Miongo miwili wamekataa kubadilisha jina la mtaa wa Tandamti kuwa Mshume Kiyate

Mnabuduhe,
Sina sababu ya kumchukia mtu yoyote kwani kufanya hivyo ni mtu
kujitishwa zigo zito kichwani ukawa linakuhangaisha siku zote.

Laiti ungekuwa umekisoma kitabu cha Abdul Sykes wala usingekuja
na maswali haya kwani nimeeleza historia nzima ya uandishi wa historia
ya TANU kuanzia African Association 1929.

Anaeleza Dossa Aziz niko nyumbani kwake Mlandizi pamoja na Ally Sykes
na mama mmoja wa Mmarekani Mweusi mwandishi wa Washington Post,
Dossa Aziz anaeleza kuwa mara tu baada ya uhuru siku moja yuko yeye,
Baba wa Taifa, Abdul Sykes na Mwalimu Kihere katika mazungumzo
ya kawaida tu ikazuka fikra ya kuandika historia ya TANU na ya uhuru.


Mwalimu Kihere

Baba wa Taifa akasema kati ya wanaoijua vyema African Association na TANU
ni Abdul kwa hiyo kazi ile akapewa Abdul na Baba wa Taifa akampeleka Dr.
Wilbard Klerruu Makao Makuu ya TANU amsaidie Abdul katika utafiti na
kuandika historia ile ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Dr. Klerruu ndiyo kwanza alikuwa amerudi masomoni Marekani.

Mpashaji wangu habari ananiambia Abdul alirudi Makao Makuu ya TANU
Lumumba na akaingia ofisi ile ile ambayo alikuwa anaitumia wakati wa
harakati za kudai uhuru, ofisi ambayo baadae alimwachia Nyerere, 1953.

Mpashaji wangu ananiambia alikuwa akitoka shule anapita pale Lumumba
kumwamkia Abdul Sykes si kwa heshima ya kuamkia ila kwa kuwa Abdul
alikuwa hawaagani hivi hivi alikuwa atamtupia vijisenti kidogo.

Baba wa Taifa alikuwa akipelekewa kila sura ikikamilika kuisoma.

Hapa ndipo ilipoanza tatizo la historia ya TANU hadi kutufikia sisi sasa zaidi
ya miaka 50.

Abdul alianza historia ya TANU na historia ya baba yake Kleist alipounda
African Association 1929.

Mnabuduhe,
Hapa ndipo lilipozuka tatizo hili ambalo hadi sasa bado linakuhangaisha
wewe na watu wengi kufikia kunighadhibikia mimi na kunitukana kwa nini
nimeandika historia nyijngine ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Mradi huu ulipoingiwa na tatizo hili Abdul akajitoa na akachukua nyaraka
zake na akamwacha Dr. Klerruu aendelee na utafiti na kuandika.

Kazi hii haikuchapwa kitabu na TANU kwa miaka mingi ilikuwa katika maktaba
ya TANU hadi, ''ilipoibiwa,'' na ''mwizi,'' akabadilisha hapa na pale akachapa kitabu.

Kitabu hiki ni sawasawa na kitabu cha Kivukoni, ''Historia ya TANU,'' (1981).

Ningeweza kuendelea kueleza kwani yako mengi lakini naamini kwa haya
niliyoweka hapa tatizo nimeliweka wazi na naamini nimeeleweka.
 
Al-Watan,
Ahsante sana kaka.

Kwa Mzee Kondo nilikuwa kila Mfungo wa Ramadhani ananialika mie na rafiki zangu wawili
tunafuru na yeye, ''just the four of us.''



Mimi ni mwandishi wa mwisho kuzungumza na Mzee Kondo baada ya hapa
akafunga kauli.

Hii ilikuwa 2012.

Hii ndiyo siku Mzee Kondo alinisomea jalada la ''mole,'' ndani ya uongozi wa
juu wa TANU kuanzia 1954.
 

Shukurani kwa picha na kumbukumbu.

Basi yumkini itakuwa uliliona bango la huo mtaa hapo.

Mimi nilikuwa nikienda kule Upanga (Mtitu St?, mtaa wa kwa marehemu Dr. Maro na marehemu balozi Diria halafu kwa nyuma yake pale kwa nyuma pale) kabla hajahama, rafiki zangu wa Tambaza walikuwa haweshi kwenda kwake maana walikuwa na urafiki na watoto wa pale kwake.

Alivyokuja kwenda Oysterbay nikawa nishaondoka Tanzania.
 
Kitulo,
Kuna mambo nyuma yake.

Labda niseme jambo.

Vipi watu hawa wampe mtaa Yusuf Makamba Gerezani wamuache Dossa Aziz na Abdul Sykes?

Kuna mtu aliwaamrisha kufanya hivyo au walipitiwa?



