Mikasa ya kusikitisha ya rafiki zangu iliyowahi kunisikitisha sana

Mikasa ya kusikitisha ya rafiki zangu iliyowahi kunisikitisha sana

Glenn

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2015
Posts
69,329
Reaction score
164,730
Wakuu sana pokeeni salamu zangu.

Naomba leo nisimulie visa viwili vya kusikitisha ambavyo niliwahi kushirikishwa na rafiki zangu kwa nyakati tofauti.

KISA CHA KWANZA:
Huyu ni rafiki yangu kipenzi sana, na naomba nimpe jina Tonia (jina sio halisi)


Tonia nilikutana naye katika mazingira yangu ya kazi. Ni msichana mrembo sana na aliyebarikiwa karibu kila kitu ambacho binti/ke angetamani kuwa nacho na mwenye mvuto ambao ulisababisha kila mahali apitapo kazi zisimame kwa muda ili kumtazama.

Nakumbuka siku ambayo alikuja ofisni kwangu na alipotoka alipishana na vijana kama watano hivi wa kazini kwangu...walimsindikiza kwa macho hadi anatoka getini cha ajabu kila mmoja aliguna kwa sauti na wengine wakasema ee Mungu unajua kuuumba😅

Kwa kadiri siku zilivyokwenda tulijikuta kila mtu akivutiwa na mwenzake, mvuto ambao mwisho wa siku tulijikuta
tukiwa marafiki wakubwa.

Kutokana na safari yetu mpya ya urafiki, ziliingia zama zile za kila wakati kutamani kujua mwenzie yuko wapi na
anafanya nini kwa wakati husika.

Ulifika wakati Tonia akawa na wivu mkubwa na kutaka kuwa nami kila wakati. Hili halikuwa gumu kwangu kutokana na nature ya kazi yangu kuwa mimi ndiye alpha na omega kazini kwangu.Kila wakati aliponimiss ilikuwa ni kunyanyua simu na kutoa taarifa kuwa D..najiandaa kuja...uko ofisni au...nije?

Kutokana na muonekano, ukarimu wake hakika nami Glenn nilihisi kuwa sasa Mungu nami amenikumbuka na kunipa paradiso na pumziko la moyoduniani japo niseme kweli uhuru wangu ulifia pale kwasababu kila tulipokwenda si hotelini' shopping au popote tulipopita tuligeuka kivutio' hii ilininyima kutembea kwa miguu tukiwa pamoja.


Niwe mkweli Tonia alibadili upepo wote ndani ya moyo wangu kwa jinsi alivyoonyeshs kunikubali, kunipenda
na alivyonisemesha kwa upendo ambao haukuwa na chembe ya unafiki.

Alichokosea Tonia ni kitendo cha kuonyeshs kunipenda kwa moyo wake wote bila kujua linapokujasuala la kupenda Glenn huwa hujui kutania kwa hiyo ikawa ni sawa petrol na kiberiti kilichowashwa vimewekwa
pamoja. Naomba nihame hapa naona nashindwa kuhimili kusimulia..

Zilipita siku, miezi hatimaye miaka, kuna siku Tonia alipata msiba wa mtu ambaye kwa wakati huo alimfahamu kama SHANGAZI YAKE nimeandika kwa herufi kubwa kwasababu ndiko mkasa wake wa kusikitisha uliko.

Wakati Tonia anapata huo msiba mimi nilipata safari ya ng'ambo hivyo sikuweza kumsindikiza. Baada ya majuma matatu nilirejea kutoka safarini.

Baada ya kurejea nilimpasha habari na hakukawia kuondoka huko alilokwenda msibani alinifuate town.
Aliporejea alinyoosha moja kwa moja kazini.

Mara alipowasili na kuniona alikuwa ana uso wa simanzi kupita kawaida na kama kawaida alikimbilia kifuani na kunikumbatia kwa muda mrefu na akalia sana hadi nilikuta nakosa uvumilivu nami simanzi ilinijaa sana japo nilijikaza kiume na kuanza kumbembeleza na kumsihi ajikaze na ajipe moyo aache kulia maana hiyo ni kazi ya Mungu.

Pamoja na kumtulliza sana sikuona dalili ya kufarijika kwa Tonia na ilikuwa kama nimetonesha kidonda kibichi moyoni mwake. Katika kuendelea kumfariji ghafla Tonia alisema kwa sauti ya ya chini na yenye simanzi:

(Glenn, tangu nikufahamu umekuwa rafiki wa kweli, mpenzi ambaye sijawahi kujuta kupendwa nawe na kama baba kwangu kwani hujawahi kuniangusha kwa lolote na umeyabadilisha maisha yangu kwa kiwango cha juu sana hivyo kutokana na heshima hiyo naomba nikushirikishe SIRI ya familia yangu iliyofichwa kwa muda wa miaka 25 na ambayo leo hii inaniliza kwa uchungu) note: Tonia alikuwa na umri wa miaka 25.

