Sasa Mzee wa kazi wewe unashauri nini kifanyike ili sisi wabongo tuwe wakweli
Ukweli unakuja na maendeleoya kiuchumi na kiteknolojia tu.
Kuna story moja ya kitambo, wachezaji wa timu ya mpira ya Tanzania walienda Misri kwenye mechi, kwenda Misri, wakawa wanafanya shopping, wakashangaa dukakubwa halafu halina mtu kuwaangalia, wakatakakuiba, wengine wakakatazana.
Walivypotokahapo wakaambiwa bora hamjaiba, mngeiba mgelitia taifa aibu sana, kwa sababu duka zima limejaa camera, unaweza kuona hakuna mtu anayekuangalia, kumbe kuna camera kila sehemu na watu wamekaa vyumbani huko wanawaangalia tu.
Katika mfumo ambao teknolojiaimeendelea, watu hawana budi kusemaukweli tu.
Utabisha kwamba hukupita barabarani kukatiza red light? Unapewa video evidence inaonesha kila kitu.
Kitu kingine, ni kila mwananchi kupenda ukweli.
Juzi kuna Jaji alikuwa confirmed hapa US, Justice Kavanaugh.Nilishangaa sana washikaji wake wa chuo walimchoma kwamba huyu jamaa anadanganya, alikuwa mlevi mbwa tu chuo hata hawezi kuwa anakumbuka mambo kama anavyosema.
Kibongobongo mshkaji wakowachuo anataka kuwa jaji wa mahakama kuu, lazima ujipoendekeze umpambe.
Hata marais wastaafu wanashindwa kumkemea rais wa sasa, rais pekee aliyeweza kumkemea rais aliyemfuatia alikuwa Nyerere.
Sisi utamaduni wetu umejengwa katika misingi ya unafiki. Hata kupanda cheo mtu anapanda si kwa sababu ya uwezo, bali kwa unafiki na kujua kuwaramba nyayo mabosi.
Katika mfumo kama huo, kuwa msema kweli nikujihatarisha.
Ndiyo maana unaona watu waongo waongo, na viongozi hawaandiki vitabu vya maisha yao, wanaogopa wataandika uongo mwingi.
By the way, nilisikia Kikwete anaandika kitabu cha maisha yake hapo NYU, sijui kimeishia wapi.
Nataka nisikie atadanganya vipi ma scandal yote yaliyotokea utawala wake.