Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
- Thread starter
- #141
Twanga kuburudisha Mbagala Kuu
Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 6th December 2010 @ 21:00 Imesomwa na watu: 25
BENDI ya muziki wa Dansi ya African Stars ‘Twanga Pepeta' Ijumaa inatarajiwa kutoa burudani kwenye Ukumbi wa Nawina Resort Mbagala Kuu Dar es Salaam.
Mratibu wa Onesho hilo Zahor Said, alisema kuwa onesho hilo litakuwa maalumu kwa wakazi wa Mbagala Kuu na vitongoji vyake ikiwa ni pamoja na kuwapa burudani hiyo.
Alisema katika kuhakikisha wanatoa burudani safi kutakuwa na utambulisho wa vikundi vya unenguaji ambavyo vimekuwa vikitamba Tanzania.
Said alisema vikundi hivyo ni Kiduku na Khanga Moja ambapo lengo la kuwaita katika onesho hilo ni kutoa burudani kwa wakazi wa Mbagala.
Bendi inaongozwa na waimbaji mahiri kama Chaz Baba, Kalala Junior, Dogo Rama, Luiza Mbutu, Janeth Isinika na marapa Khalid Chokoraa na Ferguson.
Wakati kwa wapiga vyombo kuna James Kibosho, mpiga ngoma, Soud Mohamed ‘MCD' mpiga tumba, huku solo gitaa likipapaswa na Miraji Shakashia ‘Shakazulu'.
Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 6th December 2010 @ 21:00 Imesomwa na watu: 25
BENDI ya muziki wa Dansi ya African Stars ‘Twanga Pepeta' Ijumaa inatarajiwa kutoa burudani kwenye Ukumbi wa Nawina Resort Mbagala Kuu Dar es Salaam.
Mratibu wa Onesho hilo Zahor Said, alisema kuwa onesho hilo litakuwa maalumu kwa wakazi wa Mbagala Kuu na vitongoji vyake ikiwa ni pamoja na kuwapa burudani hiyo.
Alisema katika kuhakikisha wanatoa burudani safi kutakuwa na utambulisho wa vikundi vya unenguaji ambavyo vimekuwa vikitamba Tanzania.
Said alisema vikundi hivyo ni Kiduku na Khanga Moja ambapo lengo la kuwaita katika onesho hilo ni kutoa burudani kwa wakazi wa Mbagala.
Bendi inaongozwa na waimbaji mahiri kama Chaz Baba, Kalala Junior, Dogo Rama, Luiza Mbutu, Janeth Isinika na marapa Khalid Chokoraa na Ferguson.
Wakati kwa wapiga vyombo kuna James Kibosho, mpiga ngoma, Soud Mohamed ‘MCD' mpiga tumba, huku solo gitaa likipapaswa na Miraji Shakashia ‘Shakazulu'.


