Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Nyota kutemwa Taifa Stars?
Wednesday, 29 December 2010 20:34

kayuni-tff.jpg
Sweetbert Lukonge na Clara Alphonce

WAKATI Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) likikutana leo na uongozi wa klabu za Simba na Yanga kujadili maombi yao kuhusu wachezaji wao waliomo Taifa Stars, mazoezi ya kikosi hicho yamemtia moyo kocha wake, Sylvestre Mash.

Marsh ambaye alikuwa akiongoza mazoezi hayo alisema kuwa anaridhishwa na kiwango kinachonyeshwa na wachezaji wake wakati wa mazoezi na kuongeza kuwa hiyo ni changamoto kwake kuhakikisha wanakuwa fiti zaidi kabla ya kwenda Misri.

Stars ipo kambini ikijiandaa na michuano mipya ya Bonde la Nile inayoshirikisha nchi za Ukanda wa Ziwa Victoria inayotarajia kuanza Januari 5 jijini Cairo.

Akizungumza na Mwananchi jana, Marsh alisema kuwa wachezaji wote wapo katika hali nzuri na wanendelea na mazoezi kwa nguvu jambo ambalo linampa matumaini makubwa ya kufanya vizuri katika mashindano hayo yaliyoandaliwa na Chama cha Soka nchini humo (EFA) kwa kushirikiana na serikali ya nchi hiyo ili kudumisha udugu kwa mataifa yote yanayotoka katika ukanda huo.

"Tunaendelea vizuri na maandalizi yetu kama kawaida, vijana wapo katika hali nzuri ya kiushindani na wanajituma zidi katika mazoezi jambo ambalo ni jema na linalonipa matumaini ya kufanya vizuri katika mashindano hayo," alisema Marsh.

Naye mchezaji wa Kagera Sugar ambaye pia ameitwa katika kikosi hicho kwa mara ya kwanza, Godfrey Taita amesema kuwa amevutiwa na hali ya ushindani iliyomo kikosini na kuongeza kuwa atahakikisha anapigana kwa nguvu zake zote ili aweze kupata namba .

"Namshukuru Mungu kwanza kwa kuniwezesha nami kuwa miongoni mwa wachezaji walioitwa katika kikosi hiki, hali hiyo imeniongezea hamasa zaidi ya kuhakikisha napigana kwa nguvu zote ili niweze kupata namba ya kudumu katika kikosi hicho licha ya kuwepo kwa ushindani mkubwa ambapo inabidi kupigana kiume ili kupata nafasi hiyo.

Wakati huohuo, hatima ya wachezaji wa Simba na Yanga katika kikosi hicho itajulikana leo baada ya kujadili kwa barua za klabu hizo mbili.

Klabu hizo ziliomba juzi TFF iwaachie wachezaji wao waliomo kwenye kikosi hicho.

Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Sunday Kayuni alisema jana kuwa wamepokea barua hizo juzi na tayari walikuwa wamezijibu klabu hizo jana kuwa leo watakuwa na kikao na kujadili suala hilo.

Alisema kwa sasa hawezi kuzungumzia lolote kabla hajakutana na klabu hizo,lakini wakikutana basi wataweka wazi kama watakuwa wamewaruhusu au waendelee kubaki Stars au la.

Klabu hizo ambazo zinakabiliwa na michuano ya Afrika ziliomba TFF iwaachie wachezaji wao ili waweze kujiandaa vyema kwa michuano hiyo ya kimataifa kwani mashindano hayo yana umuhimu zaidi kuliko yale ya kirafiki ambayo Stars inatakiwa kushiriki kule Misri

Stars inatarajiwa kuondoka nchini Januari 3 kwenda Misri kwa ajili ya mashindano hayo ambayo yatashirikisha nchi tano ambazo ni, Misri, Kenya, Uganda, Tanzania na Sudan. Mchezo wa ufunguzi utakuwa baina ya Misri watacheza dhidi ya Taifa Stars.

 
Waamuzi saba kuchezesha pambano la Cheka Monday, 27 December 2010 09:30

Imani Makongoro
WAAMUZI saba kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania wanatarajiwa kuchezesha pambano la kitaifa kati ya bondia Francis Cheka na Mada Maugo litakalofanyika Jumamosi kwenye Ukumbi wa PTA, Sabasaba jijini Dar es Salaam.

