Mikanganyiko katika Biblia ni kigezo kinachowapa watu uhalali wa kusema hakuna Mungu

Mikanganyiko katika Biblia ni kigezo kinachowapa watu uhalali wa kusema hakuna Mungu

MKuu naomba niseme kuwa kama hukuona aliyekuwa anaongea hapo ni malaika aliyemtokea Yusuph ndotoni niruhusu niseme kuwa wewe ni mbishi..
ni wewe toka mwanzo uliyedai kwamba unabii haukutimia sababu tu,malaika alitaja "YESU",badala ya emanuel!!!
mimi ni mbishi kweli,ila nina focus mkuu.
Melkizedek hakuwahi kuwa Mungu Mkuu...
Na hakuna sehemu iliyomtaja hivyo..
Tatizo husomi biblia..
ndio maana nikasema hujasoma bible umeikariri😂😂
wewe umesema melkizedeki ndiye pekee aliyewahi kuwa mfalme wa amani,nikakupa andiko alipotajwa yeye Yesu na sifa zingine lakini kama melkizedeki pia,ikimaanisha yeye anabeba sifa za melkizedeki.
bado chalii,huelewi.
Na ndo maana hata Paulo kwa kujua kuwa hamuelewi chochote kuhusu melkizedeki aliwaambia hivii..

WAEBRANIA 5:10-12

kisha ametajwa na Mungu kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.
Ambaye tuna maneno mengi ya kunena katika habari zake; na ni shida kuyaeleza kwa kuwa mmekuwa wavivu wa kusikia.
paulo ni mtumishi wa Mungu,sio msomi wa theolojia aliyeshindwa kuielewa kabisa.
Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu.

Nimesoma na nikakataa kuwa mtumwa..
Unafikir kwanini Yesu anafananishwa na Melkizedeki na sio melkizedek afananishwe na yesu?
hili ni swali la kijinga mkuu,nilikuuliza una taarifa kwamba alifananishwa na mwana kondoo?,au ulikuwa unasoma ili umalize kitabu mkuu😂😂
 
Huwa hatutaki stori, wewe leta ushahidi ya kuwa kipindi cha Mtume Biblia ilikuwepo.

Hili swali hakuna anaye weza kulijibu. Nasubiri majibu hapa.
Ushahidi wa namna ipi unaoutaka wewe? We hujui Biblia ni mkusanyiko wa vitabu vyote vya habari za Mungu tangu adamu? Sasa hivo vitabu vya zamani iweje visiwepo wakati wa mtume wenu? Mudi ni mtu wa miaka ya juzi tu wakati hata hii miaka tuliyonayo sasa 2023 ilikuwa imeshaanza kuhesabiwa. Ushahidi upi unautaka sasa....unataka huo ushahidi utoke kwenye kitabu gani
 
ni wewe toka mwanzo uliyedai kwamba unabii haukutimia sababu tu,malaika alitaja "YESU",badala ya emanuel!!!
mimi ni mbishi kweli,ila nina focus mkuu.

ndio maana nikasema hujasoma bible umeikariri😂😂
wewe umesema melkizedeki ndiye pekee aliyewahi kuwa mfalme wa amani,nikakupa andiko alipotajwa yeye Yesu na sifa zingine lakini kama melkizedeki pia,ikimaanisha yeye anabeba sifa za melkizedeki.
bado chalii,huelewi.
Hakuna andiko ulilonipa linalosma yesu kuwa mfalme wa Amani na Narudia Tena hakuna...
Kama lipo liquote hapa..
Yesu anasifa Moja tu ya Melkizedeki nayo ni ya ukuhani..
Yesu Alizaliwa....Melkizedek hakuzaliwa wala hana baba wala mama wala hana mwanzo..wala wala mwisho...

Yesu ana mama..
Yesu anabeba sifa moja tu ya Ukuhani kutika kwa Melkizedek
paulo ni mtumishi wa Mungu,sio msomi wa theolojia aliyeshindwa kuielewa kabisa.
Mkuu Nazidi kuamini kuwa Huelewi maandiko Nikukumbushe kuwa Paulo alikuwa Farisayo na Pia alikuwa Mwanafilosphia (Msomi wa Philosophy)
hili ni swali la kijinga mkuu,nilikuuliza una taarifa kwamba alifananishwa na mwana kondoo?,au ulikuwa unasoma ili umalize kitabu mkuu😂😂
SwLi la kijinga kwa kuwa umeshindwa kulijibu na I bet hutaweza kulijibu kwa sababu huna uwezo wa kulijibu..

