Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

MKASA WA PILI - Sehemu ya 48.


Inaendelea.............




Baada ya kuwa tumefika nyumbani nilimwita dereva ndani nikawa namuuliza maswali kadhaa ili nipate kufahamu pa kuanzia.

Nilimuuliza "Hivi Scolastica anakaa wapi?,huyo mwingine yeye aliniambia kwake ni Nyakato,je ni kweli?".

Dereva aliniambia "Ndiyo,bosi yule anakaa pale National ila Scola sijajua huwa anakaa wapi maana mimi wakati nafanya kazi pale kwa yule bosi nilikuwa nadhani ni ndugu maana walikuwa hawachani,muda wote walikuwa wanakuwa pamoja,nilipojua ni marafiki nilishangaa sana".

Dereva aliniuliza "Mbona umeuliza bosi kuna nini?".

Nilimwambia "Nilikuwa nataka nikawashitaki polisi ili wakawachukue".

Niilimdanganya dereva ili asinishitukie yale niliyotaka kuyafanya.

Dereva aliniambia "Bosi mimi nadhani kama uliamua tu kuwapa ile hela ungeachana nao tu,japo ni pesa nyingi lakini achana nao".

Nilimwambia "Wazo ni zuri sana,kiukweli nimeachna nao wajinga wale ipo siku watapata shida naamini watakuja tu".

Nilimwambia dereva lakini wakati huo moyo wangu ulishaamua siku nyingi kwamba niwashughulikie!.

Nilimwambia dereva "Basi sawa wewe kaendelee na shughuli zako".

Basi siku iliyofuata niliamka mapema nikajianda na mambo yangu kisha nikaondoka kuelekea site,sasa kwakuwa ilikuwa wikiendi,mke wangu alikuwa hakwenda kazini alikuwepo tu nyumbani,Kile chumba cha siri hakuwahi kabisa kukitilia mashaka kwasababu nilikuwa nikikiwekea zindiko,isingekuwa rahisi yeye kukumbuka.Yule Dalali alikuwa kanitaarifu kwamba kuna jamaa kaongea nao na alisema wangekuja kuzitazama zile nyumba hivyo nilipaswa niwepo pale site,nilipofika sikumkuta mtu zaidi yangu mimi na dereva,baada ya muda kidogo jamaa walifika pale wakiwa kwenye land cruiser nyeupe ikiwa na namba za DFP,tukasalimiana nao pale,yule dalali akawatambulisha kwangu kwamba mimi ndiye mmiliki wa zile nyumba.Jamaa mmoja aliniambia walikuwa wanataka zile nyumba mbili maana kuna familia ya bosi wao walitaka moja na mmoja wapo wa waliokuja naye pia alihitaji moja.Basi baada ya kukubaliana na hao jamaa nilimwambia dereva anirudishe nyumbani yeye aendelee na shughuli zake.

Nilipofika nyumbani kwakuwa ilikuwa mida ya saa 6 mchana nilikula na nilipomaliza nilielelekea chumbani kupumzika mpaka ilipofika mida ya saa 10 jioni ndipo nilipoamka.Nilimtafuta mke wangu hapo nyumbani sikumuona,nikamuuliza yule binti akasema alitoka kwenda kufanya mazoezi ya kutembea,ndipo nilichukua simu nikampigia Scolastica lakini haikupokelewa,nilijaribu kumpigia tena na tena lakini hakupokea simu,niliamua kumpigia yule mwanamke jeuri ambaye alikuwa mke wa bosi wa zamani wa dereva wangu nikamwambia "Samahani sana nakuomba umpigie simu Scolastica umwambie apokee simu yangu tafadhari".

Yule mwanamke aliniambia "Wewe sema shida yako bhana,Scola niko naye hapa na anakusikia".

Kiukweli toka awali sikuwa kabisa na niya ya kuwafanyia kitu kibaya ila kwasababu ya dharau za yule mwanamke ndizo zilikuwa zikichochea hasira yangu maradufu.Nilikuwa nimejaa hasira sana na sikutaka kumaliza kuongea naye nilikata simu.Nilichukua funguo za kile chumba cha siri nikaenda sasa kujiandaa ili nikawaadhibu kikamilifu.Nilipofika ndani nilichukua ile pembe nikailekezea ukutani ndipo ikaja sinema pale ukutani nikawaona wote wawili wakiwa wamekaa kwenye nyumba ambayo sikuifahamu,hawakuwa peke yao bali walikuwa na mwanamke mmoja wa makamo pamoja na mtoto ambaye umri wake ulikuwa kama miaka 3.Nilipomaliza kuwamulika niliondoa ile pembe ueleko wa ukuta nikarudi tayari kwa ajili ya kuondoka mpaka walipokuwa.

