Miongo miwili wamekataa kubadilisha jina la mtaa wa Tandamti kuwa Mshume Kiyate

Miongo miwili wamekataa kubadilisha jina la mtaa wa Tandamti kuwa Mshume Kiyate

alikua nae uzuri huyu mzee yupo na mimi nimekisoma hiki kitabu kizuri sana
Sijakisoma na sijaona hata mmoja humu aki "quote" hayo maneno yake. Mnahadithia hadithi ya vichwani mwenu.

Si muweke alichoandika la sivyo itabaki kuwa ni porojo tu.
 
Mama hiyo ni mtu aliomba akatumia kuomba msaada wa mawazo Mimi ni Mwanaume Sio mwanamke
Ukiwa muongo uwe na kumbukumbu, uliulizwa kitu kwenye ule uzi...
kitali

Ndoa yako ina muda gani? alianza pombe baada ama kabla ya ndoa?

Majibu yako yakawa...
ndoa yangu ina miez tisa na alikuwa anakunywa pombe ila alinificha ficha sasa anakunya mbele yang.istoshe mie ni mjamzito nina mimba ya miez sita.

Bado unajikana?
 
Mzee Said Shikamoo!
Sina cha kuchangua zaidi ya kuvuta kumbukumbu alizonisimulia al marhum babu yangu Kassim Liyogope aliyewahi kuwa mwenyekiti wa wa wazee mkoa wa Darul salaam !mengi alinieleza nikiwa mdogo kuweza kuzingatia sasa napata picha pana kupitia maandishi yako! Ahsante sana


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mnabudehe,
Marahaba.

Nimejitahidi kuandika takriban historia ya wazalendo wengi walijitolea
katika TANU na kupigania uhuru.

Ukisoma kitabu cha Abdul Sykes utakutananao.

Nikufahamishe kuwa Abdul Sykes hakuwa mzee alifariki akiwana na umri
wa miaka 44.

Nimuhoji Nyerere kuhusu Abdul Sykes ili nipate kitu gani kwake?

Mimi sikuhitaji Nyerere kupata habari za Abdul Sykes kwani watu wengi
Dar es Salaam wakiijua historia ya Abdul Sykes na Nyerere mmojawapo
ni baba yangu.

Historia ya Abdul na Nyerere 1952 hadi kuunda TANU 1954 ilikuwa ni kitu
mashuhuri na kinafahamika na nyaraka za wakti ule nilikuwa nimezipata.

Historia iliyonitoa jasho ilikuwa ya Abdul alipokuwa vitani Burma (1942 - 1945)
kisha aliporudi Tanganyika 1947 na kuwa katika harakati za kuingia katika uongozi
wa TAA wakati baba yake yu hai na chama kipo katika uongozi wa baba yake
mkubwa Mwalimu Thomas Plantan kama president wa TAA na Clement
Mtamila
akiwa katibu hawa wote wakisubiana sana na baba yake.

CIMG2281.JPG


Abdulwahid Sykes King's African Rifles (KAR) Burma Infantry
6th Battalion 1942 Second World War 1938 - 1945


Hiki ndicho kipindi Abdul aliongoza Dar es Salaam Dockworkers Union na migomo
iliyowatikisa sana Waingereza.

Kipindi hiki 1942 - 1947 ndicho kilikuwa, ''formative years,'' za Abdul na ndicho
kipindi kilichomsukuma kuingia katika uongozi wa TAA 1950.

Hiki kwangu mimi ndicho kipindi kilichokuwa kigumu sana katika utafiti kwani
nilitaka nikutane na watu ambao alikuwanao katika kuigeuza TAA kuwa chama
cha siasa.

Unaweza kusoma historia hii ya Abdul hapo chini bahati mbaya iko kwa Kiingereza:
Mohamed Said: The Book: Excerpts...Abdulwahid Sykes and Dar es Salaam Dockworkers’ Union, 1948 Part One

Sasa watu waliokuwa karibu na Abdul katika kipindi kile ni mdogo wake Ally, Dossa,
Tewa Said Tewa
na Islam Barakat aliyekuwa Labour Inspector.

Kwa hakika katika historia ya TANU kama Nyerere angekuwa na cha kunieleza ningekuwa
tayari nakijua.

Nashukuru kwa Majibu hayo ambayo yanazidi kunipa Maswali zaidi!
Katika kitabu chako cha Maisha ya Bwana Sykes pamoja na Interview Uliyoifanya na Bwana Gunze wa Radio Butiama,ni dhahili kabisa Unamlaumu Nyerere ambaye alikuwa kiongozi wa nchi kutomkumbuka wala kumuenzi Mzee wako wala Mchango wao!Kwanini iwapo ulikuwa na hoja nzuri na unataka kuandika kitabu kisicho na mlalio wa upande mmoja hukufanya Interview na Nyerere? Ulifanya interview na watu wengi mpaka Kenya!
Unamchukia Nyerere?
Kuhusu Kiingereza lisikupe shida wakati mwingine! labda kama andiko lipo kwa lugha ya Kiarabu au lugha zingine mbali na Kiingereza.
Asante.
 
Ukiwa muongo uwe na kumbukumbu, uliulizwa kitu kwenye ule uzi...


Majibu yako yakawa...


Bado unajikana?
Cwez kubishana na wewe Mimi kwa kaz ninazofanya mwanamke hatii pua. So ckulazimish uamin
 
Cwez kubishana na wewe Mimi kwa kaz ninazofanya mwanamke hatii pua. So ckulazimish uamin
Huwezi kubishana kwa kuwa u muongo.

