Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.

Simba, Yanga fainali Mapinduzi leo


Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 11th January 2011 @ 23:59

MIAMBA ya soka nchini Simba na Yanga leo itamenyana kuwania fainali za Kombe la mapinduzi katika uwanja wa Amaan Zanzibar.

Timu hizo zimeshakutana mara nyingi tangu kuanzishwa kwake lakini mechi ya leo ni ya
kipekee kutokana na timu hizo kukutana Zanzibar kwenye uwanja huo baada ya kupita miaka 19.

Mara ya mwisho timu hizo zilikutana Zanzibar mwaka 1992 kwenye michuano ya Kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (sasa Kombe la Kagame) na Simba kuifunga Yanga mabao 5-4 kwa mikwaju ya penati baada ya kutoka bao 1-1 kwa dakika 120.

Aidha timu hizo zinakutana zikiwa zimebakiwa na takriban miezi miwili kukutana kwenye mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara Machi 5.

Inawezekana kabisa mechi ya leo, Simba ndio yenye mcheche zaidi kwani itataka kuitumia mechi hiyo kulipa kisasi cha kupigwa mara mbili mfululizo na mtani wake Yanga mwaka jana.

Kabla ya kuanza kwa ligi Agosti mwaka jana, timu hizo zilikutana katika mechi ya ngao ya hisani na Simba kufungwa na Yanga.

Lakini pia baada ya miezi miwili tangu kupata kipigo hicho, Simba ilichapwa tena bao 1-0 katika mechi ya mzunguko wa kwanza wa Ligi, Oktoba.

Hata hivyo, timu hizo leo zinakutana zikiwa hazina nyota wake kama Juma Kaseja, Kelvin Yondani, Juma Nyoso, kwa upande wa Simba na kwa Yanga itawakosa Shadrack Nsajigwa, Nadir Haroub, na Jerryson Tegete ambao wapo kwenye timu ya Taifa inayoshiriki michuano ya Bonde la Mto Nile, Misri.

Tegete ndiye aliyefunga bao la ushindi walipokutana Oktoba kwenye Uwanja wa CCM Kirumba
Mwanza na aliapa atakuwa akiifunga Simba kila atakapokutana nayo.

Lakini mechi ya leo inatarajiwa kuwa na msisimko wa hali ya juu na matokeo hayatabiriki kwani kila upande utakuwa na wachezaji wake wapya iliowasajili kwenye dirisha dogo na wanaonekana ni wazuri hasa Davis Mwape wa Yanga ambaye karibu kila mechi anazochezea timu hiyo hakosi kufunga.

Timu hizo hazijaachana sana kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwani zimepishana kwa pointi mbili. Simba inaongoza ikiwa na pointi 27 na Yanga inashika nafasi ya pili kwa kufikisha pointi 25.

Katika michuano hiyo ya kuadhimisha kilele cha Mapinduzi ya Zanzibar, sherehe zitafanyika
leo kwenye uwanja huo.

Yanga haikuanza vizuri sana kwani ilitoka sare mara mbili, dhidi ya Zanzibar Ocean View, Chuoni na kuifunga Azam huku Simba ikiifunga Jamhuri, KMKM na kutoka sare dhidi ya Mtibwa Sugar.

Katika mechi ya nusu fainali, Simba iliifunga Zanzibar Ocean View na Yanga kuifunga Mtibwa Sugar.

Akiizungumzia mechi hiyo, Kocha wa Simba Patrick Phiri alisema anajua itakuwa ngumu lakini amejiandaa vizuri kuibuka na ushindi.

"Yanga wameshanifunga mara mbili mwaka jana, safari hii vijana wangu hawatakubali tumeajindaa kushinda mechi na tuna imani tutashinda," alisema Phiri ambaye aliipa Simba ubingwa wa ligi mwaka jana bila kupoteza mechi.

Naye kocha wa Yanga, Kostadin Papic alisema anajua atashinda mechi kwani Simba ameshaisoma na ndio maana aliweza kuifunga mara mbili mfululizo, haimpi tabu.
 

Stars yaendeleza ugoigoi Misri

Imeandikwa na Amir Mhando, Cairo; Tarehe: 11th January 2011 @ 23:55
TIMU ya soka ya Taifa, Taifa Stars jana ilishindwa kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya Bonde la Mto Nile baada ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Uganda.

Matokeo hayo yanaifanya Uganda iungane na Misri kufuzu nusu fainali, na Stars ikisubiri Burundi ifungwe na Misri ili ipate nafasi ya kuwania mshindi wa tatu, lakini Burundi ikishinda, Stars itakosa nafasi hiyo kwa vile itakuwa ya mwisho kwenye kundi lao.

Stars ilianza vizuri mechi ya jana ambapo ilikuwa ikifanya mashambulizi kadhaa, kabla Athumani Machuppa hajaandika bao la kuongoza katika dakika ya 24.

Machuppa, anayesakata soka ya kulipwa Sweden alifunga bao hilo kwa shuti baada ya kupokea mpira wa juu na kuujaza mpira wavuni.

Mapema katika kipindi hicho, kulikuwa na mashambulizi ya hapa na pale ambapo Daniel Wagaluka nusura aipatie Uganda bao katika dakika ya 10 pale alipowatoka mabeki wa Stars na kupiga shuti kali ambalo liliishia mikononi mwa kipa wa Stars Juma Kaseja.