Niliukamata mkono wangu uliyokuwa na ile irizi Kuna maneno nilitamka pale ya kwamba kwa wakati huo ninapswa niwe ndani ya nyumba walimokiwemo wale viumbe niliowaona kwenye skrini pale ukutani!.Kilikuwa ni kitendo cha kufumba na kufumbua nilikuwa pale sebuleni!,nilihakikisha hakuna anayeniona nikajisogeza mpaka kwenye kochi alilokuwa amekaa Yule mwanamke wa bosi wake wa zamani dereva wangu aliyekuwa na dharau nyingi.Yule mama mtu mzima niliyemuona kwenye skrini pale ukutani nilimkuta na niligundua alikuwa mama mkwe wake na huyo mwanamke mwenye nyodo na dharau.Nilikaa pale mpaka saa 12 jioni maana walikuwa wakiangalia tamthilia kwenye luninga,giza lilipoanza kuingia nilisikia Scolastica anamwambia yule mwanamke kwa kumnong'oneza kwamba "Mimi naenda zangu nyumbani,leo mambo yameharibika".

Nilitaka kufahamu walichokuwa wakiteta maana nilikuwa nao sahani moja.

Yule mwanamke alimwambia "Hakuna kuondoka Scola maana yeye atalala na mwanangu kule chumbani halafu sisi tutalala zetu kama kawaida hivyo si rahisi kugundua".

Basi baada ya yale mazungumzo niliona yule mwanamke wa bosi wake wa zamani dereva wangu anaingia jikoni kupika,nilibaki pale kwenye kochi na Scolastica nikiwa namtazama bila ya yeye kufahamu chochote kilichokuwa kinaendelea.Ile nyumba ilikuwa kubwa na inavyoonekana yule jamaa yake alikuwa na pesa maana haikuwa mchezo hata kidogo!,chakula kilipoiva walitenga dining room na kila mmoja alielekea kupakua,walipo pakua walirudi kukaa sebuleni kuangalia luninga huku wakiendelea kula,yule mama mke wake na huyo mwanamke yeye alikaa dinning room akiwa anamlisha yule mtoto mdogo.

Sasa nilisogea karibu na chakula cha yule mwanamke mwenye aliyekuwa na dharau nikaanza kula chakula chake!,alipokuwa akila na mimi nakula,mpaka chakula kilipoisha akawa anasema "mmh mbona leo nakula si shibi?".

Alinyanyuka tena kwenda kupakua chakula kingine,nakumbuka ilikuwa ndizi iliyochanganywa na nyama,nilimfanyia vitimbi yule mwanamke alimradi tu kumkomoa.

Kama nilivyosema hapo awali ya kwamba ukiamua kumuabudu Mungu basi muabudu Mungu na kama ukiamua kuwa wa Ibilisi basi wewe kuwa wa Ibilisi,wale watu wangekuwa wa maombi wakaombea chakula kile kwa uaminifu basi hata nisingewasogelea ila kwasababu walikuwa watu wa maombi ya kuunga unga nilikula nao pamoja chakula bila wao kufahamu!.

Baada ya kula ilipofika mida ya saa 3 usiku yule mama aliaga akawaambia yeye anaelekea kulala,wao waliendelea kubaki pale sebuleni.Ilipofika mida ya saa 4 usiku,niliona yule mwanamke ambaye ni mke wa bosi wake wa zamani dereva wangu anamsogelea Scolastica wakaanza kunyonyana ndimi(denda),kiukweli nilishituka sana nikawa naendelea kuwatazama kwa mshangao!,madenda yalipokuwa yamekolea aliamka yule mwanamke akazima ile televisheni pamoja na taa za sebuleni wakaelekea chumbani.Baada ya kufika chumbani wakavua nguo vizuri huku nikiwatazama kisha wakaelekea wote bafuni kuoga,walipomaliza nusu saa wakawa wametoka,walianza kushikana na kuchezeana kama mke na mume!,ndipo nikagundua kwamba walikuwa wanafanya mapenzi ya jinsia moja(wanasagana),kumbe hata ule urafiki wao wa karibu uliyokuwa kama undugu ambao yule dereva aliniambia bila shaka uliletwa na hiyo hali!.

