Wasalaam,
Ukifanya kauchunguzi kadogo kwa familia nyingi zenye uchumi imara (achana na accidental millionaires), utagundua kuwa ni mipira ya mbali iliyopigwa au kuchezwa na watangulizi wa familia hizo. Mipira ya mbali huchezwa na wajasiriamali wachache sana hapa duniani.
Kwetu hapa ni wachache mno wanaocheza mipira ya mbali, ndo maana utasikia mzee aliondoka na mali zake.
Ugumu wa mipira ya mbali uko hapa, sio rahisi kwa kapuku kuwekeza ili aje apate mavuno makubwa baada ya miaka kumi na kuendelea, kwanza anafikiria ataishije mpaka kufikia hiyo siku.
Pili, yasiyo julikana hapa kati kati ni mengi mno. Kwa hiyo lazima mmoja ktk familia ageuke daraja ili wengine wavuke, je unaweza kuwa daraja la wenzako ili wajukuu watoboe?? Kama huwezi basi cheza mipira ya pasi fupi fupi tu.
Kama unafikiria kucheza mipira ya mirefu au mbali lazima ujipange vizuri kichwani zaidi ili usije ukahamishwa kwenye reli, ufanye utafiti wa kutosha juu ya investment yako katika kona zote usije angukia pua baada ya mabadiliko ya tabia nchi, au sera au technology kukupitia.
Ukifanya kauchunguzi kadogo kwa familia nyingi zenye uchumi imara (achana na accidental millionaires), utagundua kuwa ni mipira ya mbali iliyopigwa au kuchezwa na watangulizi wa familia hizo. Mipira ya mbali huchezwa na wajasiriamali wachache sana hapa duniani.
Kwetu hapa ni wachache mno wanaocheza mipira ya mbali, ndo maana utasikia mzee aliondoka na mali zake.
Ugumu wa mipira ya mbali uko hapa, sio rahisi kwa kapuku kuwekeza ili aje apate mavuno makubwa baada ya miaka kumi na kuendelea, kwanza anafikiria ataishije mpaka kufikia hiyo siku.
Pili, yasiyo julikana hapa kati kati ni mengi mno. Kwa hiyo lazima mmoja ktk familia ageuke daraja ili wengine wavuke, je unaweza kuwa daraja la wenzako ili wajukuu watoboe?? Kama huwezi basi cheza mipira ya pasi fupi fupi tu.
Kama unafikiria kucheza mipira ya mirefu au mbali lazima ujipange vizuri kichwani zaidi ili usije ukahamishwa kwenye reli, ufanye utafiti wa kutosha juu ya investment yako katika kona zote usije angukia pua baada ya mabadiliko ya tabia nchi, au sera au technology kukupitia.