Midahalo ya Katiba Inayopendekezwa inaendelea saa hizi katika kumbi za makanisa kadhaa

Midahalo ya Katiba Inayopendekezwa inaendelea saa hizi katika kumbi za makanisa kadhaa

Na waisilamu nao wakianza midahalo misikitini tutafika?

sasa wasiposhirikishwa na kuelimishwa, watajuaje kuwa Katiba pendekezwa inakidhi matarajio yao kama wananchi wa taifa hili?

Pia usisahau Katiba ni mali yetu sisi sote, bila kujali imani zetu za dini na itikadi za vyama vya siasa!
 
naipenda Tanzania kuliko wewe, ndiyo maana nasema katiba ya chenge ni mbovu tusiunge mkono. Tuemdelee kutumia hii iliyopo. Mpaka pale mafisadi watakapokubali matkwa ya wanazengo
ila wewe sio mzalendo kabisa ,, samahani kama nitakuwa nimekukera ila sina lugha nyinghine rahisi zaidi ya hiyo


Wewe ndio huna element za uzalendo maana umejaa dharau kwa wtz, huwezi kumtaja mtu mmoja kuwa ndiye aliyehusika kwenye katiba huko ni kufirisika na kuishiwa hoja baba, jipange upya usichafue hali ya hewa hapa!
 
Hongera kwa kwenda kwenye nyumba ya ibada, Mchungaji ni binadamu anaweza kuipelekea nchi yetu na wananchi kupata elimu ya bure ambayo inawaelekeza kwenye mawazo yake. Wanzania tuwe watu wa kuwahoji hawa wanaoleta porojo zao. Watanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayoheshimu na kuzingatia misingi ya utu na udugu, uhuru, kujitegemea, haki, usawa, amani na utulivu, umoja na mshikamano katika nyanja zote za maisha yetu. Tunaamini kuwa misingi hiyo inaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye mfumo wa demokrasia na misingi ya utawala bora ambayo Serikali yake inasimamiwa na Bunge lenye Wabunge waliochaguliwa na wanaowakilisha wananchi. Ungana na Watanzania kutimiza azma ya kupa Katiba Mpya.

Naona umekosea njia. Viongozi wa dini tunawasikiliza zaidi ya tunavyowasikiliza wanasiasa. Viongozi wa dini hawana maslahi binafsi na katiba iliyopendekezwa wakati wanasiasa (hasa CCM), wana maslahi binafsi. Kwa kifupi, katiba hii ya Sitta na Chenge, ni hapana.

Tiba
 
Siwezi ikubali katiba iliyoandikwa na mwizi chenge.

wewe una hoja ya msingi kuipigia kura ya HAPANA Katiba Inayopendekezwa!

Ila nachelea kuweka bayana kuwa, mamilioni ya wapiga kura waliojiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura wataburuzwa kupiga kura ya NDIO! Bahati mbaya muda wa kuboresha hilo daftari hautoshi, hivyo tutalazimika kutumia daftari lililopo sasa!

za mbayuwayu.....changanya na za kwako!!!!!
 
umaanisha katiba inayoruhusu uchumi wa nchi kuhujumiwa, ndiyo ipitishwe na wananchi,, sio!!!
unamaanisha wabunge wale wenye sifa ya kujua kusoma na kuandika,, sio!!!!
tena wale ambao wakichaguliwa hawawezi wajibishwa na waliowachagua,, sio!!!
tena wale ambao hawana ukomo wa kukaa madarakani, eti mtu ni mbunge miaka 45,, sio!!!
tena wale ambao wakichaguuliwa wanahamia DSM,, sio!!!
tena wale ambao wanajali matumbo yao, kazi zao anafanya diwani, anayelipwa kiduchu,,,sioo!!!
unamaanisha ile ambayo itaendelea kuruhusu Rais wa nchi kuigeuza mikutano ya serikali kuwa ya chama tawala,, sio!!
KAWADANGANYE WENGINE SIO MIMI,
najitambua


