Mika Mwamba ndiye Producer mwenye uwezo mkubwa wa kutengeneza beats kali kuwahi kutokea kwenye historia ya Bongofleva

Mika Mwamba ndiye Producer mwenye uwezo mkubwa wa kutengeneza beats kali kuwahi kutokea kwenye historia ya Bongofleva

Nichangie kidogo hapo maana pia nimezaliwa kitambo na naujua muziki wa enzi hizo japo mie sio msanii
Ila msanii wa zamani anaposema muziki wa zamani ulikuwa haulipi kivile ana maana kwamba kipato cha msanii kilitegemea mauzo ya kanda na malipo ya show kitu ambacho baadhi ya wasanii hawakufanikiwa kupata show nyingi zaidi walitegemea mauzo ya kanda ambapo pia distributes ndio walipiga faida kuzidi wasanii hivyo maisha ya wasanii wengi yakabaki kuwa ya kawaida tofauti na wasanii wa sasa ambapo kuna YouTube ndo inawalipa sana kiasi kwamba msanii akijibrand kwenye social media akapata mashabiki wengi basi ana uhakika wa kupiga pesa mingi mtandaoni ambayo haina udalali wala magumashi ya wahindi kama kipindi kile.
Ndio maana sa hivi msanii kumiliki gari kali ni jambo la kawaida.
 
View attachment 2444461

Jina lake ni Miikka Kari, Hapo kwenye Kari alibadili iwe kwa kiswahili na tafsiri yake ni Mwamba, hivyo aliamua kujiita Miikka Mwamba ila wengi tukaizoea Mika Mwamba

miika-png.558523



Ngoma za huyu mwamba zilikuwa na vinanda vyenye ma-vibe ya kufa mtu:
  • Tamara + ni wewe - Hard Mad
  • Eno maiki - Ziggy Dee (Uganda)
  • Nakupenda Mpenzi - Dudu Baya
  • get down - Prezo ft Naziz (Kenya)
  • Twenzetu - Chege
  • Baby Gal + wange - Mad Ice
  • Maria Salome - Saida Karoli
  • Kamanda + barua - Daz Nundaz
  • wanoknok + Taswira + dingi - Mandojo na domokaya
  • Picco - Kikongwe
  • Kwenye Chati - Balozi
  • Mtoto wa geti kali - Inspector Haroun
  • Elimu mtaani + sauti ya gharama - D knob
  • Mkiwa - K sal ft Ferooz
  • Salome + Julieta + Hi - Dully Sykes
  • Raha tu - AY
  • Mambo vipi - Mchizi Mox
  • Solid Ground Family - Bush party
  • Nini mnataka mazee- Pig black

Najua wengi mmekariri ni P Funk na Master J, na hata mimi nakubali linapokuja suala la kuwatoa wasanii wengi hawa jamaa hawana mpinzani hasa ukizingatia walivyokuwa na connections nyingi kwenye media, walisaidia kazi kibao za wasanii zitufikie na waliifanya kazi kama full time job iwe kazi yao rasmi. lakini kwa upande mwengine tunapomzungumzia Mika Mwamba hizo ni level nyingine na hata wao walijua, Mikka alikuwa na uwezo binafsi wa juu sana kwenye kubuni biti, alikuwa mtundu zaidi kwenye kucheza na vyombo kwa ubunifu ulioshangaza wengi.

Mzungu alikuwa ni Full Package ambae vitu vingi kwenye upande wa biti alikamilisha mwenyewe tofauti na kina Pfunk na Master J ambao waliwatumia wagonga beat wengi waliochangia idea na kutengeneza beats ila credit zikaenda kwa hao jamaa wawili. Mfano sehemu za vinanda wanamtumia bizzman, sehemu za gitaa wanamtumia mzungu kichaa, n.k. "She got a gwan" Gitaa ni Mzungu Kichaa, strings ni Bizz man, Kick zile ni Soggy Doggy, Majani kaja kumalizia mixing na mastering. Kwa upande wa Master J aliweza kuajiri kabisa watasha kama kina Ludigo na Said Comorie na walioandaa kazi kibao ila credit ikaishia kwa Master J.

