Mirathi ya Kobe Bryant yazua gumzo USA, utajiri wote wagawanywa kwa mke na watoto huku wazazi wakiishi kimaskini

Katika uislamu kuwatunza wazazi ni lazima na sio ombi kutokufanya hivyo ni dhambi kubwa itakayokufanya uingie jahanam.......

Mwenyezi haikubali ibada ya mtu asiyewatendea wema wazazi wake............
kwani hapa habari inahusu kuwatunza wazazi au kukosa fungu la mirathi
mjitahidi kujikita kwenye mada
 
Kuna wazazi hawafai uwape hata 10 jueni tu hivyo
 
You nailed it. Kama wazazi waliishi vyema na mkwe wao hawawezi kosa dola, yaani hata wajukuu wasikuangalie, basi kuna mahali unakosea
 
Sio principle, ni wajibu wa watoto kuwatunza Wazazi wao. Hivi mkuu, Mzee wako akiumwa, wewe hutamuuguza!?
Wajibu kwa sheria gani? Kwa kanuni gani?

Hapa tunaongelea kumtunza mtu kwa pesa, urithi, si mtu kuumwa.

Na hata kuumwa kuna professionals wamesomea hiyo kazi ya kutunza wagonjwa, mimi sina utaalamu huo, naweza kujiweka kimbelembele kumtunza mtu anayeumwa, nikamuwahisha kufariki.

Mimi kazi yangu itakuwa kumtembelea na kusimamia mambo ya msingi tu.

Acheni ujima.

There is such a thing as division of labor, do you know that?
 
Family is Family. Na wazazi ndio mwanzo wa cheni ya familia. Yaani watoto wanauana kwa ajili ya Mali za wazazi wao, lakini wazazi waishi au wafe homeless au bila huduma muhimu za maisha wakati watoto wao wana mabilioni! Sioni logic hata kidogo.

Mwenyezimungu kakujaalia mapesa, unaanzisha NGo na unachangia mapesa kibao kuwasaidia watu baki wenye mahitaji mbalimbali, ilhali wazazi wako wanaishi maisha ya kifukara, hii ni ajabu sana.

Bora mtu ufe fukara.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…