MR MAJANGA
JF-Expert Member
- Oct 4, 2014
- 3,444
- 10,687
Ibilisi aliumbwa na Nani????Iblis ni miongoni mwa MAJINI na hakuwa Malaika kama wengi wanavyodhani! Malaika hawana sifa ya uasi, hawana matamanio na wala hawana watoto . Majini wana sifa kama za wanadamu tu, wanaasi,wana jinsia, wana matamanio, wana uzao n k
MKuu Daudi!Hilo ni agano la Kwanza la damu analofanya na wanawaizrael, ndio maana akasema watalikumbuka miaka yao yote, maana yake pia ambaye asingefanya Kama maagizo ya Mungu angekuwa nje ya agano, ukitaka kujua ni agano angalia namna walivyooelekezwa kula hiyo nyama ambayo damu yake ilifanyika kuwa agano. Hamna contradiction hapo
Malaika wanaasi pia, unawafahamu Wanefili?
unaweza ukajisaidia mbele za watu?Kamleta Mungu/Allah maana kila kitu kinachotikea duniani basi ni Kwa amri yake,
Kwa kuwa Mungu/Allah hakupanga tundu lissu are kwa risasi na hakufa hata baada ya kupigwa risasi 38, ila kama Mungu/Allah akipanga ufe risasi moja Tu ilitosha,
Kwa hiyo tunaona mratibu mkuu wa kila tukio linalotoke duniani ni mipango ya Allah/Mungu
Problem of evil 🤣🤣Ibilisi aliumbwa na Nani????
Aliyemuumba alikuwa Hana uwezo wa kujua kuwa atamuasi?????
Sasa kama Mungu/Allah anakosea kwanini amchome binadamu Moto Kwa makosa yake yeye????
Kama Mungu/Allah aliumba malaika ambao hawana uwezo wa kumuasi Mungu/Allah alishindwa nini Kwa binadamu?????
Malaika Hawaasi Ameumbwa Kutekeleza Amri Ya Mungu Na Sio Ameumbwa Kujaribiwa Kama Mwanadamu, Malaika Anajua Upande Mmoja Tu Wa Mema Tu. Hao Wanafili Siwajui Ila Naamini Hawawezi Kuwa Malaika Huenda Hujaelewa Sehemu Au Labda Ndo Mikanganyiko Yenyewe TunayoizungumziaMalaika wanaasi pia, unawafahamu Wanefili?
Hilo agano si ndio pasaka yenyewe sasa, waliagizwa kula mikate isiyotiwa chachu, hata Yesu alifanya pasaka na wanafunzi wake.Asante mkuu,
Hilo ni agano la kwanza alilolifanya na wana wa izraeli! Agano hilo wanalikumbuka kwa namba gani mpaka sasa?
Mungu huyo anakataza uzinzi, na anasema mimi si mwanadamu hata nibadili neno langu wakati hapo hapo mungu huyo anazo sifa zote za kibinadamu.
Baadae tena mungu huyo huyo anamuagiza Hosea akajitwalie mke wa uzinzi, unamtetea vipi katika hilo.
Contradiction zipo nyingi.
Karibu mkuu.
swali ni Kwanini unakataza uzinzi Halafu unatoa Amri ya mtu kwenda kufanya uzinzi?Hilo agano si ndio pasaka yenyewe sasa, waliagizwa kula mikate isiyotiwa chachu, hata Yesu alifanya pasaka na wanafunzi wake.
Hosea anaagizwa kwenda kuoa mwanamke kahaba, sio kwamba Hosea ni mzinzi la hasha, Soma mistari ya chini, alikuwa anazungungumza juu ya jamii ile iliyokuwa imemuasi Mungu, Hosea alitakiwa apeleke ujumbe wa laana, na ukiwa. "Kwa maana nchi hii imejaa inafanya uzinzi mwingi kwa Kumwacha BWANA"
Ukisoma mistari ya chini unaona Mungu anampa Hosea majina ya watoto wanaozaliwa na maana ya hayo majina, lakini Mungu anamwambia katika wana waizrael litasalia kabila la Yuda tu wengine watakutana na hasira ya Mungu.
Soma sura ya pili Hosea anachowaambia wanawe, hicho ndicho Mungu alikikusudia kwa nchi ile
Kabla ya kujadili vitabu lazma tumjue mwenye vitabu vyake yupo au hayupo.Tujadili Mikanganyiko Katika Biblia Kama Ilivyoletwa Na Mtoa Mada Ili Tupate Elimu Maana Mada Imehamia Kwenye Uwepo Wa Mungu Wa Mungu,kinachojadiliwa Hapa Ni Kitabu
Nashukuru Mkuu, ila nasikitika kuwa naingia kwenye majukumu pengine mpaka jioni Kama hautajal, Mimi pia napenda kujifunza, napenda sana kusoma na kuijadili Bibilia maana mnapojadili mambo ya Mungu Kuna wengine wanapona. Ubarikiwe sanaMKuu Daudi!
