Milioni 200 inatosha nyumba na magari mawili?

Milioni 200 inatosha nyumba na magari mawili?

Hii ni chai. Huwezi kutafuta hela hadi upate 500m halafu hujui ujenge nyumba ya bei gani na gari ya bei gani latika bajeti yako ya 200m.
Huo nao pia ni ushauri in disguise! Imeandikwa, "sharpen your idea on the grindstone of criticism"
 
Nyumba ya makazi na una pesa uisimamie mwenyewe, haiwezi kuchukua miezi zote hizo 6 bhana.

Ni miezi mitatu tu inatosha msingi hadi finishing. Miezi 6 ni matumizi mabaya ya rasilimali.

Halafu mtu anaacha kazi, magari mawili ya nini, aanze na moja,la pili ama zaidi ataongeza akishajipata huko mbele ya safari.

Ujue gharama ya matunzo na mafuta ya magari yanahitajika, siyo kuendesha tu, ni gharama.

Nyumba ya kifahari kwa mil. 70 inatosha na mil. 30 kwa gari. Izo zingine asizitapanye, aziwekeze kuendeleza plan B yake.
Nyumba ya kifahari kwa mil 70 ni ipi ?
 
Hizo hela kaokota? Au kashinda bet?
Milioni 200 halafu analeta discussion za kipuuzi. Mleta mada, muulize kwanza, huyo mtu anaijua mil 200 au anaisikia tu?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mkuu ukiwa na bajeti ya millioni 30 huwezi kuomba ushauri wa kununua aina ya gari kutoka kwa wenye ufahamu wa magari?
Kwenye issues za uwekezaji inaeleweka. Lakini anunue gari gani kwa bei gani, ajenge nyumba ya bei gani...kwa mtu aliyehustle kuitafuta hadi kufika 200m amepitia mengi na ana uelewa wa mengi.
 
Hii ni chai. Huwezi kutafuta hela hadi upate 500m halafu hujui ujenge nyumba ya bei gani na gari ya bei gani latika bajeti yako ya 200m.
1. Anayeuliza haimaanishi kuwa hajui. Anaweza akawa anajua ila anataka kuboresha mawazo yake.

2. Umeshasoma kitabu cha THE MILLIONAIRE NEXT DOOR! Watu kama hao wapo hata nchi zilizoendelea.

3. Mimi nimeelezea mwitikio wangu kwa mtazamo wangu. Nilitarajia nipongezwe kwa jinsi nilivyoshauri vizuri au nikosolewe nilikokosea.

4. Kinachoandikwa humu kinasomwa na watu mbalimbali. Huenda siku za baadaye zikawa rejea kwa watu wengine. Kama mtu unafahamu jambo kwa ufasaha, itasaidia endapo utajibu kwa ukarimu kwa maslahi mapana ya kizazi cha sasa na cha baadaye.

5. Mwingine anayeupitia huu uzi anaweza asiwe ameshawahi kumiliki hata baiskeli, lakini majibu sahihi na ya kutia moyo yanaweza kumhamasisha na kumbadilisha fikra na kujikuta huko mbeleni na yeye anamiliki vinavyotamaniwa na wengi.

6. Kama swali halivunji Sheria za nchi wala hazikejeli dini za wengine, ukijibu kwa ukarimu utakuwa umewasaidia wengi japo huwafahamu. Kuna watakaosaodika, hata kama ni mmoja.

7. Kama kuna ambacho kinaonekana hakipo sawa, nilaumiwe mimi niliyeuleta huu uzi na siyo niliyeuliza kwa niaba yake. Aliuhitaji ushauri wangu, na mimi nilipotaka kujua usahihi wa ushauri wangu, nikalileta kwenye uma wa JF.
 
Mkuu ukiwa na bajeti ya millioni 30 huwezi kuomba ushauri wa kununua aina ya gari kutoka kwa wenye ufahamu wa magari?
Naweza kuuliza mkuu, tena nitaweka options kwenye maswali yangu. Ila kwa maelezo hapo mwamba hana clue mkuu. Ni kama hiyo 200m kapewa zawadi au kaokota sehemu.

Angalia jinsi mada ilivyo utaelewa nini namaanisha.
 
Nilivyo muelewa ni kwamba katika bajeti ya 200M anahitaji gari 2 katika shughuli zake na nyumba moja. Kwa hiyo bajeti ni gari gani aina zipi anunue kurahisisha shughuli zake kisha ajenge nyumba kwa gharama inayo baki. Ama mi nimeeelewa vibaya?
Naweza kuuliza mkuu, tena nitaweka options kwenye maswali yangu. Ila kwa maelezo hapo mwamba hana clue mkuu. Ni kama hiyo 200m kapewa zawadi au kaokota sehemu.