Dakika mbili baadaye Kaseja aliokoa hatari katika lango la Tanzania kutokana na shuti kali la Derick Walulya.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na safari hii ni kwa upande wa Uganda ambapo walilisakama lango la Stars kwa dakika kumi za mwanzo lakini washambuliaji wake walishindwa kulenga lango la Stars.

Katika kipindi hicho, Kocha Jan Poulsen aliamua kufanya mabadiliko ili kunusuru jahazi lake ambapo aliwatoa Salum Machaku, Saidi Maulidi na kuwaingiza Mrisho Ngassa na Idrissa Rajabu.

Hata hivyo mabadiliko hayo hayakusaidia kwani dakika ya 71 Yudah Mugalu aliisawazishia Uganda bao hilo kwa kichwa kutokana na mpira wa kona.

Katika kipindi hicho, Stars ilicheza vibaya na kuifanya Uganda kutawala karibu sehemu kubwa ya mchezo, pamoja na kocha Poulsen kufanya mabadiliko mengine ya kuwatoa Machuppa na Shaaban Nditi na nafasi zao kuchukuliwa na Jabir Azizi na Ally Ahmed ‘Shiboli' lakini hakukuwa na matunda.

Stars ilipangwa kama ifuatavyo: Juma Kaseja, Shadrack Nsajigwa, Stephano Mwasika, Juma Nyoso, Aggrey Morris, Nurdin Bakari, Salum Machaku/ Mrisho Ngassa, Shaaban Ndiri/ Ally Ahmed ‘Shiboli', Nizar Khalfani, Athumani Machuppa/ Jabir Azizi, Saidi Maulidi/ Idissa Rajabu.

 
Cecafa haifi- Musonye

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 11th January 2011 @ 23:50 Imesomwa na watu: 52; Jumla ya maoni: 0


01_11_27zuay.jpg

KATIBU Mkuu wa CECAFA Nicholas Musonye.







KATIBU Mkuu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Nicholas
Musonye amesema Cecafa haifi na haitokufa.

Akizungumza kwa simu kutoka Nairobi jana, Musonye alisema Baraza lake limeota mizizi na halitayumba hata ikianzishwa michuano gani.

Musonye ametoa kauli hiyo baada ya Chama cha Soka Misri mwishoni mwa wiki iliyopita kusema kwamba kinaazimia kuunda Shirikisho la Soka la nchi zilizopo kwenye bonde la mto Nile ambalo litakuwa likisimamia masuala ya soka ya nchi hizo pamoja na kuendesha michuano ya Mto Nile.

Mwaka huu Misri imeanzisha michuano ya nchi zilizo kwenye bonde la Mto Nile ambayo inaendelea mjini Cairo, lengo la michuano hiyo ni kuhamasisha utunzwaji wa vyanzo vya maji kwa vizazi vijavyo.

Kimtazamo, endapo Shirikisho hilo litaanzishwa linaonekana litakuwa na nguvu kutokana na zawadi kubwa katika michuano yake ambapo bingwa atapata Sh milioni 200 za Tanzania, kitu ambacho kwa michuano inayosimamiwa na Cecafa si ile ya Chalenji wala Kagame haijawahi kutoa.

Kawaida katika michuano hiyo, mshindi hupata Dola za Marekani 30,000 ambazo ni takriban Sh milioni 40 za Tanzania.

"Cecafa haifi, na haitakufa, kama kuna mtu anataka kuanzisha chama chake aanzishe au ajiunge na sisi lakini Cecafa itaendelea kuwepo," alisema Musonye.
 

Ligi Kuu yarudi Dar es Salaam

Imeandikwa na Evance Ng'ingo; Tarehe: 11th January 2011 @ 23:45

TIMU zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara zikiwemo Simba na Yanga huenda zikaanza
kuonekana zikicheza Dar es Salaam baada ya serikali kukubali kutumiwa kwa uwanja wa Taifa kwenye mechi za Ligi Kuu na michuano ya Kimataifa.

Awali, timu zinazotoka Dar es Salaam ambazo ni Simba, Yanga, African Lyon, Azam, JKT Ruvu na Ruvu Shooting zilikuwa zikitumia uwanja wa Uhuru, lakini zililazimika kuhamia mikoani baada ya uwanja huo kufungwa kwa ajili ya matengenezo.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Angetile Osiah ‘Ngeta' alisema kuwa tayari shirikisho lake limepata maagizo ya mdomo na kwa sasa inasubiria maandishi juu ya suala hilo.

Karibu mechi zote za mzunguko wa kwanza kwa timu za Dar es Salaam zilihamia mikoani ambapo Yanga, JKT Ruvu, Ruvu Shhoting na African Lyon zilikuwa Jamhuri Morogoro, Simba ilikuwa CCM Kirumba Mwanza na Azam ilikuwa Mkwakwani Tanga.

Hata hivyo huenda suala la kurudi Dar es Salaam kwa upande wa Azam likawa gumu kwani tayari uongozi wa timu hiyo ulishaanza kufanya ukarabati wa uwanja wa Mkwakwani.

Katika hatua nyingine, TFF imepiga marufuku mechi za kirafiki kuanzia Januari 15 ambayo ndiyo siku ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa ligi.

