Mimi ni mwalimu, naacha kazi nijiajiri

Mimi ni mwalimu, naacha kazi nijiajiri

Jamaa at ana 2Millions anataka kuacha kazi.Usijidanganye kijana kwa hilo.Badae mkulu ataongeza mishahara itakua minono.Uhakiki unaelekea ukingoni tuna matumaini one day tutafurahia wote.Jitahidi kupata ushauri vizuri usikurupuke mjomba.
teacher muache mwenzio aje huku aje atengeneze 6m badala ya 2m we kama umeridhika na huo mshahara mkaushie baas
 
kujiajiri si rahisi kama kuajiriwa but akikomaa n rahis sana inahitaji nia ya dhati tu
mkuu kiukweli kujiajiri ni kugumu maana inaweza kuchukua miaka kadhaa ndio mambo yakae vizuri unless uko lucky sana. imagine umeamua kuwekeza hela shamban afu ukapata hasara na uliweka hela yote kule kuna kipindi unatamani usingeacha kazi. kujiajiri inataka commitment na sacrifice sana tena kama una familia na upepo ulivo sasa hivi
 
Kabla hujaacha kazi kuna mtu mbadilishane kituo kama ni pazuri! Atakuongezea na mtaji kidogo!!
 
Unawzaje
Duuh! Wewe umejitahidi sana, mimi ni mwaka mmoja na miezi 10 sasa lakini ipo natafuta pa kukimbilia. Kazi ya kipumbavu kabisa hii. Tanzania hatuna viongozi bali ni masanamu. Yaani mtu unashika uongozi mara moja unawaongezea wanajeshi posho wakati wana posho kubwa, wamejengewa nyumba, hawana faida ya moja kwa moja kwa jamii isipokuwa kwa viongozi tuu, na ukiangalia na elimu yao ndo wale wahuni kipindi tunasoma ndo machozi yanakutoka kabisa.
Katika watu ambao naona hawana umuhimu kwenye nchi kama ya kwetu ni wanajeshi yaani hawa jamaa ni hasara
 
Mkuu fanya kitu moyo wako unapenda kama malengo yako ni kuwa kuwa na investments zako uamuzi huo ni mzuri
Kwa kuongezea mtahi ulio nao unawezaukachua mafao yako ya muda uliofanya kazi ukaongezea kwenye mtaji au ukaingia zako bank ukachukua loan alafu ukapote
Bro wangu mwaka jana mwezi wa pili aliacha kazi aliangalia mafao yako yalikuwa milioni 6 ya miaka 5 aliyokaa kazini hiyo ni michango yake na ya mwajiri akaona ni ndogo akaingia bank akakopa millioni 15 baada ya miezi 2 akapotea
 
mkuu kiukweli kujiajiri ni kugumu maana inaweza kuchukua miaka kadhaa ndio mambo yakae vizuri unless uko lucky sana. imagine umeamua kuwekeza hela shamban afu ukapata hasara na uliweka hela yote kule kuna kipindi unatamani usingeacha kazi. kujiajiri inataka commitment na sacrifice sana tena kama una familia na upepo ulivo sasa hivi
kweli mkuu me wakati naanza kujiajiri nlianza shambani na niliweka senti zote huko nkapiga hasara murua kabisa zile stress zake zlikua next level but skukataa tamaa n now am moving forward...... kujiajiri matokeo huanza kuonekana mara nyingi after 2yrs hapo ndo channel zinakua zimejiset
 
Big up ....njoo tulime matikiti na huo mtaji ndugu
 
Sikuamuamini siku nlipomuona mwalimu wangu wa shule ya msingi, japo kwa wakat ananinifundisha alikua anaelekea kwenye uzee sasaiv kawa mzee sana, nilikuta anatembeza bisi kwenye rambo, sijui kiinua mgongo chake alimalizia kusomesha wanawe??
 
Unawzaje

Katika watu ambao naona hawana umuhimu kwenye nchi kama ya kwetu ni wanajeshi yaani hawa jamaa ni hasara
Kwahiyo mkuu unaweza kushaur jeshi lifutwe kabisa?? Me navyoona kuwepo kwajeshi nivizur zaid kuliko kutokuwa najeshi alafu maadui wakajitokeza naona itakuwa nihatar zaidi, sema2 inabidi walimu waangaliwe zaidi kuliko hao wanajeshi yaan walimu wawe namishahara naposho zaidi kuliko wanajeshi
 