Pambano hilo la uzani wa kati kg 72, lililopangwa kuwa la raundi nane litasimamiwa na Oganizesheni ya ngumi za kulipwa Tanzania (TPBO), chini ya rais wake Yassin 'Ustadhi' Abdallah.

Waamuzi hao ni Steven Yuza kutoka Iringa, Mfaume Idanal wa Tanga, Kondo Nassor, Abdallah Mtemba, Omari Yazidu, Ibrahim Kamwe na Bakari Ally 'Champion, wote wa Dar es Salaam.

Waamuzi hao watapatiwa semina ya siku mbili iliyoandaliwa na TPBO itakayoanza leo kwenye Gym ya Japhet Kaseba, Mwananyamala jijini Dar es Salaam kuhusu kufuata kanuni na taratibu za mchezo wa ngumi za kulipwa Duniani .

Afisa Habari wa TPBO, Champion, aliiambia Mwananchi jana kuwa semina hiyo ya siku mbili itatoa fursa kwa waamuzi hao kujifunza kanuni na taratibu za mchezo wa ngumi za kulipwa ili siku ya pambano hilo kusiwe na malalamiko ya kuchakachua matokeo.

"Atakayeshinda siku hiyo ameshinda kihalali na atakayepigwa atapigwa kihalali, kwani kanuni na taratibu za mchezo huo zitafuatwa na waamuzi hao wataingia ulingoni kutoa maamuzi wakiwa wameiva na wako kamili bila upendeleo,"alisema Champion.

Mabondia hao watapima uzito Alhamisi katika ukumbi wa PTA, tayari kwa pambano hilo kubwa nchini.

 
Dewji kurejesha udhamini wake Simba Wednesday, 29 December 2010 20:32

Vicky Kimaro

BAADA ya muda mrefu, klabu ya Simba inatarajia kurejea tena katika medani ya soka ikijiendesha kwa udhamini wa mamilioni kutoka Kampuni ya Mohamed Enterpress ya jijini Dar es Salaam.

Tayari mmiliki wa kampuni hiyo, Mohammed Dewji ameonyesha nia ya kurejesha udhamini klabu wake kwenye klabu hiyo ya Mtaa wa Msimbazi.

Habari za uhakika ambazo Mwananchi imezipata zinasema kuwa Dewji ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mjini kupitia CCM yupo kwenye hatua za mwisho za mazungumzo na uongozi wa Simba kwa lengo la kurudi tena kwenye klabu hiyo inayokabiliwa pia na michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara na ile ya Mabingwa Afrika.

" Mo ataidhamini Simba kwa miaka miwili wapo kwenye hatua za mwisho za mazungumzo siku yoyote kuanzia sasa wanasaini mkataba, lakini amewapa sharti la kusaini mkataba wa mwaka mmoja mmoja,wakifanya vizuri kwenye mashindano yao ndio ataongeza tena mkataba,"alisema mtoa habari huyo

Mmoja wa viongozi wa Simba ambaye hakutaka jina lake litajwe alikiri : "Kwa kweli tuna shida sana ya fedha sio siri, nasi tungependa Mo atusaidie, kuna wenzangu ndio waliokuwa wanafanya naye mazungumzo na mwelekeo wameniambia kuwa ni mzuri nay Mo amekubali kutudhamini tena kwa vile tayari ameachana na Africa Lyon.

"Mimi binafsi sijaongea naye, ila wapo wenzangu ndio wanaoshughulikia suala hilo na wanakaribia kumalizana naye,"alisema kiongozi huyo.

Dewji alishawahi kuidhamini klabu hiyo miaka ya nyuma kabla ya kuachana nayo na kuinunua Mbagala Market ambayo ilipanda daraja na kisha kuibadilisha jina na kuitwa Africa Lyon.
Hata hivyo, Dewji maarufu kama'Mo' aliachana na Lyon msimu huu baada ya kufanya vibaya msimu uliopita na kuiuza kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Mafuta ya RBP Oil, Rahma Al- Kharoos.
 
Tanga wazialika kwao Simba, Yanga Wednesday, 29 December 2010 20:30

Burhani Yakub,Tanga

UONGOZI wa Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga umezikaribisha timu ya Simba na Yanga kutumia uwanja huo kama wa nyumbani kwa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom mwezi ujao kutokana na ukarabati wake mkubwa na kuuweka katika kiwango kinachotakiwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa, Fifa.

Meneja wa uwanja huo, Mbwana Msumari alitoa ushauri huo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mchakato wa ukarabati wa uwanja huo ulipofikia.

