Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
- Thread starter
-
- #2,741
Federer atwaa ubingwa wa Qatar Open
Sunday, 09 January 2011 21:04
DOHA, Qatar
ROGER Federer ametwaa ubingwa wa Qatar Open kwa kumchapa mpinzani wake Nikolay Davydenko 6-3, 6-4 katika mchezo uliodumu kwa dakika 79.
Federer amekuwa mchezaji wa kwana kutwaa mara tatu taji la Doha, baada ya kufanya hivyo mwaka 2005 na 2006.
"Ni mwanzo mzuri wa msimu," Federer aliwaambia mashabiki 8,000 waliojitokeza kwenye uwanja wa Khalifa Tennis Complex. "Nimejisikia vizuri wiki zote nilizokuwa hapa. Nilitawala mchezo kuanzia seti ya kwanza hadi ya pili pia."
Wakati alipoulizwa kuhusu nafasi yake kwenye michuano ya Australian Open mwishoni mwa mwezi, Federer alicheka na kusema, "Sipo tayari kwa sasa. Nitakuwa tayari nitakapokuwa pale. Lakini ni wazi ushindi wangu hapa utanisaidia kufanya vizuri Australia."
Davydenko, ambaye alimchapa mchezaji bora Rafael Nadal kwenye nusu fainali, alisema "alicheza vizuri zaidi yangu.Nimekuwa nikichezea naye mara kadha, lakini leo (jana0 alikuwa mwepesi zaidi. Hakunipa nafasi yoyote."
Davydenko alisema. "Kama ningejaribu kucheza kwa kulinda mstari, alikuwa na kasi zaidi. Wakati alipokuwa akianzisha mchezo alikuwa bora zaidi. Nafikiri kama ataendelea kucheza kwa kiwango hiki hakuna shaka kwamba atarudia kuwa namba moja tena.
"Sikucheza vibaya. Kiwango changu kilikuwa juu. Tatizo ni kwamba Federer hakunipa nafasi hata kidogo leo."
Sunday, 09 January 2011 21:04
DOHA, Qatar
ROGER Federer ametwaa ubingwa wa Qatar Open kwa kumchapa mpinzani wake Nikolay Davydenko 6-3, 6-4 katika mchezo uliodumu kwa dakika 79.
Federer amekuwa mchezaji wa kwana kutwaa mara tatu taji la Doha, baada ya kufanya hivyo mwaka 2005 na 2006.
"Ni mwanzo mzuri wa msimu," Federer aliwaambia mashabiki 8,000 waliojitokeza kwenye uwanja wa Khalifa Tennis Complex. "Nimejisikia vizuri wiki zote nilizokuwa hapa. Nilitawala mchezo kuanzia seti ya kwanza hadi ya pili pia."
Wakati alipoulizwa kuhusu nafasi yake kwenye michuano ya Australian Open mwishoni mwa mwezi, Federer alicheka na kusema, "Sipo tayari kwa sasa. Nitakuwa tayari nitakapokuwa pale. Lakini ni wazi ushindi wangu hapa utanisaidia kufanya vizuri Australia."
Davydenko, ambaye alimchapa mchezaji bora Rafael Nadal kwenye nusu fainali, alisema "alicheza vizuri zaidi yangu.Nimekuwa nikichezea naye mara kadha, lakini leo (jana0 alikuwa mwepesi zaidi. Hakunipa nafasi yoyote."
Davydenko alisema. "Kama ningejaribu kucheza kwa kulinda mstari, alikuwa na kasi zaidi. Wakati alipokuwa akianzisha mchezo alikuwa bora zaidi. Nafikiri kama ataendelea kucheza kwa kiwango hiki hakuna shaka kwamba atarudia kuwa namba moja tena.
"Sikucheza vibaya. Kiwango changu kilikuwa juu. Tatizo ni kwamba Federer hakunipa nafasi hata kidogo leo."