Jamaa at ana 2Millions anataka kuacha kazi.Usijidanganye kijana kwa hilo.Badae mkulu ataongeza mishahara itakua minono.Uhakiki unaelekea ukingoni tuna matumaini one day tutafurahia wote.Jitahidi kupata ushauri vizuri usikurupuke mjomba.
Hata mwajiri wako akuongezee Mshahara mara mbili ya ulonao..kutoka ndoto...ishu nzima ni kujiajiri
 
Ninakaribia 30. Nafundisha sekondari, somo la Basic Mathematics. Sina furaha na kazi yangu kwa sababu kipato hakiendani na kasi ninayoipenda. Nimegundua kuwa na degree hakuendani na kipato. Bado tunatishwa tishwa. Walimu nimegundua ni waoga. Hasa kufanya maamuzi magumu na sahihi. Mwalimu wa Tanzania anaishi kimaskini. Naacha kazi, naenda kujiajiri mwenyewe. Kwa heri utumwa, Kwaherini walimu. KWAHERINI. Usiniige kama hujajipanga. Nina sh milioni 2. naenda kuipanda. Hii sio ndogo kwangu. Sirudi tena kufunza.
Asante kwa kuokoka,karibu katika ufalme wa raha ya milele,ishi unavyotaka fanya kazi unayopenda.
 
Kuna baadhi ya members humu JF ni wajinga wajinga tu kama wajinga waishivyo.
Binafsi wazazi wangu walikuwa Walimu though by the time Baba yangu nyakati za mwisho wa uhai wake alikuwa akitumikia kama Afsa Elimu Wilaya na alibakisha miaka 4 kufikia ukomo katika ajira ya utumishi wa umma.
Mama yangu ni mstaafu kwa sasa.
Nakumbuka kipindi nahitimu kidato cha sita(2004 SONGEA BOYS) mimi na wazazi wangu tulisigana sana kuhusu kipi napaswa kusomea chuo kikuu make walikuwa na uhakika lazima nitapass. Wote waliafiki niwe mwalimu kama walivyo wao!
Binafsi sikutaka kabisa ajira yoyote iwayo amma lah iwe kama daraja tu! Kweli Mungu ni mwema alijaalia nikapata div II nikawa enrolled kusoma Accounts na mwishowe nikaajiriwa kuwa Assistant Accountant kwenye kampuni ya Wazungu. Baada ya miezi15 nikapiga chini na kurudi mtaani mpaka leo hii.
Ninayo mengi sana ya kuelezea but i reserve them all execept to all who deserves like this guy Felice1
Mdogo wangu usikatishwe tamaa na watu waoga njoo ntakupa shamba, waterpump n.k bure.
 
Ujiajiri uwe na Capital na business skills sasa
 
Una busara sana mkuu!

Kuacha kazi sio suala ma mihemuko kama hivyo! Mtu anasema anaacha ajira halafu bado ana muda wa kuanzisha thread za namna hii[emoji18] [emoji18]
Sio mihemko anawatia moyo wengine ambao wana woga wa kuthubutu! Pia hapa atakutana nawalio tangulia kuacha hapo awali wampe mbinu nyingine!
 
Ninakaribia 30. Nafundisha sekondari, somo la Basic Mathematics. Sina furaha na kazi yangu kwa sababu kipato hakiendani na kasi ninayoipenda. Nimegundua kuwa na degree hakuendani na kipato. Bado tunatishwa tishwa. Walimu nimegundua ni waoga. Hasa kufanya maamuzi magumu na sahihi. Mwalimu wa Tanzania anaishi kimaskini. Naacha kazi, naenda kujiajiri mwenyewe. Kwa heri utumwa, Kwaherini walimu. KWAHERINI. Usiniige kama hujajipanga. Nina sh milioni 2. naenda kuipanda. Hii sio ndogo kwangu. Sirudi tena kufunza.
Nilifanya kazi ya ualimu miez 6 nikataka kuacha wakanipa moyo kuwa mwanzo mgumu nikajitahidi nikamaliza mwaka mambo yakawa magumu zaidi nikataka kuacha wazee wakanipa moyo tena ila baada ya kutimiza miaka mitatu nikaona hakuna jinsi ila ni kuacha tu. Kazi nilikuwa naipenda sana ila katika sekta ya elimu kila alie juu yako anataka kutukuzwa,mazingira magumu,nilikuwa nakaa mlimba lakin mshahara nilikuwa naufata Ifakara au Dar ambapo sometimes ilikuwa inanicost hadi laki,niliomba likizo ya kulipwa nikapewa ila pesa hawakunipa mpaka leo. Bora wewe una M2 mimi nimeacha nikiwa na Laki 7 tu. Fanya kile unaona ni sahihi ila kiukweli Ualimuni mzuri ila hatuthaminiwi
 
Back
Top Bottom