Baada ya Tonia kusema maneno haya nilipata mshtuko mkubwa kwani pamoja na hayo alinisisitiza kuwa nisiwajulishe dada zake kwani hii siri kwani wao bado hawaifahamu isipokuwa kaka yake mkubwa tu
na baba na mama yake tu.

Baada ya kumhakikishia kuwa kamwe sitawaambia hii siri ndipo alipoanza kunisimua. Naomba niseme kidogo kuhusu dada zake na familia yake. Katika familia yao walizaliwa wasichana wanne na upande wa kiume wakowawili, na yeye amezaliwa wa tatu akifuatiwa na mabinti mapacha wawili warembo sana sana japo hawamfikii dada yao Tonia na wote niliwfahamu kwa ukaribu sana kwani mahusiano yetu yalianza kuvuka mipaka. Tonia ndiye binti anapendwa upendo usiokuwa wa kawaida na familia yake hasa baba kiasi cha kuwa kero kwake kwani kila kitu kidogo tu baba yake anamwita nyumbani

Turudi kwenye jambo la linalomuumiza Tonia alilloliita ni SIRI ya familia na alianza kama hivi:

TONIA: Glenn unakumbuka yule shangazi yangu ambaye nilikuonyeshs picha kuwa anafanana nami sura hadi umbo?

GLENN: Ndio namkumbue si ndiye aliyefariki sio?

TONIA: Glenn kumbe huyo ndiye mama yangu mzazi..(akali machozii)

GLENN: Tonia unasema???? kwani mama yake si .....? nilimtaja mama aliyemlea tangu udogoni.

TONIA: Ndio maana nilitangulia kukwambia ni siri ya familia, hili jambo baada ya msiba baba aliniita na kuniambia kuwa huyo aliyefariki ndiye mama yangu mzazi. Nilimuuliza baba ilikuwaje anifiche hii siri siku zote? Lakini alinijibu kuwa hakutaka nijue hili jambo alinificha kwasababu baba yangu alimtelekeza mama na mama alipitia hali ngumu hivyo hakutaka niyajua haya kwani yangeniumiza. Glenn mpenzi wangu hili jambo lina utata mkubwa nashindwa nisemeje lakini hii ndio hali halisi.

Baada ya kusimuliwa hili jambo ambalo mimi kama mtu mzima niliunganisha dots na kugundua kuwa Tonia alizaliwa kwa mtu na mdogo wake. Yaani baba yake ni mjomba na mama ni shangazi yake. Naomba hili niishia hapa nitarudi wakuu kwa mkasa wa pili


Mkasa wa pili soma post #15
 
MODS: NAOMBA MSIUHAMISHE UZI HUU PLZ; nisaodieni ku edit heading isomeke, MIKASA YA KUSIKITISHA ILIYOWAHI KUNISIKITISHA

Wakuu sana pokeenisalamu zangu.

Naomba leo nisimulie visa viwili vya kusikitisha ambavyo niliwahi
kushirikishwa na rafiki zangu kwa nyakati tofauti.

KISA CHA KWANZA:
Huyu ni rafiki yangu kipenzi sana, na naomba nimpe jina
Tonia (jina sio halisi)


Tonia nilikutana naye katika mazingira yangu ya kazi.
Ni msichana mrembo sana na aliyebarikiwa
karibu kila kitu ambacho binti/ke angetamani
kuwa nacho na mwenye mvuto ambao ulisababisha
kila mahali apitapo kazi zisimame kwa muda ili kumtazama.

Kwa kadiri siku zilivyokwenda tulijikuta kila mtu akivutiwa
na mwenzake, mvuto ambao mwisho wa siku tulijikuta
tukiwa marafiki wakubwa.

Kutokana na safari yetu mpya ya urafiki, ziliingia zama
zile za kila wakati kutamani kujua mwenzie yuko wapi na
anafanya nini kwa wakati husika.

Ulifika wakati Tonia akawa na wivu mkubwa na kutaka
kuwa nami kila wakati.
Hili halikuwa gumu kwangu kutokana na nature ya
kazi yangu kuwa mimi ndiye alpha na omega kazini
kwangu.Kila wakati aliponimiss ilikuwa ni kunyanyua
simu na kutoa taarifa kuwa D..najiandaa kuja...uko
ofisni au...nije???

Kutokana na muonekano, ukarimu wake hakika nami Glenn
nilihisi kuwa sasa Mungu nami amenikumbuka na kunipa
paradiso na pumziko la moyoduniani japo niseme kweli
uhuru wangu ulifia pale kwasababu kila tulipokwenda si hotelini'
shopping au popote tulipopita tuligeuka kivutio'
hii ilininyima kutembea kwa miguu tukiwa pamoja.


