Milion 10 inatosha kuanzisha biashara ya Baa?

Milion 10 inatosha kuanzisha biashara ya Baa?

Unatatizo kichwani yaani mimi nianza kuandika template hapa km unataka naweza kukukuandikia dodoso ili ufanye utafiti, mimi ni muelimishaji elimu ya ujasiriamali na nimebobea kwenye eneo Hilo hata hiyo biashara nimewahi kufanya
Onyesha kwa kutumia numbers, utaanzishaje biashara ya bar kwa mtaji wa milioni 10.
Mimi pia naweza nikasema I'm so and so but that doesn't mean s#!t.
Numbers hommie, numbers ....
 
Mkuu
Nina mpango wa kuandika hiyo template ambayo itakuwemo kwenye kitabu changu, but at my own time after conducting a. Market research within my mapping area as a reference in my book, hapa tunajaribu kuelimisha not showing off that we are more knowledgeable than others
Mkuu wa wakuu Benny Haraba tafadhali usichanganye sana hiyo lugha nyingine wenzio hatuelewi tuko hapa kukufuatilia pia Kaka yangu
 
Onyesha kwa kutumia numbers, utaanzishaje biashara ya bar kwa mtaji wa milioni 10.
Mimi pia naweza nikasema I'm so and so but that doesn't mean s#!t.
Numbers hommie, numbers ....
Narudia mpanga wa biashara unafaniyiwa utafiti kulingana na eneo husika vs ushindani uliopo na aina ya wateja , ( social demographics variables) aina ya watu wanao izunguka biashara Yako, elimu zao, shughuli za vyote hivyo huchagiza baisha Yako mfano wagonga mawe, waendesha bodaboda, vyuo km vipo, wafanya biashara mbalimbali
 
Mkuu

Mkuu wa wakuu Benny Haraba tafadhali usichanganye sana hiyo lugha nyingine wenzio hatuelewi tuko hapa kukufuatilia pia Kaka yangu
Sawa nimekuelewa, and sorry for my over reactions I also know that ,here we have different level of understanding, (interpretation) humu kuna wadau wenye uwezo tofauti wa kutafsiri mambo ama maandiko
 
Hapana, biashara lengo lake ni kupata faida.
Na kama ukitulia kidogo na kufanya utafiti, utapata faida. Pia siyo lazima uanze na kitu kikubwa, unaweza kuanaza na biashara ndogo na ukaikuza.
Kwa mfano grocery au Lounge ndogo yenye waitress mmoja na kibox cha chips na mishikaki au mchemsho asubuhi (hata kwenye hotpot tu).

sasa badala ya kuongea blabla hebu tuonyeshe jinsi unavyoweza kuanzisha "Bar" kwa milioni kumi.
Tuonyeshe bajeti ya mahitaji, matumizi ya kila siku/mwezi na income 9expected).
Tuanze hapo kwanza.
wewe uliyesema mil 10 haitoshi ndo ulitakiwa utoe mchanganuo wa biashara ya bar ili tuamini maneno yako.
 
Mkuu mambo vipi,

biashara ya bar inategemea na unataka kuiweka maeneo gani na unataga wateja wako wawe watu wa aina gani. ila kwa mtaji wa million 10 unaweza kuanza kwa maeneo ya nje kidogo ya mji kama ni hapa dar es salaam.

pia kama utahitaji vitu kama TVs nzuri na muziki nicheki mimi nitakupa kwa bei nzuri ya jumla pamoja na warranty ya uhakika..

kwa ushauri wa bar ninao pia ila sema kwanza unataka hii bar iwe maeno gani ndio upate ushauri
ni kweli Dar umafia mwingi nataka nikaifanye hiyo biashara mkoa wa pwani, mziki mkubwa heavy duty na size ya kati bei gani?
 
Kabla hujafanya biashara yoyote ile ni lazima uijue hiyo biashara kwa kufanya utafiti, wapinzani wako ni wakinanani nguvu zao zikoje mapungufu yao, wateja wao ni wakinanani na wanapatikana wapi, wewe nguvu zako na mapungufu yako wateja taraji, utakabliana vipi na upinzani uliopo na ujao kwakifupi ni lazima uwe na andiko la biashara,. Pia mzuki mkubwa siyo lazima inategemea eneo la biashara na aina ya wateja kwa eneo husika (audience) lapili ni sifa za wahudumu (sifa za mjasiriamali), traits, angalia pia biashara zingine km hiyo muunekano upoje kwasa na hapo baadae itakuwa vipi, (market trends)
Mkuu uko sahihi. Lakini hapa unaweza kutukanwa ukisema hivi. Jinsi alivyouliza tu tayari kuna possibility kubwa ya kufeli kama atafanya. Kwa nini? Hajazingatia uliyomwambia.
 
