Millard Ayo ana tatizo gani na habari za Upinzani?

Millard Ayo ana tatizo gani na habari za Upinzani?

Kijana si mwanaharakati, anatazama maslahi yake kwa mapana, ebu anayeona millard anakosea aingie kazini ajazie pale alipokosa yeye. Kama BBC na DW wametimuliwa unataka Millard wamfanyeje au umesahau yaliyowapata wengine?

Ila na vyama pinzani miaka yote vinalalamika kuwa havipati jukwaa la usawa toka TV za ndani lakini hata hawajisumbui kuanzisha vyombo vyao vya habari hadi wamezidiwa mbinu na WCB kijana hata hajafika chuo kaona anabaniwa kwingine kaja na mbinu ya kuwa na chombo chake cha habari.
Diamond akili nyingi za kuzaliwa
 
Simlaumu milard bila shaka anacheza vile NGOMA inadunda, dw, BBC, voa wamegongeka itakuwa Millard? Milard endelea na mambo yako usiandike habari za majirani.. Mara ghafla usije kudaiwa Kodi ya bilioni 2
 
Mwisho wa haya yote ni October ndugu. Wait and see. Watanzania wa sasa sio wa juzi. Wanaona yote na watatoa hukumu yao baada ya uchaguzi.
Unaota mchana ngoja baada ya 28 Oct utazinduka na utakuja na maneno mengine hapa. Time will talk wala sina haja ya kubishana saaana
 
Kijana huyu baada ya kupata mafanikio kupitia sisi vijana, ghafla ameanza kujisahau. Zaidi ya 90% ya followers wake instagram pamoja na subscribers wake ni wafuasi kindakindaki wa CHADEMA na hilo analijua...
Acheni majungu, Millard kufika hapo alipofika ni msingi wa kujituma yeye mwenyewe binafsi. Ninyi CHADEMA mmemsaidia nini? Kum_follow? Sasa acheni ku_follow halafu muone Kama hataendelea kupata followers.

Rais wa awamu ya sita ni JPM, na kazi iliyoanzishwa lazima iendelee hakuna namna.
 
Kijana huyu baada ya kupata mafanikio kupitia sisi vijana, ghafla ameanza kujisahau. Zaidi ya 90% ya followers wake instagram pamoja na subscribers wake ni wafuasi kindakindaki wa CHADEMA na hilo analijua...
Mbona mnampangia cha kufanya? Sasa tofauti yenu na hao mnaowatuhumu kuminya vyombo vya habari ni nini?
Mmeanza kufanya hivyo bila meno, je! Mkipata mkiota meno?
 
sasa kama vyama vyenyewe vinafungiwaonline TVs na magazeti wadhani Millard akiwa mlengo wakushoto atafanywaje na palendipo kula yake ilipo hana ruzuku. Kama Kabendera yalimkuta yale unadhani Millard hana hofu? Si kila mtu anaweza kuwa mwanaharakati na wala haina haja ya kumlaumu maana kila mtu ana haki ya kuwa na hofu
Hivi kweli Kabendera kaufyata! Yuko wapi siku hizi?
 
Hivi kweli Kabendera kaufyata! Yuko wapi siku hizi?
Kaufya mkuu.. Unajua hata kifo cha mzee wake kilikuwa chakutatanisha walisema amejitosa majini lakini kipindi hicho alikuwaga na mgogoro na utawala wakasema siyo MTZ
 
Sio kweli, Tanzania Daima, Mawio, Mwana Halisi ziko wapi. Katika utawala wowote wa kiimla vyombo vyote vya habari vinatakiwa kumtukuza Dictator na si vinginevyo. Period.
Sasa wanaoalamika wanataka Millardayo afungiwe ili ale wapi? yeye siyo mwanaharakati ile kazia anifanya apate ugali yani kibiashara zaidi
 
Hivi Chadema miaka yote hiyo mmeshindwa kuanzisha hata YouTube channel? Kweli nyie ni mazuzu namba moja duniani. Huyo Millard Ayo huwa mnamchangia hata senti 1. Msipende mtelemko nyie
 
Kijana si mwanaharakati, anatazama maslahi yake kwa mapana, ebu anayeona millard anakosea aingie kazini ajazie pale alipokosa yeye. Kama BBC na DW wametimuliwa unataka Millard wamfanyeje au umesahau yaliyowapata wengine?