Nimgusie pia Mkongwe Ludigo, huyu mtasha ndie kahusika kwenye ngoma kibao za hip hop zilizofanywa Bongo records na Mj Reecords, Ludigo hakuwa na Studio maalum ila mikono yake ipo kwenye hits kibao, pale bongo records kapika beats za Ngwea kama Mikasi, Kimya kimya, Aka mimi na Weekend, alihusika pia kwenye Mgambo ya juma nature, Aquelina ya Ocq ft Juma nature, kibanda cha simu ya Soggy, Bijou ya Dully sykes, kwa uchache tu. Kwa Master J ameandaa Album ya Wagosi, Album ya Mr Ebo , Mapacha, Fid Q na kina profesa Jay (ikiwemo Bongo Dsm) Kifupi Ludigo ndie alikuwa master mind wa ngoma kibao za hiphop ila ndio vile ngoma ikipikwa bongo records tunajua ni Majani na akifanya kwa MJ records sifa zote zinaenda kwa Master J

Tukija kwa upande wa kaka yao kiumri na kiuwezo Mika Mwamba huyu alikuwa ni next level na hata hao kina Pfunk na Master J walijua hilo, Ila tatizo ni kwamba Mika alikuwa hapendi kufahamika na ndio maana watu wengi hawakuweza hata kumfahamu kwamba ni mzungu kutokea Finland na sio raia wa Tanzania, hiyo yote ni kwasababu aliamua toka kitambo asionekane kwenye Media wala kupigwa picha, hakupenda umaaufu wala kufanya matukio ya watu kuanza kumfatilia, Interview aliyowahi kuifanya ni kwa millard ayo ipo Youtube ilikuwa 2017, hapo ni baada ya kukaa nje ya muziki mda mrefu sana.

Mika Mwamba alikuwa anakaa ulaya na bongo, anaweza akaja bongo akakaa miezi sita anapiga kazi pale Fm Studio kisha anasepa kurudi kwao, alikuwa hakai sana hapa bongo. ilikuwa ni kumvizia + timing, yaani akija tu watakaompata ndio hao watarikodi nae na kiukweli waliobahatika walipiga mshindo.


Aliachana na mambo ya mziki kwa muda mrefu ila alijaribu kutest mitambo walau mara moja na akathibitisha uzoefu wake hauozi, ee bwana eeh!! Alitubless na mkwaju ulioenda shule - Mashaallah ya Chid Benz ft Mzee Yusuf.

Inasemekana kuna watu wenye roho zao mbaya kwa kushirikiana walileta figisu mpaka Mika Mwamba akasepa ili wao na studio zao wapate majina ila nao wakaishia kushuka zaidi.
Ni raha tu (remix) - P Funk
Nini mnataka mazee - P Funk
Sauti ya gharama - P Funk
Bush Party - Bonny Luv
 
Julieta - Dully Sykes
Hi - Dully Sykes
Baby Girl - radio edit (acha ile version iliyofanyiwa video) ilikuwa ina unyama sana wa production na mixing ambao mpaka sasa producers wengine kibongo wanaweza wakawa hawana ujuzi nao
AY - Raha tu (original version)
Mez B - Fikiria (iilikuwa ngoma kali sana)
HipHop Mdundiko - Mambo Jambo
Mkao wa Kula - Mambo Jambo
Mchizi Mox - Mambo vipi

List ni ndefu sana aisee,
Fikiria ya Mez B - P Funk
 
P anaficha mambo mengi, siwezi shangaa ni Bizman kapiga pale kinanda
Sio kweli kwamba huwa anaficha. Kwenye interviews zake amekuwa akitaja watu wote aliokuwa anawatumia kwenye production. Hata kwenye baadhi ya nyimbo zenyewe walikuwa wakitajwa, mfano Akwelina katajwa Ludigo, Jirushe katajwa Marijani n.k

Kuwa producer haimaanishi ufanye kila kitu, kazi kubwa ya producer ni kuleta concept nzima ya kazi. Producer mzuri ni yule anayehakikisha anatoa nyimbo bora kwa kutafuta watu mahiri watakaofanikisha kazi na sio lazima kila kitu afanye yeye.
 
Fikiria ya Mez B - P Funk
Ahsante mkuu. Kimawazo nafikiri nilichanganya, nilikuwa ninawaza ile ngoma ya D Knob na Mez B - ni kama mti usio na mizizi, upepo upepooo, ni kama ardhi juu ya maji, Mpenzi usiniache. Hiyo aliipika Mikka
 
Nini mnataka ni beat ya P, edit hapo!
 
