Misemo gani ya kijinga na kipumbavu watu hutumia kufarijiana?

Misemo gani ya kijinga na kipumbavu watu hutumia kufarijiana?

Siku moja tulikuwa tumekaa kijiweni. Akapita tajiri mmoja wa mtaa tunaoishi kwenye Range Rover mpya, kali sana. Alikuwa anajukana kwa utajiri wake. Tulikuwa tumekaa na mzee mmoja, akaanza kuchoma choma ardhi kwa kijiti, tena kwa ghalabu huku akisema, ''hata uendeshe gari gani, wote njia yetu ni moja tu, tunaelekea huku'', akimaanisha ardhini. Na mara wote tuliokuwa pale tukajisikia kuliwazika na tukajiona na furaha, kama tumetua mzigo mzito.
Ni kweli kabisa.mzee hakukosea.
 
God will do it.

God will make a way.

Muachie Mungu tu.

Hii misemo imewaacha wengi kwenye umaskini na ufukara.
Kumuachia haimaanishi uwe Mzembe , watu wasiosoma vizuri maandiko ndio wanatafsiri na kutumia vibaya huo msemo .Lakini hata mafundisho yameelekeza mtu apambane ili kufanikiwa .

Kumuachia Mungu katika utafutaji ni kunahusisha kufanya jitihada na nyenzo muhimu ili kupata kitu hiko na kutovuka mipaka mfano kutumia njia haramu kama uuaji ,dhuluma ,ufuska nk pamoja na kutokata tamaa na kuwa na dhana nzuri juu yako na Mwenyezi Mungu wakati wa shida au mambo yakienda tofauti na matarajio na kuendelea kupambana katika njia nzuri na Bora.
 
Huu msemo sio wa kijinga bali ni ukweli na uhalisia.

Maisha ndio haya haya, Hakuna maisha mengine zaidi ya hapa duniani.
Inategemea unautumia katika nyakati gani...... Mfano umelala tu unajisikia uvivu kutoka kwenda kwenye mishe unajifariji na "aah maisha ndo haya haya" hapa uvivu unajijaza na uvivu tena
 
Back
Top Bottom