Ngeta alisema kuwa agizo hilo litaanza kutekelezeka kuanzia siku hiyo ambapo mzunguko wa pili wa ligi unaanza.

"Haitakiwi timu ya ligi kuu kuwa na mechi za kirafiki baada ya kuanza kwa ligi na kila timu ina taarifa hiyo," alisema.

Yanga ilikuwa ikutane na Zesco kwa mechi ya kirafiki kujiandaa na michuano ya Kombe la Shirikisho, mchezo ambao ulipangwa kuchezwa kwenye uwanja wa Uhuru siku moja baada ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa ligi kuu.

 
Timu zisizoshiriki ligi ya mkoa kukiona

Imeandikwa na Jasmin Shamwepu, Dodoma; Tarehe: 11th January 2011 @ 23:35

KAMATI ya Nidhamu ya Chama cha Soka mkoa wa Dodoma (DOREFA), imepanga kuzichukulia hatua timu ambazo hazitashiriki kwenye ligi ya mkoa huu inayotarajia kuanza kutimua vumbi mwisho wa mwezi huu.

Mwenyekiti wa DOREFA, Nassoro Kipenzi alisema jana kuwa hadi mwisho wa kuchukua fomu za usajili na kulipa ada ya ushiriki wa ligi hiyo ni timu tatu ambazo hazijachukua fomu na wala hazijatoa taarifa za kimaandishi.

"Kwa sasa mimi sina la kuzungumza ila kamati ya nidhamu itakaa na kuliangalia suala hilo kwa undani zaidi na kama hakuna taarifa inayoeleweka kuna adhabu ambayo itatolewa kwa ajili ya timu hizo," alisema Kipenzi.

Alizitaja timu hizo na kusema hana taarifa zake kuwa ni Chipukizi ya Kongwa, Penta Eagle ya Chamwino na Chinga ya Kondoa.

Hata hivyo, HABARILEO ilipowasiliana na viongozi wa timu hizo za wilaya, walisema kuwa hawana taarifa zozote kuhusiana na timu zao hizo.

Huku uongozi wa Chipukizi ulisema timu hiyo haitoweza kushiriki kwenye ligi hiyo kutokana na ukata unaoikabili na pia wachezaji na viongozi wanajiandaa kwa kilimo.

"Unajua hii timu ya Chipukizi ni wakulima kwa hiyo kipindi hiki wanasema hawana fedha na wanajiandaa na kilimo," alisema.

Timu ambazo zimechukua fomu hizo ni KBC, Guners, Majengo (Dodoma Mjini), Hazina, TTC, Mji (Mpwapwa), Nyomi, Kasi Mpya na Vijana Mundemu (Bahi).

Timu nyingine ni Aluta na Vijana (Chamwino), Kongwa Star na Sinza (Kongwa), City Center na Mnadani SC za Kondoa.
 
Taifa Stars bow out fighting Tuesday, 11 January 2011 21:40

juma%20kaseja2.jpg
Taifa Stars goalkeeper,Juma Kaseja.

By Jessca Nangawe
The Citizen Correspondent

The national soccer team, Taifa Stars, suffered early elimination in the Nile Basin tournament yesterday when Uganda Cranes forced them to a 1-1 draw in their final Group A match in Cairo.

Uganda Cranes' striker Yudah Magalu was the player who dashed the little hopes Taifa Stars had for a place in the semi-finals of the money-spinning tournament.

Taifa Stars seemed destined for a win until in the 71st minute when unmarked Mugalu beat goalkeeper Juma Kaseja with a tricky header off a neat Dany Wagaluka corner.

It was the second draw for Jan Poulsen's lads in the tournament. In their first match, they tumbled 5-1 to hosts Egypt before settling to a one-all draw with less fancied Burundi in their second outing over the weekend.

Taifa Stars, needing a clear victory to sail through, took off forcefully and fluffed two easy chances in the first 13 minutes, the culprits being striker Athumani Machupa and defender Stephano Mwasika.

Machupa missed what could have been the match-opener after 10 minutes when, with the net at his mercy, shot wide to the disappointment of local fans.

Another chance for Taifa Stars to score came two minutes later when Mwasika broke through, only to see his close range shot miss the target narrowly.

Machupa redeemed himself in the 24th minute when he sneaked between two Uganda Cranes defenders to unleash a powerful drive that went straight into the yawning net to help Stars go to the breather leading 1-0.

On resumption, the Ugandans, aware that a defeat could see them kiss a goodbye, appeared more aggressive and pressed upfront relentlessly in search of an equaliser, but Taifa Stars defence, built around Agrey Morris, Juma Nyoso and Shadrack Nsajigwa, remained firm until in the 71st when Magalu levelled the matter.

Sensing the danger of bowing out of the tournament, Poulsen made some changes late in the second half, bringing in Mrisho Ngasa, Idrisa Rajab and Jabir Aziz to replace Machupa, Saidi Maulid and Salum Machaku.

However, the move did not bear fruit as the Ugandans remained firm until the final whistle
 
Anxiety as Simba and Yanga meet in final
Tuesday, 11 January 2011 21:35

By Majuto Omary
The Citizen Reporter

Zanzibar. A mammoth crowd is expected at the Amaan Stadium here this evening when Simba and Yanga clash in the 2011 Mapinduzi Cup final. The final dubbed "battle of the titans" marks the end of celebrations of the 47th anniversary of Zanzibar revolution. The match starts at 4pm.

