Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
- Thread starter
- #2,761
Soka Mbeya kubuni miradi
Imeandikwa na Joachim Nyambo, Mbeya; Tarehe: 10th January 2011 @ 23:30 Imesomwa na watu: 25; Jumla ya maoni: 0
CHAMA cha soka mkoani Mbeya (MREFA) kimeelezea mikakati kiliyojiwekea katika mwaka 2011, moja kati ya mikakati hiyo ikiwa ni kubuni na kuanzisha mradi utakaokiwezesha kuondokana na adha ya kuwa ombaomba.
Chama hicho kimesema imefika wakati wa chama kusimama kwa miguu yake badala ya kuendelea kutegemea michango ya wadau hali ambayo wakati mwingine imekuwa ikikisababishia kushindwa kuendesha mambo yake kwa wakati ikiwemo mikutano ambayo ili ifanyike ni lazima wapitishe bakuli la kuomba misaada.
Makamu Mwenyekiti wa chama hicho John Mwamwaja aliyasema hayo jana na kubainisha kuwa ukata huo ndiyo chanzo cha kuahirishwa pia kwa mkutano mkuu wa mwaka uliokuwa ufanyike Desemba mwaka jana ambao hadi sasa haijulikani utafanyika lini.
"Tunaandaa andiko la mradi na utakapokamilika tutauweka wazi kwa wadau ili kwa pamoja tuone ni jinsi gani tunaweza kuuendesha.Tumekwama vya kutosha kwa kutegemea mifuko ya wadau, sasa inabidi tuwe wabunifu," alisema Mwamwaja.
Mwamwaja pia alivishauri vyama vya soka katika ngazi za wilaya pamoja na klabu kuangalia uwezekano wa kulifanyia kazi wazo hilo kwakuwa pia vimekuwa vikishindwa kutimiza mikakati vinayojiwekea kutokana na hali ya ukata inayokuwa inavikabili.
Kwa upande wa mikakati ya kuwa na timu katika ligi kuu makamu Mwenyekiti huyo alisema licha ya mikakati inayoendelea kuhakikisha timu ya Prisons inapanda daraja pia MREFA ina mkakati wa kuhakikisha timu nyingine zinapanda daraja na ikiwezekana kufikia ligi kuu ya Tanzania Bara.
Aidha alisema chama pia kinatarajia kukutana na wabunge wote wa mkoa wa Mbeya ili kwa pamoja waweze kujadili mikakati ya kulijenga soka la mkoa ili kuurejeshea heshima yake kimichezo tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo soka limeporomoka kwa kiasi kikubwa.
Imeandikwa na Joachim Nyambo, Mbeya; Tarehe: 10th January 2011 @ 23:30 Imesomwa na watu: 25; Jumla ya maoni: 0
CHAMA cha soka mkoani Mbeya (MREFA) kimeelezea mikakati kiliyojiwekea katika mwaka 2011, moja kati ya mikakati hiyo ikiwa ni kubuni na kuanzisha mradi utakaokiwezesha kuondokana na adha ya kuwa ombaomba.
Chama hicho kimesema imefika wakati wa chama kusimama kwa miguu yake badala ya kuendelea kutegemea michango ya wadau hali ambayo wakati mwingine imekuwa ikikisababishia kushindwa kuendesha mambo yake kwa wakati ikiwemo mikutano ambayo ili ifanyike ni lazima wapitishe bakuli la kuomba misaada.
Makamu Mwenyekiti wa chama hicho John Mwamwaja aliyasema hayo jana na kubainisha kuwa ukata huo ndiyo chanzo cha kuahirishwa pia kwa mkutano mkuu wa mwaka uliokuwa ufanyike Desemba mwaka jana ambao hadi sasa haijulikani utafanyika lini.
"Tunaandaa andiko la mradi na utakapokamilika tutauweka wazi kwa wadau ili kwa pamoja tuone ni jinsi gani tunaweza kuuendesha.Tumekwama vya kutosha kwa kutegemea mifuko ya wadau, sasa inabidi tuwe wabunifu," alisema Mwamwaja.
Mwamwaja pia alivishauri vyama vya soka katika ngazi za wilaya pamoja na klabu kuangalia uwezekano wa kulifanyia kazi wazo hilo kwakuwa pia vimekuwa vikishindwa kutimiza mikakati vinayojiwekea kutokana na hali ya ukata inayokuwa inavikabili.
Kwa upande wa mikakati ya kuwa na timu katika ligi kuu makamu Mwenyekiti huyo alisema licha ya mikakati inayoendelea kuhakikisha timu ya Prisons inapanda daraja pia MREFA ina mkakati wa kuhakikisha timu nyingine zinapanda daraja na ikiwezekana kufikia ligi kuu ya Tanzania Bara.
Aidha alisema chama pia kinatarajia kukutana na wabunge wote wa mkoa wa Mbeya ili kwa pamoja waweze kujadili mikakati ya kulijenga soka la mkoa ili kuurejeshea heshima yake kimichezo tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo soka limeporomoka kwa kiasi kikubwa.