Basi wakati wakiwa kwenye lindi la mahaba mazito kuna namna niliifanya pale hata kama wangeniona na wakapiga kelele basi hakuna ambaye angesikia!.Niliamua sasa kujitokeza hadharani ili wanione,aliyekuwa wa kwanza kuniona ni yule mwanamke wa bosi wake wa zamani dereva wangu,kwasababu yeye alikuwa chini akiangalia juu.


Itaendelea................
 
MKASA WA PILI - Sehemu ya 49.

Inaendelea.............


Yule mwanamke aliponiona alipiga kelele na kumrusha Scolastica ambaye alikuwa juu yake na wote wakaanza kupiga kelele!,niliwafanyia ishara ya kidole kwamba wanyamaze.Niliwasogelea na kila mtu akawa ananiogopa.

Nilimwambia yule mwanamke "Mbona unaogopa,wewe si shujaa?".

Niliendelea kumwambia "Tulipokuwa tukiongea kwenye simu nilikuwa sikusikii vizuri na ndiyo maana nimekuja uniambie vizuri ili nikusikie".

Walipokuwa kimya huku wakiendelea kutetemeka,niliwauliza "Mbona mpo kimya?".

Scolastica aliniambia "Tunaomba utusamehe sitorudia tena".

Mpaka wakati huo hawakujua ni nini kilitokea maana wote ni kama walipigwa na bumbuwazi,Yule mwanamke yeye alikuwa akipiga kelele na kumuita yule mama mkwe wake lakini hakuna aliyesikia zile kelele zake!.Kwakuwa nilikuwa nimekasirishwa na namna walivyonifanyia toka mwanzo nilihakikisha nawaadhibu ili liwe fundisho kwao huko waendako.Nilimsogelea Scolastica nikamshika mkono palepale akawa kasinzia na kujilaza kitandani asijue nini kinaendelea,ndipo nilipomsogelea yule mwanamke wa bosi wake dereva wangu aliyekuwa nikampulizia upepo usoni akawa hajielewi!,nilimsogeza kwenye kitanda nikaanza kumkung'uta bakora kisawasawa,alikuwa akilia sana lakini sikujali,nilipomaliza kumkarabati mbele nilimgeuza na nyuma pia nikaanza kumuingilia,alianza kuhema kama mtu aliyekosa pumzi,nilipoona naweza kumuua kwa zile bakora ndipo nilimwachia akaanguka chini kama gunia,wakati huo nilipokuwa nikiwakarabati nilikuwa nikitumia dawa moja ambayo niliichanganya kishirikina pamoja na ile dawa niliyopewa na mzee Nchibaronda,ile dawa ilikuwa na nguvu na uwezo wa ajabu, endapo nilikuwa nikitumia ile dawa na nikakupiga bakora za kim-kakati ni lazima ufe au uzimie,kwakuwa wao walikuwa wameniudhi toka awali,niliapa lazima wanitambue mimi ni nani kwa wakati huo.

Yule mwanamke alipoanguka pale kitandani kama gunia huku akiwa hoi,ndipo nikamsogelea Scolastica naye nikamuamsha na wembe ulikuwa ni uleule kama aliyoupata mwenzake,baadae sasa ili niwaonyeshee kwamba nilikuwa si mtu wa kawaida,niliwaamsha wote nikawa namshughilikia mmoja na mwingine akishuhudia na nikimaliza kwa huyu nahamia kwa huyu,nilipoona sasa hawana nguvu,wakiwa wote wamezidiwa na bakora ndipo niliwaachia.Scolastica nilitokea kumpenda sana ila kwasababu huyo rafiki yake alikuwa na maneno ya shombo ndiye aliyemponza,nilimwangalia sana Scolastica alikuwa akitia huruma,yeye ndiye aliyesababisha nikwaacha hai maana asingekuwa yeye nilikuwa nina waua pasipokuwa na huruma maana namna yule mwanamke alivyokuwa kanikwaza nilikuwa nikimwangalia hasira haziniishi.

Sasa sikutaka kuondoka nikawaacha hivihivi nilitaka niwaaibishe kwa yule mama mkwe wa mke wa bosi wa zamani wa dereva wangu.Niliwachukua nikawarejesha kama kawaida,niliikamata ile pembe niliyokuwa nayo nikawanyooshea,ndipo waakaanza kusagana kama nilivyowakuta,nilihakikisha watafanya vile mpaka yule mama mkwe atakapo wakuta wakiwa uchi kama walivyozaliwa,ule mlango niliudhibiti usifunge kabisa!,walianza kushughulikiana kama mwanzo walivyokuwa wakifanya na safari hii sikutaka kabisa waelewe kitu wala wasikie kitu,akili yao iwe hapo kwenye lile tendo mpaka watakapokutwa na yule mama.Nilikaa pembeni kushuhidia ile shoo ya maajabu,kwakuwa walikuwa wanafanya bila kupenda,sauti kubwa za miguno zilimfikia mama mkwe chumbani ndipo aliamka kutaka kuja kuangalia kulikuwa na kitu gani,namna zile sauti zilivyokuwa ni kama mwanaume na mwanamke wanafanya ngono huku wakitoa sauti za mahaba,hivyo ndivyo ilivyokuwa,waliendelea kufanya ule uchafu wao kwa spidi kali pasipokuelewa jambo lolote.

