Ego is the Enemy
JF-Expert Member
- Mar 21, 2014
- 8,201
- 16,246
Jamaa nimeingia mtandaoni anavyo vitabu vingi balaa mkuu. Ingawa sijavisoma Ila naona kidogo Kama vina diverge na interests zangu. Ingawa Kuna ishu ya souls,mind na body naona Kama anavyo vinavyoelezea.Kiongozi kuna huyu mtu anaitwa Watchman Nee hebu tafuta vitabu vyake naamini utavipenda sana.
Ninavyo vingi sana vitabu vya huyu jamaa. Ningeweza ningekupakilia hapaJamaa nimeingia mtandaoni anavyo vitabu vingi balaa mkuu. Ingawa sijavisoma Ila naona kidogo Kama vina diverge na interests zangu. Ingawa Kuna ishu ya souls,mind na body naona Kama anavyo vinavyoelezea.
Ila ngoja nipakue nikiwa na muda napitia kimoja kuliko kumcheki Fulani leo akafanyeje
Mada yako ni nzuri sana. Kabla sijaendelea kujenga hoja. Yapo ninayo kubaliana na wewe na yapo ambayo nahitaji ufafanuzi zaidi. Mathalani unapo sema Wachawi wanamtia hofu mtu na si uhalisia. Naomba unipe maana halisi ya Uchawi,kisha tutamjua Mchawi au Wachawi ni kina kwa wingi.Mitaani kumekua na visa mbalimbali mfano ulishawihi kukutana na kitu kireefu imevaa nguo nyeupe ukatoka mbio balaa kila unapokimbia unakikuta mbele yako , au ushawahi kukutana na ng’ombe wa mguu mmoja akakukimbiza au kitu chochote kisichokua cha kawaida chenye kuhusiana na uchawi au kusikia watu wakihadthia matukio ya namna hiyo. Kuna wale wanaoenda kutafuta pesa za ndagu wanaambiwa saa nane ya usiku nenda sehemu Fulani chochote utakachokiona usikimbie wala usikikwepe, mara anatokea simba anataka kukurukia au inatokea treni iko speed kali inatakiwa usiipishe. Ajabu ni kwamba ukikutana na kitu kirefu cheupe ukikipita mkono wa kushoto (?) kitu hicho hakikudhuru au usipoipisha hio treni haikudhuru…..Ukweli ni kwamba kupita upande wa kushoto wa kitu hicho kirefu hausaidii lolote wewe kushambuliwa na kitu hicho, vitu vyote nilivyoorodhesha hapo vinapokutokea hua sio halisi they are just an illusions. Usipokimbia kitu hicho unakua umedhibiti hofu ndani ya roho yako wachawi wanatumia hofu yako kukuHaunt.
Uoga wa dhidi ya jambo fulani huambatana na kutolijua jambo hilo,ila kama unajua ni ngumu sana kuogopa.Wachawi wote duniani wanapenda kuogopewa they feed up from your fear, unapomuhofu mchawi basi unakua umemuongezea nguvu ya kukuwinda pindi unapoacha kumuogopa tu basi hata kusumbua tena kuna mstari mmoja Jose mtabmbo anaimba kwamba “unaniwangia mimi nimelala, utajijua si wewe ndio unakesha” nachomaanisha ni kwamba unapokutana na kitu kisicho cha kawaida ukawaeza kudhibiti hofu yako ukaacha kukimbia basi kitu kile hakitakudhuru maana utakua hujaonyesha hofu since vitu hivyo tunavyokutana navyo hua sio halisi ni kwamba Mind yetu inakua imelazimishwa kuona vitu hivyo ni halisi ila behind the curtain unakuta ni hakuna kitu hicho au ni mtu wa
Hapa kuna Uchawi na mazingaombwe. Vyote ni uhalisia,yaani vipo.By default wanauwezo wa kutengeneza vitu visivyo halisi kuwa kama halisi yaani Illusions projection au reality manipulation yaanii anaweza kutengeneza kitu kwa kutumia uwezo wake huo ukaona labda ukuta sehemu lakini sio ukuta sio halisi, lakini illusions hizo zinaweza kuwa na maadhara kwenye maisha halisi ya mwanadamu mfano mtu kaonyesha barabarani pale hakuna gari kumbe kuna gari wewe ukavuka likakukupitia. Kuna wakati mtu anaweza kua kafariki lakini mtu huyo hajafa kiuhalisia kama tunavyoona bali kachukuliwa kimazingira na kuhamishwa dimension nyingine, pale msibani sisi tunabaki tunaona mtu ndio tumemzika kumbe tumezika kipande cha mgomba au chochote kile
Hili jambo unatakiwa ulifanyie utafiti zaidi,hasa ujue wapi ni sehemu sahihi ya kuchukua marejeo.Soul imegawanyika katika sehemu tatu ambazo ni Mind,Impression na Intellect..Mind imegawanyika katika pande tatu ambazo ni Conscious mind, Unconscious mind na Subconscious Mind. Conscious mind ni sehemu ya Mind ambayo inahusika na kushughulikia yale mambo yote ambayo tunayafahamu either kwa kuona,kusikia au kuhisia, kiufupi Conscious mind inashughulikia yale ambayo yapo katika utambuzi/ufahamu wetu. Ndio maana wewe mwanadamu wa kawaida huwezi kuwaza nje ya vile vitu unavyofahamu kama unabisha jaribu kuwaza kitu ambacho hakipo au hakina ufanano na kitu ulichowahi kuona au kusikia… Conscious mind inajihusisha na memories,perception,feeling, sensation na fantasies zilizomo ndani ya utambuzi wetu, Conscious mind hua inashirikiana na Subconcious mind hivyo basi hua zinataka kufanana maana au ufanyaji wa kazi so chunga zisikuchanganye.
Kwa kuzingatia mfano wako wa Computer hivyo ulivyo vitaja sehemu zake kwenye Computer zinafahamika,swali langu ni Conscious na Subconsciuos Mind katika mwili wa mwanadamu ziko wapi ?imeweewa alogarithim iitwayo FIFO (First In First Out) ambapo data zile zinazoingia kwenye Data Buffer zitaanza kuchakatwa kisha zitatolewa nje kisha ndio zije nyingine.
NB: Data Buffer unaweza kuiita kwa lugha rahis Random Acess Memory (RAM)
kwenye mada yangu moja iliyopita nileeleza kwamba Subconcious mind ndio sehemu ya utanzaji wa kumbuku za kila kitu unachoona na kukifanya maishani mwako nikaifananisha na Data Cache and Cockies … Sasa basi kwenye Conscious mind kunafanya kazi kama kwenye Computer, kwakua ndio sehemu inayohusika na kuwaza/kufikiri yenyewe hua haitunzi kumbukumbu ya kile inachokifanyia kazi na yenyewe ina tumia huo mfumo wa FIFO wazo litakaloanza kuingia ndio hilo litakalofanyiwa kazi taarifa ya wazo hilo itapelekwa kwenye Subconscious mind kuhifadhiwa lakini pia Conscious mind inauwezo wa kuchakata data moja tu kwa wakati mmoja tu.Conscious mind inachukua taarifa mbalimbali kwa kutumia kuona,kusikia, kunusa,kuhisi,kugusa au kuonja. Conscious mind inakusanya na kuchambua kila kinachoendelea kwenye mazingira yako na kukichambua kwa njia hiyo ya FIFO kama kuna kitu inataka kukiwaza ila kilishawahi fanyiwa kazi basi Conscious mind itaResquest kwenye sotorage centre kitu hicho yaani kwa Subconcious mind
Ndio vipo vyoteHapa kuna Uchawi na mazingaombwe. Vyote ni uhalisia,yaani vipo.
Akili/mind ipo ndani ya Roho/soulHili jambo unatakiwa ulifanyie utafiti zaidi,hasa ujue wapi ni sehemu sahihi ya kuchukua marejeo.
Soul bila shaka ni Roho, hii roho ni nini hasa ,na Mind bila shaka ni Akili. Unaweza kuniambia Mind katika mwili wa mwanadamu iko wapi ?
Kiufupi ni kwamba Soul imebaba mind na mind ina hizo conscious na subconscious mind ndani mwake. Roho ipo ndani ya ubongo (Brain)Kwa kuzingatia mfano wako wa Computer hivyo ulivyo vitaja sehemu zake kwenye Computer zinafahamika,swali langu ni Conscious na Subconsciuos Mind katika mwili wa mwanadamu ziko wapi ?
Hili umelijuaje ?Akili/mind ipo ndani ya Roho/
Swali langu limemili katika sehemu mahususi ya Roho,unapo sema Roho imebeba akili,nitakuuliza vipi kwa mtoto ambaye yuko tumboni na ni hai,vipi kwa mtoto mchanga na vipi kwa chizi ? Maana yake kilicho hai kina Roho,yaani kina akili. Vipi kuhusu mimea ?Kiufupi ni kwamba Soul imebaba mind na mind ina hizo conscious na subconscious mind ndani mwake. Roho ipo ndani ya ubongo (Brain)
Mind ni software part ambayo huwezi kuiona ila utaona matendo yake.
Natumaini unachanganya kati ya roho na nafsi.. nafsi ndio hukaa moyoniHili umelijuaje ?
Roho ni nini ? Yaani naomba unipe maana ambayo inazuia yote yasiyo husu Roho kuingia na inaruhusu yote yanayo husu Roho kuingia.
Hapa ndipo songombingo huanza.
Mimi navyo fahamu ni kuwa akili mahala pake ni moyoni,na hufanya kazi sambamba na Ubongo.
Je wewe binafsi unafahamu nini kuhusu Roho na akili?Swali langu limemili katika sehemu mahususi ya Roho,unapo sema Roho imebeba akili,nitakuuliza vipi kwa mtoto ambaye yuko tumboni na ni hai,vipi kwa mtoto mchanga na vipi kwa chizi ? Maana yake kilicho hai kina Roho,yaani kina akili. Vipi kuhusu mimea ?
Unaposema Roho ipo ndani ya Brain hii si kweli.
Mfano wa Roho katika mwili wa mwanadamu ni kama mfano wa Mafuta katika gari.
Hapa sijachanganya,sababu tamko Nafsi,nalifahamu vizuri sana tena kutokeakatika lugha yake ya asili. Nafsi ni wewe, yaani ili uipate nafsi ni uchukue Roho ujumlishe na Mwili. Yaani Roho na Mwili unapata nafsi. Na hilo tamko Nafsi kuna wakati humaanisha Roho.Natumaini unachanganya kati ya roho na nafsi.. nafsi ndio hukaa moyoni
Naam nakubaliana na weweHapa sijachanganya,sababu tamko Nafsi,nalifahamu vizuri sana tena kutokeakatika lugha yake ya asili. Nafsi ni wewe, yaani ili uipate nafsi ni uchukue Roho ujumlishe na Mwili. Yaani Roho na Mwili unapata nafsi. Na hilo tamko Nafsi kuna wakati humaanisha Roho.
🙏Kwenye Qur'aan tunapewa majibu kuhusu Roho,mtume wetu watu wake walikuwa wana muuliza sana kuhusu Roho,na majibu ni kuwa kuhusu Roho nimepewa elimu ndogo sana.
Anasema Allah mtukufu :
85. Na wanakuuliza khabari za Roho. Sema: Roho ni katika mambo ya Mola wangu Mlezi. Nanyi hamkupewa katika ilimu ila kidogo tu. (Israa : 85)
Ndio maana nimeeleza sehemu kwamba Dark power na Light power zote zinaweza kukupatia ufahamu sasa ni mtu mwenyewe kutambua ufahamu alionao unatoka katika nguvu gani.Hizi ni elimu pweke unatakiwa ujue wapi unapata elimu kuhusu vitu hivi hasa nafsi,roho na akili,watu wengi sana hawana elimu sahihi kuhusu vitu hivi.
Umeuliza swali zuri sana. Niliwahi kuandika mada maalumu kuhusu ROHO. Nikaipa anuani hii "Ukweli kuhus Roho na yote yanayo ihusu".Je wewe binafsi unafahamu nini kuhusu Roho na akili?
Kwa maana rahisi Dark Power ni nini ?Ndio maana nimeeleza sehemu kwamba Dark power na Light power zote zinaweza kukupatia ufahamu sasa ni mtu mwenyewe kutambua ufahamu alionao unatoka katika nguvu gani.
Ni Mungu anifunuliaye yale nisiyoyafahamu maana anasema Ukimpokea yeye basi atakuonyesha mengi makuu usiyoyajua
Mara nyingi natumia neno hilo kumaanisha Shetani/IbirisiKwa maana rahisi Dark Power ni nini ?
Sahihi kabisa na hatuwezi kuyajua yoteLakini ukweli unabaki pale pale hatujui mengi kuhusu Roho ila machache ambayo ametufunulia Mola muumba.
Upo sahihi. Lakini hakuna mwanadamu aliyefanya kitu kwa asilimia 💯 yaani ukamilifu. Naamini bandiko langu linamapungufu kibao ila pia lina usahihi kiasi fulani. So kazi ni kwa msomaji kuangalia madhaifu tu au mazuri piaSasa wewe unakosea katika jambo hili sababu unatumia akili yako na maelezo ya wakubwa wako katika uliyo yasoma kuhusu vitu hivi. Huwezi kupatia hata siki moja,sababu uwezo wa akili zetu zina ukomo.
Tuko pamoja.
Naanzia hapa. Umesema kweli kabisa. Kutokana na udhaifu wa akili yetu na baadhi ya mambo kutoweza kuyadiriki katika uhalisia wake. Mola wetu akawa anatimiliza mitume na manabii (Siyo hawa feki ambao tunaishi nao ) kwa ajili ya kujibu maswali kwa yale yaliyo fichikana,kama vile baada ya kufa hufata nini,au roho ni nini,akili ni nini au nini lengo la kuwepo duniani, chanzo cha uhai ni nini (swali hili liliwasumbua sana Wanafalsafa wa Magharibi ikatokea kila mmoja akaelezea kwa mtazamo wake).Upo sahihi. Lakini hakuna mwanadamu aliyefanya kitu kwa asilimia 💯 yaani ukamilifu. Naamini bandiko langu linamapungufu kibao ila pia lina usahihi kiasi fulani. So kazi ni kwa msomaji kuangalia madhaifu tu au mazuri pia
Je kwanini asitimilize kwa watu wa sasa wenye kumtafuta - kutafuta hekima yake?Naanzia hapa. Umesema kweli kabisa. Kutokana na udhaifu wa akili yetu na baadhi ya mambo kutoweza kuyadiriki katika uhalisia wake. Mola wetu akawa anatimiliza mitume na manabii (Siyo hawa feki ambao tunaishi nao ) kwa ajili ya kujibu maswali kwa yale yaliyo fichikana,kama vile baada ya kufa hufata nini,au roho ni nini,akili ni nini au nini lengo la kuwepo duniani, chanzo cha uhai ni nini (swali hili liliwasumbua sana Wanafalsafa wa Magharibi ikatokea kila mmoja akaelezea kwa mtazamo wake).
Alishatimiliza tayari,kilicho baki ni kufata na kutafakari. Yaani alicho kitoa kina kidhi haja.Je kwanini asitimilize kwa watu wa sasa wenye kumtafuta - kutafuta hekima yake?