Milembe Alivyouawa Kwenye Pagale

Milembe Alivyouawa Kwenye Pagale

Mdakuzi

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
4,294
Reaction score
6,872
Baada Agosti 27, 2024 mahakama kutoa hukumu ya kesi tukio kuuawa kwa Milembe Maunga, na watuhumiwa watatu kukutwa na hatia, wakihukumiwa kunyongwa, kwa sasa napata fursa ya kulielezea tukio hilo kwa kina namna lilivyokuwa.

Yatakuwa maelezo marefu kidogo, ila nitajitahidi kulielezea lote kwa awamu hadi nifikie mwisho. Hivyo, nitakuwa nikiendelea kwenye eneo la maoni.

Naanza...

Mauaji ya Siri: Mapenzi, Wivu, na Kifo

USIKU ulikuwa umetulia sana huko Mwatulole, wilaya ya Geita, mnamo Aprili 25, 2023.

Milembe Suleiman Hungwe alikuwa amepanga mipango ya siku inayofuata, lakini hakujua kwamba huo ulikuwa usiku wake wa mwisho duniani.

Akilini mwake, hakukuwa na wasiwasi wowote. Kila kitu kilionekana kikiwa kawaida, lakini nyuma ya pazia, jambo kubwa lilikuwa linapangwa dhidi yake.

Ndani ya kuta za nyumba isiyoisha kujengwa, yaani pagale, iliyomilikiwa na Milembe, palikuwa na siri nzito. Siri iliyogubikwa na wivu wa kimapenzi.

Twende pamoja
Milembe, ni mwanamama imara aliyefanikiwa sana kazini kwake, nyuma ya maisha yake ya siri kulikuwa na jambo moja alilolificha kwa uangalifu mkubwa—uhusiano wake wa kimapenzi.

Milembe na Dayfath Suleiman Maunga hawakuwa tu marafiki wa kawaida. Kwa muda mrefu, walikuwa wapenzi wa jinsia moja (lesbian), uhusiano ambao waliishi nao kwa siri kubwa.

Katika jamii yao, uhusiano kama huo ulikuwa kinyume katika mila na desturi, jambo lililowalazimu kuficha hisia zao.

Dayfath alikuja kwenye maisha ya Milembe kwa njia ya kawaida—alianza kama mfanyakazi wake katika biashara ya duka la vipodozi la Milembe.

Lakini muda ulivyopita, hisia za kimapenzi zilianza kuchanua kati yao. Wakianza kuishi kinyumba maeneo ya Usagara, Mwanza, wakiishi na mama yake Milembe, msaidizi wa kazi za nyumbani, na baadhi ya ndugu.

Ulimwengu wao ulikuwa ni wa siri sana, lakini ni ulimwengu ambao siku moja binti wa Milembe, Grace Evarist Gervas, aligundua kitu kuhusu mama yake na Dayfath ambacho kilimshangaza sana.

Itaendelea...

Ova
 

Attachments

Sehemu ya Pili;

Siri Inaanza Kufichuka!

BINTI wa pekee wa Milembe, Grace Evarist Gervas aliugundua uhusiano wa kimapenzi wa mama yake na mrembo Dayfath. Ilimshangaza, kwani hilo halikuwa jambo la kawaida.

Aligundua baada ya wawili hao kuwa wakiitana kwa majina ya kimahaba—Milembe akimwita Dayfath 'Wife', na Dayfath akimwita Milembe 'My King'.

Milembe na Dafath hawakujali hilo, lakini baada ya muda ulimwengu wao ulianza kugubikwa na giza lililotokana na migogoro yao ya mara kwa mara.

Kwa muda, mabishano yaliongezeka. Kila siku, yalionekana kuchochewa na sababu ndogo ndogo, lakini chanzo halisi kilikuwa ni vita ya ndani kati ya mapenzi na wivu.

Mabishano yalizidi kuwa mwiba kwenye penzi hilo. Grace anakumbuka siku ambayo mama yake alipompiga Dayfath baada ya mabishano makali.

Dayfath, akiwa kachoka manyanyaso hayo, alikusanya kila kilicho chake, na kuondoka ghafla usiku mmoja.

Baada ya tukio hilo, ilionekana kama mwisho wa uhusiano huo—lakini hapana, Dayfath hakuwa tayari kuachana na Milembe kwa urahisi hivyo.

Siku chache tu baadaye, Milembe alipokea simu toka kwa watu waliojitia ni wasamaria wema, wakimpa taarifa za kuugua kwa Dayfath.

AkIwa anaishi katika nyumba moja ya wageni. Kwa huruma ya mapenzi, Milembe alimfuata Dayfath aliko na kumrejesha nyumbani kwake.

