Mirathi ya Kobe Bryant yazua gumzo USA, utajiri wote wagawanywa kwa mke na watoto huku wazazi wakiishi kimaskini

Wabongo na watu wenye fikra za kimasikini wengi hawawezi kukuelewa.

Kwa sababu wao wanaona kuzaa ni uwekezaji wa kibiashara, kwamba unazaa mtoto kama kitegauchumi, kama mtumwa.

Nilikuwa naongea na jamaa yangu mmoja Mzanzibari, anawasema Wapemba. Anasema Wapemba wamechangamka sana kwenye biashara nje ya Pemba, lakini, ukienda Pemba, wanalemaa kwa kuzaa watoto wengi halafu wanawatumikisha wale watoto, kila mwezi watoto wanamchangia mzazi, mzazi anaishia kuoa mke wa pili na kuzaa watoto zaidi.

Kwa namna moja au nyingine watu masikini wengi, hususan wabongo, ndivyo wanavyowaona watoto hivyo, kama nguvukazi, kama kitegauchumi, kama mafao ya uzeeni.

Ile akili ya kwamba kila mtu anatakiwa kujiwekea akiba ya kumfaa uzeeni wengi hawana. Wengi wanaona watoto ndiyo akiba ya kuwafaa uzeeni.

Hii ni biashara ya utumwa kwa namna nyingine tu.
 
Kobe mwenyewe amekufa kwa ajali ya ndege, bado kijana mdogo sasa huo wosia ungetokea wapi?

Labda kama ingekuwa amefikia 50 hivi ndiyo angeanza kuwazia vya wosia.
 
Lakini watoto wa njee wa mwanamke amna kurithi mali ya Mme ambae sio baba yao[emoji854][emoji854][emoji854]
Ulaya unakuta anapewa, hata Bongo, mama akikukalia kichwani na rejea za bongo zipo nyingi Tu.
 
David Beckham, Andy Murray wote wamewasaidia mama zao,
 
1. Children don’t owe their parents a good life. Parents are the ones who owe their children a good life. Why? Because it’s the parents who choose to bring kids into the world. You choose to bring a life into this world, you’re responsible for it.

2. Parents are also responsible for preparing for their later years. It’s not the responsibility of their children to take care of them.

3. Watu tunapenda sana kutolea maoni mambo ambayo undani wake hatuyajui.

Vipi kama Kobe aliwasaidia sana wazazi wake kifedha mpaka akachoka? Kuna watu wakiona wakiona kuna chanzo kirahisi cha pesa, wanakuwa tegemezi mpaka wanakera!

4. Familia huwa zina mambo mengi. Changamoto tele. Tunajuaje changamoto zote ambazo hiyo familia ilikuwa nazo zilizopelekea Kobe kutokuwa na uhusiano mzuri na wazazi wake?

Watu wanadhani mtu ukiwa mzazi basi wewe huwezi kukosea chochote kwa mtoto wako! Jambo ambalo si kweli.

5. Wazazi wa Kobe wala siyo wazee kivile. Sioni kwa nini wawe tegemezi kwa mtoto wao mmoja [wana watoto wengine pia]. Hawana kazi? Kama hawana kazi wakatafute kazi wafanye.

6. Kobe alikuwa anawajibika kuwapa maisha bora wanae aliowaleta hapa duniani. Period.
 
US Baba yake Micheal Jackson, aliwasimamia watoto kutoka kuomba choir kanisani Hadi kufika walipo fika, Dolly Parton alianzia kuimba kwenye. Pub, mpaka alipofikia tena anacwbo moja anaomba kuhusu gauni lenye viraka, na enzi hizo walizaliwa wengi. Tumeona Baba yao Venus na Serena Williams akiwasimamia mabinti zake mpaka wakafika hapo.Tiger Woods na wengine wengi, labda Basketball ball hauhitaji nguvu za wazazi kufikia hapo Kobe alipofikia.
Ki nadharia tunaweza kusema Mtoto Hana responsibility Kwa mzazi, lakini kiutu kama Una cha ziada ni vizuri nukawasaidia wazazi wako au hata Ndugu wengine.
Au kama Mzazi alikuwa na Nafasi ya kujiwekea akiba lakini aktumia Uhuru wake vibaya.
 
Matatizo mengi ya wabongo kuelewa hoja hizi, whether wanajua au hawajui, yana mizizi ya kidini.

Washaambiwa mzazi ni sawa na Mungu wa pili hapa duniani kwenye vitabu vya dini. Sasa hapo logic yote uliyosema inavunjwa na hiyo logical fallacy moja tu ya "argument from authority".

Yani Kobe anaweza kuwa na beef na baba yake kwa sababu alimsaidia sana halafu baba yake akaishia kucheza kamari tu na kupoteza pesa, ila wabongo watamlaumu Kobe kama vile walikuwa wanaishi naye
 
Ndiyo, kusaidia wazazi kama una uwezo ni jambo zuri.

Lakini, mnaujua uhusiano aliokuwa nao Kobe na wazazi wake?
 
Mzazi ana wajibu wa kumpigania na kumlea mtoto wake afanikiwe, hao wote baba zao Kobe, Michael, Venus and Serena walifanya sawa.

Ila, uzazi si biashara useme kwamba kwa kuwa baba alimsimamia mtoto mpaka akafanikiwa, basi mtoto ni lazima amtunze baba.

Uzazi ni familia. Kitu ambacho kinaendeshwa bila kutegemea faida.

Baba anatakiwa kujiwekea mipango yake mwenyewe. Tena baba anatakiwa kumuacha mtoto ajiwekee akiba yake ya uzeeni na kuhudumia watoto wake.

