Misa ya Mkapa: Nimeona tofauti kubwa kati ya maaskofu wa Katoliki na wale wa makanisa kama la Gwajima!

Kanisa la kweli si kazi ya kumuachia Mungu, lilikuwepo na lipo whether unalipenda au hulipendi ....
 
Makanisa ya binafsi yale ni sadaka tu, ukiwa mtoaji mzuri basi unakaa kiti cha mbele karibu na askofu...
 
Ndugu yangu maisha ya kiroho ni zaidi ya kukemea mapepo.Maisha ya kiroho haimaanishi ni vita na mapambano muda wote.Bali ni safari inayohitaji ustahimilivu na kushikana mkono katika kuiishi imani ya Kristu katika kila nyanja ya maisha yetu hapa duniani ili hatimaye tuufikie wokovu.Pole kwa mafundisho yasiyo sahihi uliyofundishwa.
 
Kama ilo umeligundua leo bc pole, Romani Catholic, wasabatho, Rutheran, na Islamic hizo ni taasisi za za watu kwa ajili ya Mungu. Makanisa ya kirokole karibia yote ni taasisi inayo simamiwa na mtu. Ndo maana unasikia vitu hivi, kanisa la Kakobe, kanisa la Gwanjima, kanisa la Marisa nk. Alafu wanajiita mara manabii mara maasikofu. Kamuulize Gwanjima nani alimsimika uasikofu. Wenyewe vyeo wanajipa tu.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hebu sema panua panua panua ...tanuka sasaaaaa " gwajima"
 
KUOKOKA NI LAZIMA. USIPOOKOKA UTAANGAMIA KWENYE MOTO WA MILELE. SAA YA WOKOVU NI SASA.


Yesu ni Bwana.
 
Ingawa sikuwaona lakini! Lakini wale wa madhehebu ya kiroho huwa hawalembi maneno kwenye misiba.Lazima wapige Neno LA Mungu bila kumng'unya maneno ya kufariji.Kama mtu amekufa bila kutubu dhambi zake kwa Jina la Yesu moja kwa moja ni Jehenamu hakuna cha Eee! Mungu iweke roho ya marehemu mahali pema peponi.Hapana!
 
Kasome biblia uimalize yote ukianza kuhubiri hutohubiri kwa kuwabembeleza watu, utahubiri kwa nguvu zote tena kwa sauti kubwa. usije ukadhani wanapenda kuhubiri vile yule ni Roho mtakatifu akisha jaa unajikuta unahubiri kwa nguvu.
Ndugu yangu kwanza nikupe pole kwa mafundisho yasiyo sahihi uliyofundishwa.Roho Mtakatifu hahubiriwi kwa kupayuka payuka.Ndiyo maana kanisa linasistiza mafundisho ya msingi katika kumjua roho mtakatifu.Tofautisha hulka za mtu binafsi na roho mtakatifu.roho mtakatifu hutujia na kujidhihirisha kupitia mapaji yake saba.
1. Hekima
Ni kipaji cha Roho Mtakatifu cha kutusaidia tupende na kufurahia mambo ya Mungu.

2. Akili
Ni mwanga wa Roho Mtakatifu wa kutusaidia tumjue zaidi Mungu na ukamilifu wake pamoja na kuelewa ufunuo wake.

3. Shauri
Ni kipaji cha Roho Mtakatifu kinachotuelekeza kuchagua siku zote mambo yenye kufaa zaidi kwa sifa ya Mungu na kwa wokovu wetu.

4. Nguvu
Ni kipaji cha Roho Mtakatifu kinachotutia moyo wa kushika sana amri za Mungu na mambo ya utumishi wake tusiogope watu wala matukano wala mateso wala kufa.

5. Elimu
Ni kipaji cha Roho Mtakatifu kinachotutia maarifa ya mambo ya ulimwengu huu, kwa kutambua mapungufu yake pamoja na mitego, werevu na udanganyifu wa shetani akitujaribu mwenyewe au kwa kupitia vitu kama watu.

6. Ibada
Ni kipaji cha Roho Mtakatifu kinachotufanya tumpende Mungu kama Baba yetu mwema na watu wote kama ndugu; kwa msingi huo kutimiza utumishi wa Mungu na yote yale yenye kumpa Mungu sifa na heshima.

7. Uchaji wa Mungu
Ni kipaji cha Roho Mtakatifu kinachotutia hofu ya kumchukiza Mungu kwa dhambi kama vile mtoto mwema aogopavyo kumtia baba yake uchungu.
 
Acha dhambi acha huo uzinzi acha kujipa moyo, mahubiri ya taratibu kama yale watu hawawezi kuacha dhambi. Na ndio maana ukisoma biblia kuna muda Yesu alikua anakemea anapowaombea watu na anapo wahubiria. Kuna muda alikua anakua mkali.
Huyo ni Yesu yupi? Au yule wa Karemii Congo?

Yesu was so polite, ukali not like Gwajiboy au Mwingira wanaokula wake za watu plus kutembelea chopa huku waumini hawana hata hela ya yebo huku wanaitikia panuaaaaaa......na bado wanasubiria muujiza wa kuwa matajiri!!
 
Ulichelewa sana kuijua tofauti hiyo. Hawa wanapita shuleni kwa miaka mingi na kuchujwa sana. Hao wa kiroho wa kujipa uaskofu na kujipandisha wenyewe bila vigezo hawawezi kushindanishwa na wa kanisa katoliki!!?
 
Siku utakapopata neema ya kuupokea wokovu, utagundua kuwa muda wote tunawindwa na adui. Ukiokoka unakuwa umetangaza vita. Maadui wakuu watatu ni:

1. Shetani
2. Mwili wako
3. Dunia.


KUOKOKA NI LAZIMA IKIWA HUTAKI KUANGAMIA.
 
Roman Catholic ni dhehebu duniani linaloamini mtu hata akiwa jambazi akafa na ujambazi wake waliobaki wakimwombea anaenda mbinguni, madhehebu mengine yote hayaamini katika hilo,yanaamini mtu hutengeneza njia yake kabla hajaondoka
 
Roman Catholic ni dhehebu duniani linaloamini mtu hata akiwa jambazi akafa na ujambazi wake waliobaki wakimwombea anaenda mbinguni, madhehebu mengine yote hayaamini katika hilo,yanaamini mtu hutengeneza njia yake kabla hajaondoka
Ukatoliki ni UPAGANI wa Dola ya Rumi ulioingia kwenye Ukristo kijanja kijanja, pamejaa ibada za sanamu, ibada za kuombea wafu, na kila aina ya upagani. Sheria zao ni zaidi ya Biblia, Papa ni zaidi ya Neno la Mungu (Biblia). NI HATARI ZAIDI YA HATARI!
 

Toa kwanza nukuu ya kwenye Biblia ndio uje na ufafanuzi wa haya mapaji yako. Roho Mtakatifu anajidhihirisha/manifestation kwa jinsi na namna ya mapenzi ya Mungu kutokana na mazingira husika. Ona kwa wale wafuasi/wanafunzi 120 Siku ya Pentekosti Matendo 2. Nyie Mafarisayo mlisema wamelewa mvinyo mpya asubuhi. Ona kwa Hannah, Eli akasema kalewa nk. Roho Mtakatifu hapangiwi na Mwanadamu Bali humratibisha mwanadamu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…