Mikoa Tajiri Tanzania kwa mujibu wa BOT

arushaaaaaa namba ngapi? wiizi mtupu
chezea utalii wote ule khaaaaaaaaaaaa
 
yaani arusha wamezidiwa na morogoro, shinyanga na iringa?
kumbe hawa jamaa ni kelele mingimingi tu.

Mafisadi wamezidi arusha..... maendeleo hayawezi onekana....... watu binafsi wana utajiri sana lakini serikali apeche alolo...
 
Mafisadi wamezidi arusha..... maendeleo hayawezi onekana....... watu binafsi wana utajiri sana lakini serikali apeche alolo...
Tunakumbuka bilionea mmoja wa Tengeru Arusha alifia mahenge morogoro akimiliki migodi kadhaa ya ruby?
 
we mwehu kweli unaishi dunia hii kweli?we hujui dar imeongoza kwa sababu ya wachaga?kila penye mchaga ndo penye maendeleo...kwa hyo ww cheza na wachaga utalala njaa mkuu..utadeki bahari kwa ulimii

Una mawazo ya kisisiem,kwa hiyo wachaga wanaiendeleza dar na sio kil,arusha, vp kuhusu Mby na R.city.
 
Nashangaa hata mkoa wa Tanga umeushinda Kilimanjaro Duuuh...
 
Utajiri wa Arusha upo kwa Mabilionea (Bob Sambeke, Erasto na wenzake) tu lakini kama Mkoa hauna kitu mbwembwe tu.
 
basi watu washinyanga wapole sana mkuu wamekubali kuendeleza mikoa mingine na wao wanafulia tu!

Unajua viongozi wengi wa Shinyanga wamekuwa wasaliti wa wananchi na bahati mbaya sana watu wa mkoa huo,wamelala sana.Kuna viongozi kama Luhaga Mpina ambaye yuko Simiyu sasa baada ya kutengwa toka Shinyanga na John Pombe Magufuli ni wasukuma wanaopaswa kuwa mfano na ku- inspire vijana wa kisukuma wapiganie ustawi wa mikoa yao.Hata hivyo bahati mbaya ni kuwa viongozi na wanaoutamani uongozi wengi hawana njozi ya kuinua watu wao bali kujiinua wenyewe binafsi labda na familia zao.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Madini ya dhahabu, mbuga za wanyama za Serengeti na Masai Mara plus kilimo
Vema. tatizo lipo wapi sasa, wananchi wa Mara ndo wamelala usingizi au?!, fikiria asilimia kubwa ya Mbuga ya wanyama ya Serengeti ipo Mkoa wa Mara, lakini Mkoa wa Mara hakuna kampuni za Tours, badala yake wanaofaidika na Mbuga ya Serengeti ni watu kutoka Arusha na Mwanza kidogo
 
....wachagga mmeshika mkia kwa uzalishaji?] Siyo uzalishaji kaka/dada, GDP haipimwi kwa uzalishaji, inapimwa kwa mchango wa zao la mwisho katika pato la Taifa hasa kupitia kodi. Inawezekana Arusha wengi ni wakwepa kodi.
 
Hizi takwimu labda ni za mwaka 1980's hapo sawa, lakini kama ni za hivi karibuni mimi kwa upande wangu naona mkoa wa Mara unatakiwa kuwa ndani ya tano bora na kama utataka vigezo ntakupatia vipo vingi tu
tupe vigezo mkuu.

Inawezekana ni mgodi tu ndio unauweka mkoa wa MARA kuwa juu...
 

Arusha si ndio jiji la mabilionea na wafanya biashara maarufu? inakuaje tena inapitwa mpaka na iringa?
 
Fedha za utalii zinaliwa na wajanja ndio maana hazionekani.
 
Source BOT - Link The Citizen!!!!!

Kwenye Website ya BOT Hii taarifa haipo!!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…