Yule mama alipofika pale mlangoni aliingia chumbani kuangalia kulikuwa kuna nini!,alipofika na kushuhudia yale yaliyokuwa yakiendelea,alikuwa kama kapigwa na shoti asiamini kile alichokiona!.Yule mwanamke na Scolastica wao walikuwa bize kwenye mahaba mazito kiasi kwamba hakuna aliyefahamu chochote.Nilipohakikisha yule mama mkwe kashuhudia ile sinema nilirudi kwenye hali yangu ya mwanzo ambayo hakuna mtu yeyote mle ndani ambaye angeniona ila mimi niliwaona wao,hapo kabla ni kwamba wale wanawake walikuwa wakiniona mubashara,ila yule mama mkwe alipoingia mle chumbani niliamua kupotea wasinione wote ila mimi nikawa nawaona wao,sasa nilipoona yule mama akiwaangalia niliwarudisha wao pia kwenye hali yao ya kawaida ili aibu iwashike,walipokutana uso kwa uso ndipo Scola akaruka kama digi digi asielewe ni nini kilikuwa kimetokea,Kila mtu alikuwa akimshangaa mwenzake!.

Yule mama aliwauliza "Ndiyo mnafanya nini hiki wanangu?".

Yule mama aliendelea "Haya mambo mmeyaanza lini?".

Yule mama aliuliza "Ina maana kumbe mwanangu asipokuwepo ndiyo mambo haya mnayoyafanyaga?".

Yule mama alikuwa akiongea huku akionyeshwa kusikitishwa na kile kilichokuwa kinaendelea.

Aliendelea kusema "Mama........mbona unanitia haibu hivyo,ina maana mwanangu hakutoshelezi mpaka mfanye huu uchafu?"

Wakati wote huo hakuna aliyejibu kitu kwasababu ya ile aibu na wakati huo walikuwa uchi kama walivyozaliwa,basi baada ya kushuhudia yale yaliyotokea na kuhakikisha nimewaaibisha niliondoka zangu kurejea nyumbani maana ilikuwa usiku wa saa 8.

Haya mambo yote niliyafanya wakati nikiwa bado ninamtumikia Ibilisi na mali zake,hivyo sikuwa na akili ya kawaida kama niliyonayo leo,kuua kwangu ilikuwa kitu cha kawaida sana ambacho leo siwezi hata kufikiria tu,kutembea na wake za watu kwangu ilikuwa kawaida sana,kuwaingilia wanawake na wanaume kinyume na maumbile kwangu ilikuwa kawaida na sikuwaza chochote,ningekuwa na akili kama nilizonazo leo sidhani kama huo ushenzi ningeufanya!,Kuna watu wazima na akili zao timamu ambao mpaka leo kumuingilia mwanamke au mwanaume mwenzie kinyume na maumbile kwao ni jambo la kawaida ila ndugu zangu tambueni ya kwamba hiyo si akili ya kawaida,kama unafanya hivyo tambua bado una alama ya Ibilisi ambayo hutokaa uchomoke labda ujisalimishe kwa Mungu akupatie ulinzi wake,vinginevyo utafia mikononi mwa shetani,Yangekuwa mazuri mpaka leo ningekuwa nayafanya lakini baada ya kugundua hakuna jema huko bali ni uangamivu niliamua kuachana nayo na kumrudia Mungu na kuwa mtu mwaminifu kabisa.

Basi nilirudi mpaka mle chumbani nikaziacha zile zana za kazi kisha nikakifunga kile chumba vizuri na kuelekea zangu chumbani,nilimkuta mke wangu amelala na hakuweza kujua chochote ndipo nikapanda kitandani kulala.

Asubuhi mke wangu alikuwa wa kwanza kuamka na alianza kuniuliza "mume wangu jana ulikuwa wapi na umerudi muda gani maana nilikutafuta bila mafanikio,kupiga simu yako ikawa inaita ikiwa sebuleni".

