Midahalo ya wagombea urais kuelekea Uchaguzi Mkuu 2020

Midahalo ya wagombea urais kuelekea Uchaguzi Mkuu 2020

Nyani Ngabu,
Hii hoja yako Ina mashiko.
Mie nashauri mdahalo uwe wa Kiingereza ili kuwapa viewers wote including foreigners kujua Tanzania inaweza kuongoza na mtu mwenye uelewa wa maswala kwa kiwango gani....!!!
1995 nilishuhudia mdahalo huo na kiukweli Marehemu Mkapa was the right candidate.

Mwaka huu wa 2020 nategemea kuona list ifuatayo kwenye Mdahalo huo:
  1. John Pombe Magufuli...CCM.
  2. Bernad Callius Membe....ACT.
  3. Tundu Antipas Lissu-CHADEMA.
  4. Ibrahim Haruna Lipumba- CUF.
Angalizo kwa waandaji :LUGHA NI UNG'ENG'E.
Kwa KINGE Le profeseli na "MTU FURANI" wataogopa kushiriki maana KINGE kwao mtihani yaani cha UGOKO.
 
Naunga mkono hoja.
Huu ndo ulikuwa muda muafaka kwa vyombo vya habari kama ITV ambao wana footage ya matukio mengi ya zamani kuringa na kujimwambafy kwa kutuonyesha zile 'rare' walizokuwa nazo!
 
Hata Waandishi wa wakati huo walikuwa heavy weight sio hawa wa siku hz habari mwanzo mwisho ni '…kwa mujibu…inaaminika…' no facts
Kabla ya hapo watu wengi walikuwa wanadhani Mkapa ni ‘lightweight’ kwa sababu bungeni hakuwa mchangiaji machachari wa hoja.
 
Mwishoni mwa juma lililopita nilileta mada hapa jukwaani kuhusu Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Bw. Thabo Mbeki, alivyomkumbuka hayati Rais mstaafu Benjamin Mkapa.

Kwenye bandiko hilo, nami nikatoa maneno mawili matatu kumhusu Rais huyo mstaafu Mkapa, kwa jinsi nilivyomjua mimi, kiumbali.

Moja ya mambo niliyoyakumbuka ni ule mdahalo wa wagombea urais wa mwaka 1995 ambapo ndo ulikuwa uchaguzi wa kwanza katika kurudi kwenye mfumo wa vyama vingi.

Nilisema hivi kuhusu ushiriki wa Rais Mkapa kwenye huo mdahalo:
View attachment 1522615

Hilo bandiko linapatikana hapa.

Siku chache baadaye, mwenzetu Bw. Pascal Mayalla akaleta makala ya January Makamba, ya kumkumbuka marehemu rais huyo mstaafu.

Moja ya mambo ambayo Bw. Makamba aliyazungumzia, ulikuwa ni ule mdahalo wa wagombea urais wa mwaka 1995, mdahalo ambao nadhani ndiyo uliomtambulisha vizuri Rais Mkapa kwa umma wa Watanzania.

Katika kumbukumbu yangu, mimi nilisema Rais Mkapa alifanya vizuri sana kwenye huo mdahalo. Licha ya kwamba hakuna kipimo sahihi cha kupima na kuona yupi alishinda, kwa maoni yangu, Rais Mkapa alishinda mdahalo ule.

Na kwa maoni pia ya January Makamba, nadhani ni sahihi pia nikisema hata yeye January aliona kuwa Mkapa alishinda.

Yeye Bw. Makamba alisema hivi:

View attachment 1522626

Kusoma zaidi alichokiandika Bw. Makamba, bofya hapa.

Tokea mwaka huo wa ‘95, nadhani hatujawahi tena kuwa na mdahalo wa kitaifa wa wagombea urais.

Ningependa sana mwaka huu wa uchaguzi tuwe na mdahalo wa wagombea hiyo nafasi. Ila, sitashikilia pumzi yangu kusubiri hilo kutokea.

Lakini pia, nimeona si vibaya kuleta ombi/ wazo hili hapa.

Ombi ama wazo lenyewe ni kuipata video ya mdahalo wa ‘95.

