redio
JF-Expert Member
- Aug 27, 2016
- 5,813
- 12,921
Cameroon vs England robo fainali 1990,winga wa cameroon Paul Rose mfede alikosa magoli ya wazi kabisa , England ilisonga mbele kwa goli 3-2 Garry lineker aki ifungia Engand penalty 2 katika muda wa nyongeza. Cameroon ilikua ikiongoza ongoza mbaka dk za 80 na usheeMimi mpaka leo naamini World Cup bora kuiona ni ile ya mwaka 2006. Jinsi Italy walivyopambana mpaka kutwaa taji. Italy ile iliyoundwa na wakongwe kama Luca Toni, Buffon, Pirlo, Materazzi, Del Piero, Canavarro, Zambrotta, Camoranesi na wengineo.
Italy njia aliyopitia mpaka kutwaa ubingwa ilikuwa ngumu sana. Mechi kama ya Nusu Fainali dhidi ya wenyeji Ujerumani ni ya kukumbukwa muda wote.
Pia kuna mechi za kukumbukwa kama robo fainali ya Argentina Vs Ujerumani ambao Argentina aliongoza muda mwingi wa mchezo, kocha wa Argentina alikuja kufanya mistake ya kumtoa Requelme jambo ambalo lilipelekea kuwarudisha mchezoni Ujerumani.
Halafu kuna mechi inajulikana kama Battke of Nuremberg, kati ya Uholanzi Vs Ureno ambapo jumla ya kadi za njano 16 na nyekundu 4 zilitoka.
Hayo ni kwa uchache tu, yote kwa yote World Cup ya 2006 ilikuwa bora sana kwa upande wangu.
Wewe unaikubali ipi na kwanini?
1990 Cameroon ana mfunga Argentia katika mechi ya ufunguzi 1- 0, Argentina yenye Maradona na Canigia tena wachezaji wawili wa Cameroon wakipewa red card. Ukitaka kujua Africa ilikua na wanasoka wenye vipaji basi unge bahatika kuiona ii mechi. Cameroon wali upiga mpira kama hawachezina kigogo cha dunia Chenye Maradona na Canigia. Wakati uo soka bado haijaanza kuitwa football.