Michano/Hiphop/Freestyle

Michano/Hiphop/Freestyle

Upendo umefika mwisho, wapendanao wanajinyonga/

Wengine ni vitisho, kama mikwara ya Mandonga/

Hakuna upatanisho, kila mmoja anachonga/

Kifo ndio hitimisho, hata kama alikukonga/

Unaempenda hakupendi kama uteja wa unga/

Usiye mpenda haendi kama kamba umemfunga/

Dharau haijengi siyo tofari la nyumba/

Mapenzi yana mengi bwana mdogo chunga/

Mnunulie simu wenzako wampe vocha/

Jifanye mwalimu ajifanye kocha/

Mpe za kujikimu akakufanye ndondocha/

Yanakata stimu mapenzi ulofa/

Hiyo bastola unayonunua, haitaua kabisa vibaka/

Bali mwenyewe utajiua, utakapokuta mkeo wamempakata/

Wachache wana mapenzi ila tenzi kuwapata/ hauwezi bila Mwenyezi utadata/ kindezi kisa penzi atakukamata/

Kwa mwenye Benz atakuacha/ hauna malezi linavuja pakacha/ hata uwe mbezi na pesa ya kutakata/ bado utafanyiwa ushenzi kwa muuza kashata/

Ule muda unasaka mahitaji, ili Family njaa isijelala/

Wife yupo kifuani kwa mshikaji, huku akikuita fala/

Mapenzi hayana Falsafa, hata uwe umesoma sana/

Mapenzi yanaleta maafa, sio Tarime mpaka Tanga wanauwana/
[emoji419]
 
Humu tunadumu wagumu kwenye bato../
Usifuate mkumbo kama mateka wa freemason../
muulize Mvumbo navyo'ogopeka kama nato../

Wajinga wanavimba kwa mistari ya chabo../
Wakiotea wanaringa, utaskia mi ndo rapgod../
 
Haunipi raha, nikitizama zambi zako/
Iweje unaishi dar na hupajui cambiaso/
usihukukumu kama huijui kesho yako/

Natema bars kwakujiamini coz am dangerous/
Huwezi kuwa kama mimi labda uwe mimimars/
Vichwa panzi nawashusha chini kama chupi ya manzi/
na kabla hawajifika chini nawachana bila ganzi/
 
Usilete busara kwenye vita../
Ukitaka utajiri wa kimasihara, jitoe kafara 666../

Kila idara napewa sifa, kama simba wa mbagara anavyoshine insta../
Na bado sitaki ustar, wala machawa kabsa../

Nachohitaji ni kufika far, nakuona hip-pop inapaa kimataifa../

Sina info za michapo kama mange../
Ila nina bonge la nako so wenye punch-laini wajipange../

Namwaga madini, underground muyapande/
 
Usilete busara kwenye vita../
Ukitaka utajiri wa kimasihara, jitoe kafara 666../

Kila idara napewa sifa, kama simba wa mbagara anavyoshine insta../
Na bado sitaki ustar, wala machawa kabsa../

Nachohitaji ni kufika far, nakuona hip-pop inapaa kimataifa../

Sina info za michapo kama mange../
Ila nina bonge la nako so wenye punch-laini wajipange../

Namwaga madini, underground muyapande/
Unavo chana madogo wanakimbia/

Punch nzito mdundo heavy zaid ya magunia,
ya mpunga, ama pumba natania/

Kwa hizi flow mapunga, waoga wanakimbia/

Hawakai humu kwa hiz ngumu tunazotema/

Huu mdundo wa kigumu bila ndumu hautosema/

Nitawazika wote RIP walale pema/

Kwa hizi flow kali mpaka bubu atasema/
 
Penye amani upendo unatanda..|
Tangu zamani hawagusi hizi anga..|
Veteran kwenye huu mziki usiobamba..|
Underground nae-shine gizani kama shetani au mwanga..|
Nalinda culture utasema bowseman wakanda..|

Masera Vichwa maji na mimi haziivi/
Ni sawa na kum-compare De Opera na prof shivji/
Kunidisi sio rahisi kama kukata div/
We endelea kutema shit utadhani chizi..|
Ila jua huniwezi ata uvae hirizi..|

Huwezi badili mwendo hata uvae buti..|
Unajiona tembo wakati unapigo za pusy pusy..|
Kiufupi na kuona mrembo yaan byuti byuti..| (na)
ukitaka skendo nakugeuza amberuty..|
 
Penye amani upendo unatanda..|
Tangu zamani hawagusi hizi anga..|
Veteran kwenye huu mziki usiobamba..|
Underground nae-shine gizani kama shetani au mwanga..|
Nalinda culture utasema bowseman wakanda..|