Unataka nikuwekee ulivyobambwa kwa uongo wako kwenye uzi mwengine?

Nakushauri tu, Mohamed Said kishakwambia amekuelewa ungekuwa unaufahamu japo kidogo ungeelewa kuwa anakwambia nini.

Sasa hapa hatutaki utumbo kama huo uliouzoea, niliokuwekea. Hapa ukisema vita ya maji maji ulikuwa ya "kikabila" uje na kitu tukuelewe si utumbo halafu hata jemedari wa hiyo vita humuelewi.

Peleka ujinga wako kwa wajinga wenzio. Ndicho ulichoambiwa, kama huelewi.
 
Sijakisoma na sijaona hata mmoja humu aki "quote" hayo maneno yake. Mnahadithia hadithi ya vichwani mwenu.

Si muweke alichoandika la sivyo itabaki kuwa ni porojo tu.
ha ha ha ha ha aisee we mzee ni MNAZI kweli kweli
 
Ukiwa muongo uwe na kumbukumbu, uliulizwa kitu kwenye ule uzi...


Majibu yako yakawa...


Bado unajikana?
Teh teh teh

Alikuwa hajui kama JF kuna hansards kila anachokiandika members kinabaki kama kumbukumbu.

Angemuuliza Yericko Nyerere naye tulivyoweka uongo wake hadharani.

JF kuna vituko sana.
 
Huwezi kubishana kwa kuwa u muongo.

Unataka nikuwekee ulivyobambwa kwa uongo wako kwenye uzi mwengine?

Nakushauri tu, Mohamed Said kishakwambia amekuelewa ungekuwa unaufahamu japo kidogo ungeelewa kuwa anakwambia nini.

Sasa hapa hatutaki utumbo kama huo uliouzoea, niliokuwekea. Hapa ukisema vita ya maji maji ulikuwa ya "kikabila" uje na kitu tukuelewe si utumbo halafu hata jemedari wa hiyo vita humuelewi.

Peleka ujinga wako kwa wajinga wenzio. Ndicho ulichoambiwa, kama huelewi.
JF siyo sehemu ya porojo kuna watu makini wanasoma hapa sasa huyu jamaa anaokota maneno kwenye vijiwe vya mapuya analeta JF.
 
Kitwana Kondo alibadilisha jina la Hill Road, Oysterbay, alikokuwa akikaa. Akauita mtaa Yasser Arafat Road. Jirani zake hawakufurahia.

Mpaka leo mtaa unaitwa Hill Rd.

Sent from my Kimulimuli
 
Kuna tafiti zozote zinazosimulia alikuwa kwa nani kiuhalisia, hizo siku tatu alizo "potea"?

Hapa nahisi kuna historia nzuri.
Taarifa nyingi zinadai alikuwa Kigamboni,kwani Waasi wa kambi ya Jeshi "colito" sasa "Lugalo " waliizingira Ikulu na wao wakitaka Oscar Kambona achukue nchi,yasemekana yeye hakuwakatalia Waasi bt aliwageuka kwa kuwasiliana na Waingereza na Wanaigeria ambapo wakafanikiwa kuja kuyazima na kuwakamata Wanajeshi waasi na Mwl kurudi hadharani..

Shida ilikuwa jeshi lile lilirithiwa kwa Mwingereza (K.A.R ) na ikawa chanzo cha kuanzishwa jeshi jipya JWTZ.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Taarifa nyingi zinadai alikuwa Kigamboni,kwani Waasi wa kambi ya Jeshi "colito" sasa "Lugalo " waliizingira Ikulu na wao wakitaka Oscar Kambona achukue nchi,yasemekana yeye hakuwakatalia Waasi bt aliwageuka kwa kuwasiliana na Waingereza na Wanaigeria ambapo wakafanikiwa kuja kuyazima na kuwakamata Wanajeshi waasi na Mwl kurudi hadharani..

Shida ilikuwa jeshi lile lilirithiwa kwa Mwingereza (K.A.R ) na ikawa chanzo cha kuanzishwa jeshi jipya JWTZ.



Sent using Jamii Forums mobile app
Alikuwa Kigamboni kwa nani kwa siku zote tatu?
 
Kuna ulazima sana wa kuita jina lake,nini madhara ya kutoita.maana tuna mambo mengi sana ambayo ni prioprities.
 
Kitwana Kondo alibadilisha jina la Hill Road, Oysterbay, alikokuwa akikaa. Akauita mtaa Yasser Arafat Road. Jirani zake hawakufurahia.

Mpaka leo mtaa unaitwa Hill Rd.

Sent from my Kimulimuli
Al Watan,
Yassir Arafat Road
upo Oyster Bay na mimi nimeuona kwa jicho langu
ila sina uhakika kama ni ule Hill Road.
 
Al Watan,
Yassir Arafat Road
upo Oyster Bay na mimi nimeuona kwa jicho langu
ila sina uhakika kama ni ule Hill Road.
Yassir Arafat ndio ulikuwa ukiitwa Hill Road. Umetoka huku Msasani Rd huku kwa Apson Mwang'onda halafu ukapanda kilima mbele kidogo (nafikiri ndiyo asili ya jina la Hill Rd), ukaenda mpaka Kenyatta Drive karibu na beach.

Kama ulifika Oysterbay kwa Mzee wetu Marehemu Kitwana Kondo huu ndio ulikuwa mtaa wake pale.

Google Map bado upo kama Hill Rd

Ona hapa
 
Back
Top Bottom