Kwa bahati mbaya Nilimaliza theology na nilifanya kazi miaka zaidi ya sita kama Mchungaji mpaka pale nilipoona bora kujivika Akili kuliko kuwa na Akili nusu za kuamini
 
Ushahidi wa namna ipi unaoutaka wewe? We hujui Biblia ni mkusanyiko wa vitabu vyote vya habari za Mungu tangu adamu? Sasa hivo vitabu vya zamani iweje visiwepo wakati wa mtume wenu? Mudi ni mtu wa miaka ya juzi tu wakati hata hii miaka tuliyonayo sasa 2023 ilikuwa imeshaanza kuhesabiwa. Ushahidi upi unautaka sasa....unataka huo ushahidi utoke kwenye kitabu gani
Mkuu Achana naye huyo nimempa Ushahidi wa kihistoria na wa kiFizikia na wakivitabu vilivyopo ambavyo ni manuscript..

Muongezee muulize Quran inaposema Alkitab (Watu wa kitabu) inakusudia watu gani kama kulikuwa hakuna kitabu kwanini Quran itaje Watu wa kitabu ambao wanatajwa ni Manaswara (Wakristo) na Mayahudi...

Kuna vitu vingine mtu anaamua kujitoa akili tu....
 
Ni majestic plural (wingi wa kujitukuza), kwa wanaojua kiarabu watakuwa wanaelewa
Thats Question same Goes to Elohim (Mungu)..
Eloh (Means mungu) Im (Wingi)
So Elohim Maana yake ni Mungu kw Wingi yaani Miungu..
NA Ndo maana hata kwenye Biblia kila anapotojwa Elohim mara nyingi Utaona kuna wingi..

"Mungu akasema Na Tuumbe"...
"Mungu akasema Ngoja tushuke huko chini"
 
Hakuna andiko ulilonipa linalosma yesu kuwa mfalme wa Amani na Narudia Tena hakuna...
Kama lipo liquote hapa..
mkuu nafikiri una tatizo jingine,tofauti na nililoliona awali😂😂😂
Yesu anasifa Moja tu ya Melkizedeki nayo ni ya ukuhani..
Yesu Alizaliwa....Melkizedek hakuzaliwa wala hana baba wala mama wala hana mwanzo..wala wala mwisho...
nikisema ulikwenda kuisaidia theolojia utakataa.

Yesu ana mama..
Yesu anabeba sifa moja tu ya Ukuhani kutika kwa Melkizedek
😂😂😂😂
Mkuu Nazidi kuamini kuwa Huelewi maandiko Nikukumbushe kuwa Paulo alikuwa Farisayo na Pia alikuwa Mwanafilosphia (Msomi wa Philosophy)
nimeandika vile kumtofautisha nawewe,maana ulimnukuu kwa nia ya kujilinganisha naye.

SwLi la kijinga kwa kuwa umeshindwa kulijibu na I bet hutaweza kulijibu kwa sababu huna uwezo wa kulijibu..
real😂😂,umeanza kubeti sasa.
nimekuuliza swali jepesi tu,una taarifa alifananishwa na mwana kondoo pia??
Kwa bahati mbaya Nilimaliza theology na nilifanya kazi miaka zaidi ya sita kama Mchungaji mpaka pale nilipoona bora kujivika Akili kuliko kuwa na Akili nusu za kuamini
kwahiyo kwa sasa unaweza kuuelezea umma kwamba umekuwa na akili😂😂,toka lini mtu mwenye akili huwa anasema"jamani mimi sasa nina akili"na je ndio hizi hizi uko nazo hapa au tuzitarajie nyingine kama masihi wa wayahudi?
 
nimeandika vile kumtofautisha nawewe,maana ulimnukuu kwa nia ya kujilinganisha naye.
Mkuu hana tofauti na mimi kwa Chchote,Tofauti ni kwamba kawahadaa watu wengi sana
real😂😂,umeanza kubeti sasa.
nimekuuliza swali jepesi tu,una taarifa alifananishwa na mwana kondoo pia??
Inaonekana hata Lugha Hujui..
Unajua hata kwanini alifananishwa Na kondoo?
KWeli elimu ni nzuri sana ukiwa nayo..
kwahiyo kwa sasa unaweza kuuelezea umma kwamba umekuwa na akili😂😂,toka lini mtu mwenye akili huwa anasema"jamani mimi sasa nina akili"na je ndio hizi hizi uko nazo hapa au tuzitarajie nyingine kama masihi wa wayahudi?
Nilijibu ni kutkana na akili yako na nimejibu kulingana na mawazo yko...

