
Kama JoJo nahisi ladha imeisha,
Najaribu kujikaza lakini yanatisha,
Ni kama mtego bahati mbaya nishakamatika,
Nshazurula kuomba kazi kiatu kikaisha,
Nikajaribu biashara zikanifilisisha,
Nishajaribu michezo ya bahati sijabahatisha,
Umaskini kama ukimwi nishaathirika,

Afu ubaya ya wenzangu yanatamanisha,
Ukicheki ni vitoto vinawaka Insta,
Mixa body builders akina calisa,
Dada zetu na ma make up wametakatika.😍

Nishajaribu mpaka wizi nikakamatika,
Ilikuwa bahati wangezika au kusafirisha,
Nishatest mpaka drugs kujifarijisha,
Na zile steam za mjani zinapagawisha,😵‍💫

Nishatafuta mibaraka ya kila kanisa,
Mpaka padri amenikariri nipo kila misa,
Wale waganga wa Sangoma wa kutajirisha,
Wamekula pesa zangu wametajirika.😞

Naomba Mungu awe fair atuletee gharika,
Masikini Tumechoka tunahangaika,
Wanasiasa wakiomba kura wananikasirisha,
Me mwenyewe kula yangu haijafahamika,
Maisha ni kama muvi mi bado sijapata picha,
Sioni hata mwanga limetanda Giza,
Maisha yananipiga nimechakalika,
Sioni maana yake nayatamatisha,🤕
 
Dear God mi nakuomba uwe fair,
Uovu umetawala vipi mbona hujakemea?
Yalianza kama mchicha umeacha yanamea,
Masikini hatuna sehemu nyingine ya kusemea,
Mafisadi wauaji juu ya nchi wanatembea,
Na mashoga sikuizi kama condom wameenea,
Dada zetu wanauzwa sioni kama una care,
Kinachosakwa ni noti ile Pesa ya kuhemea,
Speaking of money mbona umeacha Pesa inatuonea?
Kwani Sisi Ni Nani mbona hatuipati au tumeikosea?
ilibidi Serikali wafanye mpango darasan tukaisomea,
Ng’ombe wa masikini hazai hata dokta mwaka akimtibia,
 
Nipeni heshima yangu Maua mpeni Roma

Kwa Bomu la Hiroshima mjapani hawezi pona

Ni vita ya kiuchumi magu afe Kwa Corona

Mama atawale nchi msoga wauze Dona

Mengi nimeona yanayokera kila Kona

Daily twafa Kwa Sonona TB malaria homa

Hospital hakuna dawa, watawa wanasonya

Jifanye kuunda ukawa upigike kama Ngoma

Alitenda miujiza bure, Yesu akaponya

Leo leta sadaka tule, mwamposa huoni Noma?

Sa Nani atutee nasikia waziri shoga

Mange anasapoti upinde watoto wasikose mboga

Waziri wa michezo sijui Nani kamroga

Naona analeta mchezo daily anavoyakoroga

Tuzo maigizo isidingo kweli Noma

Utasikia sikuhizi Ngosha haimbi hip-hop mbona
 
Hii ni forum ya jamii/uzi wa wasanii
Tupo live kama tv/toka enzi za tape na cd/
Rap cv/nina zaidi ya four degree/
rapper tena mc/versi zangu hazichuji kama big g/
Masihi,nabii wa hii kacha/tungo ni dizasta na flow ni rapcha/
Freestyle kitengo,wacha niki so sihitaji biki/
natakatisha marapa kama jiki/kila bars hiti....
 
Tupo na mvumbo/
Direct bars sio za mafumbo/
Mistari ina viungo /utasema tupo tanga/tunawapepeta kwa nyungo /rapers wachanga/word play master niite pele/nani atamfunga paka kengele/
Revolution is socialised ni digital era/Nishai yani mpaka ai inapiga akapera/
 
Harakati kama Zuzu nimefuzu kwenye hii kitu/

Situmii nguvu nang'ata fuvu kama mbwa mwitu/

Vina zaidi ya Ruvu ama Kikuvu sio Maji matitu/

Hivyo ni ukauzu ku battle na Isuzu kwenye kazi za misitu/

Haina mizungu wala ucheshi wa Mpoki/

Miba kama nungu nungu ukinigusa huchomoki/

Demu usiende kwa mzungu makalio yawe poa kama pot/

Unatakiwa kumshukuru Mungu ukikohoa chupi haidondoki/
 
Harakati kama Zuzu nimefuzu kwenye hii kitu/

Situmii nguvu nang'ata fuvu kama mbwa mwitu/

Vina zaidi ya Ruvu ama Kikuvu sio Maji matitu/

Hivyo ni ukauzu ku battle na Isuzu kwenye kazi za misitu/

Haina mizungu wala ucheshi wa Mpoki/

Miba kama nungu nungu ukinigusa huchomoki/

Demu usiende kwa mzungu makalio yawe poa kama pot/

Unatakiwa kumshukuru Mungu ukikohoa chupi haidondoki/
Oi oi
 
Hustlers leo lunch ni michano/
Pasi kali mpaka usiku saatano/
Ni kazi na dawa sio sindano/
Hip hop bila madawa tunaishi humo/
real life man sio hadithi za chitemo/
Dakika kumi za maangamizi/
shujaa nimefika tena sio mvamizi/
pumzi ndefu hata nikipiga mbizi/
haturap tutoke,tunarap for fun/
......
endelea
 