Heee Mwakaboko kwa hili umeishiwa kama unafikiri Katiba ndiyo inayokwenda kupiga kura na kukuchagulia wabunge na viongozi wako nakupa pole!najua huelewi unachokifanya hata huyo mbunge unayetaka kumwajibisha akikosea utajikuta ndani ya miaka 5 una wabunge 10 jinsi navyokuona umejaa hasira, visasi na kutokuamini maamuzi yako, fikiri kwanza kabla ya kuongea.
 
heri yako wewe umebahatika kuisoma, mamilioni ya watanzania hawajaiona wala hawaijui rangi yake, na hawataiona hiyo Katiba pendekezwa hadi siku ya kupiga kura ya maoni, tena si kwa bahati mbaya bali ni mkakati maalum wa watawala kutumia kanuni ya 'wajinga watawale'



Ha ha ha ha yaani humu kuna wachangiaji wengine ni vituko, hivi hayo mamilioni ya WTZ unayoyasema ni yapi?ni akina nani hao nitajie maeneo 10 ambayo katiba haijapelekwa, kama wewe hukuisoma wewe usiudanganye umma!!! eti hata rangi yake hawaijui????? hujielewi wewe acha dharau.
 
Naona umekosea njia. Viongozi wa dini tunawasikiliza zaidi ya tunavyowasikiliza wanasiasa. Viongozi wa dini hawana maslahi binafsi na katiba iliyopendekezwa wakati wanasiasa (hasa CCM), wana maslahi binafsi. Kwa kifupi, katiba hii ya Sitta na Chenge, ni hapana.

Tiba

Acha kuwa mburula wewe unayoyasema yangekuwa yanafanyika maovu yangeendelea???na wasi wasi na wewe na hao wchumia tumbo unaowatetea badala ya kuhubiri injili watua waache dhambi na kumgeukia Mungu mnaanza kuwaamulia watu namna ya kupiga kura na tena mnawakataza hivi hayo Mamlaka mmeyapata wapi? au kwa BELZEBULI???maana hata siwaelewi nyumba za ibada mnazigeuza kuwa kumbi za midahalo ha ha ha ha ha nyie WAGALATIA.
 
Heee Mwakaboko kwa hili umeishiwa kama unafikiri Katiba ndiyo inayokwenda kupiga kura na kukuchagulia wabunge na viongozi wako nakupa pole!najua huelewi unachokifanya hata huyo mbunge unayetaka kumwajibisha akikosea utajikuta ndani ya miaka 5 una wabunge 10 jinsi navyokuona umejaa hasira, visasi na kutokuamini maamuzi yako, fikiri kwanza kabla ya kuongea.
Ila inayoruhusu uchumi wa nchi kuhujumiwa wewe unao iko poa, mbunge kukaa madarakani miaka 45 as if hakuna Watz wengine wenye uwezo unaona poa tena anapata wadhifa huo kwa njia za rushwa, Ndiyo maana Noran anatucheka
 
Acha kuwa mburula wewe unayoyasema yangekuwa yanafanyika maovu yangeendelea???na wasi wasi na wewe na hao wchumia tumbo unaowatetea badala ya kuhubiri injili watua waache dhambi na kumgeukia Mungu mnaanza kuwaamulia watu namna ya kupiga kura na tena mnawakataza hivi hayo Mamlaka mmeyapata wapi? au kwa BELZEBULI???maana hata siwaelewi nyumba za ibada mnazigeuza kuwa kumbi za midahalo ha ha ha ha ha nyie WAGALATIA.
Hao unaowasema hapa vibaya, Idd Amin, yeye alienda hatua ya mbali zaidi kwa kuwaua kabisa. Lakini miezi kadhaa baadaye Mungu aliinua Taifa Tukufu Mbele za Mungu la Tanzania kumuondoa madarakani. Hao wamepakwa mafuta na Bwana, tunawaheshimu kuliko maelezo. Ila wewe endelea kula mpunga
 
Wewe ndio huna element za uzalendo maana umejaa dharau kwa wtz, huwezi kumtaja mtu mmoja kuwa ndiye aliyehusika kwenye katiba huko ni kufirisika na kuishiwa hoja baba, jipange upya usichafue hali ya hewa hapa!
Unaonesha dhahiri kuwa wewe ni mgeni katika nchi hii. Pole kwa kukugusa eneo ambalo hulipendi, ni ukweli ulio dhahiri kuwa wewe sio mzalendo kwa Taifa letu, mawazo kama haya ya kiovu hayawezi toka kwa mzalando bali kwa wasio litakia mema taifa letu zuri. Unaunga mkono wizi wa raslimali za nchi halafu unajiita mzalendo, this is very strange to me, can't you learn from the past!!!
 