Angalia jinsi mada ilivyo utaelewa nini namaanisha.
 
Gari moja ni la kazi - safari za "mashambani" na "mikoani". Gari la pili ni dogo kwa mizunguko ya mjini na safari fupi.
asisahau na gharama za matengenezo ya hayo magari mawili.

Shilingi milioni mia mbili siyo nyingi kama hivyo anavyodhania (kwa vile hajazikamata), hasa hapo anapotaka kununua vitu visivyoingiza fedha, bali vinaziondoa kwenye mzunguko.
 
Nilivyo muelewa ni kwamba katika bajeti ya 200M anahitaji gari 2 katika shughuli zake na nyumba moja. Kwa hiyo bajeti ni gari gani aina zipi anunue kurahisisha shughuli zake kisha ajenge nyumba kwa gharama inayo baki. Ama mi nimeeelewa vibaya?
Uko sahihi.
 
Naweza kuuliza mkuu, tena nitaweka options kwenye maswali yangu. Ila kwa maelezo hapo mwamba hana clue mkuu. Ni kama hiyo 200m kapewa zawadi au kaokota sehemu.

Angalia jinsi mada ilivyo utaelewa nini namaanisha.
Nimebaini hili:
1. Watanzania wengi ni wakatishaji tamaa!

2. Watanzania wengi ni kama vile wana hasira hata na mtu wasiyefahamiana naye!

3. Lakini Watanzania wengi pia ni watu wenye busara pia!

JF inawaleta wote pamoja! Ni juu yako wewe kujua kukibaini ukihitajicho.
 
1. Anayeuliza haimaanishi kuwa hajui. Anaweza akawa anajua ila anataka kuboresha mawazo yake.

2. Umeshasoma kitabu cha THE MILLIONAIRE NEXT DOOR! Watu kama hao wapo hata nchi zilizoendelea.

3. Mimi nimeelezea mwitikio wangu kwa mtazamo wangu. Nilitarajia nipongezwe kwa jinsi nilivyoshauri vizuri au nikosolewe nilikokosea.

4. Kinachoandikwa humu kinasomwa na watu mbalimbali. Huenda siku za baadaye zikawa rejea kwa watu wengine. Kama mtu unafahamu jambo kwa ufasaha, itasaidia endapo utajibu kwa ukarimu kwa maslahi mapana ya kizazi cha sasa na cha baadaye.

5. Mwingine anayeupitia huu uzi anaweza asiwe ameshawahi kumiliki hata baiskeli, lakini majibu sahihi na ya kutia moyo yanaweza kumhamasisha na kumbadilisha fikra na kujikuta huko mbeleni na yeye anamiliki vinavyotamaniwa na wengi.

6. Kama swali halivunji Sheria za nchi wala hazikejeli dini za wengine, ukijibu kwa ukarimu utakuwa umewasaidia wengi japo huwafahamu. Kuna watakaosaodika, hata kama ni mmoja.

7. Kama kuna ambacho kinaonekana hakipo sawa, nilaumiwe mimi niliyeuleta huu uzi na siyo niliyeuliza kwa niaba yake. Aliuhitaji ushauri wangu, na mimi nilipotaka kujua usahihi wa ushauri wangu, nikalileta kwenye uma wa JF.
Sawa.
 
Nyumba ya kifahari kwa mil 70 ni ipi ?
Kwa mtu kama mimi, nikisimamia ujenzi mil. 70 ninajenga nyumba ya kupendeza sana.

Nyumba hiyo itakuwa na master kubwa, sebule kubwa, jiko, vyumba viwili self contained na dinning room.

Nje kutakuwa na car park, bwawa la kuogelea, bwawa la samaki, banda la mlinzi na fance la nguvu.

Hayo yote nitacheza nayo kwa 50m na 20m iliyobaki ntaipiga decoration ya kufa mtu na kubaki na change.

Ujue mkuu, kwenye ujenzi, simamia mwemyewe na manunuzi ya vifaa madukani usitume fundi wala familia, nenda mwenyewe, maana kwenye manunuzi makubwa ya ujenzi kama huo kuna discount kubwa.

Pia waweza kutathimini katika location ulipo, kama bei za mabati, nondo na saruji siyo ghali sana, ukiona inafaa waweza kuorder viwandani ukaokoa gharama.

Sijaculculate kukuwekea mchanganuo kwa sababu ninaongea kwa uzoefu.

Ila ukitaka, haya yote niliyoongea naweza nikakuwekea hesabu zake vile vile.
 