Zanzibar President Dr Ali Mohammed Shein is expected to lead hundreds of Isles soccer enthusiasts to cheer the two teams, according to Mapinduzi Cup head of communications Hamad Maulid Hamad. "We're very happy that President Shein has agreed to grace the final, this is a clear indication that this year's Mapinduzi Cup will end on a high note," Maulid confirmed here yesterday.

Matches involving the two teams, which pull droves of soccer fans in the country, are always a matter of wits, and today's final is expected to follow that tradition.

Soccer enthusiasts, who are interested in witnessing the match will have to part with Sh10,000 each for VIP seats and Sh 5,000 for seats near the VIP stands. Entrance fee for the remaining seats stand at Sh3,000.

This will be the first time in nearly two decades for Simba and Yanga to meet in a final of any tournament in the Isles.
The two teams last clashed here in 1992 during the East and Central African club championship (now Kagame Cup) final and Simba won 7-5 in post match penalties. Both teams will be unfortunate not to have on board some of their key players, who are in Egypt with Taifa Stars for the Nile Basin tournament.

Yanga coach Kostadin Papic said yesterday that they were set to win the Mapinduzi Cup for the second in the event's history. Yanga last won the title in 2007. His Simba counterpart Patrick Phiri described the final as an ideal opportunity for his team to avenge a 1-0 loss they suffered in the Premier League first round match.
 
30 players picked to form Ngorongoro Heroes
Tuesday, 11 January 2011 21:33

Doris Maliyaga
The Citizen Correspondent

Dar es Salaam. Hopes are high as a panel of coaches appointed to pick players for the Under-20 national team, Ngorongoro Heroes, completed its assignment successfully.

The panel headed by Charles Boniface Mkwasa managed to select 30 players whose exceptional skills during the recently ended Uhai Cup caught the eye of soccer enthusiasts.

Mkwasa, who is also the national women's team, Twiga Stars head coach, told The Citizen that the 30-man provisional squad would be summoned soon for a training camp.

Uhai Cup that involved youth teams from all Mainland Premier League clubs saw Ruvu Shooting gun down JKT to lift the trophy at Karume Stadium on Monday.

"The tournament was very competitive, it helped us pick the best players to form Ngorongoro Heroes…I hope this time around, we'll have a team to reckon with," he said.

According to him, the provisional squad would be trimmed to 25 players ahead of the forthcoming regional and continental assignments.

Coaches Adolph Rishard and Jamuhuri Kihwelu echoed Mkwasa's words, adding that Ngorongoro Heroes would leave their mark in all tournaments this year.

"The players have displayed magnificent performance in this year's edition of the Uhai Cup, this gives us hopes of sparkling in the coming events," the duo shared comment. Kihwelu added that for the players to develop desired patterns, they should spend a long time in the camp.

"Yes, they impressed us with their skills, but they should play together for a long time, by doing so, Tanzania will have a formidable team," the outspoken coach said.
 
Grief as ace basketball player dies Tuesday, 11 January 2011 21:31

Oliver Albert
The Citizen Correspondent

Dar es Salaam. The sports family has been gripped by grief after a prominent basketball player, Neema Emmanuel, died here yesterday.

Neema, well known for her dazzling pace and scoring magic, was an instrumental player of Police Dar es Salaam.

The fallen star's death, which happened at Upanga in the morning, will deal a big blow to her family and team that is currently contending in the RBA championship.
According her family members, Neema died at Tumaini Hospital due to delivery complications.

This is the second blow for the basketball fraternity within two years after the demise of Jeshi Stars' ace Grace Daudi.

Daudi, who served in various clubs in the region plus the national team for over two decades, died in 2008.

Commenting on the death of Neema, Police Dar es Salaam coach Pascal Nkuba said his team and country at large have lost one of the best players. "It's painful that we've lost her, this is a big loss for my team and Tanzania," he said, adding that it would be difficult to bridge the gap.

Looking upset, Nkuba said: "I was shocked when I received the news of her death, no one expected her to leave us this soon.

"We can't protest God's plans, but the basketball community will cherish her contribution forever," the coach said.

Nkuba said Neema would be laid to rest today at the Kisutu graveyard in Dar es Salaam.
Neema, born on March 13, 1978 in Dodoma, is survived by one son.
 
Mkwasa vows to help Ruvu Shooting avoid relegation Tuesday, 11 January 2011 21:30

Doris Maliyaga
The Citizen Correspondent

Dar es Salaam. Newly appointed Ruvu Shooting head coach Boniface Mkwasa officially got down to work yesterday with a promise to propel the army team to higher heights.

Mkwasa, also the national women's soccer team coach, replaces Fred Felix Minziro, whose fairy tale marriage with Ruvu came to an abrupt end early this month.

His appointment came only hours after the army team's youth team emerged new Under-20 championship kings.
Mkwasa was among those who witnessed Monday's final of the event dubbed "Uhai Cup" between Ruvu Shooting and JKT Ruvu at Karume Stadium. Ruvu Shooting won 2-1.

