Mikataba anayoingia Waziri Makamba ina mkono wa mkuu wa nchi? Kwanini hatusikii akiikemea? Wananchi wanabakia kunung'unika Taifa lao kufisadiwa

Ikiwezekana na TANESCO yenyewe ibinafsishwe kabisa, TPA ibinafsishwe kabisa..

Kuna wakati tunalaumu sana hawa Seniours lakini kuna shida sana kwenye jamii yetu inapofika kwenye management and operations ya hivi vitu...
 
Kwahiyo ndugu yangu, kwenye kufanya utafiti kulihitaji negotiations ?
Kwenye kulipa fidia kulihitaji negotiations?

Mimi nadhani kwenye hatua hii ya uwekezaji katika "uvunaji na biashara" ndio kunahitaji negotiations baina ya sisi kama nchi na wawekezaji.
Hapo ndipo tumetafuta watu wa kutushauri ili tusije tukaingia mikataba isiyo na maslahi kwa sababu tu hatuna uzoefu kwenye mambo hayo.

Kama tunaendelea kulinganisha hatua hii ya uwekezaji na hatua zingine za mradi huu (utafiti na fidia) eti kwa sababu tu hatua zote ni hatua za uwekezaji katika sekta ya gesi, basi kutakua na shida kwa kweli mahala katika uelewa wetu.

Ni sawa na kusema tumpe fundi rangi kazi ya kupiga bati kwa sababu hatua zote ni za ujenzi wa nyumba. Sio sawa mkuu.
 
Kuwa Consultant kwenye liproject likubwa kama hilo la LNG unahitaji kuwa na uzoefu wa kutosha sio blah blah maana watu wanaweka hela hapo..na project inainvolve multination companies..
 
Umesema trilion 70 au bilioni 70
 

Kwa ufupi tu majukumu ya PURA wamepewa wazungu.

Waivunje basi hiyo PURA kama wameshindwa kutimiza majukumu yao.

Kazi ya AG ni ipi??

Kwa AG mbona wapo wataalam wa oil and gas??
 
Tueleweshane kwanza. Transaction advisor ni nani?
 
U
Andiko zuri.
Wataalam wa Sheria wanaoifahamu hii sekta ngeni, kwa vyo vyote hawapo kwa sasa.
Kuwapa kazi hii Waingereza peke yao, kutaendelea kutufanya kuwa tegemezi.
Ilitakiwa kuwe na ubia wa hiyo Kampuni ya Uingereza na mojawapo ya Kampuni za Sheria za Kitanzania ili kupata huo ujuzi.
Vinginevyo, tutaendelea kuwategemea wataalam wa nje.
 
Mkuu kufanya survey kwa Gps au Totatl station na kutengeneza mchoro mpaka kampuni ya nje?

Wanasheria kutuangusha huyegemea na mkuu wa nchi.
Mkuu,IKO HIVI,Kama hio teknolojia ipo hapa nchini au kama kuna ambao wanafikiri wanaweza kuwa na TEchnolojia hio basi waende wamuone waziri na kuthibitisha kwamba wanao uwezo na sio ubabaishaji.Naamni kabisa atrawasikiliza.Kuhusu wanasheria Tusidanganyane kadiri mkataa unavokuwa mrefu na vocaulary nyingi ndivyo ambavyo wanasinzia..
 
Haijalishi wao kutokunegotiate ila hawatatupa USHAURI WOWOTE ILI SISI TUFAIDIKE. Rais Mkapa alianza kujenga barabara zetu kwa pesa yetu. Nasikia wakandarasi wakwao huko mlikoenda walikatazwa kufanya kazi na wachina walikubali. Wanashangaa mpaka sasa tunendelea na ujenzi na wao wamejiunga. TUACHANE NA HAWA TUKUSANYE WAZALENDO WATATUELEKEZA VIZURI SANA. NI HILO
 
Kigogo yupo kazi hakuna wa kumkemea

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Huyo Makamba na Mama ni kitu kimoja.
Kumbuka Mama alikuwa akivujisha siri za Serikali kwenda kwa Makamba a.k.a kigogo2014.
Mpaka walipokamilisha mradi.
 