Baba hatakiwi kumnyenga mwanawe kwa sababu tu mwanawe kafanikiwa, vipi kama asingefanikiwa? Vipi kama angefariki mdogo sana? Vipi kama mtoto hampendi mzazi na hataki kumsaidia? Hiyo ni haki yake pia.
 
Ndiyo, kusaidia wazazi kama una uwezo ni jambo zuri.

Lakini, mnaujua uhusiano aliokuwa nao Kobe na wazazi wake?
Pia, jambo zuri si lazima liwe jambo la lazima.

Kobe katengeneza utajiri wake, bila kujali uhusiano wake na wazazi wake, Kobe ana haki ya kutumia utajiri wake anavyotaka.

Yani hata kama Kobe hana ugomvi na baba yake, Kobe alikuwa na uhuru wa kusema yeye kifalsafa haamini katika habari za watu kurithishana mali. Watu warithishane vipaji tu na yeye anagawa mali zake nje ya familia. Baba yake alishacheza NBA Philadelphia, San Diego, Houston, Italy, France, alitakiwa kuwa kashajipanga mwenyewe tayari.

Na Kobe angekuwa sawa tu, mali zake ana uhuru wa kupanga nani azirithi.

Kama mnampenda sana baba yake Kobe, tafuteni mali zenu mkampe na nyie.
 
Ndiyo, kusaidia wazazi kama una uwezo ni jambo zuri.

Lakini, mnaujua uhusiano aliokuwa nao Kobe na wazazi wake?
Mimi nina zungumzia dhima ya kawaida ya kibinadamu. Sasa ukienda hatua nyingine ya kwamba Baba au Wazazi hawakumtendea vizuri Mtoto au wanatabia ya kufanya mambo visivyo, Kwa sababu ya kuwepo kwake nao wanafanya matumizi visivyo kisa yupo Kobe au Mtoto wao , basi hapo tutahamia kwenye jambo Hilo au matendo hayo.
 
Hata kwenye dhima ya kawaida ya kibinadamu, inawezekana ubinadamu zaidi ni kumlea mtoto na kumuacha aishi maisha yake kwa uhuru.

Atumie pesa na mali zake anavyotaka, akijisikia kusaidia wazazi sawa, akisikia kugawa mali zake kwa watu baki sawa.

Ukianza kumuwekea mategemeo mtoto kwamba lazima akutunze uzeeni, au kum blackmail kwa kutumia hoja ya "ni ubinadamu" atunze mzazi, kwa sababu wewe mzazi umemtunza utotoni, unaondoka kwenye malezi ya ubinadamu, unaenda kwenye malezi ya biashara, kwamba unawekeza kibiashara kwa mtoto ili yeye aje kukulipa.

1.Malezi ya kifamilia si biashara.

2.Ubinadamu ni pamoja na kumuachia mtoto aishi maisha yake kwa uhuru.

3. Mzazi ana wajibu wa kule mtoto, mtoto hana wajibu wa kulea mzazi.

4. Ukiondoa wajibu wa mtu kulea watoto wake kupata vitu vya msingi maishani, mtu anavyotumia pesa zake alivyozipata mwenyewe ni maamuzi yake.

5. Hoja ya "Ubinadamu" kwenye kuhudumia wazazi inawezekana ikawa ni kukosa ubinadamu wa kumhurumia mtoto. Mtoto tayari ana wajibu wa kuhudumia watoto wake, tusimpe mzigo zaidi wa kuhudumia watoto na wazazi wakati huo huo.
 
Mwenyezimungu amrahisishie huko alipo. Yaani sielewi kwa mapesa aliyokuwa nayo, angewatengea wazazi wake japo kiduchu ili kuwastiri. Labda alidhani, kama tulivyo binadamu, kwamba bado ana umri mdogo kwa hiyo atawasaidia baadae.

Ndio maana ni vizuri kuandika Mirathi haraka iwezekanavyo. Kifo hakina warning letter.
 
Urithi unapaswa kuwa kwaajili ya watoto tu, Kama aliyefariki ni mume basi mke awe msimamizi na kama aliyefariki ni mke basi mume awe msimamizi.

Ukiwaweka wazazi kama warithi inabidi wawe ni wazazi wenye busara sana, wazazi hawawapendi watoto wote katika uwiano sawia, unaweza mpa mzazi kitu kwa moyo mweupe kabisa na yeye akampa mtoto amtakaye, na pengine huyo mtoto pendwa wa mzazi wako naye kuna vitu wewe unampa, in return huyu mtoto pendwa (ndugu yako) anaweza asiwasaidie watoto wako Kwahiyo ni kubet tu.

Hapo ibaki busara ya Vanessa na wajukuu kuwahudumia wazee wa Kobe basi.
 
Katika uislamu kuwatunza wazazi ni lazima na sio ombi kutokufanya hivyo ni dhambi kubwa itakayokufanya uingie jahanam.......

Mwenyezi haikubali ibada ya mtu asiyewatendea wema wazazi wake............
Na huo pia ni utamaduni wetu wa Afrika, na haswa wajibu wa mwanamume yoyote wa kiafrika aliye timamu. Kufanya vinginevyo kwa kweli ni kujitafutia laana tu. Katika amri kumi za Mungu, amri mojawapo ni kuwaheshimu Baba yako na Mama yako, ili siku zako zipate kuwa nyingi na zenye heri hapa duniani
 
Afrika nzima wana utamaduni huo???
 
ya wamarekani tuwaachie wenyewe, wana vitu va ajabu sana hawa watu
 
Basi hapo mwenyewe jitu jeusi unatamani kuwa mwarabu. Hongera ukifa kwenye uislamu utabadilika na kuwa mwarabu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…