Niwe mkweli Tonia alibadili upepo wote ndani ya moyo
wangu kwa jinsi alivyoonyeshs kunikubali, kunipenda
na alivyonisemesha kwa upendo ambao haukuwa na chembe
ya unafiki.

Alichokosea Tonia ni kitendo cha kuonyeshs kunipenda kwa moyo
wake wote bila kujua linapokujasuala la kupenda Glenn huwa hujui kutania
kwa hiyo ikawa ni sawa petrol na kiberiti kilichowashwa vimewekwa
pamoja.........naomba nihame hapa naona nashindwa kuhimili kusimulia..

Zilipita siku, miezi hatimaye miaka, kuna siku Tonia alipata msiba wa mtu
ambaye kwa wakati huo alimfahamu kama SHANGAZI YAKE
nimeandika kwa herufi kubwa kwasababu ndiko mkasa wake wa kusikitisha
uliko.

Wakati Tonia anapata huo msiba mimi nilipata safari ya ng'ambo hivyo
sikuweza kumsindikiza. Baada ya majuma matatu nilirejea kutoka safarini.

Baada ya kurejea nilimpasha habari na hakukawia kuondoka huko alilokwenda
msibani alinifuate town.
Aliporejea alinyoosha moja kwa moja kazini.

Mara alipowasili na kuniona alikuwa ana uso wa
simanzi kupita kawaida na kama kawaida alikimbilia
kifuani na kunikumbatia kwa muda mrefu na akalia
sana hadi nilikuta nakosa uvumilivu nami simanzi ilinijaa
sana japo nilijikaza kiume na kuanza kumbembeleza na kumsihi
ajikaze na ajipe moyo aache kulia maana hiyo ni kazi ya Mungu.

Pamoja na kumtulliza sana sikuona dalili ya kufarijika kwa Tonia
na ilikuwa kama nimetonesha kidonda kibichi moyoni mwake.
Katika kuendelea kumfariji ghafla Tonia alisema kwa sauti ya
ya chini na yenye simanzi:

(Glenn, tangu nikufahamu umekuwa
rafiki wa kweli, mpenzi ambaye sijawahi kujuta kupendwa nawe
na kama baba kwangu kwani hujawahi kuniangusha kwa lolote
na umeyabadilisha maisha yangu kwa kiwango cha juu sana
hivyo kutokana na heshima hiyo naomba nikushirikishe SIRI
ya familia yangu iliyofichwa kwa muda wa miaka 25 na ambayo
leo hii inaniliza kwa uchungu) note: Tonia alikuwa na umri wa miaka 25.

Baada ya Tonia kusema maneno haya nilipata mshtuko mkubwa
kwani pamoja na hayo alinisisitiza kuwa nisiwajulishe dada zake kwani
hii siri kwani wao bado hawaifahamu isipokuwa kaka yake mkubwa tu
na baba na mama yake tu.

Baada ya kumhakikishia kuwa kamwe sitawaambia hii siri ndipo
alipoanza kunisimua.
Naomba niseme kidogo kuhusu dada zake na familia yake.
Katika familia yao walizaliwa wasichana wanne na upande wa
kiume wakowawili, na yeye amezaliwa wa tatu akifuatiwa na
mabinti mapacha wawili warembo sana sana japo hawamfikii
dada yao Tonia na wote niliwfahamu kwa ukaribu sana kwani
mahusiano yetu yalianza kuvuka mipaka. Tonia ndiye binti anapendwa
upendo usiokuwa wa kawaida na familia yake hasa baba kiasi cha
kuwa kero kwake kwani kila kitu kidogo tu baba yake anamwita
nyumbani

Turudi kwenye jambo la linalomuumiza Tonia alilloliita ni SIRI
ya familia na alianza kama hivi:

TONIA: Glenn unakumbuka yule shangazi
yangu ambaye nilikuonyeshs picha kuwa anafanana nami
sura hadi umbo?

GLENN: Ndio namkumbue si ndiye aliyefariki sio?

TONIA: Glenn kumbe huyo ndiye mama yangu mzazi..(akali machozii)

GLENN: Tonia unasema???? kwani mama yake si .....? nilimtaja mama
aliyemlea tangu udogoni.

TONIA: Ndio maana nilitangulia kukwambia ni siri ya familia, hili jambo
baada ya msiba baba aliniita na kuniambia kuwa huyo aliyefariki
ndiye mama yangu mzazi.
nilimuuliza baba ilikuwaje anifiche hii siri siku zote?
Lakini alinijibu kuwa hakutaka nijue hili jambo alinificha kwasababu
baba yangu alimtelekeza mama na mama alipitia hali ngumu
hivyo hakutaka niyajua haya kwani yangeniumiza.