Nimezunguka sana mtandaoni na huko YouTube, lakini nimeambulia patupu.

Pascal Mayalla wewe ni mwandishi wa habari wa muda mrefu. Naamini bado una uhusiano na watu waliomo kwenye vyumba vya habari vya vyombo vya habari hapa.

Sikumbuki vizuri ni stesheni zipi za runinga ambazo zilirusha matangazo ya ule mdahalo. CTN? ITV? DTV? Radio One labda?

Sasa Bw. Mayalla, unaweza kutumia uzoefu na nyenzo zako ulizonazo kututafutia video [au hata audio] ya huo mdahalo?

Mimi si muangaliaji sana wala si mfuatiliaji sana wa stesheni za runinga za hapa Tanzania. Ila kama kuna stesheni ambazo labda zina chaneli huko kwenye YouTube, zinaweza kuipandisha video ya huo mdahalo kwa faida ya umma.

Kama inawezekana, tusaidie Bw. Mayalla...

Shukran jazilan na ahlan wa sahlan.
Mdahalo ukifanywa kwa kingereza utapendeza zaidi,

Lakini Yule ataukimbia tu!
 
Midahalo ajabu mtu mwingine utasikia Ohhh ifanyike kingereza kwa Nini isiwe kwa kifaransa? Lugha kuu zinazoongoza duniani Ni kingereza na kifaransa kwa Nini wengi wakomae kutaka kingereza tu?
PhD ya korosho chali
 
Mwishoni mwa juma lililopita nilileta mada hapa jukwaani kuhusu Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Bw. Thabo Mbeki, alivyomkumbuka hayati Rais mstaafu Benjamin Mkapa.

Kwenye bandiko hilo, nami nikatoa maneno mawili matatu kumhusu Rais huyo mstaafu Mkapa, kwa jinsi nilivyomjua mimi, kiumbali.

Moja ya mambo niliyoyakumbuka ni ule mdahalo wa wagombea urais wa mwaka 1995 ambapo ndo ulikuwa uchaguzi wa kwanza katika kurudi kwenye mfumo wa vyama vingi.

Nilisema hivi kuhusu ushiriki wa Rais Mkapa kwenye huo mdahalo:
View attachment 1522615

Hilo bandiko linapatikana hapa.

Siku chache baadaye, mwenzetu Bw. Pascal Mayalla akaleta makala ya January Makamba, ya kumkumbuka marehemu rais huyo mstaafu.

Moja ya mambo ambayo Bw. Makamba aliyazungumzia, ulikuwa ni ule mdahalo wa wagombea urais wa mwaka 1995, mdahalo ambao nadhani ndiyo uliomtambulisha vizuri Rais Mkapa kwa umma wa Watanzania.

Katika kumbukumbu yangu, mimi nilisema Rais Mkapa alifanya vizuri sana kwenye huo mdahalo. Licha ya kwamba hakuna kipimo sahihi cha kupima na kuona yupi alishinda, kwa maoni yangu, Rais Mkapa alishinda mdahalo ule.

Na kwa maoni pia ya January Makamba, nadhani ni sahihi pia nikisema hata yeye January aliona kuwa Mkapa alishinda.

Yeye Bw. Makamba alisema hivi:

View attachment 1522626

Kusoma zaidi alichokiandika Bw. Makamba, bofya hapa.

Tokea mwaka huo wa ‘95, nadhani hatujawahi tena kuwa na mdahalo wa kitaifa wa wagombea urais.

Ningependa sana mwaka huu wa uchaguzi tuwe na mdahalo wa wagombea hiyo nafasi. Ila, sitashikilia pumzi yangu kusubiri hilo kutokea.

Lakini pia, nimeona si vibaya kuleta ombi/ wazo hili hapa.

Ombi ama wazo lenyewe ni kuipata video ya mdahalo wa ‘95.

Nimezunguka sana mtandaoni na huko YouTube, lakini nimeambulia patupu.

Pascal Mayalla wewe ni mwandishi wa habari wa muda mrefu. Naamini bado una uhusiano na watu waliomo kwenye vyumba vya habari vya vyombo vya habari hapa.