Shibe mwana malevya njaa mwana malegeza.

Kila mbuzi ale kwa urefu wa kamba yake.

January ata kama anatamaa sio vile; ni mtu mwenye msimamo.

Ingelikuwa tamaa alizuia uuzwaji wa viroba vyenye thamani ya mabilioni angekuwa na tamaa angetafuta mpambe wake wa kuchukua mabillioni kuwaongezea muda wa kuuza aliokuwa anapanga yeye.

That is to say haya yanayofanyika wizarani kwake sio kwa financial benefit zake; inawezekana wengine ndio wana motives hizo kwa sababu he is clueless on the sector.

The minister ukimsikiliza he is just plain stupid on the energy industry; nitaweka wager ya asilimia 60 maamuzi yake ni ushauri wa ovyo kutoka kws Thabit Jacob mtu ambae aelewi ata increase in energy prices zinaathiri makampuni ya size gani.

Makamba is just an ignorant
 
Hivi ni mikataba gani huwa inatakiwa kupelekwa bungeni?
 
Naona watu wengi wanabeza timu ya akina Kabudi katika hii deal.
Nadhani kuna mahala tunakosa taarifa sahihi.

Kwa niaba ya Tanzania, mazungumzo (negotiations) yatafanywa Government Negotiations Team (GNT) ambayo mkuu wake kwa mujibu wa Rais Samia ni Prof Kabudi.

Kazi ya huyu mshauri, ni kuipa uzoefu, ufahamu na kuijengea uwezo timu yetu hii juu ya namna gani masuala ya uwekezaji wa sekta ya gesi yanafanya kazi.
Hawa washauri wao wana uzoefu mkubwa kwenye sekta hii, tuutumie uzoefu wao ili nasisi timu yetu inapokua kwenye meza ya mazungumzo ifanye negotiations ikiwa well informed ili mwisho wa siku tupate better deal.

Ni sawa na mzaramo anapotaka kwenda kuoa Ukerewe, atamtafuta mzee mmoja wa kikerewe ampe taratibu za kutoa posa huko Ukerewe zikoje. Akishafahamu taratibu hizi, zitamsaidia huyu wazaramo kuweza ku negotiate posa katika grounds zenye mashiko katika tamaduni za kikerewe.
Hapa haimaanishi kwamba mzee wa kikerewe (mshauri) anaoa kwa niaba ya mzaramo.

Ndivyo ilivyo kwenye hili suala la LNG, hakuna haja ya kuibeza role ya Kabudi na timu yake kwa sababu ya huyu mshauri.
Hawa watu wana kazi mbili tofauti zinazoungana kuleta tija ya pamoja.
 
Hiyo kampuni na ale wanaotaka mladi wote ni wa hukohuko sasa unadhani watajibana wenyewe, kwa nini asingetafuta hata washauli hata china au urusi kuliko kuwafata hao ambao ndio wanataka miradi hiyo kisha wajifunge kamba shingoni?
Mnacheza nyie na jasho la watanzania.
 

Wabunge wa CCM wamejazwa bungeni kwa uchafuzi wa 2020 waambie wahoji hiyo mikataba. Je muulize Kabudi baba wa mikataba yeye anasemaje au kapewa kitengo cha ulaji wa bure.
 

Jasho la watanzania?! Kwani hiyo gas ipo kwa jitahidi za watanzania? Au unaoungea usichokijua?
 
Wabunge wa CCM wamejazwa bungeni kwa uchafuzi wa 2020 waambie wahoji hiyo mikataba. Je muulize Kabudi baba wa mikataba yeye anasemaje au kapewa kitengo cha ulaji wa bure.
We jamaa vipi? Hapa tunajadili huyu jamaa madudu anayofanya na kupiga madili habari ya uchaguzi inatoka wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…