Mifumo ya kidunia ilishaamua mwanaume aishi kwa kukandamizwa na kufanyiwa ulaghai/ udanganyifu

Hii inaweza isitokee mapema kwasababu dunia hii idadi ya watu ishakuwa kubwa hesabu zinataka tupungue kwa usalama wa baadae, kwahiyo wataona bora wanaume tuwe wachache ili uzao uwe kidogo
Ni kweli. Tunaongelea mambo ya mamiaka na miaka yajayo baada ya kutokea mambo mengi mno. Hili si suala la wewe au wajukuu kushuhudia. Tutakachoshuhudia ni jinsi tunavyoilazimisha nature kufanya maamuzi.
 
Suala la kuongezeka kwa single mothers nalo limeshamili sana sasa hivi. yaani sasa hivi kila binti ana mtoto wengine wamepeleka watoto mikoani uko kwa bibi zao ili wapate uhuru wa kudanga.
 
Mkuu ulimwengu una muingiliano mkubwa sana kwa sasa uyo mwanamke ana smartphone, anaangalia tv, ana mashoga zake n.k hata akiwa mtiifu kwako hakuna guarantee ya kusema atabaki kuwa ivyo ivyo siku zote
 
Naona kama kuna kitu kinakung'ang'ania kichwani.. Tumalize hivi both administrative na leadership skills zina matter..Muhimu zisizidiane .
 
Ushauri wangu upo hapo kwenye aya nne za mwisho
Wanawake wa mwanzo waanzilishi wa kudai haki za wanawake walielewa kuwa mabadiliko hayahitaji lelemama, wakatengeneza platform ya kusikika, kwa kuanza wakaanza na hatua kubwa sana yakuweka mkutano Beijing, wapaze sauti wapate kusikika ulimwenguni. Hata hivyo haikuwa rahisi wakapewa majina ya kila aina.

Now, mabadiliko ya hizo sheria hamuwezi kuyapata kwa kuandika JF, Y’all need to act, mtumie mifumo kumanipulate changes etc etc. Ni wakati wenu sasa wa kudai usawa, if at all mnaona mnaonewa.
 
Sikatai mwanamke kupewa haki. Kinacholeta mkanganyiko ni hii kasumba ya wanawake kuwa vigeugeu. Wanataka usawa kwa sababu ya 50/50 ni kitu kizuri hakina shida ila lazima utambue kwamba usawa unakuja na wajibu yaani kama zamani ulikua unawekwa kando kwenye suala la ajira na kusubiri kuhudumiwa na mwanaume sasa hivi umepewa nafasi kwenye kinyang'anyiro cha ajira maana yake lile takwa la mwanaume kukuhudumia litaondolewa. Sasa mwanamke anataka usawa kwa kigezo cha 50/50 lakini zile privelages alizokua anazipata kutoka kwa mwanaume including kuhudumiwa hataki kuziachia ndipo hapa harakati za 50/50 zinaonekana ubabaishaji fulani tu wa kutaka mseleleko.
 
Great thinker! Congrat mkuu.... Jinsia ya kiume ina vita sana. Mashoga yote ni sera ya 50/50.
 
Mimi naamini kama jambo kwenye jamii watu hawalifurahii basi watatafuta kila namna ya kuliondoa, ukiona watu hawataki kuhangaika kuliondoa au jukumu la kuliondoa wanaisakizia jinsia nyingine wakati ni wao ndio wanaolalamika, basi ujue hao watu hawako serious na hawana haki ya kumlaumu yeyote sababu wana uwezo wa kuchukua hatua ila wameamua kutegeana na kushindana
 
Wewe ndio umeandika ukweli, ndio maana mimi huwa siwaamini wanaume wanaolalamika na kusema wao ndio wana jukumu kubwa na zito kuliko wanawake, jukumu lenyewe eti kutafuta pesa tu ambalo siku hizi wanawake wengi nao wanalifanya na huku wana ya kwao mengine yanawasubiri ambayo wanaume wengi hawataki kuyagusa
 
Ishu sio kutafuta pesa ishu ni kukubaliana nani anawajibika ku-provide monetary expenses katika ndoa/mahusiano. Wanawake wamepewa access zote za kujipambambania kama elimu, kumiliki mali, kufanya biashara, nafasi ya uongozi kisiasa n.k lakini linapokuja suala la ku-provide monetary expenses bado wanaamini ilo ni jukumu la mwanaume peke ake.
 
Kikubwa ni sisi wanaume kukaa pembeni kimnya na kuulinda uanaume wetu kimnya kimnya, tuwaache waharibu watengeneze mfumo jike usio na maana yeyote alafu baadae watakuja na mbinu mpya za kurudisha, kulinda na kuupambania mfumo dume kwa haraka sana.

Nb: mwanake hana haki ya kuwa sawa na mwanaume kupitia mfumo wao wa 50/50 mwanaume yupo juu maradufu na wakitaka kujua hili wa wapime wanawake kwenye natural disasters mfano mafuriko watapata majibu sahihi mwanamke ni nani.
 
Naunga mkono hoja mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…