Sent using Jamii Forums mobile app
Kumbukumbu yangu ule MTAA WA YUSUF MAKAMBA kabla yake palisheheni Gereji na ulikuwa Hovyo,ni Mzee Y.R.Makamba alifanya jitihada za kuwaondoa MAFUNDI wote na pia Uwanja wa Kidongo Chekundu na kuwapeleka TABATA DAMPO na kufanikisha kuwekwa Lami mitaa ile.Manispaa ilishakuwa imewashindwa.

Ndipo ikaja kupewa jina la MAKAMBA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Al-Watan,
Ahsante sana kaka.
Ni Mtitu Street.

Mimi nimeishi Masaki ndiyo hiyo Oyster Bay toka 1979.
 
Ligema,
Hilo tu ndiyo kapewa mtaa ilhali Yusuf Makamba alikuwa akifanyakazi
anayolipwa mshahara.

Tusemeje sasa kwa Dossa Aziz aliyetoa mali yake kupigania uhuru
wa Tanganyika na akiishi mitaa hiyo toka udogo wake?

Unadhani nani alistahili zaidi heshima hiyo?
 
Al-Watan,
Ahsante sana kaka.
Ni Mtitu Street.

Mimi nimeishi Masaki ndiyo hiyo Oyster Bay toka 1979.
Sasa yule mole mbona hututajii Ulamaa?

Au unatakakuleta habari kama za Seif Sharif Hamad kusema maneno aliyoambiwa na Nyerere hayasemi?
 
Sasa yule mole mbona hututajii Ulamaa?

Au unatakakuleta habari kama za Seif Sharif Hamad kusema maneno aliyoambiwa na Nyerere hayasemi?
Al-Watan,
Kaka mbona nishamtaja?
Huyu hapo chini:
Mohamed Said: KISA CHA ALI MWINYI TAMBWE NA KITWANA SELEMANI KONDO 1950s

Mohamed Said June 09, 2017 0

KISA CHA ALI MWINYI TAMBWE NA KITWANA SELEMANI KONDO 1950s
Mohamed Said June 09, 2017 0


Ali Mwinyi Tambwe na Karume


Kushoto: Dr. Harith Ghassany na Mohamed Omari Mkwawa Tanga 2009


Mohamed Omari Mkwawa akionyesha kitabu cha Dr. Harith Ghassany,

''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,''


Dr. Harith Ghassany akiwa Kipumbwi

Chief David Kidaha Makwaia
 
Unafahamu njia ya kutoka Dar mpaka Rufiji ilivyokuwa katika '50s?

Kwa kukujuza tu, mpaka leo hii njia hiyo huzuka Simba si mchezo, sasa fikiri 50s ilikuwaje?

Halafu fikiri tena mtu anatoka na baiskeli kwenda kuhamasisha wanachama wajiunge na chama ili namba itimie.

Kwa punguani hayo si mapigano kwani punguani hufikiria kupigania maana yake risasi, mabomu, ngumi na mambo kama hayo.

Tumia kichwa chako kufikiri japo kiduchu na si kukiwacha kuwa mzigo tu juu ya mabega yako.
 
Izi ndo historia za kupandisha uzalendo wetu lakin mashulen tunasoma binadam alitokana na sokwe,binadam wa kale aliishi mapangon wengine wanasema binadamu wa kale alikuwa anakula mizizi basi tabu tuuu,ndo apo uzalendo unakuwa 0%

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mnabuduhe,
Uliniuliza swali na mimi nikakupa jibu.

Mbona umekuwa kimya.
Ningependa sana nikusikie.
 
Tatizo lenu udini na chokochoko mmeweka mbele. Acheni huo udini then historia itakuwa na maana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Eti shujaa? Unajua maana ya shujaa? Chokochoko tu zimekujaa. Mshume Kiyate shujaa wa nini zaidi ya kuwa mdai uhuru kama watu wengine Tanganyika?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo lenu udini na chokochoko mmeweka mbele. Acheni huo udini then historia itakuwa na maana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mberoya,
Umefanya kujumuisha unasema, ''tatizo lenu,'' ilahali hapa aliyeandika
hayo ni mimi mtu mmoja.

Umesema, ''udini,'' huo ''udini,'' uko wapi katika kuomba kibao cha mtaa?

Historia ishakuwa na maana kama unavyosoma nimeweza kuandika upya
na kuweka masahihisho katika historia iliyokosewa.
 
Eti shujaa? Unajua maana ya shujaa? Chokochoko tu zimekujaa. Mshume Kiyate shujaa wa nini zaidi ya kuwa mdai uhuru kama watu wengine Tanganyika?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mberoya,
Mshume Kiyate
kwangu mimi ni shujaa na ikiwa wewe unaona hana
sifa hiyo sawa hakuna neno.

Unaweza kunionesha oicha nyingene yoyote ya mtu ambae amekuwa
karibu na Baba wa Taifa kwa kiasi hiki?

Angalia picha hizo hapo chini:





Ikiwa wewe humjui Mzee Mshume Kiyate ni nani basi tuulize tukufahamishe.
Kuuliza si ujinga.
Mohamed Said: KITENDAWILI KATIKA KUTUNUKU MAJINA YA MITAA YA DAR ES SALAAM KWA WAPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…