Misemo gani ya kijinga na kipumbavu watu hutumia kufarijiana?

Misemo gani ya kijinga na kipumbavu watu hutumia kufarijiana?

Waliokudharau leo kesho watakuheshimu.
 
Ubaya wa misemo ya kiswahili inapingana yenyewe kwa yenyewe mfano
"Subira huvuta heri" inapingwa na
"Ngoja ngoja utakuta mwana si wako"

Hata huu wa Malipo ni hapahapa itakua tu na msemo mwingine wa kuupinga
Kuna swali la Kiswahili la kidato cha Nne,ambalo huuliza baadhi ya misemo,nahau na methali zimepitwa na wakati.Jadili
 
Hatuagizwi na Maboss sisi wenyewe Maboss.....Jichanganye kama hutalala Njaa
 
Kuna swali la Kiswahili la kidato cha Nne,ambalo huuliza baadhi ya misemo,nahau na methali zimepitwa na wakati.Jadili
Mfano wa misemo iliyopitwa na wakati ni
"Ukiona mwenzako ananyolewa zako zitie maji" huu msemo umepitwa na wakati watu wananyolewa na mashine nywele zinatakiwa ziwe kavu siyo lazima kuloanisha nywele.

Huo Msemo ufutwe hauleti maana kwa sasa
 
Kumuachia haimaanishi uwe Mzembe , watu wasiosoma vizuri maandiko ndio wanatafsiri na kutumia vibaya huo msemo .Lakini hata mafundisho yameelekeza mtu apambane ili kufanikiwa .

Kumuachia Mungu katika utafutaji ni kunahusisha kufanya jitihada na nyenzo muhimu ili kupata kitu hiko na kutovuka mipaka mfano kutumia njia haramu kama uuaji ,dhuluma ,ufuska nk pamoja na kutokata tamaa na kuwa na dhana nzuri juu yako na Mwenyezi Mungu wakati wa shida au mambo yakienda tofauti na matarajio na kuendelea kupambana katika njia nzuri na Bora.
Sasa kama wewe ndio unapambana kwa juhudi zako binafsi, Huyo Mungu haitajiki na hana msaada wowote.

Ni kujifariji na kujipa matumaini uchwara kwamba kuna Mungu anayewezesha mipango yako ilhali ni wewe mwenyewe unapambana kwa juhudi zako binafsi.
 
Back
Top Bottom