Mmmmh, hapana. Hakuna producer nchi hii mwenye/aliyekuwa na uwezo wa kutengeneza mdundo kumzidi majani.
 
View attachment 2444461

Jina lake ni Miikka Kari, Hapo kwenye Kari alibadili iwe kwa kiswahili na tafsiri yake ni Mwamba, hivyo aliamua kujiita Miikka Mwamba ila wengi tukaizoea Mika Mwamba

miika-png.558523



Ngoma za huyu mwamba zilikuwa na vinanda vyenye ma-vibe ya kufa mtu:
  • Tamara + ni wewe - Hard Mad
  • Eno maiki - Ziggy Dee (Uganda)
  • Nakupenda Mpenzi - Dudu Baya
  • get down - Prezo ft Naziz (Kenya)
  • Twenzetu - Chege
  • Baby Gal + wange - Mad Ice
  • Maria Salome - Saida Karoli
  • Kamanda + barua - Daz Nundaz
  • wanoknok + Taswira + dingi - Mandojo na domokaya
  • Picco - Kikongwe
  • Kwenye Chati - Balozi
  • Mtoto wa geti kali - Inspector Haroun
  • Elimu mtaani + sauti ya gharama - D knob
  • Mkiwa - K sal ft Ferooz
  • Salome + Julieta + Hi - Dully Sykes
  • Raha tu - AY
  • Mambo vipi - Mchizi Mox
  • Solid Ground Family - Bush party
  • Nini mnataka mazee- Pig black

Najua wengi mmekariri ni P Funk na Master J, na hata mimi nakubali linapokuja suala la kuwatoa wasanii wengi hawa jamaa hawana mpinzani hasa ukizingatia walivyokuwa na connections nyingi kwenye media, walisaidia kazi kibao za wasanii zitufikie na waliifanya kazi kama full time job iwe kazi yao rasmi. lakini kwa upande mwengine tunapomzungumzia Mika Mwamba hizo ni level nyingine na hata wao walijua, Mikka alikuwa na uwezo binafsi wa juu sana kwenye kubuni biti, alikuwa mtundu zaidi kwenye kucheza na vyombo kwa ubunifu ulioshangaza wengi.

Mzungu alikuwa ni Full Package ambae vitu vingi kwenye upande wa biti alikamilisha mwenyewe tofauti na kina Pfunk na Master J ambao waliwatumia wagonga beat wengi waliochangia idea na kutengeneza beats ila credit zikaenda kwa hao jamaa wawili. Mfano sehemu za vinanda wanamtumia bizzman, sehemu za gitaa wanamtumia mzungu kichaa, n.k. "She got a gwan" Gitaa ni Mzungu Kichaa, strings ni Bizz man, Kick zile ni Soggy Doggy, Majani kaja kumalizia mixing na mastering. Kwa upande wa Master J aliweza kuajiri kabisa watasha kama kina Ludigo na Said Comorie na walioandaa kazi kibao ila credit ikaishia kwa Master J.

Nimgusie pia Mkongwe Ludigo, huyu mtasha ndie kahusika kwenye ngoma kibao za hip hop zilizofanywa Bongo records na Mj Reecords, Ludigo hakuwa na Studio maalum ila mikono yake ipo kwenye hits kibao, pale bongo records kapika beats za Ngwea kama Mikasi, Kimya kimya, Aka mimi na Weekend, alihusika pia kwenye Mgambo ya juma nature, Aquelina ya Ocq ft Juma nature, kibanda cha simu ya Soggy, Bijou ya Dully sykes, kwa uchache tu. Kwa Master J ameandaa Album ya Wagosi, Album ya Mr Ebo , Mapacha, Fid Q na kina profesa Jay (ikiwemo Bongo Dsm) Kifupi Ludigo ndie alikuwa master mind wa ngoma kibao za hiphop ila ndio vile ngoma ikipikwa bongo records tunajua ni Majani na akifanya kwa MJ records sifa zote zinaenda kwa Master J

Tukija kwa upande wa kaka yao kiumri na kiuwezo Mika Mwamba huyu alikuwa ni next level na hata hao kina Pfunk na Master J walijua hilo, Ila tatizo ni kwamba Mika alikuwa hapendi kufahamika na ndio maana watu wengi hawakuweza hata kumfahamu kwamba ni mzungu kutokea Finland na sio raia wa Tanzania, hiyo yote ni kwasababu aliamua toka kitambo asionekane kwenye Media wala kupigwa picha, hakupenda umaaufu wala kufanya matukio ya watu kuanza kumfatilia, Interview aliyowahi kuifanya ni kwa millard ayo ipo Youtube ilikuwa 2017, hapo ni baada ya kukaa nje ya muziki mda mrefu sana.