Huo nao pia ni ushauri in disguise! Imeandikwa, "sharpen your idea on the grindstone of criticism"
Watu huwa wanauliza nina 50m au 70m gari gani nzuri kwa ajili ya shamba au safari ndefu za mara kwa mara.
Hapa huyu mtu kashapiga hesabu yake atatumia 50m au 70m kwenye gari.
 
Hajawahi kumiliki nyumba wala gari lake binafsi. Kwa zaidi ya miaka kumi aliyokuwa kwenye ajira alikuwa akiishi na kutumia gari la taasisi.

Sasa anataka kuachana na ajira ili asimamie kwa karibu miradi yake. Ametenga milioni 200 kwa ajili ya nyumba na magari mawili.

Anataka magari mawili kwa sababu miradi yake itamuhitaji kusafri mara kwa mara hivyo anataka gari moja la masafa marefu na gari dogo kwa mizunguko ya mjini.

Ushauri wangu kwake:
1. Atenge milioni tatu kwa ajili ya pango la nyumba kwa miezi sita. Katika kipindi hicho cha miezi sita ahakikishe nyumba yake inakamilika.

Yeye alitaka kuinunua iliyokwishajengwa (kuna inayouzwa milioni tisini) lakini nimemshauri kuwa ya kujenga mwenyewe ni bora zaidi hasa ikizingatiwa kuwa atakapoacha kazi atakuwa na muda mzuri wa kuisimamia kwa karibu.

2(A). Anunue gari dogo (saloon) lisilozidi mililioni thelathini: AUDI, BENZ, BMW, n.k. Akikosa ya bei hiyo show room atafute kwa watu binafsi.

2(B). Anunue gari la masafa marefu lisilozidi milioni sabini. Mashaka yangu ni uwezekano wa kupata gari bora nchini kwa hiyo bajeti, hasa ikizingatiwa kuwa gari lake pendwa la masafa marefu ni LAND CRUISER PICK UP! Lakini sina uhakika kama ataweza kupata "zima" kwa bei hiyo.

Ingelikuwa ni wewe ungemshaurije?
Mkuu huyo 'jamaa' mwenye hiyo bingo la 200m siyo wewe kweli?

Nakumbuka kulikuwa na babu yangu mmoja, alipenda sana kuongea kwa 3rd party kama hivi.

Siku moja akaja kwangu akaanza vistori vyake kunisema mimi kimafumbo... 'Kuna kajamaa kamoja kijijini kameoa juzi juzi tu hapa hakajamaliza hata mwaka, eti kanaenda kwenye mabar na kumuacha mkewe msichana mbichi ndani, nikawa namwambia babu kigori unakiacha ndani unaenda kwenye pombe, wahuni watamgeuza mke wao'...

Kabla sijamuuliza ni nani huyo, nikamkata jicho la kipelelezi, alivyonibaini nataka kumshushua, tukajikuta wote tunaangua vicheko.
 
# Roca fella

MIlioni 200 nunua kiwanja Jenga nyumba za kupangisha.

millioni 200 nunua ist kwa shilingi 5 milioni uza kwa shilingi 9 milioni kila moja. Unapata faida ya milioni 3 ukitoa na ushuru na Kodi kadhalika.

milioni 200 ni mtaji wa kufuga kuku wa mayai na nyama na watakupa faida hawana Kodi Wala ushuru.

milioni 200 ni mtaji wa kuuza vipodozi na utatoboa,

milioni 200 mtaji wa biashara ya samaki

milioni 200 ni mtaji wa biashara ya hosteli kwa wanafunzi wa vyuoni.

milioni 200 ni mtaji wa biashara ya nafaka

milioni 200 ni mtaji wa biashara ya pombe kisiwani Zanzibar, utapiga hela unauzwa bia Bei nafuu

Milioni 200 unaweza kufanya chochote na ukatoboa maisha ni kutumia akili yako.
 
Umeulizwa mtu ana 200m inakuwaje anauliza vitu basic kama hivi?
Kana kwamba haitoshi unasema ana miradi ya 500m yaani ndio unazidi kuleta mkanganyiko.
Mtu ana ndoto ya kuwa na kwake lakini ana 200m hajui ajenge nyumba ya aina gani? Ana miradi ya 500m lakini bado hajui kubajeti 200m apate nyumba na gari. Hebu acheni kuchanganya vijana na stori zenu za mamilioni.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sasa mleta mada amekuja kumsemea anaeitaji ushauri, cha ajabu yeye ndio anajibu kama ndio mhusika mkuu..kwanini usimshauri ajiunge jamii forums na zaidi ni bure tu kuingia, ili ajibu mwenyewe na kupokea ushauri mwenyewe, yeye ndio anajua, sasa unavyojibu ni kama uko kwenye ubongo wake [emoji23][emoji23][emoji1] unless unachota watu akili
 
Back
Top Bottom