Aliendelea kuniuliza "Kwani ulienda wapi na nani alikufungulia mlango?".

Sasa lile swali la mlango liliniwazisha akili lakini nilimjibu "Kuna rafiki yangu alinipigia simu mida ya jioni wakati wewe umeenda kufanya mazoezi,alitaka nikaonane naye kwake tuzungumze biashara moja hivi,mbona mama jana nimerudi mapema tu,sema nilikuta umelala,nilipogonga sana mlango dada wa kazi akaja kunifungulia".

Aliniuliza "Mbona hukuondoka na gari?,ulitumia usafiri gani?".

Nilimwambia "Nilichukua bodaboda maana jamaa aliniambia ningemkuta akiwa ananisubiri na gari yake,hivyo sikuona sababu ya kuchukua gari?".

Mke wangu aliniambia "Ok sawa mume wangu,lakini nisamehe pia kwa kugonga mlango muda mrefu bila kusikia,unajua huyu mwanao aliyeko tumboni ananifanya sikuhizi nalala kama nimekufa?".

Nilifahamu fika nilikuwa nimemdanganya,sikuwa na namna nyingine ya kujitetea,niliona nidanganye tu ili asije kunishitukia.Baada ya yale mzungumzo,aliniaga akasema anaelekea kwenye mazoezi ya kutembea,aliniacha nikiwa bado nimelala!,nilipona ameondoka niliamka fasta kuelekea kwenye kile chumba cha siri kutengeneza dawa fulani hivi ambayo ilikuwa inafubaza akili,nilipomaliza niliondoka nikakifunga kile chumba nikaingia kwenye kile chumba cha yule dada wa kazi nikaipuliza ile dawa juu ikaenea chumba kizima,ilikuwa siyo rahisi kugundua maana nilitaka yule dada wa kazi atakapoingia mle chumbani tu,basi akili yake ibadilike na endapo mke wangu akimuuliza kama ni kweli alinifungulia mlango asikatae aseme ndiyo.Nilipohakikisha kila kitu kipo sawa nilirudi zangu chumbani kulala!.



Itaendelea...................
 
MKASA WA PILI -Sehemu ya 50.

Inaendelea.............


Niliamka muda ukiwa umeenda sana,mke wangu tayari alikuwa ameshatoka kufanya mazoezi,kwakuwa ilikuwa jumapili mke wangu alinambia nimtoe out kuelekea mjini.Sasa kwasababu alikuwa akifahamiana na marafiki zake wengi walikuwa wamekubaliana kwamba siku hiyo tungekuwa wote tukipata vyakula na vinywaji kwa pamoja ili wao pia wanifahamu mimi kama shemeji yao.Nilifahamu kabisa wanawake wa mjini ili wakupe heshima ya kutosha ni kuhakikisha unawanywesha na kuwalisha mpaka wachanganyikiwe,uzuri kwa kipindi hicho pesa ilikuwepo ya kutosha,sikutaka kabisa dharau za kijinga!.Sasa kwakuwa mke wangu alikuwa akijua kuendesha gari nilimwambia dereva siku hiyo akae apumzike.Tulipomaliza kujiandaa tulielekea sehemu moja ambayo ilikuwa imechangamka wakati huo ikijulikana kama Villa park resort,tulipofika hapo tulimkuta yule rafiki yake mke wangu wa siku zote wanayefanya naye kazi na baada yetu walikuja akina dada wengine wawili wakiwa kwenye Toyota Spacio,hawa akina dada sikuwahi kuwafahamu na ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kuwaona,hivyo kwa pamoja kwenye meza tulikuwa 5,kwenye ile meza mwanaume nilikuwa mimi peke yangu.

Mke wangu aliwaambia "Jamani huyu ndiye mume wangu anaitwa ..........".

Pia mke wangu akaniambia "Baby hawa ni marafiki zangu,huyu mwingine bila shaka unamfahamu ila hawa wawili sidhani kama unawafahamu".

Akaendelea kuniambia "Huyu anaitwa........"(alimtambulisha aliyekuwa upande wake wa kushoto)

Akaendelea kuniambia "Na huyu anaitwa .........."(alimtambulisha aliyekuwa upande wake wa kulia).

Kwakuwa na mimi sikutaka kabisa unyonge nilimuita muhudumu nikamwambia awasikilize kila mtu anachotumia awahudumie.Niliwaambia wanywe na kula mpaka watosheke!.Baada ya muda kidogo kupita alinipigia simu Zainati,hiyo ilikuwa mida ya saa 9 alasiri,nilisimama kuelekea pembeni kidogo kuongea naye.