Alisema uwanja huo tayari upo katika hatua za mwisho za ukarabati na kwamba utafunguliwa Januari 10 mwakani ambapo timu zitakazoruhusiwa kuutumia ni zile zinazoshiriki Ligi Kuu pekee.

Msumari alisema baada ya kukarabatiwa uwanja huo utatumika kibiashara zaidi badala ya kihuduma kama ilivyokuwa awali na kwamba
michuano midogo kama ya ligi daraja la tatu haitaruhusiwa tena kuchezeshwa hapo.

Alisema uongozi wa uwanja huo umeamua kutoa ushauri kwa timu hizo mbili pamoja na timu nyingine za Ligi Kuu ya Vodacom kwani
Mkwakwani kuna mapato makubwa ikilinganishwa na viwanja vingine vilivyo nje ya Dar es salaam.

Alisema wakati baadhi ya timu kubwa za ligi kuu zikiingia katika migogoro na wachezaji wao kutokana na kudaiwa mishahara kwa sababu ya
mapato madogo yanayopatikana kwenye viwanja vya nje ya Dar es Salaam.
Mkwakwani una rekodi ya kuwa juu kwa viingilio.
 
U-20 Majimaji watia aibu, wacheza peku Wednesday, 29 December 2010 20:29

Salome Milinga na Neema Kimaro

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida baadhi ya wachezaji wa timu ya vijana ya Majimaji ya Songea inayoshiriki michuano ya Uhai jana walishindwa kucheza soka dhidi ya wenzao wa Mtibwa Sugar kufuatia kukosa vifaa, vikiwamo viatu.

Wchezaji hao walilazimika kukaa nje ya uwanja kufuatia viatu vyao kutumiwa na wenzao wa walioanza katika mchezo huo na hivyo kumlazimisha kocha kutofanya mabadiliko.

Katika mchezo huo, Mtibwa Sugar iliibuka na ushindi wa mabao 4-0 yaliyofungwa na Michael Mgima dakika ya 29, 56,73 na 80.

Kocha mkuu wa Majimaji, Omary Hussein alisema baada ya mchezo huo kuwa wameshindwa kufanya vizuri kutokana na matatizo mengi yanayowakabili.

Alilitaja la wachezaji wake baadhi kukosa viatu na hivyo kushindwa kucheza.

"Tumekubaliana na matokeo hayo lakini kupoteza kwetu mchezo huu kunatokana na mengi, kubwa zaidi ni wachezaji wangu kukosa viatu, pia uchovu nao umechangia kwa kiasi fulani, lakini zaidi ni viatu.

"Kama kila mmoja wetu alivyoona wachezaji wetu hawana viatu, hata hivyo wanavyotumia kwa hakika ni vibovu sana hivyo tuanawomba wadhamini wa mashindano hayo kutoangalia upende wa jezi tu, waangalie pia viatu kwani bila viatu pia hatuwezi kufanya lolote," alisema Hussein .

Alisema timu nyingi zinazotokea mikoani na ambazo hazina wadhamini zinakabiliwa na ukata mkubwa ambao hata kuzisaidia timu zao za vijana inakuwa kazi ngumu na ndiyo maana wachezaji wa timu hiyo wameshindwa kucheza.

Katika hatua nyingine, timu ya soka ya vijana ya Simba juzi jioni iliitandika Toto Afrika ya Mwanza kwa mabao 3-1 na kuongoza katika kundi lake.

Wakati huohuo, Azam, mabingwa wa mwaka juzi leo watashuka uwanjani kucheza na AFC ya Arusha Arusha asubuhi na jioni itakuwa zamu ya Ruvu Shooting dhidi ya Polisi Tanzania.
 
Papic awazuga Dedebit Phiri apata kikosi tishio
5591.jpg
Kosta Papic MICHAEL MOMBURI
KOCHA wa Yanga, Kosta Papic ameanza kucheza na akili za Dedebits ya Ethiopia lakini kocha wa Simba, Patrick Phiri ameisoma timu yake na kuwaachia wachezaji wake wanne wajiunge na Taifa Stars inayokwenda Misri lakini kwa masharti.

Simba inashiriki Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo imepangwa kuanza na Elans Club ya Comoro huku Yanga ikicheza na Dedebits ya Ethiopia mechi zote zikipangwa kucheza kati ya Januari 27-30 mwakani, Simba ikianzia ugenini na Yanga ikicheza Dar es Salaam.