In an interview with The Citizen yesterday, Mkwasa said he was optimistic Ruvu Shooting will make an impact in the second round of the Premier League, which resumes this weekend.
"It's a big challenge, but I believe I'll manage to turn around the team's fortunes," Mkwasa said.


, the former Young Africans and national team player, said.
Ruvu Shooting are among the relegation-haunted teams, and a glance at the league table suggests they likely to forfeit their Premier League status.

Ruvu Shooting, then under the tutelage of Minziro, wound up their first round campaign with nine points after 11 outings, four points ahead of bottom-placed Arusha's AFC.

For the past one week or so, Ruvu have been camping in Zanzibar under close supervision of assistant coach Seleman Mtunge.
Meanwhile, Sports director Leonard Thadeo says organizing youth competitions is one of the best ways to turn around the country's sports fortunes.

Thadeo said impressive skills displayed by youngsters during the just concluded TFF Under-20 championship, was a clear indication that Tanzania was endowed with abundant talent.

He praised Tanzania Football Federation [TFF] for staging the event and urged other national sports to follow suit.
"It is time other national sports associations cultivated a culture of organizing age-category competitions for young players," he said.
 
Rockets hold on without top scorer to edge out the Celtics Tuesday, 11 January 2011 21:29

Boston. Boston Celtics coach Doc Rivers watched his team lose to the undermanned Houston Rockets and saw trouble coming from far down the road.

Playing without leading scorer Kevin Martin, the Rockets beat Boston 108-102 on Monday to snap a five-game losing streak. Afterward, Rivers lamented his players' lack of effort and warned them to take these regular season games more seriously or risk having a long summer to think about them.

"I've got to somehow figure out a way of getting them to see the urgency of the whole season, and not the single game," Rivers told reporters. "Playing Game Seven on the road … and not just in the finals, if you make it there, but in the playoffs, in the East, which is going to be difficult."

With the loss, Boston (28-9) fell behind the Miami Heat (30-9) for the best record in the Eastern Conference and the potential home-court advantage in the playoffs.

Home-court was crucial in Boston's 2008 championship, but last year the aging Celtics opted to rest up for the postseason instead of chasing the best record. They overcame the disadvantage in beating Cleveland and Orlando in the playoffs before losing Game 7 of the NBA finals to the Lakers in Los Angeles.

With LeBron James and Chris Bosh joining Dwayne Wade in Miami, this season the Celtics can count on more of a struggle within the conference.
"This year's not like last year, where you can coast," Rivers said. "If you don't have home court this year, you could go home."
Aaron Brooks returned from an ankle injury to score 24 points for Houston, hitting a pair of free throws with 18 seconds left after Boston cut a 12-point deficit to four.

Kyle Lowry had 17 with eight assists, Luis Scola scored 12 with nine rebounds and Jordan Hill had 12 points and eight rebounds for the Rockets.

"The guys never folded, never gave them an inch," coach Rick Adelman said. "Every time we come up here we have people out and we end up winning the game. It's nice to see. It just goes to show what you can do when you go out there and bust your tail."

It was the third straight year the Rockets have won in Boston and the third time they have been missing key players: Tracy McGrady in 2009; Yao Ming, Trevor Ariza and Martin last year; and Yao, Martin and Miller this time.
(AFP)
 
Hardy ready for return to the octagon Tuesday, 11 January 2011 21:28

Nottingham. Dan Hardy says he will have a point to prove when he makes his rumoured return to *the octagon.

The Nottingham fighter is believed to be close to signing a contract to lock horns with Anthony Johnson in Seattle on March 26.
The fight looks likely to be the *co-main event of ‘UFC Fight Night 24' – and the 28-year-old knows how *vital the contest will be.
Hardy said: "The fight with ‘Rumble' Johnson in Seattle is the perfect fight for both of us and it makes sense.

"He's coming off a loss and a year lay-off and needs a good win to remind people of what he can do.
"I am coming off a bad loss and have something to prove as well.

"Both of us are *desperate for a win and neither can afford a loss."
‘The Outlaw' Hardy will certainly be *hoping for a change in fortunes after losing his last two contests. He joined the UFC two years ago and opened his account with four consecutive wins, including *victories over Marcus Davis and Mike Swick.

Those successes earned him a *title shot against welterweight *champion Georges St-Pierre, which the *British star lost by a unanimous *decision last March.

He then returned in October and suffered a first-round knockout to Carlos Condit and will now be *looking for an upturn in form against Johnson.

The American will be fighting for the first time since November 2009 after suffering a knee injury that promoted a lengthy recovery time.
A three-fight winning streak – KO wins over Kevin Burns, Luigi Fioravanti and Yoshiyuki Yoshida – came to an end with a submission loss to Josh Koscheck at UFC 106. (AFP)
 

Elisante aanza vema bingwa wa mabingwa


Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 11th January 2011 @ 23:30

MCHEZAJI Gofu Bora wa Mwaka wa zamani, Elisante Lembris ameanza kwa kasi michuano ya Bingwa wa Mabingwa kwenye viwanja vya Klabu ya Gymkhana Moshi, Kilimanjaro jana.

Mchezaji huyo kutoka klabu ya Gymkhana Arusha (AGC) ambaye mwishoni mwa wiki iliyopita alipoteza taji lake la Kombe la Mwenyekiti na pia nafasi ya kuibuka mchezaji bora mara ya pili mfululizo ameanza kwa kasi akionesha nia ya kutaka kuibuka bingwa baada ya kurejea na mikwaju 75.