Kabla hujafanya biashara yoyote ile ni lazima uijue hiyo biashara kwa kufanya utafiti, wapinzani wako ni wakinanani nguvu zao zikoje mapungufu yao, wateja wao ni wakinanani na wanapatikana wapi, wewe nguvu zako na mapungufu yako wateja taraji, utakabliana vipi na upinzani uliopo na ujao kwakifupi ni lazima uwe na andiko la biashara,. Pia mzuki mkubwa siyo lazima inategemea eneo la biashara na aina ya wateja kwa eneo husika (audience) lapili ni sifa za wahudumu (sifa za mjasiriamali), traits, angalia pia biashara zingine km hiyo muunekano upoje kwasa na hapo baadae itakuwa vipi, (market trends)
Ushauri mzuri lakini sio hitaji la jamaa na inawezekana ashayafanya hayo yote.. Anachotaka kujua ni kama milioni 10 aliyonayo inaweza kutosha.
 
Hapana, biashara lengo lake ni kupata faida.
Na kama ukitulia kidogo na kufanya utafiti, utapata faida. Pia siyo lazima uanze na kitu kikubwa, unaweza kuanaza na biashara ndogo na ukaikuza.
Kwa mfano grocery au Lounge ndogo yenye waitress mmoja na kibox cha chips na mishikaki au mchemsho asubuhi (hata kwenye hotpot tu).

sasa badala ya kuongea blabla hebu tuonyeshe jinsi unavyoweza kuanzisha "Bar" kwa milioni kumi.
Tuonyeshe bajeti ya mahitaji, matumizi ya kila siku/mwezi na income 9expected).
Tuanze hapo kwanza.
maneno machache ila umempa ushauri wa maana sana aanzie hapa "anza kidogo" .....infact ni biashara hujawai fanya
 
bar ni jiko mkuu, utundu wa mtu wa jikoni ni hirizi tosha. mziki inategemea aina ya wateja walioko hilo eneo, kama ni watu wazima sana hawapendi makelele. level ya uchumi wa wateja wako pia inaamua uweke vinywaji vya aina gani na status gani.
 
10m kwa bar usijaribu, ndogo sana ,,, pengine unaweza kodi frem sehemu ambayo kuna kaeneo flani kwa mbele,,, then hio frem jenga kikaunta cha kishkaji, kwa nje weka tent lenye kukaa meza kama 4 na viti vyake,,, alafu hapo ndani kaunta zikae walau meza 2, nunua sub woofer , nunua TV 2 size kati tu weka ndani na nje, nunua fridge moja isiyo ya kampuni ili uweze kuweka vinywaji vyote bila bughudha,,, jenga kakibanda ka chips na mishikaki pembeni,,,, anza na bia kreti 20, soda 5, maji katon 5, pombe kali pc kadhaa kadhaa tu ,,, tafuta dada mmoja wa nje na kaunta mmoja anza mdogo mdogo "
 
bar ni jiko mkuu, utundu wa mtu wa jikoni ni hirizi tosha. mziki inategemea aina ya wateja walioko hilo eneo, kama ni watu wazima sana hawapendi makelele. level ya uchumi wa wateja wako pia inaamua uweke vinywaji vya aina gani na status gani.
vip kuhusu wahudumu wanawake wazuri wazuri wenye mvuto!
 
10m kwa bar usijaribu, ndogo sana ,,, pengine unaweza kodi frem sehemu ambayo kuna kaeneo flani kwa mbele,,, then hio frem jenga kikaunta cha kishkaji, kwa nje weka tent lenye kukaa meza kama 4 na viti vyake,,, alafu hapo ndani kaunta zikae walau meza 2, nunua sub woofer , nunua TV 2 size kati tu weka ndani na nje, nunua fridge moja isiyo ya kampuni ili uweze kuweka vinywaji vyote bila bughudha,,, jenga kakibanda ka chips na mishikaki pembeni,,,, anza na bia kreti 20, soda 5, maji katon 5, pombe kali pc kadhaa kadhaa tu ,,, tafuta dada mmoja wa nje na kaunta mmoja anza mdogo mdogo "
kuliko kunishusha ni bora ukatoa ushauri kulingana na matakwa yangu, ulipaswa kusema ongeza mil 5 au 10 ingine au fanya ivi na vile ili utimize lengo ivyo ulivyosema ni bora niache na kuacha siwezi vile nimeamua mpango utimie.
 
Mkuu uko sahihi. Lakini hapa unaweza kutukanwa ukisema hivi. Jinsi alivyouliza tu tayari kuna possibility kubwa ya kufeli kama atafanya. Kwa nini? Hajazingatia uliyomwambia.
theory nyingi sana! sina uzoefu na bar ila nina uzoefu wa biashara zingine iyo ni tofauti na mtu ambaye hajawai fanya biashara kabisa.
 
10m kwa bar usijaribu, ndogo sana ,,, pengine unaweza kodi frem
kuliko kunishusha ni bora ukatoa ushauri kulingana na matakwa yangu
Samahani, unaonekana una kiburi na dharau na unapenda kubishana na hutaki ushauri!

Tuanzie hapa kwenye mziki 'heavy duty', hapa nilivyokuelewa unataka disco kwa kifupi unataka wenye bar wengine waufyate!

Chukua hiyo milioni kumi nenda nayo pale congo (Kariakoo) ulizia full package ya disco sound bei ya chini ni kiasi gani! Kitachobaki kafungulie bar!
 
Back
Top Bottom