Masera Vichwa maji na mimi haziivi/
Ni sawa na kum-compare De Opera na prof shivji/
Kunidisi sio rahisi kama kukata div/
We endelea kutema shit utadhani chizi..|
Ila jua huniwezi ata uvae hirizi..|

Huwezi badili mwendo hata uvae buti..|
Unajiona tembo wakati unapigo za pusy pusy..|
Kiufupi na kuona mrembo yaan byuti byuti..| (na)
ukitaka skendo nakugeuza amberuty..|
Umeni-poke nikakubali nimejileta,
ku-check tungo yaani zote ni utata,
umeshuka kiustadi na matata,
napiga mbinja kiukweli umenipata.

Wasanii hawana budi kukufata,
maujuzi mistari unavoikata,
nasema waje tu haraka wasije nyata,
wasichelewe iskariot tamkuta.

😀😀😀
 
Umeni-poke nikakubali nimejileta,
ku-check tungo yaani zote ni utata,
umeshuka kiustadi na matata,
napiga mbinja kiukweli umenipata.

Wasanii hawana budi kukufata,
maujuzi mistari unavoikata,
nasema waje tu haraka wasije nyata,
wasichelewe iskariot tamkuta.
Anytime niko tayari kutema mistari/
navyowachana utasema mpo hospitali kufanya surgery/
Natem punch-lain ila ni heavy zaidi ya jabari/
Amini Usipoelewa haya madini we ni ndezi kama mjomba nchomar/
 
Anytime niko tayari kutema mistari/
navyowachana utasema mpo hospitali kufanya surgery/
Natem punch-lain ila ni heavy zaidi ya jabari/
Amini Usipoelewa haya madini we ni ndezi kama mjomba nchomar/
😅😅 You killin! 🙌🏾
 
Humu tunadumu wagumu kwenye bato../
Usifuate mkumbo kama mateka wa freemason../
muulize Mvumbo navyo'ogopeka kama nato../

Wajinga wanavimba kwa mistari ya chabo../
Wakiotea wanaringa, utaskia mi ndo rapgod../
Hii nimechelewa kuiona, kama kobe kwenye Mfungo/

Ni kweli mitaa inapona, inaposikia zako tungo/

Ni wengi wamekula kona, maana tunawapiga mtungo/

Hatuchani tunashona, kama wasusi wa ungo/

Hii sio tatu chafu/ hii ni mbombo ngafu/ watapasua mapafu/ ni ngangari zaidi ya Cuf/

Hapa Mvumbo hapa Yuda/ ni vifungo kwa waluga/ tungo kila muda/ pungo kwa wajuba/

Hip Hop iendelee, una Rhymes andika huku/

Ili Vipaji visipotee, kama mkojo wa kuku/
 
Yatapita Remix

Verse

Shida hazikimbiwi, mwenzako pesa ninazisaka/

Kesho yetu haitafsiriwi, kwa hizi nguo za viraka/

Viatu watapaka Kiwi, na kujifanya wanakutaka/

Ila nyuki hakumbatiwi, usijaribu watakung'ata/

Mbele ni ukungu, tulipo pana moto/

Ila na sisi tuna Mungu, na sisi tuna ndoto/

Mateso na kushuka hadhi/ mbeleko sina kazi/

Leso kama una kibanzi/ kesho bado haijafanya kazi/

Tunaisubiri kwa matumaini/ ila hatujui tutapata lini/

Tumebadili mpaka dini/ na bado tupo chini/

Chini ya bajeti ya Mtanza, wenzetu wapo fiti/

Insta ni ya kina Boma Liwanza, Kokobanga Gademiti/

Unasema nasema yatapita, mbona hayapiti/

Bado tunahangaika, na hatuna ridhiki/

Mama maisha ni vita, najua vingi unamiss/

Rabda ni fungu la sita, la saba tutakuwa sisi/

Ipo siku tutafaidi, mpenzi wangu vumilia/

Giza linapozidi, jua asubuhi inakaribia/
 
Natokea mitaa ya maskini..|
kujitegemea sio mpaka ufike miaka ishirini..|.
Ulicho nacho kithamini, kabla ya wanaokitolea macho hawajakufitini..|.

