Michano/Hiphop/Freestyle

Michano/Hiphop/Freestyle

AChia jala 2

Majibu;

Unajisifu una gundu na bado unafanya ukora/ unanifuata macho mekundu ili kunipora/

Piga risasi usoni mwangu na sikuitii ving'ora/ nishayachoka maisha yangu hivyo kupumzika ni bora/

Unapagawa na hizi noti unadhani ninastarehe/

Huliwezi hili koti hata nikisema ulipokee/

Wewe una marafiki/ wanaokujali/ una amani moyoni/

Mimi wote masnitch/ kisa hizi mali, nawindwa mpaka ndotoni/

Kisa mkuu wa Idara/ hiki cheo nimetoa ndugu kafara/ mke sitakiwi kumlala/ shetani tushafunga ndoa ya mitaala/

Kariakoo nina biashara, Temeke Kino na Ilala, ukiona msafara/ wangu kwenye barabara/ unaweza ukajiona fala/

Ila hizi pesa kwangu ni chungu zaidi ya shubiri/ sisaidii walio wangu hata dawa wakisubiri/ alikufa baba yangu kwa kukosa tiba Muhimbili, masharti kwangu napaswa kuyakabili/

Ili niishi/ vipi unapata ushawishi/ unazitaka kwa ubishi/ na kukomaa kama Shishi?/ Ukichukua hazikubakishi/ hivyo tuliza dishi/

Haya ma Range na majumba/ yasifanye u change mwanayumba/ omba Mwenyezi akupe Vumba/ halali ule enzi na sio kubumba/

Nayatamani maisha yako/ unayatamani yangu kisa vitita/

Sio kila aliye mbele yako/ anafurahi kukupita/
Uandishi mzuri, uchawi huwa ni flow
Nikipata time ntakuja utachagua topic then we can do a battle mistari iwe migumu meusi
 
Kichwa kipo deep Kama pango/
My Life is fun liKe rango, but still nna mipango/
Naamini sir God atanifungulia milango/
Japo masnitch wanawish nishuke viwango/
Nile makombo, nikose pesa ya pango/
Ila bado sikai kinyonge mchizi na struggle, Nazidi saka tonge ado ado/
 
Nimeona leo humu mtu ameweka post anasema mdororo na anguko la hiphop Tz. It's not true hip-hop ni life
Mwenye muda tupange siku twende kwa battle
 
Nimeona leo humu mtu ameweka post anasema mdororo na anguko la hiphop Tz. It's not true hip-hop ni life
Mwenye muda tupange siku twende kwa battle
Mzee unataka battle, Utaiweza hii mikato
Hizi si verse za kitoto, wala haziitaji minatoo.
Nikiwa kulia kaa kushoto, Hiphop kiti cha moto.

Tuendelee..🤣
 
Wake up skiza hizi fasihi, stanza za digrii mtaani nabii/

Kutoka chugga chalii, mwenye upendo utii na bidii/

Kipenzi wa mama, mamama jua limezama/

Muda hausimami ulishavuka ujana, yote umemalizana/

Busara ka za jo na anna, saint asiye na laana/

Move on tafuta na bwana, nishamove on nakula ujana/

Naijua leo sikumbuki jana, nkiwaza kesho sioni maana/

Zaidi michezo ya kut*ana, kichwa changu kigumu/

Kama pusha marijuana, sijawahi kuacha ndumu/

Cha mapinduzi kidumu, chama nilijua utakwama/

Penzi limekua sumu, mipasho skendo na drama/

Naspit ukweli humu, humu kugumu/

Kama dent mwenye room, aliyekosa boom/

Hana uhakika wa milo, max ana uhakika wa zero/

Kimajukumu nipo active, mood inafanya niwe selective/

Selective na story za uongo, nani kampenda nani/

Wakikutana hawaendani, usiamuamini mbongo/

Vita zishapigana kumjua muongo, Hakuna aliyeshinda/

Mtaani wanauza mirinda, humu wanaiponda coca/

Nimeshachoka naropoka, walio unique wapeni maua/

Mnawajua wavimbe bichwa, komwe litawaumbua/

Askari kijana smart niliyepitia depo, nipo kama sipo/

Nipo poa cool and good, Arusha is my hood/

Usiniulize kuhusu dar-lini, niulize nitamiliki car-lini/

Learn the difference, mtoto wa mjini swagga za kijanja/

Mjanja najua mshamba, hachekwi akiomba namba/

Flow classic and intelligent, kichwani nna vyombo/

Konyagi sio sahani na mabakuli, k vant mlevi nguli/

Nalewa napiga na puli, sijaona yoyote mzuri/

Mzuri kama miss, eyes haziwezi niongopea/

Internet never forget misy, jf pm mipicha ya kushea/

Tunza hiyo kitu mamy, K Ina thamani haina spea/

Mitandao imejaa umbea, fundi wa kupandisha stimu/

Mtundu kungwi na tena mwalimu, hanna tu posho/

Fundi midondoko 40bars michosho, fundi sishikiki/

Fundi sio wa pikipiki, mapikipiki yamaha au mahonda/

Najua kupenda najua kusifia, najua na kuponda/

Nipo real sio fake, P funk majani kwenye mdundo/

ashasadiki hiki kipaji mantiki mpangilio na muundoo
 
Mzee unataka battle, Utaiweza hii mikato
Hizi si verse za kitoto, wala haziitaji minatoo.
Nikiwa kulia kaa kushoto, Hiphop kiti cha moto.

Tuendelee..🤣
Sitaki bato, nataka unipe mnato
Panda kwa kitanda, minyege ishapanda
Kiunoni hiyo mishanga, utanikom huo msambwanda
Zima taa juu ya d*du kaa, sipendi mwanga
 
Punchlines ndo nini haswa mkuu nipe na mifano kwa verse maarufu za wasanii ili nielewe vzur.
Mifano ni kama hii...

ukiwa na nyundo mkononi, ni rahisi kupigilia msumari
Fid Q

Mi ni jua la utosini sizuiliki Kwa miwani
Stamina

Siui mende Kwa nyundo maana nitaumia Mimi
Professor Jay

Kwenye mtihani wa Maisha uwe na max za kuvutia
One

Bora kurogwa kuliko kukosa Uhuru
Langa ( huu mstari niliuelewa nilipolala sentro)

Nimeapishwa Kwa damu iliyomwagika Soweto, ndo maana unaponisikia nanukia harufu ya ghetto
Nikki wa pili
 
Back
Top Bottom