Kwanza nawapa salamu, nazingatia itifaki/
Nadhani Mvumbo mnamfahamu, kwenye mistari mimi ndiye chaki/
Naandika zaidi ya kalamu, mwana Hip hop kindaki ndaki/
Ma mc's wa Jamii Forums, karibuni nyuma msibaki/
Leo mitandaoni ukisema usome, habari zimejaa ukakasi/
Huku Kiba anasema UNIKOME, huku Idriss akaripoti Polisi/
Huku Kigwa kavunja ngome, Le M'bebez kapiga pasi/
Haya yasikufanye ulale ukorome, pambana watoto wasile nyasi.
Tafuta pesa ule bata, usiishie kula mishikaki ya bati/
Ukijiona supa staa jali fyucha ikibidi vaa saa kisha unyuti/
Jiheshimu wape heshima bodi usihaibishe suti/
Haujalelewa kwa maadili we ni kichaa hata ungekuwa kuruti/


Bebi kaingia mkalishe kwenye kochi huna mpe kiti/
Uku kwetu hakuna mikeka ni mwendo wa single beti/
Huna umeme nunua tochi sikuhizi kila kona imekuwa kibiti/


Kimbia kama kipanga usifanye unapiga kama shoti/
Wakikuvamia wape waende usibishane nao wavulie koti/
 
Wanaogopa ninapoingia, hizi level hawawezi/

Mistari yao inajirudia, kama damu ya hedhi/

Kidume nakanyagia, hata wakiweka utelezi/

Hivyo unaponisikia, usikae ki ndezi/

Huu ndio muda/ natawala mbuga/ Mungu anipe nini Macmuga/

Haina kuzuga/ wakuda/ nawavuruga/ mwenyewe nimewafuga/ leo chemba/wanapeana vilemba/ kama Unguja/

Kama vagi usijitusu, ukijaribu nakucharanga/

Hapa ni visu juu ya gadem visu, kama Kokobanga/
 
Hip hop na mathematics/ ni kama ujamaa na Carl Max.

Huu uzi una vichwa balaa🔥🔥🔥🔥
 
Mabaya na mazuri, ndiyo sifa ya ubinadamu/

Na kuzama kwenye kaburi, ndio mwisho wa hatamu/

Alikuwa mashuhuri, na hata umtukane anatabasamu/

Ila ukimletea sana jeuri, fact utazikuta Instagram/

The Kokobanga, visu juu ya gadem visu/

Dah! Mungu amepanga, machozi kwenye tishu/

Ulituhusia tupige kazi, 5 star hayo mambo ni gharama/

Ukatupa hasira za wazi, ili tukazane kupambana/

Hukupenda uduanzi, anaekosea ulimchana/

Hata aogopewe na shazi, hukuhofia mlivaana/

Pumzika Gademitti, Mungu akupokee vyedi/

Waliokuandama na mtiti, ulishawaambia case closed/
Kaburi halina mazoea, ameshalala tunapaswa kumuombea/

Alikua mshkaji, rafiki lakini mbabaishaji/

Anakula leo anasahau kesho, alijiona sana spesho/

Gademu five star, downtown mjanja ndani ya dar/

Story nyingi za degree tatu, mabaharia sio watu/

muongo yani beautiful liar, hakuna aliyemu-inspire/

Hakuona mbele kutwa misele, pesa kidogo nyingi kelele/

nachana tena kiunderground, nimeshika sana dollar na pound/

akili kubwaz bebez, hakai mbali na swekeni meen/

mfalme wa insta kapigana kila vita, jf, fb na twitta/

yameshapita namuombea, kile neno tushaongea/

tumuache mbele ya haki, mimi na wewe hatujui nani atabaki/

kifo ni lazima iwe. leo kesho tunapaswa kujipima/
bata kidogo, shika sana neno la uzima/

ardhi inameza haitosheki, zamu kwa zamu usijione keki/

stay positive be humble, never lose focus life is a jungle/

wazuri wabaya roho ni mlango, moyo kichaka na pango/
 
Back
Top Bottom