Misa ya Mkapa: Nimeona tofauti kubwa kati ya maaskofu wa Katoliki na wale wa makanisa kama la Gwajima!

Ubaguzi sio jambo jema
 
Hivi Gwajima unamuonaje wewe? Muulize Mbasha atakusimulua vzr,alikamata msg akamhoji mke wake Frola akakili. Mpaka leo hii Mbasa ana act ku move on lkn dish limeyumba sababu ya Gwajima. Kama una ndugu yako kafa muute mwana CCM mwenzako Gwaji boy amfufue
 
Kwa yeyote aliyeko R.C, au kwenye uprotestanti, anatakiwa akubali kuzaliwa mara ya pili ili atoke kwenye level ya dini aje kwenye WOKOVU.

"YESU AKASEMA AMIN, AMIN NAKUAMBIA, MTU ASIPOZALIWA MARA YA PILI HAWEZI KUUONA UFALME WA MUNGU" Yoh 3:3
 
Kwa ufipi Gwajima haubiri anamwaga mipasho na umbea akirukaruka. Simuoni kama ni mtumishi wa mungu ila ni mtafutajimali flani ivi amazing
 
Ukiona MTU mzima anamuamini Gwajima ujue anashida kwa kichwa. Mzee wa mkono na kiuno cha baunsa
 
Maaskofu wa Kikatoliki wamefundishwa kikamilifu maisha ya Kikristo na wanajua elimu,uzoefu na hata kujitolea kimaisha kuishi maisha hayo.

Kwa msingi huo Gwajima wala si Askofu ni jina tu kajipa.
Hana elimu wala haishi maisha ya kiaskofu.
Ndiyo maana ana gombea hadi ubunge!.
Katika Biblia soma 1 Timotheo 3:2-8, Askofu anatakiwa mtu wa aina gani.
Wengi kama Gwajima, Mwamposa, Kakobe , mzee wa Upako hawamo.

1Timotheo 3:2-8
2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha;
3 si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha;
4 mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu;
5 (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)
6 Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi.
7 Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.
8 Vivyo hivyo mashemasi na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana,si watu wanaotamani fedha ya aibu.
 
Elewa kuwa Katoliki huwa inawaelimisha sana makasisi wake kabla ya kuwasimika. Hakuna kasisi wa kikatoliki ambaye hana elimu ya Philosophy, Psychology na Logic.
 
Kusoma sio tatizo unaweza kusoma alafu Mungu asikutambue.
Mungu sio kama taasisi ya kusajiri wahandisi,au basata,kwamba akikutambua,kila MTU atajua,
Hawa wachungaji,manabii,mitume,wamwendo kasi,tunawatambua kwa matendo yao,
Kaita watu wakanyage mafuta,wamekanyagana,wamekufa,kakimbia mbio!!!!
Nabii huyo,!!!!
 
Tofauti ni hawa wanavaa kanzu nyeupe na wengine wanavaa suti 😀😀
 
Tofauti ni kwa saana kanisa katoliki ni taasisi wakati hawa wengine ni ofisi binafsi za mfukoni au wasaka tonge kwa lugha ingine
 
Roman Catholic ni dhehebu duniani linaloamini mtu hata akiwa jambazi akafa na ujambazi wake waliobaki wakimwombea anaenda mbinguni, madhehebu mengine yote hayaamini katika hilo,yanaamini mtu hutengeneza njia yake kabla hajaondoka
Si kweli! Hujui chochote. Unazungumzia jambo usilolijua. Wakatoliki tunaamini na ndio mafundisho ya kanisa kwamba ili umwone Mungu hupaswi kuwa na doa lolote. Hivyo basi kwa kuwa tunajua binadamu si wakamilifu na hapa na pale tunatenda dhambi wakati mwingine bila hata kujua basi tunafanya sala ili Mungu amsamehe huyu mja wake dhambi hizo ndogondogo alizofanya kwa kujua au kutojua. Imani yetu inatufundisha kwamba hawa wenye madoa ya dhambi lazima wasafishwe kwanza kabla ya kufika mbimguni. Kusafishwa huko kunafanyika mahali panaitwa toharani (purgatory). Hawa ndio tunawaombea. Huyu ni wajibu wetu kama wakristo. Mengine tunamwachia Mungu mwenyewe.

Hata hivyo lwa mtu aliyekufa akiwa na dhambi ya mauti (mortal sin) huyu hana nafasi hiyo ya kuombewa kwa sababu yeye anakwenda motoni moja kwa moja. Mfano wa dhambi ya mauti nimkumkana Mungu hadharani, kimkufuru Roho Mt. N.k.

Tunaamini aliyekufa hawezi tena kujiombea mwenyewe. Hivyo atategemea sana akiba ya waombezi aliyojiwekea hapa duniani kuendana na jinsi alivyoishi ikristo wake vizuri.

Hivyo tinawaombea hawa ndugu zetu marehemu kwa sababu hiyo kuu kwamba sisi wakatoliki tunaamini kwamba ni wadhambi na pamoja na kukitahidi kuishinda dhambi lakininudhaifu wetu wa kibindamu inatufanya tusiweze kuwa watakatifu tukiwa hapa duniani.

Kama mtume Paulo anavyotuasa kwamba tukisema kwamba hatuna dhambi tunajidanganya wenyewe na ukweli haumo ndani mwetu, lakini tukikiri dhambi zetu Mungu ni mwaminifu hata akatusamehe.

Hivyo haiwezekani mtu afe bila kuwa na madoa ya dhambi ndogondogo. Hawa ndio tunawaombea. Wale wanaoenda motoni, yaani wenye dhambi za mauti, hata tukiwaombeaje haibadilishi kitu.

Haya ni mambo ya imani. Hayana habari ya ukweli na uongo!
 
Mbona mimi sijawahi kuona kwa Gwajima na wengine wa kiroho wakiongoza misa ya mazishi na hata ya ndoa?
 
Soma historia ya kanisa katoliki na jitihada zake za kuyazima makanisa mengine yaliyoibuka na kuukosoa mfumo wa katoliki.
 
Hii code " Paris Club" , itabd nije PM.
 
Mtu unaweza kujikuta unaabudu kanisa badala ya kumuabudu Mungu.
 
Kiongozi, hao si wakulingaisha na akina Gwajiboy, Mzee wa Upako,bMwingira nk.
 
Mnanyenyekea nini sasa wakati amri za Mungu mmechakachua ?
Wakatoliki mnafit kwenye andiko hili
[emoji116]
23 Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili.
Wakolosai 2:23

Kwa hivyo huo mnaouona ni utaratibu mzuri ni matusi kwa Mungu wa mbinguni kama kweli mnampenda Mungu na mnamnyenyekea TIINI AMRI ZAKE
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…