Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
- Thread starter
- #2,061
Yanga, JKT Ruvu 'ligwaride' Uhuru leo
na Juma Kasesa
TIMU ya soka ya Yanga leo inashuka Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam kuvaana na Maafande wa JKT Ruvu, katika mechi ya kirafiki kujiandaa na mzunguko wa pili Ligi Kuu Tanzania Bara na michuano ya kimataifa. Yanga iliyo chini ya Kocha Mserbia, Kostadin Papic inacheza mechi hiyo ya kirafiki ikiwa ni ya tatu, baada ya kupokea kipigo cha mabao 3-1 katika mechi ya kwanza dhidi ya Azam FC, kabla ya kuzinduka na kuitandika AFC Leopard ya Kenya bao 1-0.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa klabu hiyo Louis Sendeu, Papic amepanga kushusha kikosi kizima cha timu hiyo, ili kuweza kupima uwezo wa kila mchezaji ikiwa ni maandalizi ya kusaka kikosi cha kwanza ambacho kitaweza kuwapokonya ubingwa wa Ligi hiyo 'Wekundu wa Msimbazi' Simba na kufanya vema katika michuano ya kimataifa.
Sendeu alisema, mchezo wa leo ni kati ya mechi tisa ambazo Papic amepanga timu hiyo icheze ikiwa ni maandalizi ya Ligi Kuu Tanzania Bara inayotarajiwa kuanza kunguruma Januari 15 mwakani na michuano ya kimataifa, ambako Yanga inatarajia kucheza Kombe la Shirikisho.
Alivitaja viingilio vya mchezo huo kuwa ni mzunguko sh 2,000, Jukwaa la Kijani sh 3,000, Jukwaa Kuu sh 5,000, na VIP sh 7,000.
na Juma Kasesa
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa klabu hiyo Louis Sendeu, Papic amepanga kushusha kikosi kizima cha timu hiyo, ili kuweza kupima uwezo wa kila mchezaji ikiwa ni maandalizi ya kusaka kikosi cha kwanza ambacho kitaweza kuwapokonya ubingwa wa Ligi hiyo 'Wekundu wa Msimbazi' Simba na kufanya vema katika michuano ya kimataifa.
Sendeu alisema, mchezo wa leo ni kati ya mechi tisa ambazo Papic amepanga timu hiyo icheze ikiwa ni maandalizi ya Ligi Kuu Tanzania Bara inayotarajiwa kuanza kunguruma Januari 15 mwakani na michuano ya kimataifa, ambako Yanga inatarajia kucheza Kombe la Shirikisho.
Alivitaja viingilio vya mchezo huo kuwa ni mzunguko sh 2,000, Jukwaa la Kijani sh 3,000, Jukwaa Kuu sh 5,000, na VIP sh 7,000.