Sikumbuki vizuri ni stesheni zipi za runinga ambazo zilirusha matangazo ya ule mdahalo. CTN? ITV? DTV? Radio One labda?

Sasa Bw. Mayalla, unaweza kutumia uzoefu na nyenzo zako ulizonazo kututafutia video [au hata audio] ya huo mdahalo?

Mimi si muangaliaji sana wala si mfuatiliaji sana wa stesheni za runinga za hapa Tanzania. Ila kama kuna stesheni ambazo labda zina chaneli huko kwenye YouTube, zinaweza kuipandisha video ya huo mdahalo kwa faida ya umma.

Kama inawezekana, tusaidie Bw. Mayalla...

Shukran jazilan na ahlan wa sahlan.
Kwenye huo mdahalo unayotaka ccm itawakilishwa na Mr.Catalyst? Huwezi kuwa serious
 
Mwishoni mwa juma lililopita nilileta mada hapa jukwaani kuhusu Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Bw. Thabo Mbeki, alivyomkumbuka hayati Rais mstaafu Benjamin Mkapa.

Kwenye bandiko hilo, nami nikatoa maneno mawili matatu kumhusu Rais huyo mstaafu Mkapa, kwa jinsi nilivyomjua mimi, kiumbali.

Moja ya mambo niliyoyakumbuka ni ule mdahalo wa wagombea urais wa mwaka 1995 ambapo ndo ulikuwa uchaguzi wa kwanza katika kurudi kwenye mfumo wa vyama vingi.

Nilisema hivi kuhusu ushiriki wa Rais Mkapa kwenye huo mdahalo:
View attachment 1522615

Hilo bandiko linapatikana hapa.

Siku chache baadaye, mwenzetu Bw. Pascal Mayalla akaleta makala ya January Makamba, ya kumkumbuka marehemu rais huyo mstaafu.

Moja ya mambo ambayo Bw. Makamba aliyazungumzia, ulikuwa ni ule mdahalo wa wagombea urais wa mwaka 1995, mdahalo ambao nadhani ndiyo uliomtambulisha vizuri Rais Mkapa kwa umma wa Watanzania.

Katika kumbukumbu yangu, mimi nilisema Rais Mkapa alifanya vizuri sana kwenye huo mdahalo. Licha ya kwamba hakuna kipimo sahihi cha kupima na kuona yupi alishinda, kwa maoni yangu, Rais Mkapa alishinda mdahalo ule.

Na kwa maoni pia ya January Makamba, nadhani ni sahihi pia nikisema hata yeye January aliona kuwa Mkapa alishinda.

Yeye Bw. Makamba alisema hivi:

View attachment 1522626

Kusoma zaidi alichokiandika Bw. Makamba, bofya hapa.

Tokea mwaka huo wa ‘95, nadhani hatujawahi tena kuwa na mdahalo wa kitaifa wa wagombea urais.

Ningependa sana mwaka huu wa uchaguzi tuwe na mdahalo wa wagombea hiyo nafasi. Ila, sitashikilia pumzi yangu kusubiri hilo kutokea.

Lakini pia, nimeona si vibaya kuleta ombi/ wazo hili hapa.

Ombi ama wazo lenyewe ni kuipata video ya mdahalo wa ‘95.

Nimezunguka sana mtandaoni na huko YouTube, lakini nimeambulia patupu.

Pascal Mayalla wewe ni mwandishi wa habari wa muda mrefu. Naamini bado una uhusiano na watu waliomo kwenye vyumba vya habari vya vyombo vya habari hapa.

Sikumbuki vizuri ni stesheni zipi za runinga ambazo zilirusha matangazo ya ule mdahalo. CTN? ITV? DTV? Radio One labda?

Sasa Bw. Mayalla, unaweza kutumia uzoefu na nyenzo zako ulizonazo kututafutia video [au hata audio] ya huo mdahalo?

Mimi si muangaliaji sana wala si mfuatiliaji sana wa stesheni za runinga za hapa Tanzania. Ila kama kuna stesheni ambazo labda zina chaneli huko kwenye YouTube, zinaweza kuipandisha video ya huo mdahalo kwa faida ya umma.

