Mikoa 15 kukosa umeme Julai 3 na 4 kutokana na umaliziaji njia Umeme wa SGR Msamvu - Dodoma

Mikoa 15 kukosa umeme Julai 3 na 4 kutokana na umaliziaji njia Umeme wa SGR Msamvu - Dodoma

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
NISHATI: Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limetangaza kuzimwa kwa huduma katika Njia Kuu ya Kusafirisha Umeme wa Msongo wa Kilovoti 220 kutoka Msamvu hadi Dodoma ili kuruhusu umaliziaji kazi kwenye vituo vya Treni ya Reli ya Kisasa (SGR) vya Msongo wa Kilovoti 220/33

Mikoa itakayoathirika kutokana na kazi hiyo itayodumu kuanzia saa 1 asubuhi hadi saa 12 jioni Julai 3 na 4, 2024 ni Iringa, Njombe, Ruvuma, Mbeya, Songwe, Singida, Shinyanga, Simiyu, Tabora, Mwanza, Mara, Geita, Arusha, Kilimanjaro na Manyara

TANESCO imesema ukarabati huo unalenga kuimarisha mifumo ya uendeshaji wa Treni pamoja na kuimarisha ufuatiliaji wa TANESCO katika uendeshaji wa njia ya Kilovoti 220 ya SGR kati ya Msamvu na Dodoma.

IMG_20240701_201426_090.jpg

Pia Soma:

- Shirika la Reli: Treni ya SGR haitumii umeme mwingi
 
SGR ilipingwa sana na Chadema lakini leo nyumbu ndiyo wa kwanza kupanda

R.I.P Magufuli
 
Tushazoea huku njombe toka wiki ilopita wanakata tu wakijisikia,,leo saa mbili hii walikua wamekata
 
Tanesco hamkutups taarifa kwamba tozo ya nyumba inayokatwa wakati tunanunua umeme imepanda kutoka 1500 Hadi 2000. Mngetuambia tuh maana watanzania hatuna noma.
 
Back
Top Bottom