Mimi ni Muislamu. Nasema HAPANA kwa katiba pendekezwa

Mimi ni Muislamu. Nasema HAPANA kwa katiba pendekezwa

KAUMZA

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2010
Posts
699
Reaction score
237
Nimesikia Rais wetu Mhe Kikwete akisema akisema, serikali haitaanzisha Mahakama ya Kadhi na kwamba ni Jukumu la waislamu wenyewe kuianzisha na kuihudimia.

Waislamu tumekuwa tukiburuzwa na kugaragazwa katika mambo ya msingi hasa pale wenzetu wa dini nyingine wanapoweka ngumu.

Tuliomba sensa iwe na kipengele cha dini, tukashindwa baada ya usaliti wa BAKWATA. 2005 tulidanganywa ktk ilani ya CCM, tukawachagua. Lakini Hola.

Mchakato wa uundwaji wa Katiba mpya ulipoanza, tukaona ndipo pa kupatia Mahakama ya Kadhi. Rasimu ya Kwanza na ya pili, zikaja bila ya Mahakama ya kadhi.

Tulipokuja juu, Waziri Mkuu akaahidi Mswaada wa Mahakama ya Kadhi utapelekwa Bungeni februari. Kiini macho kikafanyika eti kupata ridhaa na muafaka na ndugu zetu wa upande wa pili.

Na katika Mchakato wa kuurudisha bungeni mswaada April hii, viongozi wa wenzetu wametia munda. Hawaitaki Mahakama ya Kadhi. Wamehamasisha waumini wao, wajiandikishe kwa wingi na muda ukifika, wapige kura ya HAPANA kwa Katiba Pendekezwa.

Serikali imeogopa nguvu ya wenzetu wakristo. Imesema HAPANA kwa Mahakama ya kadhi, licha ya Tafiti nyingi kuonesha, Mahakama ya kadhi haina madhara (Waziri Mkuu, Waziri wa Sheria na Mwanasheria Mkuu) waliuthibitishia Umma.

Kutokana na kudharauliwa na kupuuzwa kunakofanywa na serikali mara kwa mara dhidi ya waislamu na Uislamu, binafsi nitapiga kura ya HAPANA KWA KATIBA PENDEKEZWA.

Ewe Muislamu na ndugu zangu wa dini nyingine, tuungane tupige kura ya HAPANA kwa katiba pendekezwa
 
Mbona Kikwete kasema ni ruksa kwa Waislamu kuanzisha na kughalimia mahakama ya Kadhi!!! Hivyo ndivyo nilivyomwelewa mimi..
Kwa hiyo kama mahakama ya Kadhi ingeanzishwa ungeipa katiba pendekezwa ya Chenge kura ya NDIO pamoja na ubovu wote huo???
 
Mie pia nasema hapana,mpaka tupate kadhi kwanza.
 
Ha ha ha serikali hii ya Ccm hua inawadanganya sana watu ila hua wanaon hata hiyo kua waislam wenyewe waianzishe ni kuongeza utamu kwenye mboga
 
nimesikia rais wetu mhe kikwete akisema akisema, serikali haitaanzisha mahakama ya kadhi na kwamba ni jukumu la waislamu wenyewe kuianzisha na kuihudimia.

Waislamu tumekuwa tukiburuzwa na kugaragazwa katika mambo ya msingi hasa pale wenzetu wa dini nyingine wanapoweka ngumu.

Tuliomba sensa iwe na kipengele cha dini, tukashindwa baada ya usaliti wa bakwata. 2005 tulidanganywa ktk ilani ya ccm, tukawachagua. Lakini hola.

Mchakato wa uundwaji wa katiba mpya ulipoanza, tukaona ndipo pa kupatia mahakama ya kadhi. Rasimu ya kwanza na ya pili, zikaja bila ya mahakama ya kadhi.

Tulipokuja juu, waziri mkuu akaahidi mswaada wa mahakama ya kadhi utapelekwa bungeni februari. Kiini macho kikafanyika eti kupata ridhaa na muafaka na ndugu zetu wa upande wa pili.

Na katika mchakato wa kuurudisha bungeni mswaada april hii, viongozi wa wenzetu wametia munda. Hawaitaki mahakama ya kadhi. Wamehamasisha waumini wao, wajiandikishe kwa wingi na muda ukifika, wapige kura ya hapana kwa katiba pendekezwa.

Serikali imeogopa nguvu ya wenzetu wakristo. Imesema hapana kwa mahakama ya kadhi, licha ya tafiti nyingi kuonesha, mahakama ya kadhi haina madhara (waziri mkuu, waziri wa sheria na mwanasheria mkuu) waliuthibitishia umma.

Kutokana na kudharauliwa na kupuuzwa kunakofanywa na serikali mara kwa mara dhidi ya waislamu na uislamu, binafsi nitapiga kura ya hapana kwa katiba pendekezwa.

Ewe muislamu na ndugu zangu wa dini nyingine, tuungane tupige kura ya hapana kwa katiba pendekezwa

ebu ondoa udini na siasa, sisi waislamu wenzio kamwe hatukuungi mkono hata kidogo we jitetee mwenyewe katika hilo.
 
