Mind Illusion Projection: Jinsi ya kuidanganya mind ione vitu visivyo halisi kua ni halisi

Mind Illusion Projection: Jinsi ya kuidanganya mind ione vitu visivyo halisi kua ni halisi

Kiongozi kuna huyu mtu anaitwa Watchman Nee hebu tafuta vitabu vyake naamini utavipenda sana.
Jamaa nimeingia mtandaoni anavyo vitabu vingi balaa mkuu. Ingawa sijavisoma Ila naona kidogo Kama vina diverge na interests zangu. Ingawa Kuna ishu ya souls,mind na body naona Kama anavyo vinavyoelezea.
Ila ngoja nipakue nikiwa na muda napitia kimoja kuliko kumcheki Fulani leo akafanyeje
 
Jamaa nimeingia mtandaoni anavyo vitabu vingi balaa mkuu. Ingawa sijavisoma Ila naona kidogo Kama vina diverge na interests zangu. Ingawa Kuna ishu ya souls,mind na body naona Kama anavyo vinavyoelezea.
Ila ngoja nipakue nikiwa na muda napitia kimoja kuliko kumcheki Fulani leo akafanyeje
Ninavyo vingi sana vitabu vya huyu jamaa. Ningeweza ningekupakilia hapa
 
Mitaani kumekua na visa mbalimbali mfano ulishawihi kukutana na kitu kireefu imevaa nguo nyeupe ukatoka mbio balaa kila unapokimbia unakikuta mbele yako , au ushawahi kukutana na ng’ombe wa mguu mmoja akakukimbiza au kitu chochote kisichokua cha kawaida chenye kuhusiana na uchawi au kusikia watu wakihadthia matukio ya namna hiyo. Kuna wale wanaoenda kutafuta pesa za ndagu wanaambiwa saa nane ya usiku nenda sehemu Fulani chochote utakachokiona usikimbie wala usikikwepe, mara anatokea simba anataka kukurukia au inatokea treni iko speed kali inatakiwa usiipishe. Ajabu ni kwamba ukikutana na kitu kirefu cheupe ukikipita mkono wa kushoto (?) kitu hicho hakikudhuru au usipoipisha hio treni haikudhuru…..Ukweli ni kwamba kupita upande wa kushoto wa kitu hicho kirefu hausaidii lolote wewe kushambuliwa na kitu hicho, vitu vyote nilivyoorodhesha hapo vinapokutokea hua sio halisi they are just an illusions. Usipokimbia kitu hicho unakua umedhibiti hofu ndani ya roho yako wachawi wanatumia hofu yako kukuHaunt.
Mada yako ni nzuri sana. Kabla sijaendelea kujenga hoja. Yapo ninayo kubaliana na wewe na yapo ambayo nahitaji ufafanuzi zaidi. Mathalani unapo sema Wachawi wanamtia hofu mtu na si uhalisia. Naomba unipe maana halisi ya Uchawi,kisha tutamjua Mchawi au Wachawi ni kina kwa wingi.

Ama kuhusu dhana zinazo ambatana na wasi wasi kisha ukaona jambo dhahania ukasema ni halisi hili lipo. Na hili lina sababu zake,wengi wanao sema hayo huwa katika wenge la usingizi,au wamelewa na mara chache sana ukiwa timamu.
 
Wachawi wote duniani wanapenda kuogopewa they feed up from your fear, unapomuhofu mchawi basi unakua umemuongezea nguvu ya kukuwinda pindi unapoacha kumuogopa tu basi hata kusumbua tena kuna mstari mmoja Jose mtabmbo anaimba kwamba “unaniwangia mimi nimelala, utajijua si wewe ndio unakesha” nachomaanisha ni kwamba unapokutana na kitu kisicho cha kawaida ukawaeza kudhibiti hofu yako ukaacha kukimbia basi kitu kile hakitakudhuru maana utakua hujaonyesha hofu since vitu hivyo tunavyokutana navyo hua sio halisi ni kwamba Mind yetu inakua imelazimishwa kuona vitu hivyo ni halisi ila behind the curtain unakuta ni hakuna kitu hicho au ni mtu wa
Uoga wa dhidi ya jambo fulani huambatana na kutolijua jambo hilo,ila kama unajua ni ngumu sana kuogopa.

Wanadamu tumeumbwa na hofu. Kuna hofu ya kimaana na hofu ya kihisia. Mathalani leo hii au wewe ukimuona Simba,lazima utamuogopa au ukiona moto ghafla. Kisha mengine hufata,hofu huambatana na tahadhari,vipi ukione kitu kisicho cha kawaida yaani hujui hakika yake ni muhali kudhibiti hofu.

Kudhurika ni matokeo tu,ambayo hayahusiani na hofu au kutokuwa na hofu. Swali litakuja,umekutana na kitu gani ? Hapa ungetupa mfano.
 
By default wanauwezo wa kutengeneza vitu visivyo halisi kuwa kama halisi yaani Illusions projection au reality manipulation yaanii anaweza kutengeneza kitu kwa kutumia uwezo wake huo ukaona labda ukuta sehemu lakini sio ukuta sio halisi, lakini illusions hizo zinaweza kuwa na maadhara kwenye maisha halisi ya mwanadamu mfano mtu kaonyesha barabarani pale hakuna gari kumbe kuna gari wewe ukavuka likakukupitia. Kuna wakati mtu anaweza kua kafariki lakini mtu huyo hajafa kiuhalisia kama tunavyoona bali kachukuliwa kimazingira na kuhamishwa dimension nyingine, pale msibani sisi tunabaki tunaona mtu ndio tumemzika kumbe tumezika kipande cha mgomba au chochote kile
Hapa kuna Uchawi na mazingaombwe. Vyote ni uhalisia,yaani vipo.
Soul imegawanyika katika sehemu tatu ambazo ni Mind,Impression na Intellect..Mind imegawanyika katika pande tatu ambazo ni Conscious mind, Unconscious mind na Subconscious Mind. Conscious mind ni sehemu ya Mind ambayo inahusika na kushughulikia yale mambo yote ambayo tunayafahamu either kwa kuona,kusikia au kuhisia, kiufupi Conscious mind inashughulikia yale ambayo yapo katika utambuzi/ufahamu wetu. Ndio maana wewe mwanadamu wa kawaida huwezi kuwaza nje ya vile vitu unavyofahamu kama unabisha jaribu kuwaza kitu ambacho hakipo au hakina ufanano na kitu ulichowahi kuona au kusikia… Conscious mind inajihusisha na memories,perception,feeling, sensation na fantasies zilizomo ndani ya utambuzi wetu, Conscious mind hua inashirikiana na Subconcious mind hivyo basi hua zinataka kufanana maana au ufanyaji wa kazi so chunga zisikuchanganye.
Hili jambo unatakiwa ulifanyie utafiti zaidi,hasa ujue wapi ni sehemu sahihi ya kuchukua marejeo.

Soul bila shaka ni Roho, hii roho ni nini hasa ,na Mind bila shaka ni Akili. Unaweza kuniambia Mind katika mwili wa mwanadamu iko wapi ?
imeweewa alogarithim iitwayo FIFO (First In First Out) ambapo data zile zinazoingia kwenye Data Buffer zitaanza kuchakatwa kisha zitatolewa nje kisha ndio zije nyingine.
NB: Data Buffer unaweza kuiita kwa lugha rahis Random Acess Memory (RAM)

kwenye mada yangu moja iliyopita nileeleza kwamba Subconcious mind ndio sehemu ya utanzaji wa kumbuku za kila kitu unachoona na kukifanya maishani mwako nikaifananisha na Data Cache and Cockies … Sasa basi kwenye Conscious mind kunafanya kazi kama kwenye Computer, kwakua ndio sehemu inayohusika na kuwaza/kufikiri yenyewe hua haitunzi kumbukumbu ya kile inachokifanyia kazi na yenyewe ina tumia huo mfumo wa FIFO wazo litakaloanza kuingia ndio hilo litakalofanyiwa kazi taarifa ya wazo hilo itapelekwa kwenye Subconscious mind kuhifadhiwa lakini pia Conscious mind inauwezo wa kuchakata data moja tu kwa wakati mmoja tu.Conscious mind inachukua taarifa mbalimbali kwa kutumia kuona,kusikia, kunusa,kuhisi,kugusa au kuonja. Conscious mind inakusanya na kuchambua kila kinachoendelea kwenye mazingira yako na kukichambua kwa njia hiyo ya FIFO kama kuna kitu inataka kukiwaza ila kilishawahi fanyiwa kazi basi Conscious mind itaResquest kwenye sotorage centre kitu hicho yaani kwa Subconcious mind
Kwa kuzingatia mfano wako wa Computer hivyo ulivyo vitaja sehemu zake kwenye Computer zinafahamika,swali langu ni Conscious na Subconsciuos Mind katika mwili wa mwanadamu ziko wapi ?
 
Hapa kuna Uchawi na mazingaombwe. Vyote ni uhalisia,yaani vipo.
Ndio vipo vyote
Hili jambo unatakiwa ulifanyie utafiti zaidi,hasa ujue wapi ni sehemu sahihi ya kuchukua marejeo.

Soul bila shaka ni Roho, hii roho ni nini hasa ,na Mind bila shaka ni Akili. Unaweza kuniambia Mind katika mwili wa mwanadamu iko wapi ?
Akili/mind ipo ndani ya Roho/soul
Kwa kuzingatia mfano wako wa Computer hivyo ulivyo vitaja sehemu zake kwenye Computer zinafahamika,swali langu ni Conscious na Subconsciuos Mind katika mwili wa mwanadamu ziko wapi ?
Kiufupi ni kwamba Soul imebaba mind na mind ina hizo conscious na subconscious mind ndani mwake. Roho ipo ndani ya ubongo (Brain)
Mind ni software part ambayo huwezi kuiona ila utaona matendo yake.
 
Akili/mind ipo ndani ya Roho/
Hili umelijuaje ?

Roho ni nini ? Yaani naomba unipe maana ambayo inazuia yote yasiyo husu Roho kuingia na inaruhusu yote yanayo husu Roho kuingia.

Hapa ndipo songombingo huanza.

Mimi navyo fahamu ni kuwa akili mahala pake ni moyoni,na hufanya kazi sambamba na Ubongo.
Kiufupi ni kwamba Soul imebaba mind na mind ina hizo conscious na subconscious mind ndani mwake. Roho ipo ndani ya ubongo (Brain)
Mind ni software part ambayo huwezi kuiona ila utaona matendo yake.
Swali langu limemili katika sehemu mahususi ya Roho,unapo sema Roho imebeba akili,nitakuuliza vipi kwa mtoto ambaye yuko tumboni na ni hai,vipi kwa mtoto mchanga na vipi kwa chizi ? Maana yake kilicho hai kina Roho,yaani kina akili. Vipi kuhusu mimea ?

Unaposema Roho ipo ndani ya Brain hii si kweli.

Mfano wa Roho katika mwili wa mwanadamu ni kama mfano wa Mafuta katika gari.
 
Hili umelijuaje ?

Roho ni nini ? Yaani naomba unipe maana ambayo inazuia yote yasiyo husu Roho kuingia na inaruhusu yote yanayo husu Roho kuingia.

Hapa ndipo songombingo huanza.

Mimi navyo fahamu ni kuwa akili mahala pake ni moyoni,na hufanya kazi sambamba na Ubongo.
Natumaini unachanganya kati ya roho na nafsi.. nafsi ndio hukaa moyoni
Swali langu limemili katika sehemu mahususi ya Roho,unapo sema Roho imebeba akili,nitakuuliza vipi kwa mtoto ambaye yuko tumboni na ni hai,vipi kwa mtoto mchanga na vipi kwa chizi ? Maana yake kilicho hai kina Roho,yaani kina akili. Vipi kuhusu mimea ?

Unaposema Roho ipo ndani ya Brain hii si kweli.

Mfano wa Roho katika mwili wa mwanadamu ni kama mfano wa Mafuta katika gari.
Je wewe binafsi unafahamu nini kuhusu Roho na akili?
 
Natumaini unachanganya kati ya roho na nafsi.. nafsi ndio hukaa moyoni
Hapa sijachanganya,sababu tamko Nafsi,nalifahamu vizuri sana tena kutokeakatika lugha yake ya asili. Nafsi ni wewe, yaani ili uipate nafsi ni uchukue Roho ujumlishe na Mwili. Yaani Roho na Mwili unapata nafsi. Na hilo tamko Nafsi kuna wakati humaanisha Roho.

Kwenye Qur'aan tunapewa majibu kuhusu Roho,mtume wetu watu wake walikuwa wana muuliza sana kuhusu Roho,na majibu ni kuwa kuhusu Roho nimepewa elimu ndogo sana.

Anasema Allah mtukufu :

85. Na wanakuuliza khabari za Roho. Sema: Roho ni katika mambo ya Mola wangu Mlezi. Nanyi hamkupewa katika ilimu ila kidogo tu. (Israa : 85)

Hizi ni elimu pweke unatakiwa ujue wapi unapata elimu kuhusu vitu hivi hasa nafsi,roho na akili,watu wengi sana hawana elimu sahihi kuhusu vitu hivi.
 
Hapa sijachanganya,sababu tamko Nafsi,nalifahamu vizuri sana tena kutokeakatika lugha yake ya asili. Nafsi ni wewe, yaani ili uipate nafsi ni uchukue Roho ujumlishe na Mwili. Yaani Roho na Mwili unapata nafsi. Na hilo tamko Nafsi kuna wakati humaanisha Roho.
Naam nakubaliana na wewe
Kwenye Qur'aan tunapewa majibu kuhusu Roho,mtume wetu watu wake walikuwa wana muuliza sana kuhusu Roho,na majibu ni kuwa kuhusu Roho nimepewa elimu ndogo sana.

Anasema Allah mtukufu :

85. Na wanakuuliza khabari za Roho. Sema: Roho ni katika mambo ya Mola wangu Mlezi. Nanyi hamkupewa katika ilimu ila kidogo tu. (Israa : 85)
🙏
Hizi ni elimu pweke unatakiwa ujue wapi unapata elimu kuhusu vitu hivi hasa nafsi,roho na akili,watu wengi sana hawana elimu sahihi kuhusu vitu hivi.
Ndio maana nimeeleza sehemu kwamba Dark power na Light power zote zinaweza kukupatia ufahamu sasa ni mtu mwenyewe kutambua ufahamu alionao unatoka katika nguvu gani.
Ni Mungu anifunuliaye yale nisiyoyafahamu maana anasema Ukimpokea yeye basi atakuonyesha mengi makuu usiyoyajua
 
Je wewe binafsi unafahamu nini kuhusu Roho na akili?
Umeuliza swali zuri sana. Niliwahi kuandika mada maalumu kuhusu ROHO. Nikaipa anuani hii "Ukweli kuhus Roho na yote yanayo ihusu".

Hapa nakuwekea kama ilivyo mada hiyo.



"Katika mambo makubwa mno yenye kuwatatiza watu tangu dunia inaumbwa ni hili jambo kuhusu ROHO.

Wamepita Wanafalsafa wa kale na wa sasa, Wanasayansi wa zamani na wasasa, watu wa dini, na wasio kuwa hao katika kuelezea Roho ni nini, hatimae wamekuja na mitazamo mingi yenye kutatiza watu na isiyokuwa na ithibati wala hakika yoyote.

Lakini hao wote mpaka Wakana Mungu ( Atheists) wakakubaliana ya kuwa KIFO ni ule muda ambao maisha hukoma kwa kiumbe, au Roho kuacha mwili. Suala la Roho limebaki kuwa jambo lililo fichikana kuhusu hakika yake na undani wake, na Mola wetu hakutoa elimu juu ya Roho isipokuwa kidogo mno, na jambo hili limebaki kwake kwa mapana yake.

Mola wetu anasema katika Qur'aan, juu ya ukweli kuhusu ROHO.

85. Na wanakuuliza khabari za Roho. Sema: Roho ni katika mambo ya Mola wangu Mlezi. Nanyi hamkupewa katika ilimu ila kidogo. (Israa : 85)

Hii inaonyesha ya kuwa suala la elimu juu ya Roho ni elimu kubwa mno na sisi tumepewa elimu ndogo sana juu ya ROHO na jambo hili linabaki kuwa kwake Mola wetu kwa undani wake.

Kama hali iko hivi, ni nini Roho ? Ni zipi sifa zake? Ni zipi tabia zake na ni upi uwezo wake ? Maswali haya watu hujiuliza sana.

Katika Elimu hiyo ndogo tuliyopewa na Mola wetu, tunaipata kutoka katika vyanzo vya uhakika na kuaminika ya kuwa, Roho ni kitu kisicho onekana, chenye mafungamano ya moja kwa moja na mwili.

Lakini Roho hiyo ina sifa kadhaa kwazo huwa tunazitumia kuelezea vitu vyenye kushikika (Tangible things), kama vile hupulizwa na Malaika kuupa mwili uhai na hutolewa kipindi mja anapokufa, hukutana na kuzungumza.

Mwili unakufa ila Roho haifi, roho hubaki milele. ROHO ni katika vile viumbe ambavyo vina mwanzo ila havina mwisho.

Huu ndiyo ukweli kuhusu ROHO kwa ufupi.

Zingatia : Wasomi wakubwa na wahakiki wa mambo, wametofautiana juu ya Roho na Nafsi, ya kuwa je ni kitu kimoja au ni vitu viwili vyenye kutofautiana. Wapo walio sema ya kuwa Roho na Nafsi ni vitu viwili tofauti na kutofautiana kwake hulingana na muktadha wa hali, wengine wakasema ya kuwa Nafsi ni mjumuiko kati ya Roho na Mwili, na wapo waliosema ya kuwa Roho ni Nafsi na Nafsi ni Roho.".

Hiki ndicho nilichokiandika katika mada hiyo.

Ama kuhusu akili, akili kiasili ni tamko la Kiarabu lenye maana ya "Kizuizi", waarabu kamba ya kumfungia mbuzi asitoke nje ya eneo iliitwa "aql" . Kwa maana ya kisheria AKILI ni kizuizi kinachomfanya mwanadamu asikozee katika maamuzi. Ndiyo maana ukisoma katika elimu ya Mantiki (Logic) wanakwambia ya kuwa Mantiki ni ya kutumia akilo kwayo humfanya mtu asikosee katika kujenga hoja. Tunarudi kule kule katika maana ya msingi. Yaani akili ni kizuizi kinachomfanya mja asikosee katika kutenda mambo.

Tuendelee na mjadala kutokea hapo.
 
Ndio maana nimeeleza sehemu kwamba Dark power na Light power zote zinaweza kukupatia ufahamu sasa ni mtu mwenyewe kutambua ufahamu alionao unatoka katika nguvu gani.
Ni Mungu anifunuliaye yale nisiyoyafahamu maana anasema Ukimpokea yeye basi atakuonyesha mengi makuu usiyoyajua
Kwa maana rahisi Dark Power ni nini ?

Lakini ukweli unabaki pale pale hatujui mengi kuhusu Roho ila machache ambayo ametufunulia Mola muumba.

Sasa wewe unakosea katika jambo hili sababu unatumia akili yako na maelezo ya wakubwa wako katika uliyo yasoma kuhusu vitu hivi. Huwezi kupatia hata siku moja,sababu uwezo wa akili zetu zina ukomo.

Tuko pamoja.
 
Kwa maana rahisi Dark Power ni nini ?
Mara nyingi natumia neno hilo kumaanisha Shetani/Ibirisi
Lakini ukweli unabaki pale pale hatujui mengi kuhusu Roho ila machache ambayo ametufunulia Mola muumba.
Sahihi kabisa na hatuwezi kuyajua yote
Sasa wewe unakosea katika jambo hili sababu unatumia akili yako na maelezo ya wakubwa wako katika uliyo yasoma kuhusu vitu hivi. Huwezi kupatia hata siki moja,sababu uwezo wa akili zetu zina ukomo.
Tuko pamoja.
Upo sahihi. Lakini hakuna mwanadamu aliyefanya kitu kwa asilimia 💯 yaani ukamilifu. Naamini bandiko langu linamapungufu kibao ila pia lina usahihi kiasi fulani. So kazi ni kwa msomaji kuangalia madhaifu tu au mazuri pia
 
Upo sahihi. Lakini hakuna mwanadamu aliyefanya kitu kwa asilimia 💯 yaani ukamilifu. Naamini bandiko langu linamapungufu kibao ila pia lina usahihi kiasi fulani. So kazi ni kwa msomaji kuangalia madhaifu tu au mazuri pia
Naanzia hapa. Umesema kweli kabisa. Kutokana na udhaifu wa akili yetu na baadhi ya mambo kutoweza kuyadiriki katika uhalisia wake. Mola wetu akawa anatimiliza mitume na manabii (Siyo hawa feki ambao tunaishi nao ) kwa ajili ya kujibu maswali kwa yale yaliyo fichikana,kama vile baada ya kufa hufata nini,au roho ni nini,akili ni nini au nini lengo la kuwepo duniani, chanzo cha uhai ni nini (swali hili liliwasumbua sana Wanafalsafa wa Magharibi ikatokea kila mmoja akaelezea kwa mtazamo wake).
 
Naanzia hapa. Umesema kweli kabisa. Kutokana na udhaifu wa akili yetu na baadhi ya mambo kutoweza kuyadiriki katika uhalisia wake. Mola wetu akawa anatimiliza mitume na manabii (Siyo hawa feki ambao tunaishi nao ) kwa ajili ya kujibu maswali kwa yale yaliyo fichikana,kama vile baada ya kufa hufata nini,au roho ni nini,akili ni nini au nini lengo la kuwepo duniani, chanzo cha uhai ni nini (swali hili liliwasumbua sana Wanafalsafa wa Magharibi ikatokea kila mmoja akaelezea kwa mtazamo wake).
Je kwanini asitimilize kwa watu wa sasa wenye kumtafuta - kutafuta hekima yake?
 
Back
Top Bottom