Michuano hiyo inakutanisha wachezaji walioshinda mataji katika michuano tofauti ya taifa katika kalenda ya Chama cha Gofu Tanzania (TGU) mwaka jana.

Nafasi ya pili katika raundi hiyo ya kwanza wanakabana koo wachezaji watatu kila mmoja akiwa na mikwaju 77 ambao ni Michael Makala kutoka Gymkhana Dar es Salaam (DGC), Jimmy Mollel kutoka AGC na mwenyeji Frank Roman ambaye ni Mchezaji Gofu Bora wa Mwaka 2010.

Mchezaji chipukizi Isaac Anania wa Moshi anafuatia akiwa na mikwaju 78 sawa na Godfrey Leverian wa Morogoro Gymkhana na John Said wa AGC.

Idd Mzaki wa DGC na mwenzake Adam Mwanyeza kila mmoja alirejea na mikwaju 79, wakati
bingwa wa Kombe la Mwenyekiti, chipukizi Nuru Mollel ameanza vibaya kwa kurejea na mikwaju 80 akifuatiwa na Adam Abass wa Moshi 81 na Hamis Ally wa DGC mikwaju 91.

Ally ambaye alishika nafasi ya pili Kombe la Mwenyekiti ikiwa ni mafanikio yake makubwa ya
kwanza kwa zaidi ya mwaka alisema mchezo haukuwa mzuri kwake safari hii.

"Kila kitu kilikuwa kibaya, sina cha kujitetea, nafikiri mchezo umenikataa," alisema.

Michuano hiyo ya siku tatu ya viwanja 54 inaendelea leo na itamalizika kesho ambapo mshindi na Mchezaji Bora wa Mwaka watakabishiwa Kombe.
 
Afande Sele sasa kutoka kama Sugu


na Ruhazi Ruhazi


amka2.gif
MSANII mahiri wa muziki wa kizazi kipya nchini Selemani Msindi ‘Afande Sele' kutoka mkoani Morogoro, ameamua kufuata nyayo za gwiji wa muziki huo Joseph Mbilinyi ‘Mr II au Sugu', kwa kuachia kazi za kijamii zaidi.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu kutoka Morogoro jana, Afande Sele alisema kuwa, Watanzania wamebadilika na sasa wako tayari kwa harakati na wanazipokea hata kupitia muziki.
Kauli hiyo ya Afande Sele imekuja siku chache baada ya Sugu kusema kuwa, muziki atakaoupiga kuanzia sasa utakuwa ule wa harakati na si muziki wa kuburudisha, kwa kuwa Watanzania wengi kwa sasa wana maisha magumu hivyo hawahitaji kuburudishwa.
"Kaka Watanzania wa sasa sio wale wa miaka mitano au kumi iliyopita, hiki ni kizazi kinachoangalia maisha hivyo nimeamua kuwaandalia muziki wa harakati na sio ule wa burudani kama ilivyokuwa zamani," alisema Afande Sele.
Alisema, muziki unaoelekezea matatizo ya wananchi na kusaka ufumbuzi, ndio unaotakiwa kuliko miziki ya aina nyingine ambayo haina tija kwa taifa wala kwa wananchi.
Aidha, Afande Sele alisema harakati zake na wasanii wengine nchini zitakuwa na maana iwapo vyombo vya habari vya moto kama radio na Tv zitawaunga mkono kwa kuzicheza kazi zao badala ya kujikita katika muziki wa kuburudisha.
"Unajua mimi siku zote ninasema magazeti yanafanya kazi vizuri lakini tatizo liko kwenye radio na TV hawa mara nyingi hawatoi kipaumbele kwenye muziki au sanaa yenye tija kwa taifa ndio maana hata wasanii na wanamuziki wengi nchini hawafanikiwa kwa sababu kazi zao zinabaniwa," alisema Afande Sele.


h.sep3.gif

 
Waninga atoka kivyake TOT Plus


na Abdallah Menssah


amka2.gif
MCHARAZAJI mpya wa drums wa TOT Plus, Joseph Waninga, yuko mbioni kukamilisha albamu yake binafsi itakayokuwa na ladha mchanganyiko za zouk, dansi, mchiriku na takeu. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jijini Dar es Salam jana, Waninga alisema kuwa, albamu yake hiyo itakusanya vibao sita, alivyovisifu kwa kudai ni moto wa kuotea mbali.
"Vibao hivyo ni ‘Umasikini', ‘Mtoto Mapepe', ‘Sera za Mapenzi', ‘Haki ya Mtu Haipotei', ‘Mwana Mkiwa' pamoja na moja niliyoimba kwa lugha ya Kimakonde, ‘Kukombwa Asipali Sinu'," alisema Waninga.
Aidha, Waninga alisema kuwa, katika albamu hiyo atawashirikisha pia wasanii wenzake mbalimbali wakongwe na mahiri kama vile; Mhina Panduka ‘Toto Tundu' na nyota wa zamani wa Bongo Star Search, Mrisho Rajab.
Alisema kuwa, albamu hiyo ya kwanza kwa upande wake, itakamilika mwishoni mwa Machi na mwanzoni mwa Aprili itaingia sokoni.