Makocha hao ambao timu zao zitashiriki kombe la Mapinduzi linaloanza wikiendi ijayo mjini Zanzibar walizungumza na Mwanaspoti jana Jumatu na kutoa msimamo na mwelekeo wao katika mambo mbalimbali likiwemo suala la wachezaji wao walioko kwenye Taifa Stars inayoshiriki michuano maalum ya kombe la Nile Basin.

Papic alisema mipango yake inaenda vizuri lakini ameiweka kando kwa muda Dedebits ya Ethiopia atakayokutana nayo kwenye kombe Shirikisho na wala hataki kujua lolote kwa sasa mpaka amalize mtihani wa kwanza ambao ni kombe la Mapinduzi.

"Kazi tuliyonayo sasa ni kombe la Mapinduzi na ndiko wachezaji wote walikoelekeza akili zao, tunaamini kwamba hichi ndio kipimo cha kwanza kuuthibitishia umma kwamba tumejiandaa na tunaweza kufanya kitu huku tunakokwenda kwenye shirikisho,"alisisitiza Papic.

"Sihitaji kujua chochote kuhusiana na Dedebits kwasasa bado ni mapema, tunafanya kwanza kazi moja, wala sijahangaika chochote najua ninachofanya,"alisisitiza Papic ambaye Mwanaspoti inafahamu kuwa amezungumza maneno hayo kuichezea akili Dedebits kwani habari za ndani zinadai amekuwa akiichimba timu hiyo kiundani kwa siku kadhaa sasa kwa kuwatumia marafiki zake wa karibu ambao wengine ni makocha wa kigeni.

Akizungumzia wachezaji wake walioko Stars alisema; "Nimezungumza nao wameniambia kwamba hawataki kucheza hayo mashindano ndio maana nimeshauriana na uongozi tuandike barua ya kupinga wao kujumuishwa kwenye hicho kikosi ili tuwe na muda mrefu wa kufanya maandalizi ya Shirikisho."

"Ile michuano ambayo Stars inakwenda kushiriki haina faida yoyote kwetu, tungeitumia kutengeneza timu za vijana ambapo Tanzania ingepeleka mseto wa timu vijana chini ya miaka 17 na ile ya 20, wachezaji wangepata uzoefu na ingesaidia siku zijazo kwavile hata tukishinda hilo kombe halina faida kwetu kombe la Shirikisho na Mabingwa ndio muhimu,"alisisitiza Papic.

Phiri ambaye timu yake iliondoka jijini Dar es Salaam jana kwenda Zanzibar kuweka kambi alisema; "Nimewaruhusu wale wachezaji wanne waende kwa vile ninaamini kwamba watakuwa kwenye kikosi cha kwanza kitakachocheza mechi zote."

"Ile michuano inashirikisha Uganda, Sudan, Misri, Kenya ni timu ngumu ambazo hao wachezaji wangu watazidi kupata changamoto mpya na kuimarika zaidi kwa ligi ya mabingwa, nazungumza hivyo kiufundi na jinsi ninavyoona halisi."

Kocha huyo ambaye timu yake itakwaana na mabingwa wa Afrika, TP Mazembe endapo itaitoa Elans, alisema kuwa; "Nimeiangalia timu yangu kwa wiki kadhaa imeimarika sana na sidhani kama kutakuwa na mabadiliko makubwa kwenye kikosi cha kwanza."

"Ukiangalia wachezaji wote waliokuwa kwenye kikosi cha kwanza kilichocheza mzunguko wa kwanza wako fiti, wanafanya vizuri mpaka kwenye timu za Taifa sitegemei kutokee miujiza, kama yatakuwepo mabadiliko ni kidogo sana na hii itategemea na afya za wachezaji wetu hadi ligi itakapoanza.

"Nataka kuimarisha kikosi imara cha kwanza chenye uelewano mzuri ambacho kitatusaidia sana hata kwenye ligi ya mabingwa na mzunguko wa pili, timu imara haibadiliki mara kwa mara,"alisisitiza Phiri na kusema timu yake itabaki Zanzibar mpaka ligi ya Bara ianze.
 