Mika Mwamba alikuwa anakaa ulaya na bongo, anaweza akaja bongo akakaa miezi sita anapiga kazi pale Fm Studio kisha anasepa kurudi kwao, alikuwa hakai sana hapa bongo. ilikuwa ni kumvizia + timing, yaani akija tu watakaompata ndio hao watarikodi nae na kiukweli waliobahatika walipiga mshindo.


Aliachana na mambo ya mziki kwa muda mrefu ila alijaribu kutest mitambo walau mara moja na akathibitisha uzoefu wake hauozi, ee bwana eeh!! Alitubless na mkwaju ulioenda shule - Mashaallah ya Chid Benz ft Mzee Yusuf.

Inasemekana kuna watu wenye roho zao mbaya kwa kushirikiana walileta figisu mpaka Mika Mwamba akasepa ili wao na studio zao wapate majina ila nao wakaishia kushuka zaidi.
Basu huyu mwamba alikuwa noma
 
Mwamba mkali sana, sema ndiyo hivyo industry ya muziki mara nyingi haiwapi credits producers wanaowapa samples maproducer wakubwa. Na siyo TZ tu, ni ulimwengu mzima.

Kuna jamaa wanaitwa Cubeatz, ni mapacha, wapo very lowkey lakini wameshiriki kuandaa zaidi ya 80% ya nyimbo za HipHop marekani kwa miaka sita iliyopita, lakini credits wanapewa maproducer wanaonunua samples kutoka kwa hawa jamaa.

Umefanya jambo la msingi sana kumpa heshima yake, jamaa anatengeneza mziki mzuri.
True man
 
Julieta - Dully Sykes
Hi - Dully Sykes
Baby Girl - radio edit (acha ile version iliyofanyiwa video) ilikuwa ina unyama sana wa production na mixing ambao mpaka sasa producers wengine kibongo wanaweza wakawa hawana ujuzi nao
AY - Raha tu (original version)
Mez B - Fikiria (iilikuwa ngoma kali sana)
HipHop Mdundiko - Mambo Jambo
Mkao wa Kula - Mambo Jambo
Mchizi Mox - Mambo vipi

List ni ndefu sana aisee,
Naomba kuweka kumbukumbu sawa,Ay Raha Tu original version ilikuwa ni kazi ya Bongo Records.Kwanza hiyo Beat ilibidi Eluka aifanyie kazi,baadaye akapewa A.Y.
 
Sio kweli kwamba huwa anaficha. Kwenye interviews zake amekuwa akitaja watu wote aliokuwa anawatumia kwenye production. Hata kwenye baadhi ya nyimbo zenyewe walikuwa wakitajwa, mfano Akwelina katajwa Ludigo, Jirushe katajwa Marijani n.k

Kuwa producer haimaanishi ufanye kila kitu, kazi kubwa ya producer ni kuleta concept nzima ya kazi. Producer mzuri ni yule anayehakikisha anatoa nyimbo bora kwa kutafuta watu mahiri watakaofanikisha kazi na sio lazima kila kitu afanye yeye.
Naungana na wewe.Maproducer wakubwa kama Quincy Jones,wqo hata chombo cha Muziki hawajui kupiga,lakini wana sikio na jicho la muziki.Wanajua chombo kipi kipigwe,ala ipi ipigwe vipi.Na ni mtu gani anafaa kwa kazi hiyo,wao kazi yao ni ku organise na kusimamia kazi mpaka inakamilika.
Hata P Didy.Hajui chombo hata kimoja lakini ni mmojawapo wa maproducer wenye mafanikio makubwa
Hata P Funk alishawahi kusema,kuna tofauti ya Producer na beat maker.Producer ni zaodo ya beat maker.
 
Miikka Aleksanteri Kari ndiye GOAT wangu!
 
Back
Top Bottom