h.sep3.gif

 
Manji aridhia mil. 50/- kumuua mnyama


na Juma Kasesa, Zanzibar


amka2.gif
WAKATI leo ikiandikwa historia kwenye dimba la Amani mjini Zanzibar kwa vigogo vya soka Tanzania, Simba na Yanga kuumana katika fainali ya Mapinduzi Cup, benchi la ufundi la Wanajangwani limeomba kitita cha sh milioni 50 kuhakikisha ushindi unapatikana, ombi lililokubaliwa na mfadhili wao mkuu Yussuf Manji.
Habari za uhakika kutoka ndani ya klabu hiyo zinaeleza kuwa benchi la ufundi limeomba fedha hizo ili kufanikisha ushindi ambao unadaiwa ni muhimu sana kwao kutokana na mambo kadhaa.
Baadhi ya mambo ambayo yanaifanya Yanga ihahe kwa udi na uvumba kuhakikisha inaibuka na ushindi kwao kuwa, leo ni siku ya Mapinduzi ambayo wanadai wana historia nayo, pili jopo la bodi ya wadhamini akiwamo Manji kuwako kuishuhudia mechi hiyo na tatu ni kutomhuzunisha mmoja wa wadhamini wao, Mama Fatma Karume, ambaye marehemu mumewe ndiye mwasisi wa Mapinduzi hayo.
"Baada ya kujadili hali halisi ya mechi ya kesho ‘leo', benchi la ufundi limefanya tathmini na kuomba sh milioni 50 ili kufanikmisha ushindi leo dhidi ya Simba na mfadhili kakubali, hivi karejea Dar mara moja kuhakikisha mambo hayo yanakamilika kisha atarejea kuja kushuhudia fainali leo," kilibainisha chanzo hicho.
Hata hivyo, chanzo hicho hakikuweka hadharani mchanganuo wa matumizi ya fedha hizo katika kufanikisha ushindi katika mechi ya leo.
Akizungumzia mechi ya leo, Kocha wa Yanga, Mserbia Kostadin Papic alisema haiogopi Simba, kwani vijana wake wamefanya mazoezi ya kutosha ingawaje atawakosa nyota wake watano walioko Stars, Nadir Canavaro, Shadrack Nsajigwa, Nurdin Bakari, Jerry Tegete na Stephano Mwasika, pamoja na Abdi Kassim aliyeuzwa Vietnam.
Kwa upande wake, Kocha wa Simba, Mzambia Patrick Phiri alijinasibu kuwa, lazima alipize kisasi cha kufungwa mechi ya mzunguko wa kwanza Ligi Kuu Bara Oktoba 16 mwaka jana jijini Mwanza.
Simba nayo itawakosa nyota wake watano walioko Stars ambao ni kipa Juma Kaseja, Juma Nyoso, Kelvin Yondan, Ahmed Ali Shiboli, na Rashid Gumbo.
Mji wa Zanzibar umepambwa na bendera za timu hizo, kwani pambano linalovuta hisia za mashabiki wengi wa hapa kwani miaka 20 imepita tangu kukutana, mara ya mwisho ikiwa 1992 katika fainali ya klabu bingwa ya Afrika Mashariki ambako Simba ilishinda 7-5, huku David Mwakalebela akikosa penalti muhimu iliyopanguliwa na Tanzania One wa wakati huo, Mohammed Mwameja. Mechi ya leo itaanza saa 2:00 usiku ikiwanguliwa na ile kati ya TASWA FC na Wawakilishi saa 12:00 jioni.
Simba ilifanikiwa kutinga hatua hiyo, baada ya kuiondosha Zanzibar Ocean View kwa mabao 2-1 huku Yanga ikiing'oa Mtibwa Sugar kwa idadi kama hiyo ya mabao.
Bingwa ataondoka donge la sh milioni 5 na kombe lenye thamani y ash milioni 3, huku wa pili akilamba sh milioni 3.
 
Heshima Stars yashuka Misri


na Mwandishi Maalum, Cairo, Misri


amka2.gif
TIMU ya Taifa ya soka ya Tanzania ‘Taifa Stars' ambayo ilikuwa imekwenda kuisaka heshima katika michuano ya nchi za Ukanda wa Mto Nile ‘Nile Basin' jana iliaga rasmi baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Uganda ‘The Cranes' mechi iliyopigwa Uwanja wa Polisi mjini hapa.
Katika mechi hiyo ambayo Stars iliapa kuifunga Cranes ili kufufua matumaini ya kucheza nusu fainali, ilikuwa ya kwanza kujipatia bao dakika ya 24 baada ya Athuman Machupa kupokea kiaina pasi ndefu ya Nizar Khalfan na kuwahadaa mabeki watatu wa Cranes kabla ya kugeuka na kipiga shuti kali la juu lililojaa wavuni.
Stars iliendelea kulisakama lango la Cranes huku wapinzani wao nao wakifanya mashambulizi ya kushtukiza, hadi mapumziko matokeo yalikuwa 1-1.
Kipindi cha pili, Cranes ilibadilika sana kutawala eneo la kati na hivyo kukaribisha mashambulizi ya mara kwa mara na kuzaa kona za mfululizo.
Makosa ya Kocha Jan Poulsen kumtoa mshambuliaji Machupa na kumwingiza Jabir Aziz yalizidi kuidhoofisha Stars na dakika chache baada ya mabadiliko hayo Cranes walisawazisha baada ya beki Stephano Mwasika kushindwa kumkaba mshambuliaji wa Uganda aliyepiga kichwa kikambabatiza na kujaa wavuni.
Mabadiliko mengine aliyoyafanya Poulsen jana ni kumtoa Salum Machaku, Said Maulid ‘SMG' na Shaban Nditi na kuwaingiza Mrisho Ngasa, Idrisa Rajab na Ahmed Ali Shiboli.
 