Sofapaka yazifuata Simba, Yanga Dar


na Makuburi Ally


amka2.gif
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Kenya, Sofapaka, wanazitafutia dawa timu za Simba na Yanga kabla ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika na Kombe la Shirikisho yanayotarajia kufanyika mwakani. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jijini Dar es Salaam jana, mratibu wa michezo hiyo miwili ya kimataifa ya kirafiki, George Wakuganda, alisema, michezo hiyo inatarajiwa kuchezwa Januari 15 na 16 jijini Dar es Salaam.
Wakuganda alisema michezo hiyo inatarajiwa kuchezwa iwapo michezo yao ya Ligi Kuu itasogezwa mbele katika ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara inayotarajia kuanza Januari 15.
Aidha, Wakuganda alisema Sofapaka wamethibitisha kucheza michezo hiyo ya kimataifa, ambapo taratibu zote nyingine za mchezo huo zimekamilika.
Mratibu huyo alisema Desemba 25 na 26 Simba na Yanga zilijinoa na timu ya AFC Leopard ya Kenya, baada ya mchezo huo Leopard ilimenyana na Azam FC.
 
Aliyewashambulia kina Adebayor Angola afungwa


na Mwandishi wetu, LUANDA, Angola


amka2.gif
MAHAKAMA ya nchini Angola imemhukumu kifungo cha miaka 24 jela mtu aliyedaiwa kulishambulia basi la timu ya Taifa ya Togo 'The Hawks' iliyokuwa njiani kwenda Kabinda nchini humo kwenye michuano ya kuwania Kombe la Afrika Januari mwaka huu. Mwanasheria Joao Antonio Puati's aliliambia Shirika la Utangazaji la AFP kuwa muuaji huyo alilishambulia basi la Togo kwa bunduki za kivita na kusababisha majereha kwa baadhi ya wachezaji wa timu hiyo mjini Cabinda Angola.
Lakini hata hivyo, Mahakama hiyo haijaweka hadharani jina la mtu huyo.
Mwingine aliyehusishwa na tukio hilo ni Daniel Simbai, ambaye alituhumiwa kuua maofisa wawili ndani ya dakika 30 akitumia bunduki kwa kuwashambulia na kuwaua viongozi wawili wa timu hiyo huku baadhi ya wachezaji wa timu hiyo wakijeruhiwa kutokana na shambulio hilo linalodaiwa kufanywa na waasi wa jimbo hilo (Flec).
Kutokana na shambulio hilo, timu hiyo iliyokuwa chini ya nahodha wake Emmanuel Adebayor iliamua kujitoa katika mashindano hayo na kurejea kwao.
 
Simba, Yanga zaibana TFF
IMANI MAKONGORO
KLABU kongwe nchini, Yanga na Simba zimetaka wachezaji wao nyota waliochaguliwa kwenye timu ya Taifa ya Tanzania kuondolewa ili washiriki vyema katika maandalizi ya michuano ya Kimataifa ya Afrika.

Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako alisema kuwa wamekwisha wasilisha barua kwa Shirikisho la Kandanda nchini (TFF) kuhusiana na ombi hilo na wanaamini watakubaliwa.

Mwalusako alisema kuwa hatua hiyo inatokana na kupima umuhimu wa mashindano ya Mto Nile na yale ya kombe la Shirikisho ambapo timu yake itapambana na timu ya Dedebit ya Ethiopia kati ya Januari 28 na 30 mjini Addis Ababa.

Alisema kuwa wanatambua umuhimu wa wachezaji wao katika timu ya Taifa, lakini kwa ubora, Kombe la Shirikisho lipo juu zaidi ukilinganisha na mashindano hayo ya Misri.

�Ni kweli tumewasilisha barua rasmi leo ili kuomba wachezaji wetu wasiende huko Misri kwani watakaborejea, watakuwa wamebakiza siku saba kabla ya kusafiri kwenda Ethiopia, ni muhimu wakishiriki katika mazoezi ya timu yetu,� alisema Mwalusako.

Wachezaji wa Yanga walioko Stars ni Shadrack Nsajigwa, Stephano Mwasika, Nadir �Cannavaro� Haroub, Nurdin Bakari, Jerryson Tegete na Abdi Kassim.

Watani wao wa jadi, Simba SC nao wamewasilisha barua TFF kuomba wachezaji wao waruhusiwe kufanya mazoezi na timu yao na si timu ya Taifa. Makamu wa Mwenyekiti wa Simba, Godfrey �Kaburu� Nyange alisema kuwa wamewasilisha barua hiyo kwa kutambua kuwa ombi lao litakubaliwa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom