Michuano ipi ya World Cup ilikuwa bora sana kuitazama?

Michuano ipi ya World Cup ilikuwa bora sana kuitazama?

Mi nakumbuka yale mashindano yaliyofanyika Korea kusini na Japan ambayo mechi ya kwanza walicheza France vs Senegal na Senegal akashinda moja.

Kilichokuwa kinanikera ni mechi kuchezwa asubuhi tu.

Kumbe wewe ni Katoto ka Juzi
 
Mi nakumbuka yale mashindano yaliyofanyika Korea kusini na Japan ambayo mechi ya kwanza walicheza France vs Senegal na Senegal akashinda moja.

Kilichokuwa kinanikera ni mechi kuchezwa asubuhi tu.
Ninavyokujua wewe kuamka asubuhi na mapema haijawahi kua tatizo kwako, sasa nini kilikua kinakukera mechi kuchezwa muda ule mamii?
 
Kwa kuwa mimi ni muhenga basi sina budi kusema ni ile ya mwaka 1970 Mexico
Wakati Mario Zagalo ndio coach wa Brazil
Duu kina Tostao, Carlos Alberto, Pele, na Revelino
Hiyo ilikuwa ni timu haswa ingawa pia naikumbuka ya South Korea pia ya 2002
Ila msinikosoe kwa kusifia vya zamani maana na nyie itakuja siku mtasema simu ilikuwa iPhone bwana [emoji23]
 
Ninavyokujua wewe kuamka asubuhi na mapema haijawahi kua tatizo kwako, sasa nini kilikua kinakukera mechi kuchezwa muda ule mamii?
Ujue nilikuwa mwanafunzi hapo Ses 🙈🙈 sasa hiyo mida ya mechi ndio naamka kujiandaa kwenda shule au nyingine zinachezwa muda nikiwa shule hivyo nakuwa sizioni hapo. 😀😀
 
Ujue nilikuwa mwanafunzi hapo Ses 🙈🙈 sasa hiyo mida ya mechi ndio naamka kujiandaa kwenda shule au nyingine zinachezwa muda nikiwa shule hivyo nakuwa sizioni hapo. 😀😀
Kumbe ulikua unapitwa na uhondo wa mechi!? Pole sana Shadeeya. Mwaka ule Senegal walipiga mpira mwingi saaana, kina Elhaj Diouf, Khalilu Fadiga(mzee wa cheni), kina Kamara na wengineo

Mimi chama langu Brazil lilikua limetimia haswaa. Kina El Phenomena Ronaldo Lima, Rivaldo, Ronaldinho, Cafu, R. Carlos n.k. utatokea wapi hapo kwa mfano!? Mwisho wa siku Brazil wakatoroka na kombe
 
Kumbe ulikua unapitwa na uhondo wa mechi!?
Ndio. 😀 😀
Pole sana Shadeeya. Mwaka ule Senegal walipiga mpira mwingi saaana, kina Elhaj Diouf, Khalilu Fadiga(mzee wa cheni), kina Kamara na wengineo

Mimi chama langu Brazil lilikua limetimia haswaa. Kina El Phenomena Ronaldo Lima, Rivaldo, Ronaldinho, Cafu, R. Carlos n.k. utatokea wapi hapo kwa mfano!? Mwisho wa siku Brazil wakatoroka na kombe
Kumbe ulikuwa Brazil. Hongera.
 
😀 😀 😀 njano hiyoo. Lol.Yah!!! Na mwaka jana kama sio France kutufunga lile bao moja mechi ya semi finali tulikuwa na kila sababu ya kuchukua ndoo.
Kombe lile linawenyewe Shadeeya na Belgium sio miongoni mwao ujue🤣🤣🤣
 
Kwa kuwa mimi ni muhenga basi sina budi kusema ni ile ya mwaka 1970 Mexico
Wakati Mario Zagalo ndio coach wa Brazil
Duu kina Tostao, Carlos Alberto, Pele, na Revelino
Hiyo ilikuwa ni timu haswa ingawa pia naikumbuka ya South Korea pia ya 2002
Ila msinikosoe kwa kusifia vya zamani maana na nyie itakuja siku mtasema simu ilikuwa iPhone bwana [emoji23]
Kweli wewe muhenga..
 
Naikumbuka ya mwaka 2010 mzee mzima anapata hamu ya kupiga mpira wa kichwa akasahau na kumtwanga Bartez eti katukanwa
 
Kama sijakosea Mali walifika robo au nusu fainali kwenye hizi fainali
Maaaaah weee! We binti wa lini?
Hakuna nchi ya Africa iliyowahi fika nusu fainali.
Na kwa Mwaka huo 2002, Senegal ndiyo walifika robo fainali wakitolewa na uturuki kwa bao la dhahabu.
 
Back
Top Bottom