So I think bado huna Huja so I wont repply your Quotes unless kuwa kuna hoja mpya ila vinginevyo..
Happy Gullible Day
 
Mkuu Achana naye huyo nimempa Ushahidi wa kihistoria na wa kiFizikia na wakivitabu vilivyopo ambavyo ni manuscript..

Muongezee muulize Quran inaposema Alkitab (Watu wa kitabu) inakusudia watu gani kama kulikuwa hakuna kitabu kwanini Quran itaje Watu wa kitabu ambao wanatajwa ni Manaswara (Wakristo) na Mayahudi...

Kuna vitu vingine mtu anaamua kujitoa akili tu....
Comment yako ipo namba ngapi uliyompa ushahidi nami niipitie
 
Mkuu hana tofauti na mimi kwa Chchote,Tofauti ni kwamba kawahadaa watu wengi sana
nawewe jitahidi upate walau 1,kwa.mwenendo huu utaishia kufungwa kamba kwamba umevurugika.
Inaonekana hata Lugha Hujui..
Unajua hata kwanini alifananishwa Na kondoo?
KWeli elimu ni nzuri sana ukiwa nayo..
elimu ipi mkuu,zipo zinazofanya watu wanakuwa vichaa,theologia hiyo hiyo imetuletea watu wazuri sana ila kwako imesababisha matatizo.
Nilijibu ni kutkana na akili yako na nimejibu kulingana na mawazo yko...
mimi nimemeamua kuipima elimu yako kwa matokeo,sio vyeti wala maelezo,nimegundua kumbe hata PHD za jalalani ni kwa sababu zinatua ktk vichwa ambavyo sio.
So I think bado huna Huja so I wont repply your Quotes unless kuwa kuna hoja mpya ila vinginevyo..
Happy Gullible Day
mkuu,ushauri tu.kama umeamua kutoamini Mungu na story zake,kuwa muwazi kama akina kiranga na wenzao,kataa kila kitu ili tukose hata hoja ya kuanzia kukujibu,usijifiche fiche kwenye usomi wa mabua,utakula spana zikuache mtupu na kujutia muda ulipoteza huko shule,heri ungeanzisha kilimo cha vanilla.
 
Mkuu mimi sina biblia!
na sasa hapo nashindwa kujua unataka ushahidi wa aina gani!

Maana nimekupa Ushahidi wa Kihistoria wa vikao vya kupanga na kukusanya vitabu canonical Bible selection vyote na vilikuwa between karne ya 4th mpaka karne ya Tano!..
Na ushahidi wowote wa zamani na kupangwa umeandikwa humo kwenye vikao hivyo..

Na pia nimekupa ushahidi wa Kifizikia kuwa kuna manuscript zilizokuwepo kipindi hicho..
Labda nikisema manuscdipt hunielewi..

Namaanisha yalikuwepo maandiko ya zamani yote Waliyochukua na kutafsiria Biblia..
Na nimekutajia na miaka yake nikakupa..

Sasa unataka ushahidi kwamba nikuletee mtu Akiyekuwepo kipindi hicho aongee akuambie kwamba vilikuwepo...
Si unaijua Biblia lakini ? Kwahiyo uwepo wa Manuscript ndio ushahidi wa Kifizikia ? Hapa sijakuelewa. Sababu Manuscript ni maandishi yaliyo hifadhiwa tu. Sasa ufizikia hapo unaingia wapi ?

Sipo huko, Mimi nataka unithibitishie ya kuwa kipindi Mtume yupo hai, nakala ya Biblia ilikuwepo kipindi chake, nilikupa ushahidi wa Mtume kumkataza juu ya maandiko ya kale, baada ya kumuona ameshika kipande Cha karatasi ya Taurati. Sasa usiniletee Historia ambazo hazijibu swali langu.
 
🤣🤣🤣🤣🤣
Mkuu Mche mola wako Kwa Uongo huu Sidhani kama nitaendelea na Mjadala..

Mimi mkuu Nimekuwa muislamu Takribani miaka 12 Ninachokiongea nimekisoma..
Nachukulia kama umesahau..
Na kama uko serious niambie imekusanywa na nani na lini 🤣🤣
Wakati kamati ya Watu wanne iliundwa na Uthmani na ndyo iliyofanikisha Yote...

Kuna vitu mkuu Ni bora kuvinyamazia kuliko kujiongezea Moto (Kwa imani yako)..

Na BTW hafsa Bint Umar alikuwa na baadhi ya Copy zilizokuwa kipindi cha Abu bakri..
Kwahyo.watu walipoleta Copy zao ili kuthibitisha kuwa ni zenyewe walikuwa wanahahakiki kutumia Copy ya Hafsa..