Natamani niende one to one na tuanze kujadili contradiction moja baada ya Nyingine tutaanza agano la kale tutamalizia agano jipya kama hutojali...
Ili nijifunze zaidi maana ut seems uko vizuri...
Nasubiri comfirmation yako
ASANTE..!
Ni mimi
Dr Mambo Jambo Habari Hi
Mungu huyo Aliumbaje binadamu wabishi sana?Mwanadamu ni kiumbe mbishi sana hata kama MUNGU angetuumba sote tuwe waarabu bado mngekuja na hoja ya kusema kwanini Mungu katuumba sote ni waarabu kwa nini asingetutofautisha.
Mungu muweza wa vyote, Alishindwaje kuumba binadamu wema tu watakao fuata maagizo yake siku zote?Ni sawa na watu wa Mussa walipokuwa wakiteremshiwa chakula kutoka mbinguni cha Manna na salwa....walipokuwa wakila na kushiba wakaanza kuhoji kwanini kila siku tunakula manna na salwa tu...kwanini Mungu asituache tukaenda kulima mazao mbalimbali huko mashambani!? Matokeo yake Mungu alisitisha ile ofa aliyokuwa akiwapa ya kula chakula bure pasi na kukitolea jasho na wakaachwa wakasulubike huko mashambani.
Kama Mungu/Allah kaweka njia zake binadamu anakwepa vipi?????Mungu ana elimu na mambo yote yanayotokea ulimwenguni, Kila kitu kinachotokea kilishapangwa kiwe kabla ya kuumbwa kwa hii dunia .
Mungu ameumba mwanadamu kisha akambainishia njia zote, njema na ovu kisha akampa uhuru achague wapi anaelekea.
Kuna mtu kama sikosei tandale alijisaidia mbele za watu Kwa kupewa 10,000unaweza ukajisaidia mbele za watu?
Mkuu samani hiyo logic ya kawaida sana, madawa ya kulevya yanakatazwa na ukikutwa nayo unajua nini kitakupata, lakini yanatumika hospital katika kutibu, hoja yangu Ni hii, jamii ya wana waizrael walimwasi Mungu na kuiasi hiyo amri ya kutozini, ndipo Mungu anamtuma Hosea kupeleka ujumbe kwa njia hiyo hiyoswali ni Kwanini unakataza uzinzi Halafu unatoa Amri ya mtu kwenda kufanya uzinzi?
Halafu bado unasema wewe ni mungu ujuaye yote?
Kipindi anasema acha uzinzi hakufikiria kwamba atakuja kumwambia Hosea akafanye uzinzi? Alishindwa kufikiria hilo?
Nae utasema MUNGU alipanga ajisaidie mbele za watu?Kuna mtu kama sikosei tandale alijisaidia mbele za watu Kwa kupewa 10,000
Asante kwa confirmation mimi pia nipo kwenye majukumu..Nashukuru Mkuu, ila nasikitika kuwa naingia kwenye majukumu pengine mpaka jioni Kama hautajal, Mimi pia napenda kujifunza, napenda sana kusoma na kuijadili Bibilia maana mnapojadili mambo ya Mungu Kuna wengine wanapona. Ubarikiwe sana
Ninachoomba ni kujikita katika sifa za ominiscent(mwenye kujua yote) omipresence(aliyeko kila mahali) .Mkuu samani hiyo logic ya kawaida sana, madawa ya kulevya yanakatazwa na ukikutwa nayo unajua nini kitakupata, lakini yanatumika hospital katika kutibu, hoja yangu Ni hii, jamii ya wana waizrael walimwasi Mungu na kuiasi hiyo amri ya kutozini, ndipo Mungu anamtuma Hosea kupeleka ujumbe kwa njia hiyo hiyo
Ukisema hivi unataka kuniambia kuwa Mungu/Allah Hana uwezo wa kujua kuwa kiumbe wake aliyemuumba atakunya hadharani????Nae utasema MUNGU alipanga ajisaidie mbele za watu?
Kiufupi binadamu tumepewa akili,u tashi,tamaa n.k.
Tunayoyafanya mama au mabaya ni matokeo YA KUTUMIA AKILI ZETU VIZURI AU VIBAYA.