Mimi pia nasema HAPANA, kwa sababu katiba pendekezwa ilipita kwa rushwa. Serikali iliwahonga wajumbe waisilamu ahadi ya kupeleka muswada wa sheria ya mahakama ya kadhi, nao wakakubali kuipitisha. Sikubali katiba iliyopitia vitendo vya rushwa, naitaka inayotokana na maridhiano ya pande mbalimbali zinazokinzana katika maeneo mbalimbali.
 
mimi pia nasema hapana, kwa sababu katiba pendekezwa ilipita kwa rushwa. Serikali iliwahonga wajumbe waisilamu ahadi ya kupeleka muswada wa sheria ya mahakama ya kadhi, nao wakakubali kuipitisha. Sikubali katiba iliyopitia vitendo vya rushwa, naitaka inayotokana na maridhiano ya pande mbalimbali zinazokinzana katika maeneo mbalimbali.

akili yako ndo imekomea hapo uwezo wake ktk kufikiri. Pole sana
 
akili yako ndo imekomea hapo uwezo wake ktk kufikiri. Pole sana
Asante sana. Sasa tunatokaje na hii kauli ya mgombea urais aliyetugeuka, au Ijumaa hiyo tukamng'oe Ndalichako kule NECTA? Alaaa, kumbe hayupo tena, sasa tukamng'oe nani safari hii?
 
Kura yangu ya hapana si kwasababu ya mahakama ya kadhi, kwasababu naamini mahakama hiyo inaweza kuanzishwa na dini husika kama walivyoanzisha Roman Cathoriki. Kura yangu ya hapana ni kwasababu Katiba pendekezwa imeondoka miiko ya maadali kwa viongozi wa umma, imeshindwa kupunguza madaraka ya Raisi, haijaweka ukomo wa ubunge kama ilivyo kwa uraisi na mambo mengine mengi kama tulivyopendekeza kwanye rasmu ya Warioba. Tunaunda katiba hatutaki kufanya makosa kwa kisingizio kuwa tutarekebisha mbeleni kwanini isiwe sasa.
 
Mie pia nasema hapana,mpaka tupate kadhi kwanza.

Mwaka huu na kuendelea Iwe mvua ama jua kali hamuwezi tena kuwaburuza waislam...


Tikiti maji wewe naona umepotea njia kabisa humu malumbano ya dini hayana nafasi hivi wewe Katiba na masuala ya dini wapi na wapi,Kwa taarifa yako katiba pendekezwa imeweka usawa kwa dini zote, sasa unataka wewe dini yako iingizwe kwenye katiba Daaaa ama kweli una upungufu wa madini joto afu unahamasisha iwe mvua iwe jua nenda oman,iraq au somalia tuachie Tanzania yetu ya Mwalimu Nyerere SOMA IBARA YA 41 uhuru wa imani ya dini Katiba Pendekezwa (3) Shughuli za uendeshaji wa jumuiya za dini itakua nje ya shughuli za mamlaka ya serikali, katiba yenye kifungu hiki ndiyo itakayopigiwa kura na watu wa dini zote.
 
kura yangu ya hapana si kwasababu ya mahakama ya kadhi, kwasababu naamini mahakama hiyo inaweza kuanzishwa na dini husika kama walivyoanzisha roman cathoriki. Kura yangu ya hapana ni kwasababu katiba pendekezwa imeondoka miiko ya maadali kwa viongozi wa umma, imeshindwa kupunguza madaraka ya raisi, haijaweka ukomo wa ubunge kama ilivyo kwa uraisi na mambo mengine mengi kama tulivyopendekeza kwanye rasmu ya warioba. Tunaunda katiba hatutaki kufanya makosa kwa kisingizio kuwa tutarekebisha mbeleni kwanini isiwe sasa.


hujaielewa hujaielewa sawasawa,kasome tena vizuri ukiwa umetulia utaona miiko na maadili ya watumishi wa umma afu utaona ukomo wa mamlaka ya rais kwa mujibu wa katiba.afu rasimu ya warioba haipo wajameni ilishapelekwa bungeni na uhai wake ukaishia pale, sasa ni kura tu jipange.
 
Mimi pia ni HAPANA na wangedhubutu kuweka mahakama ya kidini ndo kabisa Hata kura nisingepiga.Waislam anzisheni mahakama nyie wenyewe Kwa gharama zenu.Mkachinjane wenyewe.
 
Mimi pia ni HAPANA na wangedhubutu kuweka mahakama ya kidini ndo kabisa Hata kura nisingepiga.Waislam anzisheni mahakama nyie wenyewe Kwa gharama zenu.Mkachinjane wenyewe.

Kura ni siri yako, hatuhitaji matangazo humu ndani kama unataka matangazo kuna vyombo vingi vya habari nenda huko ukatangaze hiyo kura yako, hapa utakuwa unajaza server na kumaliza hizo mb 8 zako kaka. pole sana.
 
Lakini uzuri wa dini zetu ni rahisi sana kuzimudu. Utapiga kelele JF lakini ukitoka tu, ushalainishwa...
 
Back
Top Bottom