Ukifika kwetu kuwa makini..|.
Mademu wanauza nyeti wakati vyeti wameficha kabatini...|

Kwetu hatuli baga zetu chukuchuku..|
Kwetu usiulize mambo ya ibada wala utukufu..|
Watu wapo busy na udaku wa watu maarufu..|

Mademu wanatembea utupu bila hofu..|
Aliesema hakuna jipya, nadhani alikuwa kipofu..|
 
Kwenye haso sina utani, navuja jasho ili nivute money..|

Sina demu kwani mapenzi kitu gani..|
Mashemu wananitega kishenzi ili niwape korodani/
wanakuta mnyamwezi sina hisia kama natumia mjani..|

Naishi kwenye kizazi cha walafi na majizi..|
Naishi kipweke utadhani mkimbizi, sina mtetezi yoyote kama mwizi..|
Sina chochote kiufupi sijiwezi..|

Nshajaribu kwenda kwa waganga..|
na bado sikuona mwanga zaidi ya visanga..|

Nkaishia kutangatanga kwenye nyumba za kupanga..|
Sina mshauri , Kila nachopanga kinageuka sifuri ni majanga..|
Napiga puri toka skul, maana sina mchumba wala danga..|
 
Niko live! Simba washapigwa kimoko na Holoya/

Makavu live! Inonga anazungushwa tu kama boya/

They won't survive! Chama mpira kizembe anapokonywa/

Lile bichwa la kudaiv! Ndio sababu makolo midomo omeshonwa..

Sent from my M2006C3MG using JamiiForums mobile app
 
mvumbo fumbo la rap nalifumbua kikatili/
ya gundu nshatua kwa map kukuumbua nyoko mbili/
we ni mtoto kwa rap umepotea chocho hili/
nshazipata za chap unaugua bawasiri/

eti utabaki juu labda kwene mashine mzungu/
jichanganye useme suu nikupasue map*mbu/
usibaki upande huu ukiskia ya gundu/
nilipanga kukuzika ila nmemwachia Mungu/
Maji ya gundu maji mfu, ni maji ya maiti/

Haufai kurusha turufu, ushazikwa saiti/

Vipi kinyago wa sufu, anitishe Mwenye kiti/

Hata uumbwe maradufu, huuwezi huu mziki/

Una vya kitoto vina, Mvumbo natupa kule/

Niamkie kwa heshima, kama nakupa hela ya shule/
 
Wanajiita Visit vibonde..|
Waana kocha la misifa gadiola kibonge|
Logo inatisha ila mpira wa kinyonge..|
Jana wametandikwa kimoko cha ng'ombe..|
 
Maji ya gundu maji mfu, ni maji ya maiti/

Haufai kurusha turufu, ushazikwa saiti/

Vipi kinyago wa sufu, anitishe Mwenye kiti/

Hata uumbwe maradufu, huuwezi huu mziki/

Una vya kitoto vina, Mvumbo natupa kule/

Niamkie kwa heshima, kama nakupa hela ya shule/
salamu sio heshima ata mashoga hufanya/
nimerudi tena kwa vina bwana mdogo kukukanya/
mi ndo title la hii rap huna kipya cha kufanya/
unajitia ununda ila kwa ndani unahanya/

mwenye kiti mwenye siti chukua kiti kalia/
mwenye beat leta kati huyu mtoto atalia/
mwenye kiti mwenye dhiki ukiweza kimbia/
sina kick kwene hiki niko fiti ukiniona potea/
 
salamu sio heshima ata mashoga hufanya/
nimerudi tena kwa vina bwana mdogo kukukanya/
mi ndo title la hii rap huna kipya cha kufanya/
unajitia ununda ila kwa ndani unahanya/

mwenye kiti mwenye siti chukua kiti kalia/
mwenye beat leta kati huyu mtoto atalia/
mwenye kiti mwenye dhiki ukiweza kimbia/
sina kick kwene hiki niko fiti ukiniona potea/
Kila story ushoga/ nidhamu ya uoga/ au unatangaza soko/

Tujue unatoga/ mtoto ni mboga/ ile Kiarabu koko/

Acha soga/ umeshaniroga/ nikupige kimoko/

Si utaoga/ na ukishanipa boga/ sitafanya unoko/

Umeweka maji wazi tunanawa bila ganzi mtoto wali nazi nakupanda kama ngazi/

Usitangaze ubazazi naonekana ustadhi utanishusha hadhi wakijua wazi nimekupakua mbaazi/

Imeshakuwa ndefu meku nipe mambo yetu peku kama Mpoto/

Nakudeku unavyo 'repu' mwanakwetu unataka moto/

Game imekupuuza, stanza sio kuvaa wigi/

Ni wazi unajichuuza, kujaribu hii ligi/

Wanasema Mvumbo punguza, konokono hawezi hii speed/

Sasa badala ya kujifunza, unaleta mdomo kama Gigy/
 
Back
Top Bottom