Wakaombana radhi, kisha kurejesha tabasamu zao, lakini nyuma ya tabasamu hizo na maneno ya faraja, kulikuwa na mpango wa siri ambao ulikuwa unatokota.

Na ndani ya moyo wa Dayfath, kulikuwa na giza linalozidi kukua— giza la wivu na kisasi.

Itaendelea...

Ova
 
Sehemu ya Tatu;

Kivuli cha Kifo

USIKU wa tarehe 25 Aprili, akiwa lodge ya California, Milembe alimuita Dayfath kwa ujumbe mfupi wa simu.

“Kuna mambo mengi ya kufikiria… tunahitaji kufanya mazungumzo ya mwisho,” aliandika.

Lakini mazungumzo hayo hayakuwa tena kuhusu uhusiano wao, kwani tayari walishatibuana tena na wote kushika njia zao.

Baada ya kila ugomvi, na baada ya kila shambulio la kihisia, Milembe alihisi kuwa ni wakati wa kumaliza kila kitu kwa amani na kusonga mbele.

Lakini, hakujua kuwa Dayfath tayari alikuwa amechora mstari wa mwisho wa maisha yake.

Mazungumzo ya Milembe ya Dayfath yaliibua mpango wa kusomewa "dua" kwa jengo la biashara ya Milembe, ambalo bado lilikuwa katika ujenzi.

Ndipo majina ya Genja Deus Pastory, Mussa Ally Pastory, na Safari Bundala Lubingo yalipoibuka, kama wasoma "dua" wazuri waliopendekezwa na Dayfath.

Katika jengo hilo ambalo haijaisha ujenzi wake, eneo la Mwatulole, kilichokuwa kimefichwa hakikuwa kitu kingine ila mpango wa uharibifu ambao ulikuwa tayari umekamilika.

Usiku wa tarehe hiyo, Milembe alifuatana na wanaume hao watatu.

Hawa hawakuwa wageni kwake.
Walikuwa watu ambao alikuwa amewategemea kwa msaada wa "dua"—lakini hakujua kwamba msaada wao ungekuwa wa kumharibu.

Waliingia ndani ya Bajaj, wakielekea kwenye "site" yake ya ujenzi. Wakati huo, kila kitu kilionekana kawaida.

Hakukuwa na dalili ya maafa. Lakini nyuma ya macho ya wasaliti hawa, kulikuwa na mpango mzito ambao ungeondoa uhai wa Milembe usiku huo.

Itaendelea...

Ova
 
Sehemu ya Nne;

Ndoa ya Siri yawa Shimo la Kifo

Maisha ya Milembe na Dayfath yalikuwa ni mafumbo. Uhusiano wao ulikuwa umevunjika, lakini hisia zilitawala zaidi.

Upendo wa Dayfath kwa Milembe ulibadilika kuwa wivu usio na mipaka. Alianza kuhisi kuwa Milembe anamwacha, akihofia kuwa alikuwa akipoteza nafasi yake.

Lakini badala ya kuachilia, alichukua uamuzi mgumu—wa kutafuta njia ya kumtoa Milembe kwenye maisha yake, kwa njia ya giza na kifo.

Baada ya majibizano na wivu uliokomaa, Dayfath alizungumza na Safari Lubingo, rafiki yake wa zamani, na wakapanga kutafuta wauaji.

Safari akampata Genja na Mussa—watu waliokuwa na mikono ya damu. Walipanga na kuamua kuwa siku ya tarehe 25 Aprili, 2023 ingekuwa ndiyo mwisho wa Milembe.

Baada ya kufika kwenye "site", Milembe aliagana na wanaume hao watatu; Genja, Mussa, na Safari, wakiwa wamejiandaa kwa kazi yao ya mwisho.

"Nitawaita baadaye, baada ya kumaliza mazungumzo." Milembe alisema, akiwa na matumaini kwamba kila kitu kitatendeka kama kawaida.

Lakini, asilokuwa akilijua, tayari mawimbi ya hatari yalikuwa yameanza kupiga chini ya maji, yasiyoonekana.

Muda ulipofika, Milembe aliwapigia simu. Wakajitokeza kwa kasi na kuingia kwenye eneo la ujenzi. Na ghafla kitu cha ajabu kikatokea.

Itaendelea...

Ova
 
Wakati nasoma kisa cha haya mauaji hapa JF, sababu kubwa zilizotolewa na Wakuu humu, sababu ya Dhuruma ya Fedha ama Wanaume kuwa na Wivu wa kuibiwa Wake zao na huyo Milembe ndiyo zilizotajwa

Kumbe Kisa ni huyo DayFath kuchoka kukobolewa 🙌

Itakuwa alitaka aolewe na Mwanaume ili aweze kuwa na Watoto wake, badala ya mahusiano yao ya kukoboana pasipo kuwa na uwezo wa kupeana Mimba 🙌
 
Back
Top Bottom