Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

MKASA WA PILI - Sehemu ya 8.


Inaendelea.............


Tulitembea kwa muda wa saa 1:30 tukawa tumefika hayo maeneo ya Butiama,tulitoka Kiabakari saa 4,hivyo ukijumlisha hayo masaa tuliyotumia mpaka hapo Butiama ni kama masa 5 :30,kipindi tupo Kiabakari yule mama muuza ndizi alituambia kwamba tukifika hayo maeneo ya hapo Butiama tuulize mtu yeyote atuelekeze njia ya kwenda Ikizu.Basi kuna jamaa tulikutana naye tulimuomba atuelekeze njia ya kwenda Ikizu,Yule jamaa kuna njia alituonyesha ambayo ilikuwa inapitia porini,ingawa hakukuwa na mapori makubwa sana ila ilikuwa ni vichaka tu vidogo vidogo na mashamba ya watu,nilimuuliza kutoka hapo Butiama mpaka Ikizu kuna umbali gani?,jamaa alituambia haikuwa mbali sana maana wao walishazoea kwenda kwa kutumia baiskeli,kwakutembea ingetuchukua kama saa 3 au 4,yule jamaa kuna njia alituonyesha akatuambia "nyie ifuateni hii njia mkifika huko mbele mtakuwa mnauliza watu watawaelekeza".

Kabla ya kuanza safari ya kutoka hapo Butiama nilimpigia yule mganga nikamwambia ndiyo tulikuwa tumefika Butiama, akasema hatukuwa mbali sana,alituambia tujitahidi taratibu tungefika mapema.Nilimpgia pia na mama tukasalimiana nikamweleza namna ilivyokuwa,nikamwambia na mahala tulipokuwa,Kauli ya mama yangu mara zote ilikuwa ni kunisisitiza niendelee kuwa makini!.Zile ndizi ambazo dogo alikuwa kazibeba kwenye mfuko ilibidi sasa nimsaidie maana niliona alikuwa ameanza kuchoka.Wakati tukiwa tunatembea yule jamaa Mkenya aliyetupatia hiyo dili alinipigia simu akawa anataka kujua ni nini kilikuwa kinaendelea,nilimwambia bado tunaendelea kutafuta ile sarafu na endapo ingepatikana,basi tungemjulisha haraka iwezekanvyo!.Jamaa aliniambia kwa wakati huo naongea naye alikuwa Mwanza,kuna bosi wake alikuwa ameenda kumpokea maana kuna dili nyingine pia walikuwa wanafuatilia!,nilimwambia asiwe na shaka.

Safari ilisonga sana tukipita milimani na mashambani ambako tulikuwa tukielekezwa na kila tuliyekutana naye,Kuna mahali tulifika kulikuwa kuna mti wa Mkwaju ikabidi dogo aniambie tupumzike kidogo,basi tulipumzika pale tukaanza tena kula zile ndizi mpaka zikaisha!,Kiukweli zile ndizi zilikuwa kubwa na tamu,hivyo tulishiba sana,ishu sasa ilikuwa ni kupata maji ya kunywa,maana tulikuwa na kiu ya kufa mtu.Nilimwambia dogo "tumepumzika vya kutosha hivyo hatuna budi kusonga mbele!".

Tulifika maeneo fulani kulikuwa kumechangamka sana,ulikuwa unapigwa muziki fulani hivi wa kilugha!,Kumbe maeneo hayo kulikuwa na harusi!,bila shaka harusi za vijijini wengi wetu tunafahamu zinavyokuwaga na mbwembwe,kulikuwa kumefungwa spika zile za vipaza sauti juu ya miti,huku wakiwa wamefunga Kanga na mashuka yakipepea juu ya miringoti.Basi dogo akaniambia tutafute mji au nyumba yeyote hapo tuombe maji ya kunywa,tulitafuta nyumba zilizokuwa hapo jirani ulipokuwa ukipigwa mziki hatimaye tulifanikiwa kupata nyumba moja ambayo tulimkuta mama mmoja aliyetupokea kwa ukarimu,tulimsalimia kisha tukamwomba maji ya kunywa.

Yule mama alituuliza "Nyinyi ni wageni haya maeneo?".

Nilimjibu "Ndiyo mama".

Yule mama akasema ametuuliza kwasababu ameona sura zetu hazikuwa za hapo kijijini,Yule mama alituletea maji na baada ya kunywa nilimuuliza Kutoka hapo kijijini mpaka Ikizu kulikuwa na umbali gani?,yule mama alituambia kwamba hakukuwa mbali sana kwani bado kidogo tungefika,alituambia tuifuate ileile njia tuliyokuwa tumekuja nayo.Baada ya masaa 4 tulifanikiwa kufika hapo Ikizu,ulikuwa ni mji au kijiji kilicho changamka,dogo aliamua kukaa chini maana alikuwa kachoka sana,ndipo nilimpigia simu yule mganga nikamueleza tulipokuwa tumefikia akasema tulikuwa bado hatujafika Ikizu,alituambia lile eneo tulilokuwa tumefika palikuwa maeneo ya Nyamuswa,alituambia tutembee tena kidogo kama nusu saa hivi tukifuata barabara tutafika Ikizu,kumbe sisi tulidhani tulikuwa tumefika kumbe ilikuwa bado,ilitubidi tuamke mahali tulipokuwa tumekaa tuianze tena safari.Baada ya dakika 45 tukafika hapo Ikizu,tulipofika nilimpigia tena simu huyo mganga akatuelekeza kuna maeneo tusimame akaja hapo kutuchukua.