Kumbuka haikuwa standadised kipindi hicho..
Aliyemaliza kazi alikuwa uthman na Jpo la wTu wanne..
Narudia tena kukuuliza hizo habari wewe unazitoa wapi ? Hili swali uliniambia maana naona unaandika uongo wa wazi.

Mimi habari hizi nazitoa katika kitabu cha Imamu Suyuti kiitwacho "Al-Itiqaan fi 'Ulumil al Qur'an".

Sasa kuwa kwako Muislamu kwa miaka 12 na ukawa mjinga na muongo, hii Haina faida yoyote.

Kwanini unamzushia Hafswa uongo ? Hizo copy zilizo kuwa kipindi cha Abu Bakr, zilikuwa ngapi ? Maana unaonyesha kama zilikuwa nyingi.

Baada ya swahaba Uthman kuchukua ushauri wa swahaba Hudhaifa ndio zikaandikwa nakala tano, zikasambazwa katika miji ya Makka, Madina, Kufa, Sham na Basra na kila nakala ilitumwa pamoja na msomaji wa kuwafundisha Waislamu husika katika miji hiyo.

Nakala ya mwanzo haikujumuisha zile ndimi saba, ambazo zina zaa viraa kumi, ushauri huu akautoa swahaba Hudhaifa ukafanyiwa kazi.

Nakuuliza tena hii Historia wewe unaisoma toka kwenye vitabu gani ? Isiwe wewe ni Shia.
 
nawewe jitahidi upate walau 1,kwa.mwenendo huu utaishia kufungwa kamba kwamba umevurugika.

elimu ipi mkuu,zipo zinazofanya watu wanakuwa vichaa,theologia hiyo hiyo imetuletea watu wazuri sana ila kwako imesababisha matatizo.

mimi nimemeamua kuipima elimu yako kwa matokeo,sio vyeti wala maelezo,nimegundua kumbe hata PHD za jalalani ni kwa sababu zinatua ktk vichwa ambavyo sio.

mkuu,ushauri tu.kama umeamua kutoamini Mungu na story zake,kuwa muwazi kama akina kiranga na wenzao,kataa kila kitu ili tukose hata hoja ya kuanzia kukujibu,usijifiche fiche kwenye usomi wa mabua,utakula spana zikuache mtupu na kujutia muda ulipoteza huko shule,heri ungeanzisha kilimo cha vanilla.
Sasa mkuu Ulivyo mweupe hivyo Kwenye biblia kweli unipige spana..🤣🤣
NAchukulia kama utani tu!

Kiufupi Maybe hunijui vizuri mimi sio Muumini wa Imani yoyote ila sipendi mtu kudanganya kutumia story nazozifahamu..

Kwa sababu nazichukulia kama Story za Kina Sophie and Phylosophy 😅😅
 
Qiraa ya Hafs ndo standard ya matamshi ya Quran Dunia nzima mkuu Usibishe unless kama hukusoma Tajweed (Mujawwad na Murratal)
Huijui Qur'aan, wewe, unaikumbuka Misahafu iliyo letwa toka Morocco ? Waislamu kwa ujinga wao wakaanza kusambaza habari kwamba Ile Qur'an imeandikwa na wamagharibi, kumbe ni Qur'an sahihi ila kwa Kiraa kingine, matokeo yake ilikuwa nini ?

Halafu unakuja kuandika uongo kwamba Kiraa Cha Hafs ndio standard, kingine usichanganye kati ya viraa na Hati ya Uthman. Hapa ndipo Kuna ujinga wako wa kutokusoma.
 
SOma tena nimeandika Tarehe 15 au tarehe 8 naonba Niquotes ili uone
Tarehe ziko mbili hapo juu na nikakujibu kwanini ziko mbili ni kutokana na kukhitalfiana kwa Wanachuoni..
Sasa sahihi ni tarehe 8 rabiul awali.
 
SOma tena nimeandika Tarehe 15 au tarehe 8 naonba Niquotes ili uone
Tarehe ziko mbili hapo juu na nikakujibu kwanini ziko mbili ni kutokana na kukhitalfiana kwa Wanachuoni..
Kingine kwenye tarehe zako umechanganya juu uneweka mwezi wa kiislamu huku chini uneweka mwezi June, Sasa ili hizo tarehe ziwe tofauti na kwamba wanachuoni wametofautiana, niambie tarehe 8 June ilikuwa mwezi gani na tarehe gani kwa hesabu za kiislamu au Waarabu. Sababu mwezi huo ulikuwa unajulikana na munasaba wake kwa mwezi wa kalenda ya miladia haikuwa June.
 
Back
Top Bottom