Mikoa Tajiri Tanzania kwa mujibu wa BOT

Wachumi njooni hapa tujue kwanini taarifa za makusanyo ya kodi ziko tofauti kabisa na mchango wa mikoa husika katika pato la taifa ......

Takwimu za BoT labda walichukua kwenye magulio MTAZAMO kwa takwimu za TRA Arusha ni mkoa wa pili kutaifa kwa kuchangia kuendesha serikali ya nchi kwa maana ya kodi mbalimbali. Lakini bado kuna taasisi kama Ngorongoro mafaili yao yako Large Tax Payers DSM, hivyo takwimu za Ilala si za Dar es Salaam peke yake
 
Last edited by a moderator:
Wachumi njooni hapa tujue kwanini taarifa za makusanyo ya kodi ziko tofauti kabisa na mchango wa mikoa husika katika pato la taifa ......
acha kupotosha, weka total na siyo vipande. arusha inaweza kuongoza kwwenye kodi za utalii lakini iringa ikaongoza kwenye mazao ya misitu.
 
mkoa wa morogoro uko juu sana kwenye kilimo watu wengi wanaudharau cjui kwa nn? tz uongozi wetu tu umekuwa mbovu lakn tungeamua kukomaa kwenye kilimo peke yake tungekimbiza majiran zetu hasa kenya hadi ulimi uwatoke. nchi ya ethiopia uchumi wake unakua kwa % kubwa kuliko china kwa sasa kutokana na kilimo. zaidi ya 80% ya uchumi wake unategemea kilimo. after all GDP ni total ya goods and service zinazokuwa produced na eneo husika kwa muda fulani. wengi humu tumeangalia goods tu tukasahau services kama maji nk. kwa hiyo nakubaliana na moro kuizidi arusha hasa baada ya ule mkoa kugawanywa na simanjiro (mererani) iko mkoa wa manyara
 
Tukijadili hii ishu tusiweke ukabila, kwasababu mfano tu Dar es Salaam kuna kila kabila na watu wanafanya biashara wanachangia kwenye GDP ya dar, tukianza kusema mbona wachaga wako chini ntashangaa coz hata ukienda Mwanza utawakuta wachaga wana boat za uvuvi, so hizo takwimu ziko sawa kabisa kama tutaziangalia kama wachumi na sio wakabila...
 
ni kweli wachaga ndio wanaofanya dar inaendelea sana ila watu watabisha huku mioyo yao ikiwasuta.kwa sasa hivi kilimanjaro ni moja ya mikoa inayoongoza kua na wazee wengi hii ni kutokana na wengi wa vijana kukimbilia mijini tena hasa katika jiji la dar.ukisema tuzungumzie arusha kwa kua nyuma katika hiyo orodha ni wazu tu kua arusha ni mkoa wenyr utajiri mkubwa wa vitu vingi kama madini,makampuni ya utalii,mahoteli meng na hata hivyo kama ulishawai kufika arusha utagundua kua ndio mkoa wenye pub ndigondogo nyingi jambo lianaloonesha kua wakazi wa arusha wengi ni wanywaaji tena wa pombe kubwakubwa hivyo ni kiashiria cha mzunguko wa pesa mzuri.so inawezekana ni wakwepaji wazuri wa kodi kama kodi ikifuatiliwa vizuri nafikiri arusha itaingia top3.lakini kwa kilimanjaro itakua ngumu kwa sababu wengi wao huenda mikoa mingine na kurudi nyumbani kujenga na kusalimia wazee wao tu.ni hayo tu wanajamvi,unaruhusiwa kuhoji pia.
 
Wachaga wana mchango mkubwa kwenye mikoa yote, wametawanyika nchi nzima kiuchumi!

Hazizungumziwi kabila hapa, inazungumziwa mikoa. Haijalishi wametawanyika wapi na wapi, mtu anaangaliwa kwao kwanza...
 
kwa nini isianzishwe zawadi na taasisi zinazosimamia uchumi au wadau wengine kwa mkoa unaweza kuongeza GDP kwa kiwango cha kuridhisha kwa mwaka na wawe wanapewa fedha nzuri itakayowasukuma viongozi na wataalamu huko mikoani kubuni mbinu za kutekeleza hilo.

mimi napendekeza wizara ya fedha itoe sh billioni moja kwa mkoa utakaongeza GDP kufikia asilimia fulani kwa mwaka.
 
Ziwa victoria tu ni zaidi ya vimbuga vyote vya arusha
 


Mkoa wa Shinyanga TAJIRI?
Hawa wachumi wanaishi hapahapa Tanzania? Mbona factors kama Elimu ambayo ningetegemea iwe factor lkn siuoni huu mkoa kuwa tajiri? Madini yasiyowasaidia wazawa wa huko?
Nafikiri hawa wachumi ndio walishindwa kumshauri rais kwa nini Watz ni masikini.
 
Yaani mikoa inayoongoza kwa utalii imepitwa hata na Morogoro na Iringa!!!?

Hayo mapato yanaendaga wapi?

Kumbe ndio maana hii nchi haiendelei......
 
Hizi tawmu ni za BRN???? Nashangaa Shinyanga, Morogoro na Iringa kuizidi Arusha kwenye orodha ili hali hakuna kiasi kinachochangiwa.
Kadiri ya BRN, ufaulu umefika 81% kutoka 56% ndani ya miaka 2 ili hali juhudi hazionekani.
 

Watu watakamulia kodi mpaka watoe moshi aiseee
 
yaani arusha wamezidiwa na morogoro, shinyanga na iringa?
kumbe hawa jamaa ni kelele mingimingi tu.

shinyanga nan Iringa kuizidi Arusha sishangai. nenda kaangalie makampuni ya kilimo yalivyowekeza kwenye hii mikoa, af angalia jinsi wananchi wanavyolima kwenye hii mikoa achilia mbali biashara yaani ni transit areas lazima wawe na vipato vikubwa zaid.
magaro yote yanayopita mkoa kama iringa kila siku yanaingiza sh ngapi?? achilia mbali viwanda kama Asas, ivory dabaga, achilia mbali shiughuli za kilimo msimu wa mwaka mzima yaani kiangazi na masika kunalimika kwa nini wasiwe matajiri zaid?

Arusha ni madini ya tanzanite tu, labda na huo utalii ambapo leo hii uchumi ukiyumba watalii hakuna arusha watalia njaa. kelele zao ni kwasabb wanaona wazungu kila leo lkn hawana kitu ni bure tuu
 
nadhani GDP haingalii makusanyo ya kodi bali inaangalia thamani ya biashara kwa ujumla ziwe za huduma ua bidhaa. kama mikoa ikishindanishwa basi wataalamu watakuwa wakitengeneza mazingira ya wananchi wao kuzalisha na kufanya biashara na kuondoa matendo ya watumishi wanaotumia nyadhifa kuwawekea wananchi vikwazo kwa kulewa nafasi zao au kutafuta rushwa.

Watu watakamulia kodi mpaka watoe moshi aiseee
 
siyo mapema mno, bali gas yote inaenda nje, pmoja na kuwa na gas lakini Lindi na mtwara zitaendelea kuwa masikini maana kama stat oil anachaukua asilimia 85% sema tu Lindi wataongoza kwa kuwa na maashimo, hata hizi record za kusema eti shinyanga imepanda juu hizi ni takwamu tunazopewa na wazungu kwa lengo la kutufariji tujue kuwa uchumi wa mkoa husika umepanda kumbe ni mbnu za kuendelea kutunyonya, kila siku tunaambiwa eti pato au uchumi wa tz umekua mbona umasikini ni ule ule kwa watanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…