Rais Samia, kwanza nashukuru umemuondoa Nape Nnauye kwasababu TCRA na Tume ya Ulinzi wa Taaifa Binfsi(PDPC), ni taasisi zilikuwa chini yake na mpaka anaondoka, hatuijaona hizi taasisi zikiwa serious katika kuchukua hatua(sijaona wala kusika waliokamatwa kwa kudhalilisha watanzania).
Naomba ikikupendeza, muondoe na Mwigulu anaeisimamia BOT ambayo nayo inapaswa kuhusika katika kusimamia na kudhibiti biashara ya kukopesha.
Mhe. Raisi, haya makampuni hayafanyi biashara hii kwa kificho kwani wanajitangaza mitandaoni mfano facebook na zaidi na ambacho ni cha kushangaza, makampuni haya ya kukopesha mitandaoni yanatoa mikopo na kupokea marejesho yao kupitia mitandao ya simu ya humu nchini halafu eti wahusika wanashindwa kukamatwa!
Ukiacha udhaliolishaji wa kusambaza taarifa za wakopaji, riba wanazotoa ni kubwa mno na sijui kama zinaendana na riba elekezi ya BOT ya asilimi 3.5 kwa mwezi na sijui kama wana leseni. Pia muda wa kulipa denii sio rafiki kabisa na zaidi wana lugha mbaya sana. Hayo ni machache tu.
Mhe, Raisi,malalamiko yamekuwa mengi na hata Spika wa BUnge, Mhe. Tulia Ackson, alililamika Bungeni kutumiwa sms za mtu anaedaiwa wakati yeye hahusiki kwa namna yoyote ile.
Mhe. Raisi, kweli inaangia akilini kwa hizi taasisi kushindwa kuthinbiti hizi App za kukopesha mitandaoni?Binafsi malalamiko hapa JamiiForums nimeanza kuyasoma hivi karibuni lakini yapo tangu mwaka jana ila mpaka leo sijui kama kweli kuna walio wahi kufikishwa katika vyombo vya sheria kwa tuhuma za kudhalilisha watu na kufanya biashara hii bila kuwa na leseni na makosa mengine.
Najiuliza, hivi viongozi wa hizi taasisi hawawezi kuweka mitego kuwakamata hawa watu?
Viongozi wa hizi taasisi hawajawahi kupokea malalamiko rasimi kutoka kwa wananchi?
Tufanye assumption kuwa hakuna malalimiko yalioyowasilishwa kwa kwa njia rasimi. Je, ndio watakaa ofisini kusuburi malalamiko rasimi ndio wachukue hatua?
Kama hawapokei au kusikia malalamiko, press realese wanazotoa mara kwa mara katika website yao za kuonya kuhusu hii biashara, udhalilishaji, n.k, msingi wake huwa ni nini kama sio malalamiko ya wananchi?
Na je, TCRA wameshindwa kuagiza makampuni ya simu kusitisha mara moja mitandao yao kutumika kibisahara na taasisi zinazokiuka sheria?
Mhe. Raisi, maswali ni mengi, lakini yote yanaonyesha udhaifu wa hizi taasisi. Hivyo, nakushauri ufanye uchunguzi na ukibaini kuna uzembe, basi viongozi wakuu wa hiizi taasisi wawajibike.
Kilichonisukuma leo kuleta hii mada ni hili bandiko la Mdau mmoja wa hapa JamiForums ambalo nakuomba na wewe Mhe. Raisi ulisome. Yako mabandiko mengi tu kwani watu hawajaanza kulalamika leo wa jana.
Bashir Yakub, WAKILI. +255 714 047 241. Swali la msingi ni kuwa hawa wanaokopesha wanapata wapi namba za ndugu zako, jamaa, na marafiki ambazo wanazitumia ujumbe kuwataarifu kuwa unadaiwa, umeshindwa kulipa mkopo,na maneno mengine yasiyo na staha. Fikiria mkopeshaji ambaye si tu hajawahi hata...
Mods naomba hii mada ibaki katika hili Jukwaa.