Tulifika hapo Ikizu ilikuwa mida ya saa 11 jioni,kiukweli yule dogo alikuwa kachoka sana,yule mzee alituchukua kuelekea kwake ambako nako kulikuwa nje kidogo ya mji wa Ikizu.Tulipofika hapo kwake kulikuwa na watu wengi ambao ilionyesha wale watu walienda kufata tiba,baada ya muda mzee alituambia alishindwa kutuambia wakati tukiwa njiani maana alisema ingetukatisha tamaa!,Mzee alituambia ile sarafu tuliyokuwa tukiitafuta alikuwa nayo ila kuna kipindi alikuja mdogo wake ambaye aliondoka na hela za zamani,aliendelea kutuambia kwamba alikuwa na muda mrefu hajakagua kwenye masanduku yaliyokuwa na hizo hela maana hakuwa na kazi nayo kwa wakati huo.Baada ya hayo maelezo yake ambayo tayari yalishanikatisha tamaa,ilibidi nimuulize huyo mdogo wake alikuwa anapatikana wapi?,alituambia mdogo wake huyo kwa wakati huo alikuwa akiishi Ukerewe ila akasema kwakuwa simu yake haikuwa na salio nikamnunulie vocha ampigie,Kwakuwa simu yangu ilikuwa na dakika za kutosha ilibidi nimpe ampigie huyo mdogo wake,kweli Mungu saidia huyo mdogo mtu akapatikana na wakaanza kuzungumza,walizungumza kwa muda meefu,baada ya mazungumzo mzee alirudi tulipokuwa tumekaa.

Mzee alituambia yule mdogo wake alikuwa anasema hiyo sarafu tuliyokuwa tunaitafuta ilikuwepo ila yeye katoka yupo Ukerewe ila inabidi twende Bunda jirani na Chuo cha Ualimu kuna mke wake alikuwa nyumbani tutamkuta na angempatia maelekezo yote,tukifika hapo akishatuonyesha hiyo sarafu ingepaswa tuache hiyo hela tuliyokuwa tumekubaliana na huyo mzee,kiasi cha shilingi laki 3 ndipo tuchukue hiyo sarafu.Kiukweli baada ya hayo maelezo nilifurahi sana na nikapata nguvu mpya japo hatukujua kutoka hapo kwenda Bunda tungefikaje maana tulikuwa tumechoka sana na giza tayari lilishaanza kuingia.Nilimuuliza dogo usiku ule tungelala wapi na kula wapi? maana tukiangalia pale kwa mganga kulikuwa hakuna uelekeo wa kulala na kula maana kulikuwa hakueleweki!,dogo alinishauri tuondoke hapo kwa mganga ili tukajadiliane mbele.
Tulimuaga yule mganga na kuondoka na wala hakuonyesha mashaka ya sisi kuondoka pale usiku!,tulivyofika maeneo ya center ya hapo Ikizu nilimwambia dogo kwakuwa nilikuwa nina elfu 1 mfukoni,tutafute maeneo walipokuwa wanauza uji ili tunywe halafu tungejua la kufanya.


Itaendelea.................
 
Stori ishaanza kukosa Radha Haina hata uzuri wowte yaani ,kisa huko chini itaendelea nachokushauri usilete huo mwendelezo badala ya kusema itaendelea andika hata siku mbili au tano kabisa ikisha kamilika ndo uilete hapo hakuna hata Cha kukielewa ,smart people always doing smart thing
 
Stori ishaanza kukosa Radha Haina hata uzuri wowte yaani ,kisa huko chini itaendelea nachokushauri usilete huo mwendelezo badala ya kusema itaendelea andika hata siku mbili au tano kabisa ikisha kamilika ndo uilete hapo hakuna hata Cha kukielewa ,smart people always doing smart thing
Mpuuzi mmoja wewe
 
Stori ishaanza kukosa Radha Haina hata uzuri wowte yaani ,kisa huko chini itaendelea nachokushauri usilete huo mwendelezo badala ya kusema itaendelea andika hata siku mbili au tano kabisa ikisha kamilika ndo uilete hapo hakuna hata Cha kukielewa ,smart people always doing smart thing
Kichwa maji mmoja ww tulia kama umepigwa roba ww
 
Stori ishaanza kukosa Radha Haina hata uzuri wowte yaani ,kisa huko chini itaendelea nachokushauri usilete huo mwendelezo badala ya kusema itaendelea andika hata siku mbili au tano kabisa ikisha kamilika ndo uilete hapo hakuna hata Cha kukielewa ,smart people always doing smart thing
Huo usmart ungeanza kuuonyesha wewe, ungeenda kukaa hizo siku mbili au tano halafu ungekuja kusoma vipande vyote.

Hebu kaa kwa kutulia, acha ngenga
 
Duu nimegundua kuwa watu wengi wanapenda stories humu ndani
Yaani mtoa hadithi usipomalizia huu mkasa utawaudhi watu wengi Sana

Hebu on a watu wanavyokutetea huku[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Stori ishaanza kukosa Radha Haina hata uzuri wowte yaani ,kisa huko chini itaendelea nachokushauri usilete huo mwendelezo badala ya kusema itaendelea andika hata siku mbili au tano kabisa ikisha kamilika ndo uilete hapo hakuna hata Cha kukielewa ,smart people always doing smart thing

Mkuu kwani ukitunga yako ukaleta kuna shida gani.
 
Stori ishaanza kukosa Radha Haina hata uzuri wowte yaani ,kisa huko chini itaendelea nachokushauri usilete huo mwendelezo badala ya kusema itaendelea andika hata siku mbili au tano kabisa ikisha kamilika ndo uilete hapo hakuna hata Cha kukielewa ,smart people always doing smart thing
Unausmart gan Ww kwahy akae anaandika muda wote familia yake unailisha Ww
 
Back
Top Bottom