Ila na vyama pinzani miaka yote vinalalamika kuwa havipati jukwaa la usawa toka TV za ndani lakini hata hawajisumbui kuanzisha vyombo vyao vya habari hadi wamezidiwa mbinu na WCB kijana hata hajafika chuo kaona anabaniwa kwingine kaja na mbinu ya kuwa na chombo chake cha habari.
Sasa watapigaje mpunga wakiondoa mianya ya malipo ya kipigaji?
 
CHADEMA kwa kweli wametuangusha katika hili. Hivi hayo mabilioni ya 2015-2020 yasingetosha kuanzisha TV ama Radio station?
Ila na vyama pinzani miaka yote vinalalamika kuwa havipati jukwaa la usawa toka TV za ndani lakini hata hawajisumbui kuanzisha vyombo vyao vya habari hadi wamezidiwa mbinu na WCB kijana hata hajafika chuo kaona anabaniwa kwingine kaja na mbinu ya kuwa na chombo chake cha habari.
 
kumlaumu millard ni kumuonea tu kijana wa watu vyombo vya kimataifa vyenyewe vimenyooshewa kidole
yeye akizingua wanaweza kumuita mbele ya kamera na kamwili kake kalivyo kadogo watakachapa bakora tu kama adhabu🤣🤣🤣🤣
 
Kijana huyu baada ya kupata mafanikio kupitia sisi vijana, ghafla ameanza kujisahau. Zaidi ya 90% ya followers wake instagram pamoja na subscribers wake ni wafuasi kindakindaki wa CHADEMA na hilo analijua.

Katika video zinazohusu Siasa, kwa miaka yote zile zenye maudhui ya CHADEMA na viongozi wake ndio zimekuwa zikiongoza kwa views, hivyo tangia mwaka 2015 amewatumia vya kutosha wafuasi wa CHADEMA lakini kutokana na kujipendekeza leo kawapiga kapuni.

Haiingii akilini hata kidogo kurusha Live matangazo ya CCM katika kila hatua za chaguzi zao, Mkutano mkuu CCM, UVCCM, mpaka umoja wa wazazi, ikiwemo na matamko ya kipuuzi ya kina Polepole, Jaji Kaijage na mpwa wao Dr. Abbas vyote vimekuwa vikipata coverage ya kutosha, lakini leo hii hata kurusha habari za CHADEMA na tundu Lissu hakuna.

Hapa tunapoongea Millardayo hana habari kuwa CHADEMA na Lissu walikuwepo Singinda, Shelui, Igunga, kahama, Shinyanga na leo wapo Musoma. Mpaka leo habari iliyopo kwake ni ile ya Lissu kupokelewa JK Airpot. Hili halikubaliki hata kidogo, hata kujipendekeza basi ni lazima uwe na aibu.

Hujuma za Millardayo anazozifanya leo zina mwisho, Tukiamua kukupuuza utabakia huna dira, kawaulize TBC watakupa habari. Siku tukiamua kuja na petition ya kukupuuza ndio utajua maana ya nguvu ya umma.

Kumlaumu leo Millard Ayo ni kutaka Kumuonea tu Mkuu na nadhani hujafanya 'Utafiti' wako vizuri na kwa kina kujua tatizo ni nini. Kama kuna Kipindi ambacho Kwanza Waandishi wa Habari na Bloggers wengi 'wanatishwa' ni hiki lakini pia hapo hapo kama kuna Kipindi ambacho Waandishi wa Habari na Bloggers wengi ndiyo wanapiga 'Pesa' kutoka katika Chama chenye 'Financial Muscle' nchini Tanzania ( kinajulikana na wengi ) ni hiki. Ayo asiwaposikiliza au kujipendekeza Kwao lile Gari lake la Kifahari alilonalo Mafuta utamjazia Wewe? Wale Wafanyakazi wake na ile Nyumba aliyoikodisha kama Ofisi Kimara Kodi utamlipia Wewe? Njia ya kwenda Msalani ( Chooni ) Nyumbani Kwake ikiota Nyasi kwa Wanafamilia wake watakuja Kwako Kula? Acheni 'Unafiki' ili Vyombo vya Habari na Wanahabari wengi wawe Imara wanatakiwa wawe na Uwezo wao wa Kipesa lakini pia Sheria 'Kandamizi' zipigiwe Kelele na Haki iwepo. Nchi nyingi za Kiafrika 'Media' zake huwa 'zinatawaliwa' na Serikali zao husika. Afrika bado sana Mkuu.
 
Back
Top Bottom