Glenn mpenzi wangu hili jambo lina utata mkubwa nashindwa
nisemeje lakini hii ndio hali halisi.

Baada ya kusimuliwa hili jambo ambalo mimi kama mtu mzima niliunganisha dots
na kugundua kuwa Tonia alizaliwa kwa mtu na mdogo wake. Yaani baba yake
ni mjomba na mama ni shangazi yake. Naomba hili niishia hapa nitarudi wakuu kwa mkasa wa pili
Nitaendelea kusoma nami
 
2. MKASA WA PILI;
Ilipita kama mwaka mmoja wa kutokuwa pamoja na Tonia...
(usiniukize sababu) nilikutana na mrembo mwingine
jina lake Vick..sio jina halisi.

Huyu Vick kwa kweli naye hana deni na Muumba
kwani amekamilika kila idara.
Yaani yeye na Tonia huenda uumbaji wao ulifanyika
alfajiri wakati muumbaji ana ari, nguvu na ubunifu huku
akili ikiwa imejaa utashi wa kufyatua vitu vya mfano.

Huyu Vick nilifahamiana naye kazini kwake kwani mimi nilikuwa
mteja wake katika biashara yake nzuri tu.

Kama ujuavyo ubinadamu una mahitaji yake yasiyopingika
hata uwe nani katika dunia hii ya Mungu.

Siku isiyokuwa na jina...japo ninaikumbuka😄😄😄
Tukajikuta tumekuwa marafiki wa kukata na shoka japo bond
haikuwa kama ya Tonia...Vick hakuwa mtu wa kupata nafasi
ya kutosha kuonana nami bali tuliweza kukaa pamoja
mara chache sana katika mwezi.

Kuna siku tulikuwa tunapiga stori za familia zetu.
Nikamuuliza hivi mbona katika mazungumzo yetu huwa unamtaja
baba tu na sijawahi kuona umposti wala kumzungumzia mama?

Baada ya swali hilo ghafla Vick alibadilika ghafla na kujaa huzuni.

Nikamuuliza mbona umeshtuka sana Vick wangu?.

Ndipo alipofunguka na kusema.
Glenn; bila shaka umehisi nilifiwa na mama yangu, hasha.
Mama yangu ni mzima wa afya na Jumapili ijayo ninaweza
kwenda kumtembelea wilaya flani.

Lakini kuna mkasa mzito ulionifanya mimi na mdogo wangu
kukosa upendo na mama yetu mazazi.

Baba yetu ndiye baba na mama kwetu kwakweli.

Nikamuuliza hili linawezekana je Vick?

Ndipo aliposema; Baba yetu alizaa na mama yetu
alipokuwa kidato cha pili.

Baada ya baba kufikia kidato cha 4 aliamua amzalishe
mama tena ili amfanye asiondoke kwa bibi amsubirie amalizie
masomo yake ili waje kuungana pamoja kama mke na mume.

Lakini cha kushangaza mdogo wangu akiwa na miezi 3,
mama alikutana na
Mtu aliyekuwa mpenzi wake kabla ya baba hivyo walianza
uhusiano wao upya na mama alitoroka na kwenda kuishi
na huyo.

Huko alipoolewa hakumweleza huyo mume wake kuwa aliwahi kuzaa.

Ulifika wakati baada ya miaka kadhaa huyo mume wake
alipata fununu kuwa mama yetu alizaa na mwanaume
mwingine lakini alipoulizwa alikana katu katu kuwa yeye
hajawahi kuzaa na hana watoto.

Glenn baba yetu alipitia wakati mgumu mno baada ya
mama yetu kutoroka.

Kuna wakati alilazimika kutokuendelea na kidato cha 5
ili atulee kwa kushirikiana na bibi kwani umri wa bibi ulisonga sana.

Baba alibahatika kupata kazi katika shirika flani binafsi.
Kuna wakati alilazimika kwenda nasi kazini alipokosa
mahali pa kutuacha.

Mama yetu alikuja kututafuta baada ya miaka 22 kupita na
kilichomsababisha atutafute ni baada ya mume wake
kuachishwa kazi yake nzuri na kuwa mlevi kupindukia.

Hivyo mama alitutafuta baada ya kusikia sisi na mdogo
wetu na baba yetu kipenzi kuwa tumefanikiwa kimaisha.

Lakini pamoja na kumfahamu mama kuna nyakati najuta
kumfahamu kwani ni mtu asiye na shukrani.

Tunajitahidi kumsaidia lakini amejaa lawama anaona
kama hatufanyi anavyotamani tumsaidie..
 
Back
Top Bottom