Nilimwambia "Hello mama wewe mzima?".

Aliniambia "Mi mzima baba,uko wapi?".

Nilimwambia "Nimekuja mjini mara moja kuna kazi naifanya".

Aliniambia "Sawa nakuomba ukimaliza shughuli zako uje nyumbani mara moja"

Nilimuuliza "kuna usalama kweli?"

Aliniambia "Usalama upo baba nataka tu nikuone".

Nilimwambia"Sasa mimi kwenu sipafahamu nitafikaje".

Aliniambia "Utamwambia dereva wako akulete mpaka maeneo ya Capri point,ukifika utanipigia simu".

Nilimwambia "Leo nipo peke yangu mama dereva kapumzika kidogo na gari nimeacha nyumbani".

Aliniambia "Sawa haina shida baby utachukua tu hata taxi ukifika huku maeneo ya Capri point utanijulisha nije nikuchukue".

Nilimuuliza "Kwani hapo nyumbani upo na nani?".

Nilijaribu kumdodosa ili nifahamu maana kwenda kwenye nyumba za matajiri tena wa kiarabu ilitaka kidogo ujasiri au nguvu za ziada.

Aliniambia "Mimi sipo nyumbani baby nipo kwa mama mdogo,kwao...........(Alimtaja yule ndugu yake ambaye alikuwa mtoto wa mama yake mdogo niliyemuua siku zilizokuwa zimepita baada ya kunidharau akitaka kuniachanisha na Zainati)".

Basi baada tu yakuniambia vile nilijua tayari ile ni fursa maana toka siku ile nilipoenda kwenye hiyo nyumba nilisema yule mama ambaye alikuwa mama yake na yule binti ni lazima nije nimshughulikie siku moja kwakuwa alikuwa mzuri sana.Nilimwambia Zainati nikitoka mjini ningepitia huko kwao.

Nilirudi mpaka pale kwenye meza nikamuita mke wangu pembeni nikamwambia "kuna mahali inapaswa nikimbie mara moja nimehitajika haraka,naweza kuwahi kurudi au nikichelewa tutakutana nyumbani!".

Kwakuwa kipindi hicho mke wangu alikuwa anywi wine sababu ya ujauzito,nilifahamu angeweza kuendesha gari mpaka nyumbani bila shida yeyote.

Nilimwambia mke wangu "Kuna hela hapo kwenye droo ndani ya gari milioni 2 hivyo msiwe na wasiwasi,waambie rafiki zako waagize wanachotaka".

Niliwaambia wale rafiki zake mke wangu kwamba "Jamani mimi nawaacha kidogo maana nimepata simu ya dharula".

Niliwaaga nikaondoka zangu kuelekea kwanza nyumbani kujiandaa,nilimshukuru sana Zainati kunipigia simu muda ule maana nilikuwa sijui nitapiga stori gani na ile kruu ya wale wanawake maana hayakuwa mazoea yangu kabisa!.

Nilichukua taxi mpaka nyumbani,nia na malengo ya mimi kurudi nyumbani,ni kwenda kutengeneza dawa ambayo ningejipaka mwilini na nitakapofika hapo nyumbani kwa mama yake mdogo Zainati nikimpa tu mkono basi ilikuwa imekweisha,Yule mwanamke nilipanga toka siku ya kwanza kwamba lazima na yeye nimuweke kwenye listi ya wanawake wazuri niliyotembea nao.

Kila kitu nilichokifanya kwa mke wangu enzi hizo akiwa shemeji yangu ile siku ya kwanza mpaka nampata ndiyo kitu nilichoenda kukifanya kwa mama yake mdogo Zainati,maana hawa wote wawili wao niliwatengenezea dawa ya kujipaka,nia na madhumuni ya kufanya hivyo nilitaka niwe najilia kiulaini kila ninapomuhitaji kwa wakati ninaotaka na sikutaka kuwakomoa bali kujipatia raha na starehe!,wale wanawake wote ambao nilitaka kuwakomoa dozi yao ilikuwa tofauti kabisa na hii!.Basi baada ya kumaliza kuianda ile dawa na kujipaka nilivalia nadhifu sana,kiukweli nilikuwa nina pendeza sana wakati huo maana nilikuwa nina ang'avu na sura ya pesa!.Pesa haikuwa tatizo kwangu,ndiyo maana safari zote za hapo mjini ulikuwa hukosi milioni 2 kwenye gari yangu.

Nilipomaliza kuvaa nabkupendeza nilijipulizia marashi yaliyokuwa na harufu nzuri nikaondoka zangu nje,nilimpigia simu dereva wangu nikamwambia anitafutie dereva taxi yeyote anayemfahamu aje nyumbani kunichukua.Haukupita muda mrefu kuna namba ngeni ilinipigia simu kumbe alikuwa huyo dereva taxi aliyeelekezwa na dereva wangu,alitaka nimuelekeze nyumba ipo maeneo gani nikamwambia anisubiri barabarani.Tuliondoka nyumbani kuelekea sasa kwao Zainati,tulipofika maeneo ya Capri point nilimpigia simu Zainati nikamuelekeza tulipokuwa tumesimama,hayo maeneo nilikuwa ninayafahamu maaana siku zile wakati nikiwa naenda kwenye lile tukio la kumuua yule ndugu yake nilipafahamu vizuri,sasa sikutaka aelewe chochote ndiyo maana tukapaki mbali kidogo na yale maeneo ya hapo kwa mama yake mdogo.Zainati alikuja kunichukua kuelekea nyumbani,nilipofika yule mama sikumkuta pale nje,hatimaye tukaingia ndani nikamkuta yule binti wa kike ambaye alikuwa mtoto wa mwisho wa yule mama,hakukuwa na mtu mwingine tofauti na Zainati na yule binti hapo sebuleni.Baada ya dakika kama 5 yule mwanamke alitokea chumbani akiwa anakuja pale sebuleni!,hakukaa maana alikuwa kama akitafuta kitu,hivyo alikuwa na hae hae!.

Zainati alimwambia "Mama huyu ni yule mchumba wangu ambaye nilikueleza siku ile".

Yule mama aliniambia "Ooh karibu baba".

Nilimwambia "Shikamoo mama".

Sasa nilisimama kumsalimia nakampa na mkono kama salamu nyingi za kitanzania tulivyozoea.

Yule mama aliitikia "Marhaba baba karibu sana".

Yule mama alisema "Basi nyie endeleeni maana niko bize kidogo".

Yule mwanamke akaondoka akatuacha pale sebuleni mimi na Zainati na yule mtoto mdogo wa kike.



Itaendelea..................
 
Uongo mwingine Huu hapa ashura apitie Nairobi nchi ya watu faster hivo? acha uongo hangeweza ku cross border ya sirari bila pass!!!
 
Uongo mwingine Huu hapa ashura apitie Nairobi nchi ya watu faster hivo? acha uongo hangeweza ku cross border ya sirari bila pass!!!
Mkuu umesoma kweli hiki kisa vizuri au umekurupuka,kwani aliyekwambia walipita bila pasipoti nani?,au kuna mahali nilisema walipita bila pasipoti?
 
Uongo mwingine Huu hapa ashura apitie Nairobi nchi ya watu faster hivo? acha uongo hangeweza ku cross border ya sirari bila pass!!!
Mkuu ukiona Kuna uongo basi acha usisome.

Mnaleta maneno yenu mnamchelewesha mtoa mada kutusimulia bwana wee
 
Jamani kama unaona ni story ya kutunga si uache kusoma,maana watu mmekomaa ya kutunga ila bado unasoma,mnakera sana kwa kweli
Hata uongo uliiusoma/ulisemwa ukaujua ''uongo'' hakuna kifungu JF au popote kinasema usimsikilize ''muongo '' au usimjue muongo''!! utamjuaje bila kumsoma muongo na njia zake???? elewa kwanza na tafakari vizuri kabla ya kuandika ulichokiandika.
 
Hata uongo uliiusoma/ulisemwa ukaujua ''uongo'' hakuna kifungu JF au popote kinasema usimsikilize ''muongo '' au usimjue muongo''!! utamjuaje bila kumsoma muongo na njia zake???? elewa kwanza na tafakari vizuri kabla ya kuandika ulichokiandika.

Sawa kaka wewe mwerevu na mkweli tumekubali [emoji1376]
Chukua kombe[emoji471]umetisha kabisa na upo smart kichwani kwakweli tumekufurahia
Asante
 
Uamuzi ni wako uendelee kusoma au uachane nayo.
Kwanza Tarime hakuna majini pale!!! yatakaa wapi wakati kila mtu wilayani anakula bangi tena basi lile la kibuyu mbichi, unatumia ring ya baiskeli kulivuta!! wala lango la kuzimu hakuna pale!! kwa sababu moja kubwa!!

majini kamwe hayawezi kukaa mahali ambapo watu wana tabia hizi hapa chini ...

1;Hawatawadhi!! hebu fikiria mtu anatemebea na nyaa ya siku tano Makalioni, hili mkurya kwake ni sawa tu, hajui hayo!! ukitaka mkosane maisha yote!! mwambie mkurya ashike kopo la chooni akatawadhe nyaa yake utakiona!!

wanaita kinyesi! mtakosana dakika sifuri!! km mie muongo nenda hapo kipunguni kajaribu ujioneee!! na kwa taarifa yako kawaida ya nyaa zao ni ngumu km jiti kavu!

hii natokana na matumizi makubwa ya ugari ile ya uresi na Mahemba kwa kimoro! ili kukwepa kujichafua aendapo haja kubwa! pia kwenda chooni mara kwa mara! mkurya aweza piga siku saba bila nyaa! hii imefanya nyaa zao ziwe ngumu na hkn shoga kure!! hebu fkiria nyaa inayo pitisha kimba km jiti!!!! kajimshsdede si katavunjika??

Ukikutana na Mkurya tuu! Tarime yote ile! Mugumu mpaka Isbania nchini kenya, jua hili la utamaduni wa kuto tawadha linawahusu hawa wotee watoto, wake kwa wanaume! hata humu wamo nawajua Wakurya wote!! km nabisha wajitokeze wakatae!!!

2; Wilaya nzima!! lango la kuzimu katika wilaya ile hakuna, uliza mchawi yeyote hata waturutumbi tu hkn, ukiwa na majini sijui mchawi wewe ni panga tu lina kuhusu! tena lile kali la mara moja unapigwa mchana kweupeeee! ukasimulie vizuri na baada ya kukufanyia hivi hakimbii mtu!! sijui kuogopa police nooo!! na

polisi pia ktk kamata yao!! waje vizuri!! wajipange hasa au ataenda yeye polisi, ndo maana yaitwa kanda Maalumu!!!! tangu zamani za mkolioni ni utamaduni wao usiwahukumu! wako vizuri sana. na ndivo walivyo!

3; Wakurya hawana majini wala uturutumbi!! wao ni kata funua! moto mchibuyu ukiongea kijini jini wanajua unajifwanya. unawazungusha tu! na ubabaishaji mwingi hutaki kufanya kazi, mvivu tu weye mapanga shwaaa!! ile wilaya yote mchawi hakatizi salama!! sembuse majini!! kuna wachawi humu waulize!

4;Hakuna mkurya anajua kiswahili kilichonyooka km cha jini Maimuna kure taarime! ni Mura Tata mbuya, Ohoire kwishne, anachapa kaziii kazi na wewe!! ukiongea kiswahili kireefu kule Tarime ni sawa msomi kuongea kwa Mzaramo kiingerza!!

5;hawana muda wa kusikiliza vitu vyenye ukakasi mazungumzo mareeefu!! sijui ukanunue vinguo vipajama!! weee! avae nanii!! mkurya kabisa ararie kipajama wajameni uwiiii!! tuniani kuna mambo hivi kihuhutyoo! cha kuratee!! kikipigwa hakuna muda wa kusubiri unatoka ivoivo unaanza faster!!! kwa kufuata nyayo!! utasikia ''chegheyee!!! ''chegheyeee! Kong'wiii!!??

km alikuja na vijini vyake pale anakuja kaka mkubwa tu anamaliza huo ujinga wooote!! wao ni kazi kazi tu!! kina mama watoto wababa! ni twende kazi! kazi mwanasiasa akija vibaya na maneno ya kizembezembe ni viboko tu hawataki mchezo!!

Si unaona yule afisa usalama Bwire mwenye mafunzo ya kijeshi! alivo muingia kizembe zembe Mkurya original Zakharia tena raia tu, alicho kipata kila mtu anajua nadhani yule jamaa aliacha kazi,

hata Magu kwenda kule huwa anajipanga sana sana!! hakutabiriki sembuse kajini makata hako! hkna bunduki kanapigwa fimbo tu na wasichana vigori tu wanaotoka saro!!

Mkurya ataiba ng'ombe saa ngapi? kukamua saa ngapi? kukamata Lighembe saa ngapi eti Mkurya kabisaa akafute fute vi maji ndani, eti sababu mtu ana kajini kake hapa kanamsumbua kalifungua mabomba usiku!!! thubutuuuu!!! kata futa kenyewe!

Hii ni hadithi ya kutunga sema hivo km ulitaka kuifanya kweli ungeiongelea kwa mazingira ya Wazaramo wa DSM. hapo sawa! kure Mara bin Tarime ni kama ri nchi ra jirani!! haikufaa kuwa Tansania yenu hii!!!
 
Back
Top Bottom