Mtoa mada ni vizuri wakati unaongea ujue unaongelea nini? Watanzania tunasifa ya kutokujua chochote, kutokujali na kutokuelekezana kwa hiyo tukiwa na ujinga tunaambukizana nchi nzima. Mimi ninemelikataa hilo na sitaki kuwa mmoja wenu kwa kujiambukiza ujinga. Please note maana ya neno mdahalo na matumizi yake. Hicho ulichokieleza hapa sio mdahalo na hivyo hata maana unayotaka kuikusudia hapa haieleweki kabisa na watu tulio na akili timamu bila kujali itikiadi zetu za kidini
 
Heee kweli hii kali ya mwaka yaani mnashikiwa akili kiasi hicho?mnaamuliwa mambo yenu ya msingi na mtu mmoja?mmeshindwa kusoma mkaamua wenyewe?halafu mnachekelea?nyie kumbe hata mkiambiwa muanze kula majani mpate miujiza mnaweza kula bila woga maana uwezo wenu wa kufikiri umefikia mwisho kweli mwisho wa dunia umekaribia mna masikio lakini hayasikii, mna macho lakini hayaoni mmekua kama wagalatia sio bure mmeshalogwa nyie!!!!!!!

Hata kama ukiwatukana Wakristo wote pamoja na viongozi wao wote. Kweli ya Mungu itasimama daima. Remember the sons of darkness will not overpower the sons of light. the sons of light will light and hold the candles in every room and the light will consume the darkness, at the end of the day you will have no where to hide, Remember the light that was lit at Calvary, several people even famous ones have tried to put it down, but failed. Hata kabla ya kwenda kanisani I had already made up my decision about the Katiba. Huwa siamuriwi na mtu, bali napima maelezo yanayotolewa na kuona kama yana ukweli ndani yake. Maelekezo ya maaskofu yana ukweli ndani yake. Kataa kubali, huo ndiyo ukweli.

WEWE NI MTUMWA, MIMI MTU HURU
 
Mungu amenipa nafasi leo nimeenda Kanisani, wakati matangazo ulipofika Waraka wa Maskofu wetu ukasomwa. Halafu Mchungaji wetu akatoa elimu ya bure kuhusu katiba hii pendekezwa. Hatimaye akasema tuipe kura za hapana. Akasisitiza maoni ya msingi ambayo wananchi waliyatoa, wajanja wameyatoa ili kulinda maslahi yao na uroho wao wa madaraka. Kila mwenye kuwaza vizuri na kuitakia mema nchi yetu nzuri yenye kila kitu kilichopo katika uso wa nchi, mwenye kupinga uchumi wa nchi kuhamishwa kijanja kijanja, bila shaka ataungana na viongozi wa dini kusema hapana kwa katiba pendekezwa

Safi sana!! Ila Kadinali katufikirisha sana hata kama ni maoni yake binafsi!!!
 
Acha kuwa mburula wewe unayoyasema yangekuwa yanafanyika maovu yangeendelea???na wasi wasi na wewe na hao wchumia tumbo unaowatetea badala ya kuhubiri injili watua waache dhambi na kumgeukia Mungu mnaanza kuwaamulia watu namna ya kupiga kura na tena mnawakataza hivi hayo Mamlaka mmeyapata wapi? au kwa BELZEBULI???maana hata siwaelewi nyumba za ibada mnazigeuza kuwa kumbi za midahalo ha ha ha ha ha nyie WAGALATIA.

Wewe unaweza kutukana kama unavyoweza kwa kuwa hicho ndicho unacholipwa kukifanya lakini ukweli unabaki pale pale kwamba katiba iliyotungwa na mafisadi hatuwezi kuipigia kura ya ndio. Huo ndio ukweli. Tena washauri Mabwana zako hii kitu waifute kabisa kama hawataki aibu.

Tiba
 
heri yako wewe umebahatika kuisoma, mamilioni ya watanzania hawajaiona wala hawaijui rangi yake, na hawataiona hiyo Katiba pendekezwa hadi siku ya kupiga kura ya maoni, tena si kwa bahati mbaya bali ni mkakati maalum wa watawala kutumia kanuni ya 'wajinga watawale'

Kwakeli unamatatizo wewe unayejiita President Elect, kwanini unaweka vikwazo? Eti “watanzania hawataiona hiyo Katiba pendekezwa hadi siku ya kupiga kura ya maoni”

Usiwe muongo na kuwaongopea Watanzania kwa hilo. Uwe muungwana. Acha tabia yako ya kuwa na maneno yasiyo na msingi wowote. Cha msingi kwa sasa ni kuwasisitiza
Wananchi kuwa ni muhimu waisome na kuielewe Katiba Inayopendekezwa ili kufanya uamuzi sahihi wakati wa upigaji kura ya maoni kulingana na ratiba ilivyopangwa.
 
umaanisha katiba inayoruhusu uchumi wa nchi kuhujumiwa, ndiyo ipitishwe na wananchi,, sio!!!
Unamaanisha wabunge wale wenye sifa ya kujua kusoma na kuandika,, sio!!!!
Tena wale ambao wakichaguliwa hawawezi wajibishwa na waliowachagua,, sio!!!
Tena wale ambao hawana ukomo wa kukaa madarakani, eti mtu ni mbunge miaka 45,, sio!!!
Tena wale ambao wakichaguuliwa wanahamia dsm,, sio!!!
Tena wale ambao wanajali matumbo yao, kazi zao anafanya diwani, anayelipwa kiduchu,,,sioo!!!
Unamaanisha ile ambayo itaendelea kuruhusu rais wa nchi kuigeuza mikutano ya serikali kuwa ya chama tawala,, sio!!
Kawadanganye wengine sio mimi,
najitambua

wewe hujitambui, ni vema ungeisoma ukaangalia kati ya hayo uloyataja hapo yamo? Yako sehemu gani? Acha kudanganya watu bhana, kuwa mzalendo.
 
Wewe unaweza kutukana kama unavyoweza kwa kuwa hicho ndicho unacholipwa kukifanya lakini ukweli unabaki pale pale kwamba katiba iliyotungwa na mafisadi hatuwezi kuipigia kura ya ndio. Huo ndio ukweli. Tena washauri Mabwana zako hii kitu waifute kabisa kama hawataki aibu.

Tiba

Kelele za Chura hazimzuii tembo kunywa maji, we ombea tu mabaya juu ya Katiba hii Inyaopendekezwa lakini hakika nakuambia kwa uweza wa Mola hii itapita na itakukuta aibu kubwa wewe na wenzio wote mnaoipinga kwasababu itafika wakati itakubidi uiheshimu kwani ni Sheria Mama.
 
Hata kama ukiwatukana Wakristo wote pamoja na viongozi wao wote. Kweli ya Mungu itasimama daima. Remember the sons of darkness will not overpower the sons of light. the sons of light will light and hold the candles in every room and the light will consume the darkness, at the end of the day you will have no where to hide, Remember the light that was lit at Calvary, several people even famous ones have tried to put it down, but failed. Hata kabla ya kwenda kanisani I had already made up my decision about the Katiba. Huwa siamuriwi na mtu, bali napima maelezo yanayotolewa na kuona kama yana ukweli ndani yake. Maelekezo ya maaskofu yana ukweli ndani yake. Kataa kubali, huo ndiyo ukweli.

WEWE NI MTUMWA, MIMI MTU HURU

We ni mtumwa wa ubishi kama mbogo.
 
Back
Top Bottom