Kama inawezekana, tusaidie Bw. Mayalla...

Shukran jazilan na ahlan wa sahlan.
Kuna mgombea mmoja wa chama kikubwa nchini alimkimbia mwandishi wa habari wa BBC yule dada Zuhura Yunus, ila mwenzake
Lowasa alijitia kichwa ngumu kufanyia mahojiano, alipopigwa maswali mawili matatu akaanza kulalamika eti Zuhura anamuonea.
 
Nasikia Joe Biden pamoja na kuongoza kwenye polls nyingi lakini anataka kusepa mdahalo na Trump kwa kisingizio cha Covid19 na Trump kutotoa taarifa zake za Kodi. Sasa sisi tunao jifunza demokrasia tutaweza hayo mambo ya midahalo Kama wanao jiita wanademokrasia wanafanya hayo.
 
Mgombea Wa kwanza kulala Mbele atakuwa mgombea Wa ccm has a mkisema lugha Ni kizungu
 
Nasikia Joe Biden pamoja na kuongoza kwenye polls nyingi lakini anataka kusepa mdahalo na Trump kwa kisingizio cha Covid19 na Trump kutotoa taarifa zake za Kodi. Sasa sisi tunao jifunza demokrasia tutaweza hayo mambo ya midahalo Kama wanao jiita wanademokrasia wanafanya hayo.
Na kwanini mnapenda kuiga mambo ya kipumbavu na yasiyo na tija, badala ya kuiga mambo yenye manufaaa.
 
CCM huwa hatutaki midahalo ya wagombea Uraisi sababu wapiga kura wengi asilimia 80 wanaishi vijijini na wengi hawana TV Wala Radio Wala mitandao ya kijamii tofauti na ulaya na Marekani hata hao wa mjini Ni wachache Wana TV na Radio na huingia mitandao ya kijamii

Na Ni useless sababu wengi wenye TV na waingia mitandao ya kijamii huwa hawaendi kupiga kura huwa wako tu majumbani wanafuatilia uchaguzi wakiwa kwenye sofa set zao!!

CCM tunaenda waliko wapiga kura ndio maana ofisi za CCM ziko kila Kijiji na kila mtaa na ziko active tofauti na vyama vingine
Na hii ndio silaha yetu ya ushindi...ujinga,ujinga,ujinga!
 
CCM huwa hatutaki midahalo ya wagombea Uraisi sababu wapiga kura wengi asilimia 80 wanaishi vijijini na wengi hawana TV Wala Radio Wala mitandao ya kijamii tofauti na ulaya na Marekani hata hao wa mjini Ni wachache Wana TV na Radio na huingia mitandao ya kijamii

Na Ni useless sababu wengi wenye TV na waingia mitandao ya kijamii huwa hawaendi kupiga kura huwa wako tu majumbani wanafuatilia uchaguzi wakiwa kwenye sofa set zao!!

CCM tunaenda waliko wapiga kura ndio maana ofisi za CCM ziko kila Kijiji na kila mtaa na ziko active tofauti na vyama vingine



Hoja Dhaifu kabisa

Mbona mnanunua Vyombo vya Muziki na Kwenda na wasanii wengi kwenye Campeni,Je hamtambui nafasi ya Viziwi huko????

Mbona Press conference na mikutano ya NEC mnarusha live,Je huwa hamjui kuwa Vijijini hakuna TV Wala Radio??

Mdahalo ni Unatupa fursa ya kuwapima wagombea wetu kwa kina,lakini pia ni indication nzuri ya Uwepo wa Demokrasia,kwa mantiki hiyo na Unga hoja mkono
 
Mdahalo huo labda uwahisishe wagombea urais wa vyama vingine lkn siyo ccm. Kwasabb kwa namna mgombea wa ccm alivyo mzito kuongea na jinsi asivyojua kupangiilia hoja hawezi kukubali aibu imfike.
 
Mdahalo uendeshwe kwa lugha ya mabeberu....awepo Membe..Lissu na Jiwe
 
Back
Top Bottom