Uwanja wa Taifa ruksa Ligi Kuu


na Makuburi Ally


amka2.gif
SERIKALI imeruhusu timu za Ligi Kuu Tanzania Bara kuutumia Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara inayotarajiwa kuanza Januari 15, mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Angetile Osiah, alisema uamuzi huo umefikiwa baada ya Uwanja wa Uhuru kufungwa kutokana na matengenezo.
Osiah alisema, hatua ya kuruhusiwa kuutumia Uwanja wa Taifa, imefikiwa jana baada ya kikao kati ya TFF na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
Kabla ya serikali kuruhusu kuutumia Uwanja wa Taifa, michezo ya Ligi Kuu ilikuwa ikichezwa Uwanja wa Uhuru ambao ulifungwa kupisha matengenezo madogo kwa ajili ya kumuapisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete.
Pamoja na suala hilo la kuapishwa katika uwanja huo, lakini serikali imeufunga tena uwanja huo kwa ajili ya matengenezo ya majukwaa uwanjani hapo.
Kwa uamuzi huo wa serikali, sasa kuna uwezekano mkubwa kwa Simba na Yanga ambazo zilikuwa zimechagua viwanja vya CCM Kirumba na Jamhuri Morogoro kurejea jijini ikiwamo mechi yao ya Machi 5.
 
Pigo netiboli, Neema Emmanuel hatunaye


na Tullo Chambo


amka2.gif
HAKIKA ni majonzi kwa familia ya Wananetiboli na wanamichezo kwa ujumla kutokana na kuondokewa na mshambuliaji mahiri, Neema Emmanuel aliyefariki dunia usiku wa kuamkia jana jijini Dar es Salaam.
Habari zilizopatikana kutoka Ofisi ya Michezo ya Jeshi la Polisi Tanzania, marehemu Neema alikutwa na mauti hayo katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es Salaam ambako alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya ujauzito.
PC Neema, mahiri kwa kutumia mkono wa kushoto, aliwahi kung'ara vilivyo na timu za Polisi Tanga kisha Polisi ya Dar es Salaam ambayo alikuwa nayo hadi sasa na timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Queens' alikuwa akimudu vilivyo nafasi za GA na GS, pia alikuwa mahiri katika mpira wa kikapu akiwa na timu yake ya kazini na Mkoa wa Dar es Salaam ‘Dream Teams.
Msiba wa marehemu uko nyumbani kwake Polisi Barracks ambako anatarajiwa kuzikwa leo makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi ameni.
 
TFF yazitaka Yanga, Lyon kumalizana na waliotemwa


na Mwandishi wetu


amka2.gif
KAMATI ya Katiba na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imezitaka timu za Yanga na African Lyon kumalizana na wachezaji wake katika masuala ya mikataba kabla ya hatua ya usajili wa wachezaji msimu ujao.
Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah, alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa Yanga walikuwa na matatizo na wachezaji wake wanne: Wisdom Ndlovu, Steven Marashi, John Njoroge na Ally Msigwa.
Osiah alisema, kamati hiyo ilikutana Desemba 30 mwaka jana na Januari 7, mwaka huu, na vikao hivyo kuhudhuriwa na mchezaji Ally Msigwa pekee, ambaye kamati iliamuru alipwe sh milioni 7.
Aidha Osiah alisema pamoja na kwamba Msigwa ndiye aliyefika katika vikao, Yanga wamewasilisha barua TFF kwamba wanawalipa wachezaji wake Steven Marashi na Wisdom Ndlovu.
Alisema, pamoja na Yanga, pia African Lyon wanatakiwa kuwalipa wachezaji wake Abdul Masenga na Geofrey Komba ambao nao walisitisha mikataba yao, hivyo kutakiwa kuwalipa kila mmoja sh milioni 4.3 kabla ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Osiah alisema mbali na wachezaji hao, pia kutokana na mkanganyiko wa mkataba kati ya African Lyon na Yusuf Soka, ambao ulisababisha kuchelewa kuondoka kwa mchezaji huyo kwenda Sweden kwa ajili ya majaribio katika kituo cha michezo nchini humo, sasa hivi umemalizika.
Katika hatua nyingine, Osiah alisema, baada ya kuanza kwa hatua ya pili ya Ligi Kuu Tanzania Bara, inayotarajia kuanza Januari 15 hakutokuwa na michezo ya kimataifa ya kirafiki kutokana na kalenda yake ya mwaka na kuwataka walioandaa michezo hiyo ndani ya Ligi Kuu kuachana na mipango hiyo.
Osiah alisema, wanaoandaa michezo hiyo walitakiwa kupata baraka za TFF kwa kuanzia vyama vya wilaya na mikoa, kuliko kuandaliwa na mdau mmoja.



 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom